Posts

Showing posts from July 12, 2025

Waganga Wakuu wamemtunukia Rais Tuzo, Dkt. Mpango awapongeza, atoa maelekezo mahususi

Image
Na. John Mapepele Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametunukiwa tuzo maalum ya kutambua mchango wake kwenye Sekta ya Afya na Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri hii leo. Tuzo hiyo aliitoa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa kwa niaba ya Waganga hao na kumkabidhi Makamo wa Rais, Mhe. Dkt. Philipo Mpango aliyekuwa mgeni rasmi katika Mkutano huo wa Mwaka wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri jijini Dodoma. Mbali na tuzo hiyo pia Waganga Wakuu wamemtunukia Makamo wa Rais tuzo hiyo pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa na Waziri wa Afya, Jenista Mhagama. Dkt. Mpango amewapongeza Waganga Wakuu nchini kwa kazi wanayofanya ya kuwahudumia wananchi huku akiwataka waendelee kuimarisha huduma na sekta ya afya kwa ujumla na kuzingatia maadili ya taaluma yao. Alisisitiza kuwa Serikali itatekeleza mara moja maombi ya kuboresha stahili za wataalam hao kulingana hali halisi ya uchumi. “Nawaelekeza Mawaziri ...

Kongamano la Rushwa latoa matumaini ya kuendelea kutokomeza Rushwa nchini

Image
Na. Nnacy Kivuyo, DODOMA   Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amesema Tanzania inaendelea kufanya vizuri katika mapambano dhidi ya rushwa kila mwaka kutokana na utawala bora uliopo nchini.   Aliyasema hayo wakati akifungua Kongamano la Maadhimisho ya siku ya Mapambano dhidi ya Rushwa Barani Afrika yaliyofanyika jijini Dodoma. Alisema kuwa kuanzishwa kwa Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi ndani ya Mahakama Kuu pamoja na Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2023 ni hatua nyingine muhimu katika kuhakikisha vitendo vya rushwa vinadhibitiwa ipasavyo nchini.  “Ndugu washiriki, Tanzania imepiga hatua kubwa katika jitihada za kutokomeza rushwa, ikiwa ni pamoja na kutunga na kufanya maboresho ya sheria mbalimbali zinazolenga kupambana na vitendo hivyo. Tuendelee kuzitumia sheria hizi sambamba na kutoa elimu ili kuhakikisha wananchi wanafahamu nafasi na wajibu wa kila mmoja katika kuitoko...

Baraza la Biashara kuvutia sekta binafsi kuwekeza Dodoma

Image
Na. Nancy Kivuyo, MTUMBA Mwenyekiti wa Baraza la Biashara la Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri ameeleza kuwa Jiji la Dodoma linakua kwa kasi kutokana na uwezeshaji mkubwa unaofanywa na serikali katika miundombinu mbalimbali. Aliyasema hayo katika kikao cha Baraza la Biashara la Wilaya ya Dodoma kilichofanyika katika ukumbi mkubwa wa mikutano wa halmashauri katika Mji wa Mtumba. Alisema kuwa anapongeza mwitikio wa sekta binafsi katika uwekezaji Dodoma. “Ninyi watu wa sekta binafsi nawapongeza sana kwa kufanya uwekezaji wenye tija ikiwemo hoteli kubwa za kisasa zipo hapa Dodoma, kumbi za mikutano na maduka makubwa” alisema Shekimweri ambae pia ni Mkuu wa Wilaya ya Dodoma. Aliongeza kuwa analipongeza Baraza la Biashara la Wilaya kwa kuweka sera za kuvutia wawekezaji. “Nalipongeza baraza hili kwa kuweka sera Madhubuti zinazofanya wawekezaji kuzikimbilia fursa zilizopo ndani ya Jiji letu la Dodoma. Tuendelee kufanya vizuri kwasababu hapa ndipo kitovu cha makao makuu ya nchi k...