Posts

Showing posts from January 28, 2025

Alhaj Shekimweri ahamasisha umuhimu wa mazoezi kwa wachezaji Dodoma Jiji FC

Image
Na. Coletha Charles, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri, ameitembelea Timu ya Dodoma Jiji FC, inayondelea na mazoezi ya maandalizi ya msimu wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa lengo la kuwahamasisha wachezaji na viongozi wa timu kwa ajili ya kujiandaa vema. Akizungumza na wachezaji na viongozi wa timu kwenye uwanja John Merlin, Mkuu wa Wilaya alisisitiza umuhimu wa maandalizi mazuri kwa ajili ya msimu wa pili wa ligi kuu na kuwataka wachezaji kufanya mazoezi ili kuhakikisha wanapata mafanikio. Alisema kuwa, wanatakiwa kuweka mikakati yenye uhalisia kwa sababu wanaenda kwenye kipindi kibaya ambapo kusipokuwa na utulivu na maelewano wataishia kulaumiana na kushutumiana. “ Tunaenda ‘second round’ ya ligi yetu hatuko sehemu nzuri sana, hatuko sehemu mbaya sana katika mechi 16 nafikiri tuna ‘point’ 19 wastani wa ‘point’ moja kwa kila mechi. Kwahiyo, kuna haja ya kuwa familia moja kama alivyoongea mwalimu kwa kuelewa nini kipo mbele yetu. Tuna mechi 14 tu za kuju...

Dodoma Jiji FC kujichimbia Arusha kujiwinda na duru ya pili ya NBC PL

Image
Na. Mussa Richard, DODOMA Klabu ya Soka ya Dodoma Jiji FC, imepanga kwenda kukita kambi jijini Arusha ili kujiandaa na mbilinge mbilinge za duru ya pili ya Ligu kuu ya NBC Tanzania bara, ambapo imepanga kucheza michezo miwili ya kirafiki kujiandaa na michezo ya Ligi kuu, Dodoma Jiji itaanza kuzisaka alama tatu mbele ya Pamba Jiji katika uwanja wa Jamhuri Dodoma Februari 05, 2025. Akizungumzia kambi hiyo Mtendaji Mkuu wa Dodoma Jiji FC, Johnson Fourtnatus alisema “ Tumekubaliana kwenda kuweka kambi mkoani Arusha kwa muda wa siku sita, na tutacheza michezo miwili ya kirafiki na timu zinazoshiriki Ligi daraja la kwanza Tanzania bara, tukianzia kesho ambapo tutacheza na Mbuni FC, na tarehe 31 tutacheza mchezo wa mwisho wa kirafiki kukamilisha kambi yetu na tarehe 2 Februari, 2025 timu itarudi Dodoma kuendelea na kambi kuelekea mchezo dhidi ya Pamba Jiji FC ". Katika hatua nyingine Fourtnatus akaweka wazi mpango mkakati wa klabu ya Dodoma Jiji FC, katika duru ya pili ya Ligi kuu ...