Posts

Showing posts from November 6, 2024

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uwazi mtupu Jiji la Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA UCHAGUZI wa Serikali za Mitaa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma unafanyika kwa uwazi kwa mujibu wa kanuni zilizopo ili wananchi wafurahie kukua kwa demokrasia. Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko Kauli hiyo ilitolewa na Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu mwenendo na shughuli mbalimbali za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa zinazoendelea ofisini kwake leo. Dkt. Sagamiko alisema kuwa hakuna mpango wowote wenye nia ovu ya kuminya demokrasia kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi wa viongozi wa mamlaka za serikali za mitaa. Alisema kuwa tangu mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaanza ulikuwa wa wazi na shirikishi ukiruhusu vyama vyote kushiriki kikamilifu. Akiongelea zoezi la uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kugombea nafasi za uongozi alisema kuwa vyama vyote 19...