Posts

Showing posts from August 4, 2026

Jiji la Dodoma lawapa vijana fursa mikopo ya 10%

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeendelea kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia mikopo ya asilimia 10, hatua inayowapa nafasi ya kuanzisha na kuendeleza shughuli mbalimbali za uzalishaji, ikiwemo viwanda vidogo, utengenezaji wa bidhaa na utunzaji wa mazingira. Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’wale, Husna Toni mara baada ya kutembelea vikundi vya vijana vinavyofanya shughuli mbalimbali katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alisema kuwa ziara hiyo imetoa fursa ya kujifunza namna vijana wa Jiji la Dodoma wanavyotumia mikopo ya asilimia 10 kujiajiri, kuongeza kipato na kuchangia maendeleo ya jamii. “Vijana wa Dodoma wana uthubutu mkubwa katika shughuli za uzalishaji, viwanda na utunzaji wa mazingira. Hii inatuonesha kwamba fursa zipo na vijana wakipewa mitaji na mazingira mazuri wanaweza kujiajiri na kuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya taifa” alisema Toni. Aliongeza kuwa vijana wanapaswa kutumia fursa zinazopatikana, husus...

Meya Chaula: Kanda za utoaji huduma kusogeza huduma kwa wananchi Dodoma

Image
Na. Mwandishi wetu, MAKUTUPORA Uanzishwaji wa kanda za utoaji huduma katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ni mkakati unaolenga kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi, kuongeza ufanisi wa utendaji kazi na kuharakisha maendeleo katika maeneo yote ya jiji. Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika jijini Dodoma, Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula   alisema kuwa mfumo wa kanda utarahisisha upatikanaji wa huduma mbalimbali za halmashauri, kupunguza muda wa wananchi kufuata huduma katika makao makuu ya jiji na kuongeza uwajibikaji kwa watendaji. Chaula ambae ni Diwani wa Kata ya Makutupora alisema kuwa kata hiyo ipo katika Kanda Namba Sita hivyo,   wananchi watapata huduma kwa urahisi zaidi, zikiwemo huduma za usafi wa mazingira, ukusanyaji wa mapato, usimamizi wa miradi ya maendeleo, pamoja na kushughulikia changamoto zinazojitokeza katika maeneo yao kwa wakati. “Madhumuni ya uanzishwaji wa kanda hizi ni kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora ...

Jiji la Dodoma laibuka na zana za upaliliaji, Maonesho ya Nanenane

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeendelea kung’ara katika Maonesho ya Nanenane kwa kuweka vitu vya kitofauti kama zana za upaliliaji ambazo zimeundwa na mjasiriamali mdogo wa ndani ya jiji. Akizungumza na waandishi wa habari mjasiriamali, Zuberi Nguzo aliyepata fursa ya kuonesha ujuzi katika maonesho hayo alisema kuwa zana hizo zimeundwa kwa muundo wa ‘power tiller’ ya miguu mitatu zikiwa katika ubora wa hali ya juu. “Zana hizi za upaliliaji zinatumia injini ya guta lakini ina mfumo wa rejeta kama kawaida. Pia ina mfumo wa feni na upande wa nyuma kuna jembe ambalo hili ndilo linatumika kwa ajili ya upaliliaji. Katika upaliliaji inatumia mfumo wa matuta kwa maana kwamba inapita katikati ya mstari na kuweka matuta kwenye mashina ya mahindi kwasababu tairi zake tumeweka kwa kipimo cha sentimita 62, hiki ni kipimo sahihi kabisa kwa upana kwa kilimo cha mahindi,” alisema Nguzo. Alisema kuwa ameamua kubuni zana hizo kwasababu baadhi ya vifaa vya kuundia vina...

Hospitali ya Jiji la Dodoma yatoa elimu ya unyonyeshaji maziwa ya mama

Image
Na. Mwandishi wetu, NALA Hospitali ya Jiji la Dodoma iliyopo Kata ya Nala imetoa elimu ya unyonyeshaji wa maziwa ya mama na lishe bora kwa akina mama 43 waliofika kupata huduma za kliniki, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Unyonyeshaji wa Maziwa ya Mama Duniani. Akifungua maadhimisho ya wiki hiyo, Afisa Lishe katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alpha Fanuel alisema kuwa mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo akina mama kuhusu unyonyeshaji sahihi na kuzingatia lishe bora ili kuboresha afya ya mama na mtoto. “Mama anaponyonyesha anachangia ukuaji bora wa mtoto, kuimarisha uhusiano kati ya mama na mtoto, kupunguza hatari ya baadhi ya magonjwa kama mzio kwa mtoto. Pia unyonyeshaji unasaidia kupunguza hatari ya saratani ya matiti kwa mama anayenyonyesha ipasavyo,” alisema Fanuel. Aliongeza kuwa washiriki wamepata mafunzo kwa vitendo kuhusu makundi sita ya chakula na namna ya kuandaa uji wenye virutubisho unaomsaidia mama anayenyonyesha kupata lishe bora na kuongeza uzalis...