Posts

Showing posts from July 17, 2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia viongozi pamoja na wageni mbalimbali kabla ya kuzindua Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia viongozi pamoja na wageni mbalimbali kabla ya kuzindua Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akionesha nakala za vitabu vya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 mara baada ya uzinduzi

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akionesha nakala za vitabu vya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 mara baada ya uzinduzi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete (JKCC

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete (JKCC

Mkoa wa Dodoma kuja na Mpango Mkakati wa kukuza na kutangaza Utalii wa Ndani

Image
Na. Hellen Minja, DODOMA RS Utalii unatajwa kuwa na athari chanya za kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja na Mkoa kwa ujumla pale unapotumika kimkakati. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amebainisha hayo alipokua akifungua kikao Maalumu cha Maandalizi ya uzinduzi wa Kitabu cha Mpango Mkakati wa Kukuza na Kutangaza Utalii wa Mkoa huu. Kikao hicho kimewahusisha wadau wa utalii kutoka sekta mbalimbali waliokutana kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma jijini hapa lengo likiwa ni kupitia Mpango Mkakati ulioandaliwa sambamba na kuunda Kamati itakayoshughulikia kwa karibu ufanikishaji wa shughuli hiyo. “Utalii una athari nyingi za kiuchumi kama ukiwa nao maana utakuza uchumi wa mtu mmoja mmoja lakini pia wa Mkoa. Dodoma tunatamani tuwe ‘hub’ ya utalii kwa sababu tunafikika kila upande wa nchi ya Tanzania hata kama vivutio vya utalii havipo Dodoma tunataka iwe active kwenye suala la utalii” Senyamule. Akizungumza katika kikao hicho, Katibu Tawala Msaidizi Sekta za Viwanda, Bi...

Watanzania waaswa kutunza tunu ya Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu

Image
Na. Sofia Remmi, Dodoma RS Watanzania wametakiwa kuendelea kuitunza Tunu ya amani wakati nchi ikielekea kwenye zoezi la Kitaifa la uchaguzi mkuu huku wanasiasa wakitakiwa kufanya kampeni za kistaarabu ambazo hazichochei hasira na vurugu zisizo na tija. Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano Taifa, Askofu Dkt. Venance Chande, aliyasema hayo wakati wa mkutano wa kutoa taarifa ya kongamano lililoandaliwa na Idara ya Elimu ya Mahakama ya Kadhi na Baraza la Waislam Tanzania (BAKWATA) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma. Askofu huyo alisema kuwa amani ndio msingi wa maendeleo ya Taifa lolote Duniani. “Sisi watanzania hatujazoea kugombana, tumezoea kuishi pamoja kwa umoja na upendo, hatujazoea kubaguana kwa misingi ya makabila au dini zetu, hayo ndiyo maisha tuliyoyazoea kuishi” alisema Dkt. Chande. Aidha, amewataka Wanasiasa kufanya siasa za kistaarabu. “Wanasiasa, huu ni mwaka wa uchaguzi, kampeni zifanyike kistaarabu zisiwe za kuchochea hasira, washawishi kwa Ser...

Kituo cha Dharura cha Serikali chawa kivutio Afrika kwa kukinga Maafa

Image
Na Mwandishi Wetu – Dodoma Uwekezaji wa Serikali ya Tanzania katika kuimarisha mifumo ya kukabiliana na majanga kupitia Kituo cha Ufuatiliaji wa Majanga na Tahadhari ya Mapema (Situation Room) umeanza kuzaa matunda, baada ya nchi mbalimbali za Afrika kuonesha kuvutiwa na namna kituo hicho kinavyofanya kazi. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu kwa wataalamu kutoka Ghana, Togo na Burkina Faso yanayofanyika katika Mji wa Serikali Mtumba, Jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Menejimenti ya Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Brigedia Jenerali Hosea Ndagala, alisema kituo hicho kimeongeza uwezo wa nchi kuchakata taarifa za viashiria vya majanga na kutoa taarifa za viashiria vya majanga na kutoa tahadhari mapema kwa wananchi. “Uendeshaji wa kituo hiki unahusisha wataalamu kutoka taasisi mbalimbali za Serikali wanaoshirikiana kuchakata taarifa kwa pamoja, jambo linalosaidia kutoa tahadhari kwa wakati,” alisema Brigedia Jenerali Ndagala. Mkurugenzi Msaidizi wa kituo hicho, Bi....