Posts

Showing posts from August 17, 2024

Makamu wa Rais azungumza na viongozi wa CCM Mkoa wa Dodoma

Image
MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmshauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi ambaye ni Mlezi wa CCM Mkoa wa Dodoma, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Dkt. Philip Mpango ameiagiza Serikali ngazi ya Mkoa wa Dodoma kuendelea kutafutia ufumbuzi migogoro ya ardhi iliyokithiri hususan fidia kwa ardhi iliyotwaliwa na utekelezaji wa mgawanyo wa ardhi wa 70% kwa 30%.  Makamu wa Rais ametoa maelekezo hayo wakati akizungumza na Viongozi na Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma katika Mkutano uliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete mkoani Dodoma. Amesema changamoto hiyo ya ardhi mkoani Dodoma kwa kiasi kikubwa imewafanya wanachama pamoja na wananchi kuwa na manung’uniko na hata kufikia hatua ya kususia uchaguzi. Amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kushirikiana na Waziri wa Ardhi kwa pamoja na uongozi wa Jiji la Dodoma kuongeza nguvu zaidi katika kushughulikia migogoro hiyo. Dkt. Mpango amewahimiza viongozi wa Chama Cha Mapinduzi mkoani ...

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa tarehe 27 Novemba, 2024

Image
Na. Anna Stanley, DODOMA Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamedi Mchengerwa ametoa tangazo la uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka na uchaguzi utafanyika tarehe 27 Novemba, 2024. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamedi Mchengerwa Mchengerwa aliyasema hayo katika viwanja vya Chinangali park, jijini Dodoma wakati akizungumza na wananchi na kuwahamasisha kugombea nafasi za uongozi wa serikali za mitaa na kujitokeza kupiga kura. "Tangazo hili limetolewa chini ya Kanuni ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ya mwaka, 2024 pamoja na matangazo ya serikali Na. 571, Na. 572, Na. 573, Na. 574 ya mwaka 2024" alisema Mchengerwa. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Ibara ya 145 na Ibara ya 146, inaeleza uwepo wa Serikali za Mitaa pamoja na madhumuni yake ambapo miongoni mwa madhumuni ni pamoja na kupeleka madaraka kwa wananchi, alisema. “Sheria za Serikali za Mitaa, Mam...

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa nchini Novemba, 2024

Image
Na. Valeria Adam, DODOMA Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetangaza rasmi ratiba ya uchaguzi wa serikali za mitaa kwa mwaka 2024, ambao unatarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba, 2024. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa alitoa tangazo la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, ambapo alieleza kuwa tangazo hilo limetolewa chini ya Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa za mwaka 2024 pamoja na matangazo ya Serikali namba 571, 572, 573 na 574 ya mwaka 2024. "Mtiririko wa tangazo la uchaguzi wa serikali za mitaa umegawanyika katika sehemu tatu ambazo ni utangulizi, masharti muhimu ya uchaguzi na ratiba ya uchaguzi. Kwa wagombea wa nafasi za uongozi, wanatakiwa kuwa wanachama wa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu. Uteuzi wa wagombea utafanyika siku 19 kabla ya uchaguzi na endapo kutakuwa na mgombea mmoja pekee kwa nafasi husika, atateuliwa moja kwa moja” alisema Mchengerwa. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza...

Diwani Fundikira adhamiria kumaliza Kero za Wafanyabiashara wa Soko la Mavunde

Image
Na. John Masanja, CHANG’OMBE Diwani wa Kata ya Chang'ombe, Bakari Fundikira amefanya kikao na viongozi wa Soko la Mavunde chenye dhamira ya kuziangazia changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara wa soko hilo na kuzifanyia utatuzi. Diwani wa Kata ya Chang'ombe, Bakari Fundikira akiongea na waandishi wa habari Kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Kata ya Chang'ombe iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Akizungumza na waandishi wa Habari baada ya kikao hicho, Diwani Fundikira alisema moja ya changamoto walizozitambua ni pamoja na changamoto ya uwelewa wa mikataba pia kutozingatia sheria na taratibu za uendeshaji wa shughuli za kibiashara ndani ya soko. “Lengo letu sisi viongozi ni kuhakikisha kuna uelewa mzuri kwa wafanyabiashara hawa kuhusu jinsi ya kuendesha shughuli zao wakiwa kwenye mazingira rafiki kwa kuzingatia sheria na taratibu. Pia serikali yetu iweze kukusanya mapato pasipo mtu kushurutishwa wala kulazimishwa” alisema D...

Diwani Fundikila awataka wananchi kuendeleza amani kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Image
Na. Emmanuel Lucas, CHANG’OMBE Diwani wa Kata ya Chang`ombe, Bakari Fundikira amewataka wananchi kuendelea kutunza amani, upendo na mshikamano hasa katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa 2024 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohammed Mchengerwa kutoa tamko la uchaguzi wa serikali za mitaa. Diwani wa Kata ya Chang`ombe, Bakari Fundikira akisisitiza jambo Kauli hiyo aliitoa kwa waandishi wa Habari baada ya kikao na viongozi wa Soko la Mavunde kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Kata ya Chang'ombe iliyopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Diwani Fundikira alisema “kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa, Waziri mwenye dhamana Mheshimiwa Mohammed Mchengerwa ameshatoa tarehe ya uchaguzi ambayo itakuwa tarehe 27 Novemba, 2024. Rai yangu kwa wananchi wa Kata ya Chang`ombe na wananchi wengine, itakapofika wakati wa uandaaji wa daftari la wapiga kura cha kwanza tujitokeze wananchi wote wenye sifa tujiandikis...

CCM yawataka wanachama kushiriki uchaguzi ujao

Image
Na. Valeria Adam, DODOMA Kuelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma, Dkt. Philip Mpango amehizima wanachama wa CCM kujitokeza kwa wingi na kushiriki ili kuhakikisha ushindi katika chama chao. Kauli hiyo aliitoa katika hafla ya kumpokea iliyoandaliwa na Chama Cha Mapinduzi na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma. Dkt. Mpango ambae ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alisema kuwa ni muhimu kwa wanachama wa CCM kujitokeza na kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Uchaguzi ni muhimu na lazima kwa kila mwananchi kushiriki aliongeza kuwa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ni jambo la msingi kwa mafanikio ya watanzania na chama hicho, aliongeza. “Tarehe 27 Novemba, mwaka huu tutafanya uchaguzi wa serikali za mitaa na mwaka ujao tutafanya uchaguzi mkuu. Ili kukipa chama chetu ushindi katika chaguzi hizi ni lazima tujipange ili kuhakikisha tunapata ushind...