Posts

Showing posts from June 16, 2025

Jiji la Dodoma lafikisha 93% ya ukusanyaji Mapato

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule ameipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kufikia asilimia 93 ya makusanyo ya mapato ya ndani hadi kufikia tarehe 31 Mei, 2025 na kusema kuwa ukusanyaji huo unatoa matumaini ya kufikia lengo ifikapo mwisho wa mwaka wa fedha. Pongezi hizo alizitoa katika mkutano maalum wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa ajili ya kupitia na kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. Senyamule alisema kuwa kwa mujibu wa taarifa ya uchambuzi wa mapato ya mamlaka za serikali za mitaa kwa Mkoa wa Dodoma uliofanywa na wataalam wa ofisi yake hadi kufikia tarehe 31 Mei, 2025 Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilikuwa imekusanya asilimia 93. “Hivyo, niendelee kusisitiza menejimenti ya halmashauri kuongeza nguvu ya ukusanyaji wa mapato ili kuhakikisha kuwa asilimia saba iliyobaki inakusanywa kabla ya tarehe 30 Juni, 2025. Wataalamu wangu ...

RC Senyamule aipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kupata Hati safi

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MKOA wa Dodoma umeipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kupata hati safi ya ukaguzi wa hesabu za serikali kwa hesabu zinazoishia tarehe 30 Juni, 2025. Pongezi hizo zilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule katika mkutano maalum wa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kupitia na kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. “Mheshimiwa Naibu Meya, naomba nitumie nafasi hii kuipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kupata hati safi ya ukaguzi wa hesabu za serikali kwa hesabu zinazoishia tarehe 30 Juni, 2025. Hati safi hii ya ukaguzi inaifanya halmashauri kuendelea kupata hati safi tangu mwaka 2017/2018 hadi sasa. Kitendo hiki kinaipa heshima kubwa halmashauri na mkoa kwa kazi kubwa mnayoendelea kuifanya. Mafanikio haya makubwa yanatokana na ushirikiano wenu mkubwa waheshimiwa madiwani, watendaji wa jiji na viongozi mbalimbali. Hivyo, nawasihi kuendelea kudumish...