Baraza la Madiwani Jiji la Dodoma lawafukuza kazi watumishi watatu na mmoja kushushwa cheo
Na. Mwandishi wetu, DODOMA BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma limewafukuza kazi watumishi watatu na mtumishi mmoja kushushwa cheo na mshahara kufuatia kukiuka misingi na taratibu za Utumishi wa Umma. Maamuzi hayo yalifanyika katika Mkutano maalum wa Mashauri ya Kinidhamu uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Watumishi waliofukuzwa kazi ni Afisa Muuguzi Msaidizi, Muuguzi na Afisa Mtendaji wa Mtaa. Mtumishi aliyeshushwa cheo na mshahara ni Mteknolojia Maabara. Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula alilihoji Baraza la Madiwani, na kwa kauli moja liliridhia kuwafukuza kazi watumishi hao watatu na kushushwa cheo na mshahara mtumishi mmoja. Akiwasilisha taarifa ya kuhitimisha mashauri ya nidhamu ya watumishi wanne kwa Baraza maalum la Mashauri ya Nidhamu, Mkuu wa Divisheni ya Utawala na Menejimenti ya Rasilimali watu kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Gerald Ruzika alisema kuwa mkurugenzi aliunda kam...