Posts

Baraza la Madiwani Jiji la Dodoma lawafukuza kazi watumishi watatu na mmoja kushushwa cheo

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma limewafukuza kazi watumishi watatu na mtumishi mmoja kushushwa cheo na mshahara kufuatia kukiuka misingi na taratibu za Utumishi wa Umma. Maamuzi hayo yalifanyika katika Mkutano maalum wa Mashauri ya Kinidhamu uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Watumishi waliofukuzwa kazi ni Afisa Muuguzi Msaidizi, Muuguzi na Afisa Mtendaji wa Mtaa. Mtumishi aliyeshushwa cheo na mshahara ni Mteknolojia Maabara. Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula alilihoji Baraza la Madiwani, na kwa kauli moja liliridhia kuwafukuza kazi watumishi hao watatu na kushushwa cheo na mshahara mtumishi mmoja. Akiwasilisha taarifa ya kuhitimisha mashauri ya nidhamu ya watumishi wanne kwa Baraza maalum la Mashauri ya Nidhamu, Mkuu wa Divisheni ya Utawala na Menejimenti ya Rasilimali watu kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Gerald Ruzika alisema kuwa mkurugenzi aliunda kam...

Kimaro: Wananchi Dodoma waalikwa kuupokea Mwenge wa Uhuru Juni, 1 2026

Image
  Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Mwenyekiti wa Kamati ya Chakula katika maandalizi ya Mwenge wa Uhuru 2026 Wilaya ya Dodoma, Dickson Kimaro anawaalika wananchi kushiriki mapokezi ya mbio za Mwenge wa Uhuru na kuwakumbusha kuwa tukio hilo linawaungansha pamoja na kujenga mshikamano wa kimaendeleo. Mwenyekiti wa Kamati ya huduma ya Chakula Wilaya ya Dodoma Aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mapokezi ya mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma unaotarajiwa kuwasili tarehe 1 Juni, 2026 na kukimbizwa katika miradi saba ya maendeleo. Alisema kuwa maandalizi yanaendelea vizuri. “Maandalizi mpaka leo hii yapo vizuri na Kamati ya Chakula imejipanga katika eneo la chakula kwa kuhakikisha wote wanaohudhuria wanapata chai itakayotolewa katika Shule ya Sekondari, Dkt. Samia na chakula cha mchana kitakuwepo pale katika Shule ya Sekondari Umonga. Chakula cha usiku kitapatikana katika shule ya Msingi Kizota’’ alisema Kimaro. Kimaro ambae pia ni Mkuu wa...

Odero: Mwenge wa Uhuru alama ya Umoja Wilayani Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WANANCHI wa Wilaya ya Dodoma wameombwa kuonesha umoja na mshikamano wao kwa kujitokeza kwa wingi kuupokea na kuukimbiza Mwenge wa Uhuru utakapowasili na kutembelea miradi ya maendeleo inayolenga kuboresha maisha yao. Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Vincent Odero akionesha utayari wa kuupokea Mwenge wa Uhuru mwaka 2026 Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Vincent Odero alipokuwa akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu maandalizi ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 katika Wilaya ya Dodoma. Alisema kuwa Mwenge wa Uhuru ni chombo cha umoja na mshikamano ambao umekuwa ukitafsiriwa kwa vitendo wilayani Dodoma. “Wilaya ya Dodoma tumekuwa tukionesha umoja na mshikamano wa wazi linapokuja suala ya Mwenge wa Uhuru kwa miaka yote. Hili ni jambo la heshima kwetu. Nitumie nafasi hii kuwaalika na kuwaomba tena wananchi wote tarehe 1 Juni, 2026 kuupokea Mwenge wa Uhuru katika Mtaa wa Vikonje B, Kata ya Mtumba n...

ILEMELA MANISPAA YAVUTIWA UWEKEZAJI MIRADI YA KIMKAKATI DODOMA

Na. Tutindaga Nkwindi, DODOMA MADIWANI wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela wamevutiwa na uwekezaji na utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kulitaja kuwa ni jiji darasa. Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela, Kuruthum Abdallah baada ya kutembelea miradi ya kimkakati inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma.   Alisema kuwa wamevutiwa na kiwango cha uwekezaji pamoja na usimamizi madhubuti miradi hiyo na kubainisha kuwa Ilemela inakwenda kutumia uzoefu huo kama darasa. Tunaipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kumiliki na kuendesha miradi mikubwa na yenye tija kama hii. Sisi pia tuna miradi inayofanana na hii. Hivyo, ziara hii imetupa nafasi ya kujifunza mambo mengi ambayo tunaenda kuyafanyia kazi Ilemela ili tuweze kuboresha huduma na kuongeza mapato yetu ya ndani kupitia miradi ya kimkakati ” alisema Abdallah.   Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispa...

Hazina Volleyball yaiduwaza Dodoma Jiji Seti 2-0 Mwenge Super Cup

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA TIMU ya Wanaume ya Mpira wa Mikono ya Hazina (Hazina Volleyball Club) imeibuka na ushindi wa Seti 2-0 dhidi ya Timu ya Dodoma Jiji mchezo uliochezwa katika viwanja vya Chinangali Park mapema leo. Akiongelea mchezo huo, Nahodha wa Timu ya Hazina Volleyball Club, George Kalunde alisema timu yake ilijiandaa vizuri kuelekea mchezo huo ndio sababu ya kupata ushindi wa Seti 2-0. Aidha, aliipongeza Wilaya ya Dodoma kwa kuandaa mashindano ya Mwenge Super Cup Mwaka 2026 na kutaja maandalizi hayo kuwa ni ubunifu mkubwa. “Nitumie nafasi hii kuwahamasisha vijana wenzangu kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mapokezi na mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 katika Wilaya ya Dodoma, karibuni sana. Nae Nahodha wa Timu ya Mpira wa Mikono ya Dodoma Jiji, Muhidin Mwenda alisema kuwa mchezo ulikuwa mzuri pamoja na kufugwa. “Tunapenda kumshukuru Mungu tumemaliza mechi salama, pamoja na kuwa tumepoteza mechi kwa seti 2-0, siyo matokeo mazuri kwetu. Mashindano haya yamekuwa c...

Dodoma Jiji yaangukia pua dhidi ya Ujenzi Queens Mwenge Super Cup

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA TIMU ya Mpira wa Pete ya Wizara ya Ujenzi (Ujenzi Queens) imeibuka kidedea kwa kuifunga Timu ya Mpira wa Pete ya Dodoma Jiji kwa magoli 37-33 katika mchezo wa kuvutia uliochezwa katika viwanja vya Chinangali Park. Mchezo huo ulianza kwa kasi ya kawaida na kuendelea kushika kasi kadri muda ulivyokuwa ukisogea. Hadi mchezo unamalizika, Timu ya Ujenzi Queens iliikuba na ushindi wa magoli 37 dhidi ya 33 ya Dodoma Jiji. Awali Kocha wa Timu ya Mpira wa Pete ya Ujenzi Queens Mwamvita Mzee alisema kuwa wamekuwa wakipata matokeo mazuri kutokana na kufanya mazoezi mara kwa mara. “Timu yetu inaamini katika mazoezi ya mara kwa mara. Kama unavyofahamu mazoezi hayadanganyi, tumekuwa tukifanya mazoezi kwa bidii ndiyo siri ya mafanikio yetu. Zidi ni kupendana kama timu na watu kujitoa kwa ajili ya timu na kuupenda mchezo. Pia, kwetu ni utekelezaji wa maelekezo ya Mheshimiwa Rais wa Tanzania ya kufanya mazoezi kwa watumishi mahala pa kazi” alisema Mzee.   Kwa upa...

Ujenzi Queens bega kwa bega na Mwenge wa Uhuru, 2026 Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WIZARA ya Ujenzi inaunga mkono Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 utakaoanza mbio zake tarehe 1 Juni, 2026 katika Wilaya ya Dodoma kwa kushiriki katika mashindano ya Mwenge Super Cup yakilenga kuhamasisha jamii kujiandaa na mapokezi ya Mwenge huo kwa kudumisha amani na umoja wa kitaifa. Kocha wa Timu ya Wizara ya Ujenzi (Ujenzi Queens), Mwamvita Mzee Kauli hiyo ilitolewa na Kocha wa Mchezo wa Mpira wa Pete wa Timu ya Wizara ya Ujenzi (Ujenzi Queens), Mwamvita Mzee alipokuwa akiongea na mwandishi wetu muda mfupi kabla ya kuanza mchezo wao na Timu ya Mpira wa Pete ya Dodoma Jiji katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. Mzee alisema kuwa hamasa ya Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 kwa wanamichezo ni kubwa katika Wilaya ya Dodoma. “Sisi Timu ya Mpira wa Pete ya Wizara ya Ujenzi tumehamasika kuja kuunga mkono ujio wa Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 katika Wilaya ya Dodoma. Lengo ni kuonesha umoja na mshikamano baina ya wanamichezo kama dhamira ya Mwenge wa Uhuru Mwaka 2...

MIL. 544,335,626 ZAJENGA SHULE YA SEKONDARI MICHESE

Na. Dennis Gondwe, MKONZE SHILINGI 544,335,626 zimekamilisha ujenzi wa Shule ya Sekondari Michese na kuwawezesha wanafunzi 555 kupata elimu ya sekondari karibu na maeneo wanayoishi na kuwaondolea kero ya kutembea umbari mrefu kufuata elimu. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo alipokuwa akisoma taarifa ya ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari Michese kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya TAMISEMI iliyotembelea na kukagua ujenzi wa shule hiyo. Fungo alisema “k iasi cha fedha kilichotolewa kwa ajili ya ujenzi ni shilingi 544,225,626 chanzo cha fedha kikiwa ni SEQUIP. Fedha zilipokelewa Mwezi Oktoba, 2023 na ujenzi ulianza rasmi Mwezi Novemba, 2023 na kukamilika Mwezi Mei, mwaka 2024. Utaratibu wa ujenzi uliotumika ni force akaunti na mradi ulikamilíka kwa wakati na shule ilianza rasmi mwaka 2024 na kusajiliwa kwa jina la Michese Sekondari, Namba ya usajili S.6625”. Alisema kuwa u jenzi wa shule hiyo ulifanyika kwa awamu tatu, awamu ya kw...

JIJI LATEKELEZA MKAKATI WA KUBORESHA MAENEO YA WAZI

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma inatekeleza mkakati wa uboreshaji maeneo ya wazi kwa kusimamia udhibiti na usimamizi wa sheria na kufanya uondoaji wa maendelezo ya kudumu yaliyokiuka masharti na kuboresha miundombinu ya maeneo ya michezo. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo alipokuwa akisoma taarifa ya uboreshaji wa maeneo ya wazi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) iliyofanya ziara katika jiji hilo. Fungo alisema kuwa halmashauri ilifanya zoezi la mapitio ya hali ya maeneo ya wazi ili kubaini kama yanatumika kwa mujibu wa sheria. “Halmashauri inatekeleza mkakati wa u dhibiti na usimamizi wa sheria katika maeneo ya wazi, zoezi la uondoaji wa maendelezo ya kudumu yaliyokiuka masharti ya uendelezaji limefanyika katika eneo la wazi lililopo Majengo maarufu kama kwa Kato, eneo la Rose Garden na maeneo mengine 47 ambayo tayari wame...

JIJI LA DODOMA LATUMIA MIL. 23 KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imetumia zaidi ya shilingi milioni 23 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo fedha kutoka serikali kuu, mapato ya ndani na wahisani pamoja na bakaa. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo alipokuwa akiwasilisha taarifa fupi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI). Alisema kuwa katika kipindi cha kuanzia Julai, 2025 hadi kufikia Machi, 2026 halmashauri imetumia jumla ya shilingi 23,815,713,415.02 sawa na asilimia 91.19 ya fedha zilizopokelewa kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo. “Kati ya fedha hizo, shilingi 6,406,582,002.56 ni fedha kutoka serikali kuu, shilingi 16,807,859,627.46 mapato ya ndani, shilingi 601,771,785.00 fedha za wahisani na shilingi 5,279,467,344.52 ni fedha za bakaa. Kwa kipindi cha kuanzia Julai, 2025 hadi kufikia Machi, 2026, hal...