Posts

Jiji la Dodoma lachangia Mil. 70 Mwenge wa Uhuru 2026

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imechangia shilingi 70,000,000 kufanikisha Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Wilaya ya Dodoma Mwaka 2026 zilizoongozwa na kaulimbiu isemayo ‘Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa pamoja Kuleta Maendeleo’. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Akiongelea michango ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026, alisema kuwa ulichangiwa na sekta ya umma na sekta binafsi. ” Mheshimiwa Rais, Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 zimechangiwa michango yenye jumla ya shilingi 100,944,500. Wananchi wamechangia shilingi 24,044,500, Halmashauri ya Jiji la Dodoma shilingi 70,000,000 na sekta binafsi pamoja na Mashirika ya Umma shilingi 6,900,000. Kati ya fedha hizo shilingi 5,460,000 zimerejeshwa kuchangia un...

Huduma ya Maji kuimarika Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALI ya upatikanaji wa huduma ya Maji safi na salama imeendelea kuimarika hadi kufikia lita 88.7 kwa siku sawa na asilimia 55 ya mahitaji yote. Kauli ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Alisema kuwa h ali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama ni lita Mil. 88.7 kwa siku sawa na asilimia 55 ya mahitaji ya wakazi wote ambayo ni lita Mil. 159.9. DUWASA imeendelea kutekeleza miradi 38 ya shilingi bilioni 91. ambayo ikikamilika itaongeza upatikanaji wa Maji kwa zaidi ya asilimia 75 ya mahitaji ya siku. MWISHO  

Dodoma kuvuna Tani 40,930 Chakula na Nafaka

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WILAYA ya Dodoma inatarajia kuvuna tani 40,930 za mazao ya chakula na biashara katika kuwahakikishia wananchi lishe bora na kujikwamua kiuchumi. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Alisema kuwa w ilaya kupitia Divisheni ya Kilimo Mjini na wadau iliendelea kuhakikisha wananchi wanapata lishe bora na kujikwamua kiuchumi kwa kulima mazao ya chakula na biashara. “Hali ya upatikanaji wa chakula na bei ni ya wastani kwa msimu wa kilimo 2025/2026. Wakulima wameanza kuvuna na kiasi cha tani 40,930 kinatarajiwa kuzalishwa. Hata hivyo, kuna mtiririko mzuri wa mazao ya chakula yanayoingia na kupatikana katika masoko yote. Hivyo, kuhakikisha upatikanaji wa chakula katika kipindi chote cha mwaka” alisema Mbugi. Akiong...

Dodoma kupambana na VVU

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WILAYA ya Dodoma imeendelea kupambana na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU) ikiwa na maambukizi ya asilimia 2.7 kwa Mwaka 2025. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Alisema kuwa mapambano dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI yanapewa uzito mkubwa. ” Mheshimiwa Rais, hali ya ushamiri wa maambukizi ya VVU wilayani kwa mwaka 2025 ni asilimia 2.7. Aidha, chini ya Kaulimbiu inayosema   “Imarisha mwitikio; Tokomeza UKIMWI”, kwa kipindi cha Januari, 2025 hadi Desemba, 2025 j umla ya watu 89,562 (Me 34, 806 Ke 54,756) walijitokeza kupima maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kwa hiari, kati yao watu 2,432 walikutwa na maambukizi na kuunganishwa na huduma za tiba na matunzo kwa WAVIU.   Hata hivyo, katika ...

Msalala DC wajifunza mbinu za ukusanyaji mapato kupitia mfumo wa kanda Dodoma Jiji

Na. Mwandishi Wetu Halmashauri ya Wilaya ya Msalala imetembelea Ofisi ya utoaji huduma Kanda Namba Moja iliyopo Soko la wazi la Machinga, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, ili kujifunza mbinu za ukusanyaji wa mapato kupitia mfumo wa kanda ambao umesaidia kuongeza ufanisi wa makusanyo na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi. Akielezea namna ya utendaji kazi wa kanda hiyo, Nicholaus Mitembo, Meneja wa Kanda Namba Moja, alisema kuwa kanda hiyo inatoa elimu kwa wananchi na wafanyabiashara na kuwahamasisha kulipa mapato kwa hiari na kwa wakati ili kuepuka adhabu na pia kuchangia maendeleo ya eneo lao. Aidha, alisema kanda hiyo inatarajia kukusanya mapato ya shilingi 19,162,421,314.32. Nae, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, Rose Manumba, aliishukuru Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kukubali na kutoa nafasi ya kujifunza katika halmashauri hiyo. Aidha, aliwakaribisha viongozi na watumishi wa jiji hilo kutembelea Msalala kwa ajili ya kujifunza zaidi kuhusu shughuli kuu za k...

Msalala DC watembelea Jiji la Dodoma kujifunza ukusanyaji Mapato

Na. Mwandishi wetu, DODOMA Madiwani na Wataalum wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala wamefanya ziara ya mafunzo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kujifunza mbinu mbalimbali ya ukusanyaji wa mapato ili kutekeleza miradi ya maendeleo. Akiwasilisha taarifa ya ukusanyaji na usimamizi wa mapato, Mhasibu wa Mapato wa Jiji la Dodoma, Julius Shinji katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri, alisema kuwa katika Mwaka wa Fedha 2025/2026, halmashauri ilijiwekea lengo la kukusanya jumla ya shilingi 71.675,239,000 kutokana na vyanzo vya ndani. Alisema kuwa hadi kufikia tarehe 31 Mei, 2026, halmashauri ilikuwa imefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi 61,328,048,214.71, sawa na asilimia 85.56 ya lengo la makisio ya mwaka. “Ukusanyaji wa mapato unafanyika kupitia mfumo wa kanda. Halmashauri tumeunda kanda saba za utoaji huduma zenye wataalamu kutoka divisheni na vitengo mbalimbali kupitia ukusanyaji wa moja kwa moja na kwa kudhibiti mianya ya upotevu. Makisio ya mapato kwa Mwaka wa Fedha 2026/202...

Wilaya ya Dodoma yapata “clean sheet” Miradi ya Mwenge wa Uhuru 2026

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Jumla ya miradi saba ya maendeleo yenye thamani ya shilingi Bil. 9,823,862,925 iliyotembelewa na Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 katika Wilaya ya Dodoma imepitishwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 ili iweze kutoa huduma kwa wananchi. Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 (kulia) akizindua mradi wa madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Wella Miradi iliyozinduliwa na Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 ni mradi wa Nishati safi ya kupikia katika Shule ya Sekondari Dr. Samia-Dodoma wenye thamani ya shilingi 698,800,161, mradi wa uwekezaji binafsi wa Hoteli ya Starline wenye thamani ya shilingi 3,000,000,000 ukiwa pamoja na kutembelea mradi wa kusimika kamera za usalama wenye gharama ya shilingi 682,561,548, mradi wa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa Shule ya Sekondari Wella wenye thamani ya shilingi 42,800,000, mradi wa Maji safi Kata ya Nala unaotekelezwa na Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira na ujenzi wa Barabara kwa kiwango cha lami yeny...

Shilingi 519,891,609 mapato ya ndani kusimika Kamera za Usalama Jiji la Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, TAMBUKARELI HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imetumia shilingi 519,891,609 kwa ajili ya kusimika mfumo wa kamera za usalama ili kuwahakikishia ulinzi na usalama wananchi na mali zao pamoja na wawekezaji. Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo alipokuwa akiwasilisha taarifa ya mradi wa kusimika kamera za usalama jijini Dodoma kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2026 tukio lililofanyika katika Hoteli ya Starline jijini Dodoma. Akiongelea lengo la mradi huo, alisema kuwa ni kuimarisha ulinzi na usalama wa wananchi na mali zao. “Kamera hizi zinalenga kulinda miundombinu ya Umma katika Jiji la Dodoma, kudhibiti makosa ya barabarani na matendo ya uhalifu. Aidha, mradi utasaidia kutoa uhakika wa usalama kwa wadau wa shughuli za maendeleo na kulifanya Jiji la Dodoma kuwa salama kwa shughuli za uwekezaji, kidiplomasia, utalii na kuhakikisha Jiji linaendeshwa kidijitali” al...

Shilingi 698,800,161 zatekeleza mradi wa Nishati safi Sec Dr. Samia- Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, IYUMBU SHILINGI 698,800,161 za utekelezaji wa mradi wa Nishati safi ya kupikia katika Shule ya Sekondari Dr. Samia-Dodoma zimelenga kuhifadhi Mazingira kwa kurejesha taka, kupunguza matumizi ya kuni na mkaa na kulinda afya za watumiaji. Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Shule ya Sekondari Dr. Samia-Dodoma, Mwl. Leticia Singo alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa nishati safi ya kupikia kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2026 shuleni hapo. “Ndugu Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, l engo la mradi ni kuhifadhi Mazingira kwa kurejesha taka zinazozalishwa shuleni pamoja na kupunguza madhara yatokanayo na matumizi ya kuni na mkaa kwa kutumia nishati safi ya kupikia” alisema Mwl. Singo. Alisema kuwa mradi huo ulitekelezwa kwa gharama ya shilingi 698,800,161 fedha kutoka mradi wa P4R chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia chini ya Mkandarasi SUMA JKT. Akiongelea mafanikio ya mradi huo, aliyataja kuwa ni mradi umepunguza gharama za ...

Jiji la Dodoma latenga Bil. 3.9 kuongeza miundombinu mapokezi ya Kidato cha Kwanza 2027

Image
Na. Dennis Gondwe, KIKUYU KUSINI HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imetenga shilingi 3,956,990,000 katika Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2026/2027 kwa ajili ya kuongeza miundimbinu ya madarasa, viti, meza na matundu ya vyoo ikiwa ni maandalizi ya kupokea wanafunzi watakaohitimu darasa la sita na saba kwa pamoja. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Wella, Mwl. Allen Lugemalila wakati a kisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika Shule ya Sekondari Wella kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2026, shuleni hapo. “ Ndugu Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, h almashauri inategemea kupokea wanafunzi watakaohitimu darasa la sita na la saba kwa pamoja mwaka 2027. Katika kufanikisha mpango huo wa serikali, kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027, halmashauri imetenga bajeti ya shilingi 3,956,990,000 kwa lengo la kuongeza miundombinu ya madarasa, vyoo, viti na meza. Pamoja na lengo hili la msingi, shule hii ilikuwa na uhitaji wa vyumba...