Posts

Showing posts from December 8, 2024

RC Dodoma aongoza zoezi la upandaji Miti Maadhimisho ya Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara

Image
 Mamia ya wakazi wa Jiji la Dodoma wajitokeza kwa wingi kushiriki zoezi la kupanda miti katika maadhimisho ya Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara. Zoerzi hilo limeongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule katika Kata ya Makutupora. ZOezi hilo linatarajia kupanda miti takribani 100,000. Miti hiyo inapandwa jirani na barabara ya mzunguko (ring road). Tukio hilo pamoja na mkuu wa mkoa aliambanata na Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji, wakuu wa Divisheni na Vitengo, maafisa waandamizi kutoka serikalini na taasisi binafsi na wamia ya wananchi. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule akipanda mti

TARURA yatoa Salamu za Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara

Image
 

Msigwa Msemaji Mkuu wa Serikali

Image
 

TNMC yatoa Salamu za 63 ya Uhuru

Image
 

RC Senyamule apokea Bendera ya Taifa kutoka Mkoa wa Kigoma Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA MIAKA 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara yavuka mikoa katika Jiji la Dodoma baada ya Muendesha Baiskeli kutoka Mkoa wa Kigoma, Wenseslaus Lugaya kuendesha baiskeli hadi Mkoa wa Dodoma ikiwa ni ushiriki wake katika Maadhimisho ya Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara leo tarehe 9 Desemba, 2024.  Akiwa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Lugaya alimkabidhi Bendera ya Taifa, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule tukio lililoshuhudiwa na mamia ya wakazi wa Jiji la Dodoma wakiongozwa na mkuu wa mkoa. Viongozi wengine walioshuhudia tukio hilo ni Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Joseph Fungo na maafisa waandamizi wa serikali na sekta binafsi. Matukio ya picha za zoezi husika Muendesha Baiskeli kutoka Mkoa wa Kigoma, Wenseslaus Lugaya (wa pili kulia) akitoa maelezo ya utangulizi kwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule (wa pili kushoto) Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule akitoa tabasamu la miaka 63 ya...

Wahitimu DOMECO watakiwa kufanya tafiti

Na. Mwandishi wetu, DODOMA Mkuu wa W ilaya ya Dodoma , Alhaj Jabir Shekimweri ametoa rai kwa wahitimu wa Chuo cha Kati cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Dodoma (DOMECO) kuwa waandishi mahili kwa kufanya utafiti. Shekimweri a litoa hiyo katika mahafali ya Saba ya Chuo hicho kwa w ahitimu wa ngazi ya Astashahada na Stashahada ya Uandishi wa Habari na Utangazaji akiwataka kuyaishi maadili ya Uandishi wa Habari kwa sababu ni chachu ya mabadiliko katika Taifa. Alisema kuwa wahitimu hao wanawajibu wa kuf u ata watu sahihi wa kuwapa taarifa kamili ambazo hazina udanganyifu na kufanya uwiano wa taarifa za pande zote mbili na aliwahamasisha wanafunzi kutafuta vyanzo mbalimbali vya habari na kujifunza jinsi ya kuchambua taarifa. “Ujuzi na ubunifu wa kuandika kila mtu ananamna yake ya kuandika na kila mtu Mungu kampatika karama . K arama mlizopatiwa mzitumie vizuri , hebu tuone upekee wa mwandishi huyu na mwandishi mwingine, niwatie shime pia muwe na uelewa wa maudhui, muwe wajasil...

Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara, watanzania watakiwa kushiriki kila hatua za maendeleo ya nchi

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Wananchi wameshauriwa kushiriki katika kila hatua ya maendeleo ya nchi ili kuimarisha demokrasia kwasababu wanaposhiriki katika maendeleo wanapata fursa ya kuibua changamoto na fursa zilizopo sambamba na kueleza mawazo yao na kutoa mapendekezo. Hayo, yalisemwa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alipokuwa akizungumza na wadau mbalimbali wa maendeleo katika Mdahalo wa Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara, uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. “Ndugu zangu, sisi kwenye serikali, kwa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, hata kwenye hatua ya kuweka miongozo, tunawajibika sana kuhakikisha wananchi wanashirikishwa katika hatua zote za kujiletea maendeleo. Viongozi mtakubaliana na mimi hata wakati wa kupigania uhuru viongozi hawa mashuhuri tunaowasema hawakuwa pekeyao. Hata leo kuleta maendeleo ya Tanzania hatuwezi kuwa na viongozi pasipo kuwashirikisha wananchi. Wananchi wa...

Sepesha Rushwa, Acha Rushwa ya Ngono

Image
Na. Coletha Charles, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mayeka Simion Mayeka ametoa wito kwa vijana wa Wilaya ya Dodoma kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya rushwa kwa kujihusisha na kampeni mbalimbali za kuleta tija na mabadiliko katika nchi kwa sababu ni nguzo ya taifa na mchango muhimu katika kufanikisha ndoto za maendeleo.   Mayeka alisema hayo wakati akisoma hotuba kwa niaba ya Mgeni Rasmi, Patrobas Katambi, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana,   Ajira na wenye Ulemavu) kwenye kilele cha mbio ndefu na fupi za Taasisi ya Anti-Corruption Voices Foundation yenye kauli mbiu ya Badili tabia Shepesha Rushwa   katika shule ya msingi makole.   Alisema kuwa kupitia mbio hizo wamepeleka ujumbe kwa jamii kama nguzo ya maendeleo na kutoa pongezi kwa Ant-Corruption Voices Foundation kwa juhudi za kuimalisha maadili na uwajibikaji kwa sababu ni mfano bora kwa taasisi zisizo za kiserikali kwa kushirikiana na Serikali kuimalisha maendeleo ya jamii...

Ndani ya ukumbi wa Mdahalo wa Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara

Image
 

Ndani ya Ukumbi wa Jiji la Dodoma kwa ajili ya Mdahalo wa miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara

Image
 

Mdahalo wa Miaka 63 ya uhuru wa Tanzania Bara Jiji la Dodoma

Image
 

Viongozi wetu muda mfupi kabla ya kuanza kwa Mdahalo wa Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara jijini Dodoma

Image
 

Wasimamizi wa Mikopo Halmashauri Wapewa Mafunzo

Na. Coletha Charles, DODOMA Kamati ya huduma ya Mikopo ya Wanawake, Vijana na watu wenye Ulemavu ngazi ya halmashauri wamepewa mafunzo ya kuhakiki, kutathimini, sheria na kanuni za utoaji wa mkopo ili kuwajengea uwezo wa usimamizi wa mikopo hiyo. Mafunzo hayo yalitolewa katika Ofisi ya Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii, Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa lengo la kutoa muongozo wa utoaji na usimamizi wa mikopo kwa wasimamizi hao. Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii, Charity Sichona alisema kulingana na kanuni mpya za mwaka 2024 wameweka ratiba ya kufanya tathimini ya maombi ya kikundi kwa kuweka kumbukumbu. Alisema katika ngazi ya kata wasimamizi wameendelea kutoa mafunzo na kusajili vikundi. Alisema kuwa takribani vikundi 1,000 vimejisajili na hatua ya kuomba mkopo inaendelea kwa kuangalia tathimini ya miradi ya wanakikundi. “Mafunzo kama haya tulishatoa katika ngazi mbalimbali hasa kata ambapo wanajukumu kubwa la kuchakata maombi hayo na kuwapatia mafunzo wanakikundi h...

Jamii imeaswa isifumbie macho Ukatili wa Kijinsia

Image
Na. Faraja Mbise, DODOMA Jamii imeaswa kutoyafumbia macho masuala ya ukatili wa kijinsia na kutakiwa kuripoti kwenye vyombo vya sheria matukio ya ubakaji, ulawiti na ndoa za utotoni. Mamia ya wanafunzi waliojitokeza Hayo, yalisemwa na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ng’hongh’onha, Patrick Mwachambi ambaye ni muwakilishi wa mgeni rasmi, alipokuwa akizungumza na wananchi waliojitokeza katika Uzinduzi wa Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia ngazi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika Kata ya Ng’hong’onha. “Natoa wito kwa wananchi wenzangu, kuwatumia ipasavyo wataalam wetu kwasababu wako tayari wakati wote kuhakikisha kuwa vitendo vya ukatili vinakomeshwa na wahusika wanachukuliwa hatua za kisheria. Namshukuru sana Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, tumejifunza mengi kupitia wataalam. Kwahiyo, nawaomba wananchi tuzingatie elimu tuliyopewa na kuahidi kuifanyia kazi, yote yaliyoelekezwa tutayatekeleza bila kuathiri taratibu za kisheria” alisisitiza Mwachambi. Akizungumzia kampeni ya m...