Posts
Huduma ya Lishe kwa Shule za Dodoma
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Stadi za Maisha Kuwa mkombozi kwa wanafunzi wa Sekondari jijini Dodoma
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Elimu ya Stadi ya Maisha imetajwa kuwa ni chachu ya mabadiliko chanya kwa wanafunzi katika kuwajengea uwezo wa kujitambua na kukabiliana na changamoto za maisha katika shule za sekondari jijini Dodoma. Hayo aliyasema Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Daniel Mapilya wakati akifungua mafunzo kwa wawezeshaji wa stadi za maisha katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Dodoma. Alieleza kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha wawezeshaji wanapata uelewa wa kutosha juu ya namna bora ya kuwafikia wanafunzi na kuwajengea misingi imara ya maisha. “Tunapozungumzia stadi za maisha, tunalenga kumsaidia mwanafunzi kujitambua, kujiamini na kufanya maamuzi sahihi. Elimu hii itawawezesha vijana wetu kuepukana na vishawishi vinavyoweza kuathiri masomo na mustakabali wa maisha yao” alisema Mapilya. Aliongeza kwa kusema kuwa changamoto nyingi zimekuwa zikiwakumba watoto wa kike. ”…zikiwemo shinikizo la rika na mazingira yasiyo rafiki, hivyo elimu hiyo it...
Utatuzi mgogoro wa Mahomanyika watangazwa
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Nancy Kivuyo , NZUGUNI Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeunda timu mbili ya wataalam wa upangaji na upimaji na timu ya uhakiki kwaajili ya kutatua mgogoro wa ardhi wa muda mrefu katika eneo la Mahomanyika. Timu hizo zimeundwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt. Leonard Akwilapo alipokuwa akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika eneo la Mahomanyika, Kata ya Nzuguni jijini Dodoma. Alisema kuwa timu hizo zitaanza kazi mara moja ili kuhakikisha zoezi hilo linakamilika kwa wakati. “Eneo la Mahomanyika ni la serikali kwahiyo , naagiza lipangwe na kupimwa kwaajili ya kutatua mgogoro huu na kuwa kielelezo cha utatuzi wa migogoro mingine iliyopo ndani ya Jiji la Dodoma. Timu hizi zinapaswa kufanya kazi ndani ya siku 60 na kukamilisha zoezi hili ili kila mmoja ajue amepata nini na anaenda wapi” alisema Dkt. Akwilapo. A liongeza kuwa wale wote waliohusika kwenye kadhia ya mgogoro huo wa ardhi watachukuliwa kwaajili ya maho...
Timu ya ‘sustainability’ ya Jiji la Dodoma yaanza semina ya siku saba
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Nancy Kivuyo , DODOMA Mafunzo maalum kuhusu viwango vipya vya uhasibu ‘ General Requirements for Disclosure of Sustainability-related Financial Information na Climate-related Disclosures’ (IFRS S1 na IFRS S2) yameanza rasmi kutolewa kwa timu ya ‘sustainability’ ikiwa ni sehemu ya mpango wa mafunzo ya uendelevu ‘sustainabilty and ESG’ yanayolenga kuwajengea uelewa na kuongeza ufanisi katika usimamizi wa taarifa za kifedha. Akizungumza wakati wa semina hiyo ya siku ya kwanza, Mratibu wa Mafunzo ya ‘sustainability’ katika Jiji la Dodoma, Akida Huddu alisema kuwa mafunzo hayo yamelenga kutoa elimu ya jumla ya uendelevu ‘sustainability and ESG’ kwa washiriki ili kuwawezesha kusimamia kwa ufanisi shughuli zote zinazohusiana na uendelevu pamoja na kupata taarifa zitakazosaidia kutoa huduma nzuri kwa wananchi. Aliongeza kuwa uelewa wa viwango vipya vya uhasibu ni muhimu katika kuimarisha uwazi, uwajibikaji na usimamizi bora wa rasilimali za umma, hususan katika mazingira yanayoh...
Wawezeshaji Stadi za Maisha watakiwa kuwa na nidhamu na uwajibikaji
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Wawezeshaji wa Stadi za Maisha katika Shule za Sekondari Jiji la Dodoma wametakiwa kuwa na nidhamu ya hali ya juu katika mazingira ya shule watakazopangiwa pamoja na kutumia mafunzo waliyoyapata kwa kuleta mabadiliko chanya kwa wanafunzi. Hayo yalisemwa na Mwezeshaji mafunzo y a Stadi za Maisha wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Tuvacal Mjema, wakati wa mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Dodoma jijini Dodoma. Alisema kuwa wawezeshaji wanapaswa kuwa mfano bora kwa wanafunzi kwa kuzingatia maadili, kuwajibika ipasavyo na kuonyesha weledi katika utekelezaji wa majukumu yao. “Ni muhimu kwa wawezeshaji kuwa na nidhamu ya hali ya juu wanapokuwa shuleni. Tunapaswa kuishi yale tunayowafundisha wanafunzi ili waweze kutuamini na kufuata miongozo tunayowapatia kwasababu ninyi ndio taa yao inayo waangazia” alisema Mjema. Lakini pia aliongezea kwa kusema kuwa mafunzo hayo yamelenga kuwaongezea uwezo wa kitaaluma na kisaikolojia wawezesh...
Jiji la Dodoma kuchangamkia fursa ujio wa Bandari Kavu Ihumwa
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Nancy Kivuyo, DODOMA MSTAHIKI Meya wa Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula apongeza Mkakati wa Uendelezaji Bandari Kavu na kuahidi kujipanga kuhakikisha wafanyabiashara wadogo wanapata fursa ya kufanya biashara katika eneo hilo na kuchochea ukuaji wa uchumi wa mkoa na taifa kwa ujumla. Akizungumza katika ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kwenye Bandari Kavu Ihumwa iliyokuwa na lengo la kujiridhisha na mkakati wa uendelezaji wa miundombinu hiyo, alisema kuwa uongozi wa jiji utakaa kikao na kutathmini namna ya kuandaa mazingira rafiki ya biashara ili kuwawezesha wajasiriamali wa ndani kushiriki kikamilifu katika shughuli za upokeaji, uhifadhi na usafirishaji wa mizigo. Alieleza kuwa pamoja na fursa za moja kwa moja zitakazotokana na shughuli za bandari hiyo, jiji pia linatarajia kuimarisha sekta ya usafirishaji, uhudumu na biashara ndogondogo hivyo kuongeza ajira na kipato kwa wananchi. Aidha, Mstahiki Meya Chaula aliongeza kuwa jiji litafanya utaratibu wa kufanya mazungumzo na Mam...
Shule ya Viziwi Dodoma yapokea msaada wa matendo ya huruma
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Emanuel Charles, DODOMA Shule ya Viziwi Dodoma yakabidhiwa msaada wa mahitaji muhimu ya kijamii yenye thamani ya shilingi 2,00,000 ikiwa ni sehemu ya matendo ya huruma yaliyoandaliwa na Dodoma Jiji Day kwa lengo la kuhimiza upendo, ushirikiano na mshikamano. Msaada huo ulikabidhiwa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri katika shule hiyo iliyopo Kisasa jijini Dodoma ambapo alikabidhi mchele, sukari, vifaa vya usafi na taulo za kike. Alisema kuwa ipo tha wabu ya utoaji na kuwajali watu wenye mahitaji maalum. “Kutoa siyo utajiri, ni moyo. Japokuwa tulichotoa kinaweza kuonekana kidogo kwa namna moja ama nyingine, lakini naamini kitaenda kuwasaidia watoto hawa, hasa katika kupata chakula shuleni na kuboresha mazingira yao ya kujifunzia” a lisema Alhaj Shekimweri . Aidha, aliipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa mpango wake wa kuibadilisha shule hiyo kuwa ya mchanganyiko ili kuwaunganisha watoto wenye mahitaji maalumu ya usikivu na wale wasio na changamoto, ha...
Watumishi wa Kanda Namba Tatu watembelea Zahanati ya Soweto
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Watumishi wa Kanda Namba Tatu watembelea Zahanati ya Soweto jijini Dodoma ambayo imekamilika na imeanza kufanya kazi. Zahanati hiyo inajumuisha jengo la huduma ya wagonjwa wa nje (OPD), chumba cha daktari, chumba cha kujifungulia wanawake, maabara na huduma ya mama, baba na mtoto. Uwepo wa zahanati hiyo ni kusogeza huduma karibu na wananchi ambao walikuwa wanatembea umbali mrefu kufuata huduma za afya katika Kituo cha Afya Zuzu au kwenda Hospitali ya Mkoa General
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipanda mti wa Muembe (Mangifera indica) katika eneo la Bungi Kilimo, Mkoa wa Kusini Unguja tarehe 27 Januari, 2026, wakati wa kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa. Rais Mhe. Dkt. Samia alizaliwa tarehe 27 Januari, 1960 katika Kijiji cha Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipanda mti wa Muembe (Mangifera indica) katika eneo la Bungi Kilimo, Mkoa wa Kusini Unguja tarehe 27 Januari, 2026, wakati wa kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa. Rais Mhe. Dkt. Samia alizaliwa tarehe 27 Januari, 1960 katika Kijiji cha Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.