Posts

MIL. 544,335,626 ZAJENGA SHULE YA SEKONDARI MICHESE

Na. Dennis Gondwe, MKONZE SHILINGI 544,335,626 zimekamilisha ujenzi wa Shule ya Sekondari Michese na kuwawezesha wanafunzi 555 kupata elimu ya sekondari karibu na maeneo wanayoishi na kuwaondolea kero ya kutembea umbari mrefu kufuata elimu. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo alipokuwa akisoma taarifa ya ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari Michese kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya TAMISEMI iliyotembelea na kukagua ujenzi wa shule hiyo. Fungo alisema “k iasi cha fedha kilichotolewa kwa ajili ya ujenzi ni shilingi 544,225,626 chanzo cha fedha kikiwa ni SEQUIP. Fedha zilipokelewa Mwezi Oktoba, 2023 na ujenzi ulianza rasmi Mwezi Novemba, 2023 na kukamilika Mwezi Mei, mwaka 2024. Utaratibu wa ujenzi uliotumika ni force akaunti na mradi ulikamilíka kwa wakati na shule ilianza rasmi mwaka 2024 na kusajiliwa kwa jina la Michese Sekondari, Namba ya usajili S.6625”. Alisema kuwa u jenzi wa shule hiyo ulifanyika kwa awamu tatu, awamu ya kw...

JIJI LATEKELEZA MKAKATI WA KUBORESHA MAENEO YA WAZI

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma inatekeleza mkakati wa uboreshaji maeneo ya wazi kwa kusimamia udhibiti na usimamizi wa sheria na kufanya uondoaji wa maendelezo ya kudumu yaliyokiuka masharti na kuboresha miundombinu ya maeneo ya michezo. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo alipokuwa akisoma taarifa ya uboreshaji wa maeneo ya wazi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) iliyofanya ziara katika jiji hilo. Fungo alisema kuwa halmashauri ilifanya zoezi la mapitio ya hali ya maeneo ya wazi ili kubaini kama yanatumika kwa mujibu wa sheria. “Halmashauri inatekeleza mkakati wa u dhibiti na usimamizi wa sheria katika maeneo ya wazi, zoezi la uondoaji wa maendelezo ya kudumu yaliyokiuka masharti ya uendelezaji limefanyika katika eneo la wazi lililopo Majengo maarufu kama kwa Kato, eneo la Rose Garden na maeneo mengine 47 ambayo tayari wame...

JIJI LA DODOMA LATUMIA MIL. 23 KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imetumia zaidi ya shilingi milioni 23 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo fedha kutoka serikali kuu, mapato ya ndani na wahisani pamoja na bakaa. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo alipokuwa akiwasilisha taarifa fupi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI). Alisema kuwa katika kipindi cha kuanzia Julai, 2025 hadi kufikia Machi, 2026 halmashauri imetumia jumla ya shilingi 23,815,713,415.02 sawa na asilimia 91.19 ya fedha zilizopokelewa kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo. “Kati ya fedha hizo, shilingi 6,406,582,002.56 ni fedha kutoka serikali kuu, shilingi 16,807,859,627.46 mapato ya ndani, shilingi 601,771,785.00 fedha za wahisani na shilingi 5,279,467,344.52 ni fedha za bakaa. Kwa kipindi cha kuanzia Julai, 2025 hadi kufikia Machi, 2026, hal...

JIJI LA DODOMA LATOA VIWANJA 1,900 KWA WAFANYAKAZI

Image
  Na. Mwandishi wetu, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeibuka kivingine katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani kwa kuachia viwanja zaidi ya 1,900 vya matumizi mbalimbali kwa ajili ya wafanyakazi na wananchi kwa ujumla ili waweze kufurahia fursa ya kumiliki kiwanja katika makao makuu ya nchi. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa Baraza la Wafanyakazi la Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dennis Gondwe alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu nafasi ya Halmashgauri ya Jiji la Dodoma katika kujali makazi ya wafanyakazi katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika ngazi ya mkoa katika Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma. “Nitumie nafasi hii kuwashauri na kuwashawishi wafanyakazi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma na wengine wote kuhakikisha wananunua viwanja katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Hii itaweka alama kwa utumishi wao katika halmshauri, lakini kwa wale walio nje ya halmshauri itaweka alama kwa kumiliki kiwanja kihalali katika makao makuu...

MADIWANI JIJI LA DODOMA WATAKIWA KUTATUA KERO ZA WANANCHI

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma watakiwa kusikiliza kero za wananchi na kuhakikisha zinapatiwa ufumbuzi kwa wakati ili kuimarisha maendeleo na ustawi wa jamii. Hayo aliyasema Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaji Jabir Shekimweri, wakati alipokuwa akizungumza katika Mkutano wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alisema kuwa madiwani ni kiungo muhimu kati ya serikali na wananchi, hivyo wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kushughulikia changamoto zinazowakabili wananchi katika maeneo yao. “Madiwani ni sauti ya wananchi. Ni muhimu msikilize kwa umakini kero zao na kuzitatua kwa wakati ili kuondoa malalamiko yasiyo ya lazima na kuongeza imani ya wananchi kwa serikali yao” alisema Alhaji Shekimweri. Aliongeza kuwa utekelezaji wa majukumu hayo unahitaji uwajibikaji, ushirikiano na ufuatiliaji wa karibu wa miradi ya maendeleo ili kuhakikisha inaleta matokeo yaliyokusudiwa. Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya ...

OFISI ZA KANDA ZASOGEZA HUDUMA KWA WANANCHI DODOMA

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Jiji la Dodoma lilianzisha Kanda Saba kwaajili ya kusogeza huduma kwa wananchi lakini lengo kuu likiwa ni kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato ya ndani ya halmashauri ambayo yanatumika katika kuleta maendeleo kwa jamii. Akizungumza katika Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma la kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa kazi zilifanyika kwa kipindi cha robo ya tatu, Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula alisisitiza umuhimu wa matumizi ya mfumo wa kanda katika kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani. Aidha, alisisitiza umuhimu wa kubuni vyanzo vipya na kuviimarisha vilivyopo. Alisema kuwa mfumo wa kanda umeendelea kutoa mafanikio makubwa kwa kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa mapato, kuimarisha usimamizi wa vyanzo vya mapato na kuongeza uwajibikaji kwa wataalam waliopo katika maeneo husika. "Katika kipindi cha robo ya tatu, matumizi ya mfumo wa kanda yamesaidia kuongeza ufuatiliaji wa karibu wa vyanzo ...

KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI KUTOA ELIMU YA KINGA KWA VIJANA DODOMA

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Kamati ya Kuzuia na Kudhibiti UKIMWI ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kushirikiana na Taasisi ya DOYODO imeendelea kutoa elimu na mafunzo kwa jamii, hususan kwa vijana, ili kuhakikisha wanapata uelewa sahihi wa namna ya kujikinga na ugonjwa huo. Hayo aliyasema Mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Dodoma (WASEMI), Leticia Sanga tarehe 29 Aprili, 2026 wakati alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za kudhibiti UKIMWI kwa kipindi cha robo ya tatu kuanzia Januari hadi Machi, 2026 katika Mkutano wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alisema kuwa juhudi hizo zimeanza kuzaa matunda, lakini bado kuna haja ya kupanua wigo wa elimu hiyo. “Tumekuwa tukiwalenga zaidi vijana, lakini sasa tumeona umuhimu wa kuwafikia pia wazee. Wazee wengi wamekuwa waathirika wakubwa wa janga hili kwa sababu wanabeba jukumu la kuwahudumia watoto wao wanaoishi na virusi vya UKIMWI. Hivyo, nao wanahitaji elimu hii kwa kina zaidi” al...

DODOMA YAADHIMISHA MIAKA 62 YA MUUNGANO, DC SHEKIMWERI ASISITIZA AMANI NA MSHIKAMANO

Image
Na. Tutindaga Nkwindi, DODOMA MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Mhe Alhaji Jabir Mussa Shekimweri, ameongoza kilele cha maadhimisho ya miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yaliyofanyika kimkoa katika Shule ya Msingi Nane Nane, Kata ya Nzuguni, akisisitiza umuhimu wa kudumisha amani, umoja na mshikamano ili kuchochea maendeleo endelevu ya Taifa. Akizungumza katika maadhimisho hayo, Alhaj Shekimweri alisema kuwa kaulimbiu ya mwaka huu isemayo “Miaka 62 ya Muungano: Amani, Umoja na Mshikamano ni Msingi wa Maendeleo Endelevu” inapaswa kila Mtanzania aiishi kwa vitendo. Alieleza kuwa mafanikio ya taifa yanategemea mshikamano wa wananchi wake, akisisitiza umuhimu wa kulinda amani na kufanya kazi kwa pamoja ili kufikia maendeleo ya kweli na ya kudumu. “Ni wajibu wa kila mmoja wetu kuilinda amani, kuimarisha umoja na mshikamano kwasababu hayo ndiyo msingi wa maendeleo endelevu ya nchi yetu. Aidha, tujishughulishe na shughuli za kiuchumi ili kujikwamua na kuinua hali zetu za maisha” alise...

WAKAZI WA NALA WAADHIMISHA MIAKA 62 YA MUUNGANO KWA KUSHIRIKI USAFI WA MAZINGIRA

Image
Na. Mwandishi Wetu, NALA - DODOMA WAKAZI wa Mtaa wa Barazani, Kata ya Nala wamejitokeza kwa wingi katika zoezi la usafi wa mazingira linalofanyika kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi kwa lengo la kuendelea kuhakikisha mji unakuwa safi na kujenga mazoea ya kupenda kufanya usafi. Zoezi hilo la usafi limekuwa la kipekee kwasababu limefanyika sambamba na kuadhimisha Miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ambapo wananchi walionekana wenye hamasa kubwa katika kuboresha muonekano wa mtaa wao. Akizungumza na wakazi ho mara baada ya zoezi la usafi kukamilika, Afisa Mazingira kutoka Kanda Namba Tatu, Neema Komba aliwapongeza wananchi kwa kujitokeza kwa wingi na kuonesha uthamani wa kuishi katika mazingira safi. “Leo tumefanya jambo jema sana kujitokeza kufanya usafi, kwanza tumetimiza ule wajibu wetu wa kufanya usafi kila jumamosi ya mwisho wa mwezi lakini pia tupo hapa kuadhimisha kwa umoja wetu miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Muungano huo unaendelea kutukumbusha kus...

KANDA NAMBA MBILI YAADHIMISHA MIAKA 62 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR KWA KUFANYA USAFI WA JUMAMAMOSI YA MWISHO WA MWEZI

Image
Na. Tutindaga Nkwindi, DODOMA KANDA Namba Mbili imeadhimisha miaka 62 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa kufanya zoezi la usafi katika Kata ya Nzuguni, Mtaa wa Nzuguni A pamoja na Kituo Kikuu cha Mabasi Dodoma ikiwa ni sehemu ya kuenzi umoja na mshikamano wa watanzania. Zoezi hilo liliongozwa na Meneja wa Kanda Namba Mbili, Hussen Nyenye aliyeshirikiana na watumishi wa kanda hiyo pamoja na wananchi kusafisha mazingira katika maeneo hayo muhimu ya jiji. Akizungumza wakati wa zoezi hilo aliwashukuru Kikundi cha Wanawake wa Stendi maarufu kama Malkia wa Nguvu kwa kujitokeza kwa wingi kushiriki usafi huo. “Nawapongeza sana Malkia wa Nguvu kwa kuungana nasi kusafisha eneo hili muhimu ikiwa ni moja ya njia za kuadhimisha muungano wetu huku tukizingatia kaulimbiu ya mwaka huu isemayo ‘Miaka 62 ya Muungano: Amani, Umoja na Mshikamano ni Msingi wa Maendeleo Endelevu'. Pia tukumbuke kuwa mazingira safi ndiyo msingi wa kila kitu katika maendeleo ya jamii” alisema Nyenye. Kwa up...