Posts

Wanawake watakiwa kulipa kodi na kukuza uchumi katika Jiji la Dodoma

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Wanawake wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, hususan wafanyabiashara na wajasiriamali, wametakiwa kuendelea kulipa kodi na tozo kwa wakati ili kuchangia maendeleo ya jiji pamoja na kukuza uchumi wao na wa jamii kwa ujumla. Wito huo ulitolewa na Diwani wa Viti Maalum Tarafa ya Zuzu, Pilly Hassan, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayotarajiwa kufanyika tarehe 8 Machi, 2026. Alisema kuwa ulipaji wa kodi ni moja ya njia muhimu inayosaidia serikali   kupata mapato ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo kuboresha miundombinu ya masoko, barabara na huduma nyingine muhimu kwa wananchi. “Wanawake wengi wa Jiji la Dodoma tunajishughulisha na shughuli za biashara na ujasiriamali. Hivyo, tunapaswa kuwa mfano mzuri kwa kuhakikisha tunatimiza wajibu wetu wa kulipa kodi na tozo za serikali kwa hiari na kwa wakati. Kupitia kodi hii itaweza kutusaidia mambo mbalimbali na ya muhimu kama vile kujeng...

Mstahiki Meya Chaula ashauri Baraza kutumia mkakati wa hoja kwa hoja

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula ameshauri Baraza la Madiwani kujenga utaratibu wa kuwasilisha hoja moja na kuiazimia hadi itakapokamilika ndio hoja nyingine ifanyiwe kazi. Aliyazungumza hayo kwa msisitizo katika mkutano wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri jijini Dodoma. Alisema kuwa mkakati huo wa hoja moja ‘Focus Strategy’ ndiyo njia pekee ya kuleta maendeleo yanayoonekana na yenye tija kwa wananchi wanaowaongoza. "Ili tuwe na ufanisi, niwaombe kwa unyenyekevu mkubwa sana tuchague jambo moja na kuliazimia hadi mwisho. Kwa mfano, kama baraza linaona kipaumbele ni ujenzi wa matundu ya vyoo kwa shule zote za msingi katika jiji letu, basi nguvu, fedha, na usimamizi wetu wote uelekezwe hapo. Tukimaliza na kujiridhisha kuwa kila shule ina vyoo bora, ndipo tunahamia hoja nyingine ya msingi na kuendelea na mtiririko huo" alisema Chaula. Alimalizia kwa kutoa rai kuwa umoja na maamu...

Shule ya Msingi Mazengo ipo moto

Image

Huduma ya Lishe kwa Shule za Dodoma

Image
 

Stadi za Maisha Kuwa mkombozi kwa wanafunzi wa Sekondari jijini Dodoma

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Elimu ya Stadi ya Maisha imetajwa kuwa ni chachu ya mabadiliko chanya kwa wanafunzi katika kuwajengea uwezo wa kujitambua na kukabiliana na changamoto za maisha katika shule za sekondari jijini Dodoma. Hayo aliyasema Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Daniel Mapilya wakati akifungua mafunzo kwa wawezeshaji wa stadi za maisha katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Dodoma. Alieleza kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha wawezeshaji wanapata uelewa wa kutosha juu ya namna bora ya kuwafikia wanafunzi na kuwajengea misingi imara ya maisha. “Tunapozungumzia stadi za maisha, tunalenga kumsaidia mwanafunzi kujitambua, kujiamini na kufanya maamuzi sahihi. Elimu hii itawawezesha vijana wetu kuepukana na vishawishi vinavyoweza kuathiri masomo na mustakabali wa maisha yao” alisema Mapilya. Aliongeza kwa kusema kuwa changamoto nyingi zimekuwa zikiwakumba watoto wa kike. ”…zikiwemo shinikizo la rika na mazingira yasiyo rafiki, hivyo elimu hiyo it...

Utatuzi mgogoro wa Mahomanyika watangazwa

Image
Na. Nancy Kivuyo , NZUGUNI Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeunda timu mbili ya wataalam wa upangaji na upimaji na timu ya uhakiki kwaajili ya kutatua mgogoro wa ardhi wa muda mrefu katika eneo la Mahomanyika. Timu hizo zimeundwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt. Leonard Akwilapo alipokuwa akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika eneo la Mahomanyika, Kata ya Nzuguni jijini Dodoma. Alisema kuwa timu hizo zitaanza kazi mara moja ili kuhakikisha zoezi hilo linakamilika kwa wakati. “Eneo la Mahomanyika ni la serikali kwahiyo , naagiza lipangwe na kupimwa kwaajili ya kutatua mgogoro huu na kuwa kielelezo cha utatuzi wa migogoro mingine iliyopo ndani ya Jiji la Dodoma. Timu hizi zinapaswa kufanya kazi ndani ya siku 60 na kukamilisha zoezi hili ili kila mmoja ajue amepata nini na anaenda wapi” alisema Dkt. Akwilapo. A liongeza kuwa wale wote waliohusika kwenye kadhia ya mgogoro huo wa ardhi watachukuliwa kwaajili ya maho...

Timu ya ‘sustainability’ ya Jiji la Dodoma yaanza semina ya siku saba

Image
  Na. Nancy Kivuyo , DODOMA Mafunzo maalum kuhusu viwango vipya vya uhasibu ‘ General Requirements for Disclosure of Sustainability-related Financial Information na Climate-related Disclosures’ (IFRS S1 na IFRS S2) yameanza rasmi kutolewa kwa timu ya ‘sustainability’ ikiwa ni sehemu ya mpango wa mafunzo ya uendelevu ‘sustainabilty and ESG’ yanayolenga kuwajengea uelewa na kuongeza ufanisi katika usimamizi wa taarifa za kifedha. Akizungumza wakati wa semina hiyo ya siku ya kwanza, Mratibu wa Mafunzo ya ‘sustainability’ katika Jiji la Dodoma, Akida Huddu alisema kuwa mafunzo hayo yamelenga kutoa elimu ya jumla ya uendelevu ‘sustainability and ESG’ kwa washiriki ili kuwawezesha kusimamia kwa ufanisi shughuli zote zinazohusiana na uendelevu pamoja na kupata taarifa zitakazosaidia kutoa huduma nzuri kwa wananchi. Aliongeza kuwa uelewa wa viwango vipya vya uhasibu ni muhimu katika kuimarisha uwazi, uwajibikaji na usimamizi bora wa rasilimali za umma, hususan katika mazingira yanayoh...

Wawezeshaji Stadi za Maisha watakiwa kuwa na nidhamu na uwajibikaji

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Wawezeshaji wa Stadi za Maisha katika Shule za Sekondari Jiji la Dodoma wametakiwa kuwa na nidhamu ya hali ya juu katika mazingira ya shule watakazopangiwa pamoja na kutumia mafunzo waliyoyapata kwa kuleta mabadiliko chanya kwa wanafunzi. Hayo yalisemwa na Mwezeshaji mafunzo y a Stadi za Maisha wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Tuvacal Mjema, wakati wa mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Dodoma jijini Dodoma. Alisema kuwa wawezeshaji wanapaswa kuwa mfano bora kwa wanafunzi kwa kuzingatia maadili, kuwajibika ipasavyo na kuonyesha weledi katika utekelezaji wa majukumu yao. “Ni muhimu kwa wawezeshaji kuwa na nidhamu ya hali ya juu wanapokuwa shuleni. Tunapaswa kuishi yale tunayowafundisha wanafunzi ili waweze kutuamini na kufuata miongozo tunayowapatia kwasababu ninyi ndio taa yao   inayo waangazia” alisema Mjema. Lakini pia aliongezea kwa kusema kuwa mafunzo hayo yamelenga kuwaongezea uwezo wa kitaaluma na kisaikolojia wawezesh...

Jiji la Dodoma kuchangamkia fursa ujio wa Bandari Kavu Ihumwa

Image
Na. Nancy Kivuyo, DODOMA MSTAHIKI Meya wa Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula apongeza Mkakati wa Uendelezaji Bandari Kavu na kuahidi kujipanga kuhakikisha wafanyabiashara wadogo wanapata fursa ya kufanya biashara katika eneo hilo na kuchochea ukuaji wa uchumi wa mkoa na taifa kwa ujumla. Akizungumza katika ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kwenye Bandari Kavu Ihumwa iliyokuwa na lengo la kujiridhisha na mkakati wa uendelezaji wa miundombinu hiyo, alisema kuwa uongozi wa jiji utakaa kikao na kutathmini namna ya kuandaa mazingira rafiki ya biashara ili kuwawezesha wajasiriamali wa ndani kushiriki kikamilifu katika shughuli za upokeaji, uhifadhi na usafirishaji wa mizigo. Alieleza kuwa pamoja na fursa za moja kwa moja zitakazotokana na shughuli za bandari hiyo, jiji pia linatarajia kuimarisha sekta ya usafirishaji, uhudumu na biashara ndogondogo hivyo kuongeza ajira na kipato kwa wananchi. Aidha, Mstahiki Meya Chaula aliongeza kuwa jiji litafanya utaratibu wa kufanya mazungumzo na Mam...