Timu ya Watumishi Jiji la Dodoma yadaiwa ushindi mashindano ya SHIMISEMITA
Na. Lulu Luvanda, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeiaga timu ya watumishi itakayoliwakilisha jiji hilo katika Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa (SHIMISEMITA) 2026 yatakayofanyika jijini Mbeya na kutakiwa kurejea na ushindi. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akiiaga timu hiyo katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. Akizungumza katika hafla ya kuwaaga wachezaji hao jijini Dodoma, alisema kuwa mashindano hayo ni fursa ya kulitangaza Jiji la Dodoma kupitia michezo, huku akiwataka wachezaji hao kuzingatia nidhamu, maadili na misingi ya utumishi wa umma. Aliwakumbusha umuhimu wa michezo katika kuimarisha afya, mshikamano na uhusiano miongoni mwa watumishi, huku akiwataka kulitangaza vizuri Jiji la Dodoma kwa kuonesha uwezo, nidhamu na ushindani wa hali ya juu. Kwa upande wake Meneja wa Timu ya watumishi wa Jiji la Dodoma, Dkt. Sebastian Pima alisema kuwa wamefurahia kumuona Mkurugenzi...