Posts

Showing posts from January 20, 2024

TANESCO Ddodoma kuendelea kuboresha miundombinu ya umeme Jiji la Dodoma

Image
Na. Mwandishi Wetu-DODOMA SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Dodoma limetoa semina kwa madiwani wa kata zote 41 za Jiji la Dodoma lengo likiwa ni kueleza mikakati ya shirika hilo pamoja na miradi inayotekelezwa katika Mkoa wa Dodoma. Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Dodoma, Charles Mamba,akizungumza wakati akifungua Mkutano wa Madiwani, kamati ya ulinzi na Usalama Wilaya na Polisi kata wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma ulioandaliwa na Shirika la Umeme (TANESCO) Mkoa wa Dodoma Akitoa elimu jijini Dodoma, Meneja wa TANESCO Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Donasiano Shamba alisema kikao hicho kimejumuisha Madiwani, Kamati ya Usalama Wilaya na Polisi kata wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. “Kikao hiki kimehusisha madiwani kutoka kata zote 41 za Jiji la Dodoma pamoja na Polisi kata lengo ni kueleza mikakati yetu lakini pia kueleza changamoto zinazotukabili sisi kama shirika hasa suala la uharibifu wa miundombinu ya usafirishaji na usambazaji wa umeme” alisema Mhandisi Shamba...

Jiji la Dodoma lakemea utapishaji maji taka

Image
Na. Dennis Gondwe, CHAMWINO HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imekemea tabia ya baadhi ya wakazi kutapisha vyoo kipindi cha mvua na kusababisha kinyesi kwenda kwenye maji yanayotumiwa na wananchi. Maji taka Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Kitengo cha Usafi na udhibiti wa taka ngumu, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alipokuwa akiongea na mamia ya wakazi wa Kata ya Chamwino waliojitokeza kufanya usafi wa pamoja siku ya Jumamosi. Kimaro alisema “kuna tabia imeibika kwa baadhi ya wakazi wa Kata ya Chamwino kutapisha vyoo. Ndugu zangu tabia hiyo halikubaliki kutapisha vyoo kwa sababu mvua inaponyesha inasomba kile kinyesi na kupeleka kwenye vyanzo vya maji. Maji hayo tunayatumia sisi wenyewe kwa matumizi ya kawaida. Nitumie nafasi hii kuwataka wenye tabia hiyo waache mara moja na tukikukamata tutakuchukulia hatua kwa mujibu wa sheria”. Mkuu wa Kitengo cha Usafi na udhibiti wa taka ngumu, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro akitoa karipio Alisema kuwa eneo la Kat...

Kata ya Chamwino yatakiwa kuchukua tahadhari ya Kipindupindu

Image
Na. Dennis Gondwe, CHAMWINO HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imefurahishwa na muitikio wa wakazi wa Kata ya Chamwino kushiriki katika mazoezi ya usafi wa mazingira na kuwataka kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa kipindupindu. Mkuu wa Kitengo cha Usafi na udhibiti taka ngumu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro akiongea na mamia ya wakazi wa Kata ya Chamwino Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Kitengo cha Usafi na udhibiti taka ngumu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alipokuwa akiongea na mamia ya wakazi wa Kata ya Chamwino waliojitokeza kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya kata hiyo. Kimaro alisema “nichukue nafasi hii kuwashukuru sana wakazi wa Kata ya Chamwino kwa jinsi mlivyojitokeza kwa wingi kufanya usafi katika eneo la makaburi ya Hijra na maeneo mengine ya kata. Tulichokifanya hapa ni ibada tosha kwa sababu tumesafisha eneo tulipowalaza ndugu zetu. Lakini niwapongeze kwasababu mmekuwa mkijitokeza kwa wingi kufanya usafi katika makazi n...