Posts

Showing posts from August 18, 2026

Tunduma yalala Seti 2-0 kwa Dodoma CC

Image
  Halmashauri ya Dodoma la Jiji iliendeleza kasi kwenye mchezo wa Mpira wa Wavu kwa Wanaume, ikiichapa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduma kwa seti 2-0. Seti ya kwanza ilimalizika kwa 25-1, kabla ya Dodoma Jiji kushinda seti ya pili kwa 25-7 katika Michezo ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa Tanzania (SHMISEMITA) inayoendelea jijini Mbeya.

Dodoma CC yaichakaza Kibaha DC Vikapu 28-7

Image
Timu ya Mchezo wa Mpira wa Kikapu ya Wanaume ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliichakaza Timu ya Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kwa vikapu 28-7 katika Michezo ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa Tanzania (SHMISEMITA) inayoendelea jijini Mbeya.

Dodoma CC yalazimishwa sare Mpira wa Mikopo SHIMISEMITA

Image
Timu ya Mpira wa Mikono ya Wanaume ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ililazimishwa sare ya 5-5 dhidi ya Halmashauri ya Wilaya ya Magu katika Michezo ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa Tanzania (SHMISEMITA) inayoendelea jijini Mbeya.  

Dodoma Jiji yaifunga Mji Ifakara 41-3 Mpira wa Pete Mashindano ya SHIMISEMITA

Image
Na. Mwandishi wetu, MBEYA Timu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya Mpira wa Pete Wanawake imeishushia kipigo kizito Timu ya Halmashauri ya Mji Ifakara cha magoli 41-3 katika siku ya pili ya Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa Tanzania (SHIMISEMITA) yanayoendelea jijini Mbeya. Mchezo huo ulianza kwa kasi katika dakika za mwanzo, lakini kadri muda ulivyokuwa ukiendelea Timu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilionekana kuumiliki mchezo. Hadi kufikia tamati ya mchezo huo Timu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliibuka na ushindi mnono wa magoli 41-3 ya Halmashauri ya Mji Ifakara. Mchezo wa Mpira wa Mikono Wanaume Halmashauri ya Jiji la Dodoma ililazimishwa sare ya 5-5 dhidi ya Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Aidha, katika Mchezo wa Mpira wa Kikapu ya Wanaume Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliichakaza Timu ya Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kwa vikapu 28-7. Halmashauri ya Dodoma la Jiji iliendeleza kasi kwenye mchezo wa Mpira wa Wavu kwa Wanaume, ikiichapa Ha...