Wafanyabiashara Sabasaba watakiwa kujitokeza kupata elimu ya mikopo ya 10%
Na. Leah Mabalwe, DODOMA Wafanyabiashara katika Soko la Sabasaba jijini Dodoma wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika ofisi ya soko hilo kwa ajili ya kupata elimu na uelewa kuhusu utaratibu wa upatikanaji wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa makundi mbalimbali ya wananchi. Hayo yalisemwa na Afisa Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Peter Mallya wakati alipofika katika Soko la Sabasaba kwa ajili ya kutoa huduma mbalimbali zinazohusiana na maendeleo ya jamii, ikiwemo kutoa elimu kwa wafanyabiashara kuhusu fursa ya mikopo hiyo katika Mwezi wa Maendeleo ya Jamii. Alisema kuwa katika kuadhimisha Mwezi wa Maendeleo ya Jamii, Maafisa Maendeleo ya Jamii wameamua kuwafuata wananchi katika maeneo yao badala ya kusubiri wananchi wafike ofisini, hatua inayolenga kuhakikisha taarifa na elimu kuhusu fursa mbalimbali zinawafikia wananchi wengi zaidi. “Kupitia Mwezi huu wa Maendeleo ya Jamii, sisi kama Maafisa Maendeleo ya Jamii tumeamua ...