Posts

Showing posts from August 22, 2023

BEST WESTERN DODOMA CITY HOTEL SULUHU MALAZI MAKAO MAKUU

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Ujenzi wa Hoteli ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma umeitikia changamoto ya huduma ya malazi kwa mabalozi na wageni wengine wanaotembelea makao makuu ya nchi kwa huduma mbalimbali. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule alipokuwa akitoa salamu za Mkoa wa Dodoma kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) ilipotembea miradi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Senyamule alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma inakabiliwa na changamoto ya sehemu za malazi kwa mabalozi na wageni mashuhuri. “Kuwepo kwa vitega uchumi hivi Jengo la Kitega Uchumi Mtumba na Hoteli ya Best Western Dodoma City ni faida kubwa wa maendeleo ya Dodoma. Mheshimiwa Mwenyekiti mabalozi wengi walikuwa wanakuja Dodoma na kurudi Dar es Salaam, Balozi anakuja na ndege ya asubuhi anaenda wizarani akimaliza shughuli zilizompeleka anaondoka. Sasa hivi mabalozi wengi wanafikia Best Western Dodoma City Ho...

WATANZANIA TUJENGE UTAMADUNI WA KUPIMA AFYA ZETU - WAZIRI UMMY MWALIMU

Image
Na Englibert Kayombo – WAF Tanga Wito umetolewa kwa watanzania kujenga utamaduni wa kupima afya zao mara kwa mara ili kutambua hali zao kiafya mapema na kuepukana na maradhi ambayo yanaweza kugharimu fedha nyingi za matibabu na hata kusababisha ulemavu hadi vifo. Waziri Ummy Mwalimu Wito huo umetolewa leo na Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini Mheshimiwa Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Afya nchini Tanzania alipokuwa akifungua kambi ya upimaji afya ya Afya Cheki iliyoandaliwa na Uongozi wa Afya Cheki kwa kushirikiana na Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Tanga na Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga. “Watanzania wengi tunakwenda Hospitali tayari ugonjwa umeshakuwa mkubwa sana, wagonjwa wa Saratani wanakwenda Hospitali, Saratani ikiwa hatua ya nne, hatuna mazoea ya kupima afya mapema kujua hali zetu” ameeleza Mhe. Ummy mwalimu kwa kutolea mfano wa hali ya ugonjwa wa Saratani. Amesema kuwa maradhi yakigundulika mapema huwa ni rahisi kuyatibu lakini pia kupunguza madhara, hivyo kupitia...

TTB NI NGUZO YA KUTANGAZA UTALII

Image
  Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema Bodi ya Utalii (TTB) ndiyo nguzo muhimu katika kutangaza na kuvutia watalii kutembelea Nchi yetu sanjari na kuongeza mapato yatokanayo na Sekta ya Utalii.  Mhe. Mchengerwa ameyasema hayo leo wakati wa uzinduzi wa Bodi za Wakurugenzi za TTB na Hifadhi ya Taifa (TANAPA) uliofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa AICC jijini Arusha na kuitaka TTB kuanza mikakati ya kubaini fursa za uwekezaji kwenye utalii. Amesema kuwa Serikali ipo katika kufanya mapitio ya sheria ambayo itawapa mamlaka TTB kuhakikisha kwamba wanaishauri vyema kwenye eneo la uwekezaji kwenye sekta ya utalii.  “TTB mtakuwa na kazi kubwa ya kufanya kuhakikisha kuna nyongeza ya ujenzi wa hoteli mbalimbali, nyongeza ya vyumba na kufikiria kuwekeza kwenye maeneo mbalimbali ya ufukwe au kwenye visiwa” amesema Mhe Mchengerwa Amesema kuwa kwenye suala la uwekezaji wanatambua hadi leo hii idadi ya vyumba vilivyopo nchini kwa ajili ya...

DKT.MPANGO AWATAKA WAKUU WA MIKOA NA MAKATIBU TAWALA WA MKOA KUZINGATIA MAADILI NA NIDHAMU

Image
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango  amewataka Wakuu wa Mikoa pamoja na Makatibu Tawala wa Mikoa  kuzingatia maadili na nidhamu katika maeneo ya kazi  ili kuwa  picha nzuri na ya mfano kwa wengine . Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia wakati akifungua Mafunzo ya Uongozi kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa yanayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere – Kibaha Mkoani Pwani Makamu wa Rais amesema hayo leo Tarehe 22 Agosti 2023 wakati akifungua Mafunzo ya Uongozi kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa yanayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere iliopo Kibaha Mkoani Pwani.  Amesema ni lazima wakati wote  wa uongozi kutafuta  njia bora ya kuwashirikisha wengine ili msingi wa uongozi na utendaji  uwe chachu  zaidi kuleta maendeleo kwa wananchi . Pia Makamu wa Rais amewataka viongozi wa Mikoa kuongeza ...

RAIS, DKT. SAMIA AKUTANA NA RAIS WA INDONESIA, MHE. JOKO WIDODO IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Indonesia Mhe. Joko Widodo Ikulu Jijini Dar es salaam wakati wa Ziara yake ya Kikazi hapa nchini Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama na Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Indonesia Mhe. Joko Widodo wakati Wimbo wa Taifa wa Tanzania na Indonesia ukipigwa katika Viwanja vya Ikulu Jijini Dar es salaam kwenye mapokezi rasmi kwenye Ziara ya Kikazi ya Rais huyo hapa nchini Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana  na Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Indonesia Mhe. Joko Widodo wakati alipowasili katika Viwanja vya Ikulu Jijini Dar es salaam kwa ajili ya kuanza Ziara ya Kikazi hapa nchini CHANZO: Michuzi Blog