Posts

Showing posts from March 30, 2024

Jiji la Dodoma lapata hati safi miaka mitatu mfululizo

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma inajivunia kupata hati safi kwa miaka mitatu mfululizo kutokana na ushirikiano uliopo baina ya wataalam na Baraza la Madiwani katika kusimamia na kudhibiti matumizi sahihi ya fedha. Mkuu wa Kitengo cha Uhasibu na Fedha Halmashauri ya Jiji la Dodoma, CPA. David Rubibira alipokuwa akiongelea mafanikio ya serikali ya awamu ya sita Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Kitengo cha Uhasibu na Fedha Halmashauri ya Jiji la Dodoma, CPA. David Rubibira alipokuwa akiongelea mafanikio ya serikali ya awamu ya sita kwa miaka mitatu ofisini kwake. CPA. Rubibira alisema “kwa bahati nzuri kwa kipindi cha uongozi wa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Halmashauri ya Jiji la Dodoma imekuwa ikipata hati safi kwa miaka mitatu mfululizo. Hati inaangalia maeneo yafuatayo. Ukaguzi wa hesabu zilizowasilishwa na ukaguzi wa vitabu vilivyofanya malipo, nyaraka, viambata vyote na mchakato wa ukusanyaji mapato kama ulizingatia sheria, kanuni na taratibu. Hivyo, h...

TEHAMA chachu ya ukusanyaji mapato Jiji la Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Matumzi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma yamerahisisha shughuli za kutoa huduma kwa wananchi na kuongeza ukusanyaji wa mapato yakiziba mianya ya upotevu wa mapato. Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo akifafanua jambo Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo alipokuwa akiongelea mafanikio ya serikali ya awamu ya sita katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Fungo alisema “matumizi ya TEHAMA yamerahisisha sana shughuli za serikali za kutoa huduma kwa wakati na kwa urahisi kwa wananchi. Serikali ya awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan imeiwezesha Halmashauri ya Jiji la Dodoma upatikanaji wa fedha kwenye ujenzi na uboreshaji wa mifumo ya TEHAMA ikiwemo mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalam ili wawe na uelewa wa kutosha ...

Serikali yaboresha mazingira ya uwekezaji Jiji la DOdoma

Image
  Na. Dennis Gondwe, DODOMA Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan imetengeneza mazingira mazuri ya uwekezaji na kuwavutia wenye viwanda kuwekeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kukuza uchumi. Kaimu Mkuu wa Divisheni ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Abeid Msangi Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkuu wa Divisheni ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Abeid Msangi alipokuwa akiongelea mafanikio ya serikali ya awamu ya sita kwa kipindi cha miaka mitatu ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Msangi alisema kuwa kwa mazingira mazuri ya uwekezaji yanayofanywa na serikali ya awamu ya sita, Halmashauri ya Jiji la Dodoma itaendelea kunufaika na uchumi wake kuanza kutegemea viwanda. “Katika kwenda sambamba na ongezeko la uwekezaji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, tumejitika kufuata maelekezo ya Mpango Kabamba wa Jiji la Dodoma. Mpango huo umepanga m...