Jiji la Dodoma latangaza fursa za Uwekezaji katika Maonesho ya Sabasaba, 2026
Na. Mwandishi wetu, DAR ES SALAAM Halmashauri ya Jiji la Dodoma imejipanga kujitangaza kama kitovu cha uwekezaji, biashara na maendeleo ya kisasa kutokana na kuwa na fursa nyingi kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi jambo linalokuza ustawi wa wananchi na taifa kwa ujumla. Afisa Habari, Nancy Kivuyo kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma (kulia) akielezea fursa za uwekezaji kwa mdau aliyetembelea banda ya halmashauri Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Habari katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Nancy Kivuyo alipokuwa akiwaelezea wananchi waliotembelea banda lao jinsi Halmashauri ya Jiji la Dodoma inavyoshiriki katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) mwaka 2026 yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini hapa. Kivuyo alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika kuhakikisha inavutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi, imeendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji. “Mazingira ya uwekezaji yameboreshwa sambamba na mazingira ya kufanya...