Posts

Showing posts from August 28, 2024

Mikakati ya Usalama Barabarani inalenga kudhibiti ajali

Image
Na. Flora Nadoo, DODOMA Mweyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Daniel Sillo ameitaja mikakati ya usalama barabarani kuwa inalenga kudhibiti madereva walevi, wazembe na wanaoendesha kasi Pamoja na mambo mengine. Alizungumza hayo tarehe 26 Agosti, 2024 katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa Wiki ya nenda kwa Usalama Barabarani na Miaka 50 ya Baraza la Taifa la Usalama Barabarani. Sillo aliwataka madereva na wananchi wawe waangalifu na vyombo vya moto pamoja na sheria za barabarani ili kuepuka ajali za barabarani zisizo za lazima. “Mkakati wa Usalama Barabarani unalenga maeneo yafuatayo uthibiti wa madereva walevi na wanaoendesha kwa uzembe, uthibiti wa mwendokasi kwa madereva, kuwashirikisha wamiliki wa vyombo vya moto katika dhana ya uwajibikaji. Hii ni pamoja na kuhakikisha kunakuwa na madereva wenza kwa mabasi ya masafa marefu. Vilevile, kuthibiti uendeshaji wa magari bila sifa au kutokuwa na leseni...

Pikipiki zaendelea kuchangia vifo ajali za barabarani

Image
Na. Anna Stanley, DODOMA SERIKALI imeeleza kuwa vyanzo vya ajali zinazosababishwa na pikipiki zimeendelea kuchangia vifo ya watu wengi wakati mwaka 2023 zikisababisha vifo wa watu 376 na kupoteza nguvu kazi ya taifa wakati wengine wakiachwa na ulemavu wa kudumu. Kauli hiyo ilitolewa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani Kitaifa na miaka 50 ya Baraza la Usalama Barabarani yaliofanyika katika Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma. Dkt. Mpango alisema "ndugu wananchi na waheshimiwa viongozi, Pikipiki ni miongoni mwa vyombo vya moto vinavyotoa huduma ya usafiri na usafirishaji wa mizigo na abiria mijini na vijijini, ajali zinazohusu pikipiki zimekuwa nyingi mno zinaongezeka mwaka hadi mwaka kwa mfano katika kipindi cha mwezi Januari mpaka Desemba mwaka jana 2023, kulikuwa kuna jumla ya matukio 435 ya ajali za pikipiki yalioripotiwa katika kipindi hicho, idadi ya vifo vilivyotokana na ajali...

Timu ya Veterani kutoka Zanzibar yaibuka mshindi katika Bonanza Dodoma

Image
Na. Valeria Adam, DODOMA Timu ya mpira wa miguu ya Veterani kutoka Chuo cha Mafunzo Zanzibar imefanikiwa kuibuka mshindi katika Bonanza la mpira wa miguu lililofanyika katika uwanja wa Magereza jijini Dodoma na kupewa kombe. Mkuu wa Gereza kuu la Isanga, Zephania Neligwa (kulia) akimkabidhi kombe kepteni wa timu ya mpira wa miguu ya Veterani kutoka Chuo cha Mafunzo Zanzibar Bonanza hilo lilifanyika tarehe 24 Agosti, 2024 kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na uhusiano kati ya Tanzania Bara na Tanzania Visiwani na kuleta burudani kwa mashabiki. Katika mchezo wa fainali, timu ya Veterani kutoka Chuo cha Mafunzo Zanzibar ilionesha kiwango cha juu, hasa katika eneo la ulinzi ambapo waliweza kuzuia mashambulizi mengi ya wapinzani wao. Mchezaji wa timu ya Veterani kutoka Chuo cha Mafunzo Zanzibar, Haji Ramadhani alisema kuwa ushindi wao ulitokana na juhudi za pamoja na umakini wa kila mchezaji, huku wakionesha nidhamu ya hali ya juu ndani na nje ya uwanja. “Bonanza limekuwa zuri, kuanz...