Posts

Katambi: Vijana watakiwa kuyajua mema ya serikali

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi amewataka vijana wa Wilaya ya Dodoma kuyajua mema ya serikali ambayo ina neema kwa kila kijana nchini kuanzia aliyesoma hata ambae hajasoma. Akizungumza leo katika Kongamono la Vijana kuelekea mapokezi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026 wenye Kaulimbiu isemayo ‘Tanzania ni yetu sote tushikamane kwa pamoja kuleta maendeleo’, lililofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini. “Amini haujazaliwa kwa bahati mbaya, bali kwa kusudi la Mungu uliamliwa wewe uwe Mtanzania na sio nchi nyingine. Jambo la msingi ni kujitambua na kujua wajibu wako pia kujua wewe una ndoto gani na uzisimamie ndoto zako, na serikari inawajibu wa kuandaa mazingira wezeshi kwenu kwa sababu ni moja ya majukumu yake muhimu. Pia ni sehemu ya nne katika kukutengeneza wewe, Mungu kwanza, wazazi, jamii kisha serikali. Hivyo, fursa ni nyingi kwenu simamieni misimamo yenu na ajira zote ni zenu nyinyi vijana” alisema Katambi. “K...

Zoezi la usafi katika Soko la wazi la Machinga katika maadhimisho ya kuelekea kilele cha Siku ya Mazingira Duniani tarehe 5 Juni, 2026

Image
 

Vijana watakiwa kuepuka matumizi ya Dawa za kulevya Dodoma

Image
  Na. Mwandishi wetu, DODOMA VIJANA wahimizwa kuepuka matumizi ya dawa za kulevya ambayo yanatajwa kuwa na madhara makubwa ili kulinda afya zao na kuchangia maendeleo ya taifa. Akizungumza katika Kongamano la Vijana lililofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini (IRDP), Afisa Mwandamizi kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, Anna Tengia alisema kuwa dawa za kulevya ni kemikali zinazobadilisha mfumo wa fahamu wa binadamu na kuathiri mtu anavyofikiri na kutenda. Aliweka mkazo kuwa vijana wajilinde ili kujenga kizazi imara na kinachofikiria mustakabali bora wa maisha yao. “Dawa za kulevya huathiri afya ya akili na mwili wa mtumiaji. Kwa maana hiyo hupunguza uwezo wa vijana kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo” alisema Tengia. Kwa upande wake, Afisa Sheria wa mamlaka hiyo, Meshak Lyabonga wakati akitoa elimu alisisitiza kuwa matumizi ya dawa za kulevya ni kosa la kisheria na wahusika wanaweza kuchukuliwa hatua kwa mujibu...

Vijana Dodoma watakiwa kutekeleza wajibu wao katika jamii

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA VIJANA wametakiwa kujitambua, kuthamini nafasi yao katika maendeleo ya taifa na kutekeleza wajibu kwa familia na jamii kwa ujumla ili kuchangia ustawi wa nchi. Wito huo ulitolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi wakati akizungumza katika Kongamano la Vijana lililofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini (IRDP) katika Wilaya ya Dodoma ikiwa ni kuelekea mapokezi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2026 katika ya Wilaya ya Dodoma. Alisema kuwa vijana wana nafasi kubwa katika kuendeleza amani, uzalendo na maendeleo ya taifa, hivyo wanapaswa kutumia fursa walizonazo kwa manufaa yao na ya jamii inayowazunguka. “Kuelekea Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2026, ninawahimiza vijana wote kujitambua, kujua wajibu wao kwa familia, jamii na taifa kwa ujumla. Vijana ndiyo nguvu kazi ya taifa na msingi wa maendeleo endelevu” alisema Katambi. Aliongeza kuwa Mwenge wa Uhuru unaendelea kuwa chombo muhimu cha kuhamasish...

Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Vincent Odero (kushoto) akimuongoza mgeni rasmi Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Dkt. Khatibu Kazungu (katikati) kwenda kuzungumza na mamia ya wananchi waliojitokeza katika zoezi la usafi wa mazingira lililofanyika katika Soko la wazi la Machinga

Image
 

Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Vincent Odero (katikati) akitoa maelekezo kwa Mchumi, Francis Kaunda (kushoto) na Mkuu wa Kitengo cha Usafi na uthibiti taka ngumu, Dickson Kimaro (kulia) katika zoezi la usafi wa mazingira kuelekea maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani zoezi lililofanyika katika Soko la wazi la Machinga

Image
 

Jamii yatakiwa kuwajengea watoto utamaduni wa kupenda kupanda Miti na kuhifadhi Mazingira

Image
  Na. Dennis Gondwe, DODOMA WADAU wa uhifadhi wa Mazingira wametakiwa kuwajengea watoto utaratibu wa kupanda miti na kupenda kudumisha usafi wa Mazingira katika maeneo yanayowazunguka ili kuwa na mandhari nzuri ya kuvutia. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Dkt. Khatibu Kazungu alipomuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dodoma katika zoezi la usafi wa Mazingira ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani lililofanyika katika Soko la wazi la Machinga jijini Dodoma. Akizungumza na mamia ya wananchi waliojitokeza kushiriki zoezi hilo la usafi, alisema kuwa wadau wa masuala ya usafi na jamii kwa ujumla wana wajibu wa kuwafundisha na kuwarithisha watoto kupenda usafi na kuchukia mazingira machafu. “Pamoja na usafi, pia tuwakumbushe watoto wetu kupanda miti katika maeneo yanayotuzunguka. Kurithisha tabia ya kupenda kupanda miti inatuhakikishia mandhari nzuri inayotuzunguka na kuepuka tishio la mabadiliko ya tabia nchi” alisema Dkt. Kazungu. Kwa upande wake...

Baraza la Madiwani Jiji la Dodoma lawafukuza kazi watumishi watatu na mmoja kushushwa cheo

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma limewafukuza kazi watumishi watatu na mtumishi mmoja kushushwa cheo na mshahara kufuatia kukiuka misingi na taratibu za Utumishi wa Umma. Maamuzi hayo yalifanyika katika Mkutano maalum wa Mashauri ya Kinidhamu uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Watumishi waliofukuzwa kazi ni Afisa Muuguzi Msaidizi, Muuguzi na Afisa Mtendaji wa Mtaa. Mtumishi aliyeshushwa cheo na mshahara ni Mteknolojia Maabara. Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula alilihoji Baraza la Madiwani, na kwa kauli moja liliridhia kuwafukuza kazi watumishi hao watatu na kushushwa cheo na mshahara mtumishi mmoja. Akiwasilisha taarifa ya kuhitimisha mashauri ya nidhamu ya watumishi wanne kwa Baraza maalum la Mashauri ya Nidhamu, Mkuu wa Divisheni ya Utawala na Menejimenti ya Rasilimali watu kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Gerald Ruzika alisema kuwa mkurugenzi aliunda kam...

Kimaro: Wananchi Dodoma waalikwa kuupokea Mwenge wa Uhuru Juni, 1 2026

Image
  Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Mwenyekiti wa Kamati ya Chakula katika maandalizi ya Mwenge wa Uhuru 2026 Wilaya ya Dodoma, Dickson Kimaro anawaalika wananchi kushiriki mapokezi ya mbio za Mwenge wa Uhuru na kuwakumbusha kuwa tukio hilo linawaungansha pamoja na kujenga mshikamano wa kimaendeleo. Mwenyekiti wa Kamati ya huduma ya Chakula Wilaya ya Dodoma Aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mapokezi ya mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma unaotarajiwa kuwasili tarehe 1 Juni, 2026 na kukimbizwa katika miradi saba ya maendeleo. Alisema kuwa maandalizi yanaendelea vizuri. “Maandalizi mpaka leo hii yapo vizuri na Kamati ya Chakula imejipanga katika eneo la chakula kwa kuhakikisha wote wanaohudhuria wanapata chai itakayotolewa katika Shule ya Sekondari, Dkt. Samia na chakula cha mchana kitakuwepo pale katika Shule ya Sekondari Umonga. Chakula cha usiku kitapatikana katika shule ya Msingi Kizota’’ alisema Kimaro. Kimaro ambae pia ni Mkuu wa...

Odero: Mwenge wa Uhuru alama ya Umoja Wilayani Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WANANCHI wa Wilaya ya Dodoma wameombwa kuonesha umoja na mshikamano wao kwa kujitokeza kwa wingi kuupokea na kuukimbiza Mwenge wa Uhuru utakapowasili na kutembelea miradi ya maendeleo inayolenga kuboresha maisha yao. Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Vincent Odero akionesha utayari wa kuupokea Mwenge wa Uhuru mwaka 2026 Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Vincent Odero alipokuwa akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu maandalizi ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 katika Wilaya ya Dodoma. Alisema kuwa Mwenge wa Uhuru ni chombo cha umoja na mshikamano ambao umekuwa ukitafsiriwa kwa vitendo wilayani Dodoma. “Wilaya ya Dodoma tumekuwa tukionesha umoja na mshikamano wa wazi linapokuja suala ya Mwenge wa Uhuru kwa miaka yote. Hili ni jambo la heshima kwetu. Nitumie nafasi hii kuwaalika na kuwaomba tena wananchi wote tarehe 1 Juni, 2026 kuupokea Mwenge wa Uhuru katika Mtaa wa Vikonje B, Kata ya Mtumba n...