Posts

Showing posts from December 4, 2023

JAMII DODOMA YASHAURIWA KUSAIDIA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

Image
  Na. Dennis Gondwe, HOMBOLO BWAWANI JAMII imeshauriwa kutenga muda kuwasaidia watoto wenye mahitaji maalum katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ili waweze kujimudu na kufikia malengo ambayo taifa linapenda. Mdau wa elimu katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Tatu Mwangu akimpatia zawadi mtoto Kauli hiyo ilitolewa na mdau wa elimu katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Tatu Mwangu alipoungana na Jumuiya ya Shule ya Msingi Feza tawi la Dodoma kutoa msaada wa viti mwendo nane na vifaa vya elimu kwa watoto wenye mahitaji maalum katika Shule ya Msingi Hombolo Bwawani. Mwl. Mwangu alisema “katika hali ya kawaida sisi kama jamii tunawajibika kuwasaidia wote wasio na uhitaji na wenye uhitaji maalum kufikia ndoto zao. Leo kupitia familia ya Shule ya Feza wamepewa vifaa vya kuwasaidia katika kujifunza na kuweza kutembea kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine kwa wale wenye changamoto ya viungo. Tuishukuru familia ya Shule ya Feza kwa kutushirikisha wazazi. Kwa kufanya hi...

JIJI LA DODOMA LAMSHUKURU DKT. SAMIA KUJALI WATOTO WENYE MAHITAJI

Image
  Na. Dennis Gondwe, HOMBOLO BWAWANI HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imemshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali watoto wenye mahitaji maalum. Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Issa Kambi (kushoto) akimsaidia mtoto mwenye mahitaji maalum kutembea. Kulia ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Feza Dodoma, Yunus Khusanbaev nae akimsaidia mtoto kutembea Shukrani hizo zilitolewa na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Issa Kambi katika hafla ya kupokea viti mwendo na vifaa vya shule kwa watoto wenye mahitaji maalum katika Shule ya Msingi Hombolo Bwawani iliyopo jijini Dodoma. Mwl. Kambi alisema “tunamshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya kwa watoto hawa wenye mahitaji maalum katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Mfano, katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma Mheshimiwa Rais kupitia Ofisi ya Rais, Tamisemi anatuletea shilingi 26,000,000 kila mwezi kwa ajili ya chakula cha watoto hawa. Tunapop...

VYOMBO VYA HABARI JIJI LA DODOMA VYAPONGEZWA KUJALI WENYE MAHITAJI MAALUM

Image
  Na. Dennis Gondwe, HOMBOLO BWAWANI VYOMBO vya habari katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma vimepongezwa kwa utayari wao kutangaza mafanikio na changamoto wanazopitia watoto wenye mahitaji maalum katika Shule ya Msingi Hombolo Bwawani. Diwani wa Kata ya Hombolo Bwawani, Ased Ndajilo akikabidhi zawadi kwa watoto wenye mahitaji maalum Diwani wa Kata ya Hombolo Bwawani, Ased Ndajilo akihamasisha jamii kuchangia watoto wenye mahitaji maalum Pongezi hizo zilitolewa na Diwani wa Kata ya Hombolo Bwawani, Ased Ndajilo alipokuwa akitoa shukrani kwa Jumuiya ya Shule ya Msingi Feza tawi la Dodoma walipotembelea Shule ya Msingi Hombolo Bwawani kutoa zawadi ya viti mwendo nane na vifaa vya elimu kwa watoto wenye mahitaji maalumu wa Shule ya Msingi Hombolo Bwawani. Ndajilo alisema “napenda kumshukuru sana Mwenyezi Mungu, Mheshimiwa Rais, mama yetu Samia Suluhu Hassan, Mbunge na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde kwa kazi nzuri wanayofanya katika Kata ya Hombolo Bwawani. Sina budi kushukur...

MATUKIO KATIKA PICHA UGAWAJI WA ZAWADI KWA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM SHULE YA MSINGI HOMBOLO BWAWANI

Image
 

MATUKIO KATIKA PICHA UTEREMSHAJI WA VIFAA KWA AJILI YA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUM SHULE YA MSINGI HOMBOLO BWAWANI

Image
 

JIJI LA DODOMA LAZINDUA ZOEZI LA UBAINISHAJI WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

Image
Na. Dennis Gondwe, HOMBOLO BWAWANI Halmashauri ya Jiji la Dodoma imezindua zoezi la ubainishaji watoto wenye mahitaji maalum katika jamii ili waweze kupata haki yao ya elimu na matunzo kwa mujibu wa sheria. Kauli hiyo ilitolewa na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Issa Kambi alipokuwa akizindua zoezi la ubainishaji watoto wenye mahitaji maalum katika jamii uzinduzi uliofanyika katika Shule ya Msingi Hombolo Bwawani iliyopo Kata ya hombolo Bwawani jijini Dodoma. Kambi ambae ni Afisa Elimu Maalum katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema “kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma ambae alipenda sana kuwa nasi hapa leo napenda kuzindua rasmi zoezi la ubainishaji watoto wenye mahitaji maalum kwa maana ya kwenda kuwatafuta mtaani na kuwaleta kwenye vituo vyetu kama hiki na vitengo vingine. Zoezi litafanyika katika mitaa nane ya Itega, Salama, Lugala, Mnyakongo, Mtube, Nala, Chigongwe na Mbalawala”. Alisema kuwa lengo la zoezi hilo ni kuwaba...

MANENO YA MWALIMU MKUU SHULE YA MSINGI HOMBOLO BWAWANI

Image
 

NENO LA DIWANI KATA YA HOMBOLO BWAWANI

Image
 

KAULI YA MAKAMU MWENYEKITI BODI YA SHULE YA MSINGI FEZA DODOMA

Image
 

WAZAZI SHULE YA FEZA DODOMA WAPONGEZWA KUCHANGIA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

Image
  Na. Dennis Gondwe, HOMBOLO BWAWANI WAZAZI wa Shule ya Msingi Feza na jamii wamepongezwa kwa kuchangia watoto wenye mahita maalum kwa moyo na upendo sababu ni sehemu ya jamii jambo linalowapa faraja watoto. Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Msingi Feza Dodoma, Mariam Mafuru akiongea na jumuiya ya Shule ya Msingi Hombolo Bwawani Kauli hiyo ilitolewa na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Msingi Feza Dodoma, Mariam Mafuru alipokuwa akitoa salamu za shule hiyo kwa Jumuiya ya Shule ya Msingi Hombolo Bwawani alipoongoza ujumbe wa shule hiyo kupeleka zawadi kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum katika Kata ya Hombolo Bwawani. Mafuru alisema “napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru wazazi wenzangu tulioweza kushikiri na kujitoa kwa hali, mali na muda kuweza kuchangia zoezi hili na hatimae leo mafanikio yameonekana. Hiki kinachoonekana mbele yetu ni nguvu zetu sote, wazazi tumeshirikiana kwa pamoja tumeweka moyo na upendo kwa ajili ya kuwasaidia watoto wetu wapendwa. Kama famili...