Posts

Showing posts from December 21, 2023

SIKU 100 ZA WAZIRI SILAA WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI

Image
Na Eleuteri Mangj, WANMM   Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa amefanya kikao na Makamishna wa Ardhi Wasaidizi mikoa yote Tanzania Bara kutathmini siku 100 za uongozi wake tangu ameanza kuiongoza wizara hiyo.   Kikao hicho kimefanyika leo Desemba 21, 2023 jijini Dodoma ambapo Mhe. Waziri Silaa amekutana Menejimenti ya Wizara, Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa mikoa kujitatnmini katika kutekeleza maagizo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusu matumizi bora ya ardhi.   "Hiki ni kikao kazi cha kutathmini siku 100 na kutengeneza mpango wa kutekeleza maagizo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutatua matatizo ya migogoro ya ardhi na kuwahudumia wananchi wetu" amesema Mhe. Waziri Silaa.   Waziri Silaa amewasisitiza Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa Mikoa kuwa wana kazi ya kusimamia watumishi walio chini yao kwa kujipanga vizuri na wana uwezo kubadilisha jinsi sekta ya ardhi inavyoendeshwa nchini kote.   Waziri Sil...