Posts

Showing posts from September 26, 2024

Maekelezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 yatolewa Jiji la Dodoma

Image
Na. Asteris Frank, DODOMA Msimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko ametoa maelekezo ya uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 kwa umma. Msimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko akitoa Maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 kwa umma Akizungumza mbele ya vyombo vya habari ofisini kwake leo tarehe 26 Septemba, 2024 kuhusu maekelezo ya uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2024 alisema kuwa Msimamizi wa Uchaguzi amepewa mamlaka ya kutoa maelekezo kuhusu uchaguzi. “Maelekezo haya yanatolewa siku 62 kabla ya siku ya uchaguzi, kwa lengo la kuhakikisha kuwa taratibu zote zinafuatwa na kwamba wapiga kura Pamoja na wagombea wanapata taarifa zote zinazohitajika kwa wakati. Maelekezo haya yanafafanua hatua zitakazo ongoza mchakato wa uchaguzi, kuanzia uandikishaji wa wapiga kura, uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kugombea, uteuzi wa wagombea na tarehe ya siku ya uchaguzi. Maelekezo haya yanalenga kuto...

Msimamizi wa Uchaguzi Jiji la Dodoma atoa maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WANANCHI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameshauriwa kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi wa serikali za mitaa tarehe 27 Novemba, 2024 ili kuchagua viongozi bora. Msimamizi wa Uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko akitoa Maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 akiwa amezungukwa na timu ya waratibu wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Ushauri huo ulitolewa na Msimamizi wa Uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akitoa Maelekezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 kwa waandishi wa habari ofisini kwake leo tarehe 26 Septemba, 2024. Dkt. Sagamiko alisema “niwahamasishe wananchi wa halmashauri ya jiji la Dodoma kujitoleza kwa wingi siku ya uchaguzi ambayo ni jumatano ya tarehe 27 Novemba, 2024 ili kuchagua viongozi bora watakaoongoza”. Msimamizi huyo wa uchaguzi alisema kuwa wananchi wenye sifa za kushiriki wanatakiwa kushiriki. “Ninatoa wito kwa wananchi wote wenye sifa kushiriki ki...