Posts

Showing posts from January 27, 2024

MABARAZA YA ARDHI YANAMCHANGO KATIKA KUSULUHISHA MIGOGORO YA ARDHI

Na. Eleuteri Mangi, WANMM   Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia Mabaraza ya Ardhi na Nyumba imeshiriki uzinduzi wa Wiki ya Sheria jijini Dodoma yakiongozwa na Mhe. Dkt. Tulia Ackson Spika wa Bunge la Tanzania.   Uzinduzi huo umefanyika Januari 27, 2024 katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma ukitanguliwa na matembezi ya uzinduzi wa Wiki ya Sheria ambao umehusisha viongozi mbalimbali wa mahama, watumishi wa umma na wananchi kutoka jiji la Dodoma.   Akizungumzia ushiriki wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba, Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi Dodoma Bw. Jackson Kanyerinyeri amesema kuwa moja ya jukumu lao ni kutoa elimu kwa wananchi wanaotembelea banda hilo katika masuala ya ardhi, migogoro ya ardhi namna inavyotatuliwa katika mabaraza hayo hadi kutolewa hukumu.   Bw. Kanyerinyeri ameongeza kuwa wamepata wasaa mujarabu wa kuwaeleza wananchi juu ya mabadiliko ya Sheria Na 3 ya 2021 ambayo imeondoa mamlaka ya mabaraza ya Kata kusikiliza ...

MABARAZA YA ARDHI YANAMCHANGO KATIKA KUSULUHISHA MIGOGORO YA ARDHI

  Na. Eleuteri Mangi, WANMM   Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia Mabaraza ya Ardhi na Nyumba imeshiriki uzinduzi wa Wiki ya Sheria jijini Dodoma yakiongozwa na Mhe. Dkt. Tulia Ackson Spika wa Bunge la Tanzania.   Uzinduzi huo umefanyika Januari 27, 2024 katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma ukitanguliwa na matembezi ya uzinduzi wa Wiki ya Sheria ambao umehusisha viongozi mbalimbali wa mahama, watumishi wa umma na wananchi kutoka jiji la Dodoma.   Akizungumzia ushiriki wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba, Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi Dodoma Bw. Jackson Kanyerinyeri amesema kuwa moja ya jukumu lao ni kutoa elimu kwa wananchi wanaotembelea banda hilo katika masuala ya ardhi, migogoro ya ardhi namna inavyotatuliwa katika mabaraza hayo hadi kutolewa hukumu.   Bw. Kanyerinyeri ameongeza kuwa wamepata wasaa mujarabu wa kuwaeleza wananchi juu ya mabadiliko ya Sheria Na 3 ya 2021 ambayo imeondoa mamlaka ya mabaraza ya Kata kusiki...

Mkoa wa Dodoma wamtakia heri ya kuzaliwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan

Image
Na. Dennis Gondwe, KIKOMBO MKOA wa Dodoma umempongeza na kumtakia heri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa siku yake ya kuzaliwa na kumtakia maisha marefu ili aendelee kuwaongoza watanzania. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule  Pongezi hizo zilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule katika halfa ya kumbukizi ya kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyofanyika katika makao ya taifa ya kulelea watoto- Kikombo, Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Senyamule alisema “sisi Mkoa wa Dodoma tunatoa pongeza kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuongeza umri akiwa na nguvu na afya njema na maono ya kuliongoza taifa. Chini ya uongozi wake tunafuraha na amani”. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma alimtaja Rais kuwa ni mtu mwenye hekima sana na mchapa kazi. “Mheshimiwa Rais ametujengea uhusiano mzuri ndani na nje ya nchi. Hakika uongozi wake umeifanya Tanzania kuwa nchi pendwa duniani. Ameonesha ku...