Posts

Jiji la Dodoma laibuka na zana za upaliliaji, Maonesho ya Nanenane

Image
Na. Mwandhsi wetu, DODOMA Halmshauri ya Jiji la Dodoma imeendelea kungara katika Maonesho ya Nanenane kwa kuweka vitu vya kitofauti ambapo mojawapo ni uwepo wa zana za upaliliaji ambazo zimeundwa na mjasiriamali mdogo kutoka ndani ya jiji. Akizungumza na waandishi wa habari mjasiriamali, Zuberi Nguzo aliyepata fursa ya kuonesha ujuzi katika maonesho hayo alisema kuwa zana hizo zimeundwa kwa muundo wa ‘power tiller’ ya miguu mitatu zikiwa katika ubora wa hali ya juu. “Zana hizi za upaliliaji zinatumia injini ya guta lakini ina mfumo wa rejeta kama kawaida. Pia ina mfumo wa feni kama kawaida na upande wa nyuma kuna jembe ambalo hili ndilo linatumika kwa ajili ya upaliliaji. Katika upaliliaji inatumia   mfumo wa matuta kwa maana kwamba inapita katikati ya mstari na kuweka matuta kwenye mashina ya mahindi kwasababu tairi zake tumeweka kwa kipimo cha sentimita 62, hiki ni kipimo sahihi kabisa kwa upana kwa kilimo cha mahindi,” alisema Nguzo. Alisema kuwa ameamua kubuni zana hizo k...

Kuku aina ya Ayam Cemani na Brahma kuongeza kipato na usalama wa chakula Dodoma

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Ufugaji wa kisasa wa kuku umeendelea kujitokeza kama fursa yenye tija ya kuongeza kipato na kuimarisha usalama wa chakula, huku wananchi wakionesha hamasa kubwa ya kujifunza mbinu bora za kufuga kuku wa kisasa aina ya Ayam Cemani na Brahma wenye faida nyingi kiuchumi.   Akizungumza katika maonesho hayo, Mtaalamu wa Kilimo na Mifugo wa Jiji la Dodoma, Christopher Magesa alisema kuwa Kuku aina ya Ayam Cemani amekuwa akiwavutia wananchi wengi kutokana na rangi yake nyeusi inayotanda sehemu kubwa ya mwili wake, ikiwemo manyoya, ngozi na mayai yake. "Mbali na kuwa kuku wa mapambo, Ayam Cemani ni rahisi kufugwa kwa sababu ni mpole na ana thamani kubwa sokoni kutokana na sifa zake za kipekee" alisema Magesa. Aliongeza kuwa wapo pia kuku aina ya Brahma ambapo pia wameendelea kuvutia wafugaji kutokana na umbo lao kubwa, manyoya yanayofunika hadi miguuni na uwezo mzuri wa kuzalisha nyama na mayai. "Kwa usimamizi bora, Brahma ana uwezo wa kutaga...

FRIESIAN: NG'OMBE WA MAZIWA MWENYE MVUTO NANENANE

Image
 

ANGLO NUBIAN: MBUZI WA MAZIWA MWENYE TIJA

Image
 

ZERO GRAZING KICHOCHEO CHA UZALISHAJI MAZIWA KWA WINGI

Image
 

UZAO WA KUKU AINA YA AYAM CEMANI KIVUTIO NANENANE

Image
 

KUKU AINA YA AYAM CEMANI WAVUTIA WAGENI BANDA LA MIFUGO JIJI LA DODOMA

Image
 

BANDA LA MIFUGO JIJI LA DODOMA KIVUTIO NAONESHO YA NANENANE, 2026

Image
 

KLINIKI YA MACHO ZAHATI YA MPUNGUZI TAREHE 10-14 AGOSTI, 2026

Image
 

Timu ya SHIMISEMITA ya Jiji la Dodoma yajipanga kutetea ubingwa

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Kikosi cha Timu ya Watumishi wa Jiji la Dodoma cha Mpira wa Miguu kinaendelea kujifua kwa mazoezi makali kuelekea mashindano ya SHIMISEMITA 2026 yatakayofanyika jijini Mbeya, kikiwa na malengo ya kufanya vizuri na kutwaa ubingwa. Hayo aliyasema Kocha wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Watumishi Jiji la Dodoma, Given Aristides wakati wa bonanza la kimichezo lililozikutanisha Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino na Halmashauri ya Wilaya ya Gairo katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Dodoma, ambapo timu hizo zilipata nafasi ya kupima uwezo wao kabla ya kuingia kambini kwa ajili ya mashindano hayo. Alisema kuwa ushindani katika SHIMISEMITA unazidi kuongezeka kila mwaka kutokana na halmashauri nyingi kujiandaa kwa umakini, jambo linalowalazimu kuongeza kiwango cha mazoezi na nidhamu ili kufikia malengo waliyojiwekea. “Tunafahamu kuwa SHIMISEMITA ni mashindano yenye ushindani mkubwa, hivyo tunaendelea kujinoa kwa bidii kila siku. Bonanza hil...