Posts

Showing posts from March 12, 2025

Dkt. Sagamiko asema, ugawaji jimbo hauna athari kwa huduma zinazotolewa na Jiji la Dodoma

Image
Na, Nancy Kivuyo, DODOMA Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alitoa hofu Baraza la Madiwani kuwa kukidhi vigezo vya ugawaji wa Jimbo la Dodoma Mjini hauna athari katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo katika kuwahudumia wananchi. Aliyasema hayo wakati akijibu hoja za madiwani waliohudhuria katika Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kupokea taarifa ya mapendekezo ya mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. ā€œMgawanyo wa jimbo kwa upande wa tarafa hauna kikwazo chochote, kama ni kata ni kikwazo kwasababu kata moja haiwezi kuwa katika majimbo mawili. Leo tutaangalia zaidi kwenye kataā€ alisema Dkt. Sagamiko. Aliongeza kuwa, athari za mgawanyo wa jimbo kimapato unalenga mgawanyo wa majimbo na sio shughuli za kiutendaji. ā€œNiwatoe wasiwasi, utoaji wa huduma kwa wananchi utaendelea kama ilivyokua awali na Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Baraza litakua moja bila kujali jimbo analotoka diwani. M...

DC SHEKIMWERI: ā€œTufuate Utaratibu Mzuri wa Tume Huru ya Taifa Uchaguzi ili tulinde Jiji la Dodomaā€

Image
Na. Leah Mabalwe, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaji Jabir Shekimweri, awataka viongozi wa vyama vya siasa pamoja na wananchi kufuata maelekezo ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ili kutovuruga maendeleo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.   Aliyasema hayo katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Dodoma kilichoketi kujadili taarifa ya mapendekezo ya mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini na kuzalisha Jimbo la Mtumba pamoja na Jimbo la Dodoma mjini. Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la leo tarehe 12 Machi, 2025. ā€œSerikali ya awamu ya sita chini ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, inatoa fedha nyingi kwaajili ya kuboresha Mji wa Dodoma. Hivyo, napenda kuwaomba sana viongozi wangu mbalimbali wa vyama vya siasa pamoja na vijana wote kwa ujumla kuelekea katika uchaguzi mkuu wa serikali, kufuata taratibu nzuri na kuepuka vurugu, na ili kuepuka vurugu ni kufuata utaratibu mzuri wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kuanzia wakati wa kujian...

Halmashauri ya Jiji la Dodoma Kuhudumia Majimbo Mawili ya Uchaguzi

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imejipanga vema kutoa huduma kwa wananchi wote kwa kuzingatia mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini wenye mapendekezo ya kuligawa jimbo hilo kuwa Jimbo la Mtumba lenye jumla ya kata 20 na Jimbo la Dodoma Mjini lenye kata 21. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko, mara baada ya majadiliano kutoka kwa Madiwani kuhusu taarifa iliyowasilishwa na Afisa Uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Albert Kasoga ya kuwasilisha mapendekezo ya mgawanyo wa Jimbo la Dodoma Mjini, katika Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani lililofanyika tarehe 12 Machi, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Dkt. Sagamiko alisema ā€œmgawanyo huu kwa sasa unalenga mgawanyo wa jimbo kuwa majimbo mawili, bado tutaendelea kuwa na halmashauri moja kwa maana ya utoaji huduma kwa ngazi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Jiji litaendelea kuwajibika katika utoaji wa huduma katika majimbo yote mawiliā€. Akizung...

Dkt. Sagamiko amshukuru Rais Dkt. Samia, Jiji la Dodoma kuwa la mfano

Image
Na. Nancy Kivuyo, DODOMA Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko, amshukuru Rais, Dkt. Samia kwa kulifanya jiji hilo kuwa la mfano nchini na kuahidi utoaji wa huduma bora kwa wananchi alipotembelea banda hilo kwenye maonesho ya shughuli zinazotekelezwa na Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini.   Aliyasema hayo wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alipotembelea banda la Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Center kabla ya ufunguzi wa Mkutanao wa 39 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT). ā€œMheshimiwa Rais, Halmashauri ya Jiji la Dodoma ndiyo halmashauri pekee yenye muundo wa kipekee katika halmashauri zote 184 zilizopo Tanzania. Moja ya upekee huo ni Divisheni ya Uendelezaji Makao Makuu. Baada ya Dodoma kuwa makao makuu mwaka 1976 iliweza kuandaliwa Mpango Kabambe wa kuuendeleza Mji wa Dodoma ikiwemo Uwanja wa Ndege wa Msalato pamoja na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)ā€ alisema Dkt. Sagamiko...

Ujenzi Shule za Sekondari za ziada Suluhu Changamoto ya Umbali

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Kata 41 za Halmashauri ya Jiji la Dodoma zinatarajiwa kunufaika na ujenzi wa shule za sekondari za ziada kwa ajili ya kuhakikisha mtoto anapata elimu katika mazingira mazuri na kutatua changamoto ya umbali wa kupata huduma ya elimu. Hayo yalisemwa na Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony Mavunde, alipokuwa akitoa hotuba kwa madiwani, wakuu wa divisheni na vitengo, walimu, watendaji wa kata na wanafunzi waliohudhuria katika hafla ya Ugawaji Kompyuta na Printa kwa Shule za Sekondari na maafisa watendaji wa kata jijini Dodoma. Mbunge wa Jimbo la Dodoma, Anthony Mavunde alisema ā€œmoja kati ya mipango yangu mikubwa nayoendelea nayo ni kuendelea kuhakikisha kata zote za Dodoma zina sekondari, tukimaliza hayo tuongeze sekondari za ziada hasa zile ambazo watoto wanatembea umbali mrefu. Mheshimiwa mkuu wa wilaya ukienda pembezoni mwa Jiji la Dodoma, kuna maeneo ambayo watoto walikuwa wanatembea mpaka kilomita 16 kufuata shule. Ukienda Kata ya Chahwa eneo la Mahoma Makulu...

Mbunge Mavunde akabidhi Kompyuta kwa Kata 41 za Jiji la Dodoma

Image
Na. Nancy Kivuyo, VIWANDANI Watendaji wa Kata 41 za Halmashauri ya Jiji la Dodoma wapokea Kompyuta na Printa kwa ajili ya kurahisisha na kuboresha utendaji kazi wenye ufanisi za kuwahudumia wananchi. Vifaa hivyo, viligawiwa katika hafla ya Ugawaji Kompyuta na Printa kwa Shule za Sekondari za Serikali na Watendaji wa Kata jijini Dodoma, iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Viwandani.   Akizungumza wakati wa ugawaji kompyuta hizo, Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde, alisema kuwa anawapa kompyuta maafisa watendaji wa kata zote 41 kwaajili ya kuwasaidia kufanya kazi zao kidigitali zaidi. ā€œKompyuta na printa hizi natumaini zitachochea utendaji kazi ulio mzuri. Tuipongeze serikali chini ya uongozi wa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maboresho makubwa ya miundombinu kwenye sekta ya elimu jijini Dodoma ambapo kwa mwaka huu wa fedha zimetengwa shilingi bilioni 16ā€ alisema Mavunde. Nae, Afisa Mtendaji wa Kata ya Hazina, Tunu Mahmoud, alisema kuwa ameguswa na tukio l...

Mkutano Mkuu wa 39 wa ALAT wafanyika Dodoma

Image
Na. Aisha Ibrahim, DODOMA Mkutano mkuu wa 39 wa Mwaka wa Mamlaka ya Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) umefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Convention Center jijini Dodoma, uliofunguliwa na mgeni rasmi ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa lengo la kujadili na kufanya tathmini ya mipango ya ALAT na mambo mbalimbali yanayoendelea katika serikali za mitaa. Akitoa taarifa wakati wa mkutano huo, Mwenyekiti wa ALAT Taifa, Murshid Ngeze, alisema kuwa katika mkutano wa mwaka huo wamejitahidi kualika viongozi mbalimbali wakiwemo wenyeviti wa mitaa ili kupata maarifa mbalimbali yanayohusiana na uendeshaji wa serikali za mitaa. Hivyo, kwenda kuwa viongozi bora katika mitaa yao. ā€œMkutano huu tunafanya kila mwaka, lakini mwaka huu tumeenda mbali zaidi kwa kuwaalika wenyeviti wa serikali za mitaa ili watakapofika hapa waweze kupata ujumbe wa moja kwa moja na kujifunza namna ya uendeshaji na utekelezaji wa shughuli zote zinazohus...