Posts

Showing posts from March 4, 2025

Wanawake watakiwa kujitathmini katika uongozi

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Wanawake watakiwa kujitathmini katika nyanja za uongozi kwa kuonesha nia ya kuwajibika ipasavyo na kuchangamkia fursa za uongozi zinazojitokeza katika jamii. Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule alipokuwa akizungumza na maelfu ya wanawake waliojitokeza katika kongamano la kanda ya kati lililohusisha mikoa mitatu (Dodoma, Singida na Iringa) katika kuelekea kilele cha Siku ya Wanawake Duniani kongamano hilo lilifanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre, Dodoma. Senyamule alisema ā€œnaomba nitoe shime kila mmoja wetu ajitathmini hatua gani amechukua kuonesha uwezo wake wa kuongoza katika eneo alilopewa. Ni imani yangu kuwa kila mahali tunatosha kwasababu Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameonesha uwezo wa kutosha kwenye nafasi ya urais. Kwahiyo, wanawake tunaweza katika kila eneoā€. Akiongelea kuhusu takwimu za wanawake viongozi wa Mkoa wa Dodoma, alisema karibu ngazi zote za uongozi kuna viongozi wa kike na takwimu z...

Jiji la Dodoma latoa elimu dhidi ya ukatili wa kijinsia kwa wanafunzi wa kike

Image
Na. Nancy Kivuyo, DODOMA Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kupitia Divisheni ya Maendeleo ya Jamii, walitoa mafunzo kwa wanafunzi wa Shule za Sekondari Viwandani na Kikuyu ikiwa ni shamrashamra za kueleka kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani itakayofanyika kitaifa mkoani Arusha tarehe 08 Machi, 2025. Akizungumza na wanafunzi wasichana kwenye shule hizo, Afisa Maendeleo ya Jamii, Dawati la Msaada wa Kisheria, Elizabeth Godwin alisema ā€œtupo katika kuhakikisha binti anapata elimu kuhusiana na masuala ya ukatili wa kijinsia kwasababu tunaamini ya kwamba, binti anapofanyiwa ukatili wa kijinsia ndio tunapoteza ule uhalisia wa mwanamke ambae baadae ndio angekuja kuwa nguzo muhimu ya familia kama mlezi au mzazi mzuri. Tushukuru Mungu wanafunzi wameitikia wito wa elimu hii nzuri, wameonesha kuelewa juu ya elimu ya ukatili na mahali gani pa kuripotiā€. Nae Mratibu wa Elimu Kata ya Viwandani, Zaituni Mkoyi aliwaasa wasichana wanafunzi kuzingatia masomo ili waje kuwa mfano m...

Wanawake TALGWU Dodoma wakabidhi Tenki la Maji lenye ujazo wa Lita 4,000

Image
Na. Nancy Kivuyo, DODOMA Kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Kamati ya Ushauri Wafanyakazi Wanawake ya TALGWU Mkoa wa Dodoma, imetembelea Kituo cha Afya Mkonze katika kufanya matendo ya huruma na kukabidhi msaada wa tenki la maji lenye ujazo wa lita 4,000. Akizungumza na uongozi wa Kituo cha Afya Mkonze, Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri Wafanyakazi Wanawake ya TALGWU Dodoma, Siwajibu Clavery alisema, ā€œmaadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yana dhima kubwa sana hasa ukizingatia mwanamke ndio kinara wa majukumu kwenye sehemu muhimu za familia. Sisi tumeona ni vema kufanya matendo ya huruma na kutoa msaada wa tenki hili ili wagonjwa hasa wanawake waweze kupata huduma ya maji wawapo katika matibabu kituoni hapa. Tunaomba mtumie kwa lengo hili kusudiwaā€. Nae Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mkonze, Halima Kheri alisema anashukuru sana kwa msaada huo na atahakikisha linatumika vema ili huduma ya maji ya ziada kituoni hapo isikosekane. Msaada huo wa tenki la kuhifadhia...

Kongamano kuhamasisha wanawake kugombea nafasi za uongozi lafanyika Dodoma

Image
Na. Nancy Kivuyo, DODOMA Kongamano la kanda ya kati likihusisha mikoa ya Dodoma, Singida na Iringa lilifanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete huku kaulimbiu ikiwa ā€˜Wanawake na Wasichana 2025: Tuimarishe Haki, Usawa na Uwezeshajiā€™. Katika kongamano hilo, mada chokozi inayosema ā€œWanawake na Uongozi katika miaka 30 ya Beijingā€ iliandaliwa ambapo wanawake mashuhuri walialikwa kujadili mada na kutoa shuhuda mbalimbali za namna walivyoweza kufaulu katika harakati za kuwa viongozi na kushika nyadhifa mbambali nchini. Akizungumza na maelfu ya wanawake waliohudhuria katika kongamano hilo mgeni rasmi Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anna Makinda alisema ā€œwanawake changamkieni fursa za uongozi kwasababu hata sisi tumekua mfano kwenu, angalieni mheshimiwa rais wetu ni mwanamke anaiongoza nchi hii bila hofu, nyie mnashindwa hata kugombea udiwani?. Akina mama amkeni, awamu hii tunaelekea kwenye uchaguzi hivyo tunawategemea uwakilishi kwenye ubunge, udiwani na nafasi zi...