Posts

Katibu Mkuu Uchukuzi aipa tano TASAC kwa kuendelea kuwafikia wadau

Image
Na. Immaculate Ruzika, DODOMA Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara, leo ametembelea banda la Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) katika maonesho yanayoendelea kwenye viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma.   Akiwa katika banda hilo, Prof. Kahyarara alipatiwa maelezo kuhusu juhudi za TASAC katika kuhakikisha usalama, ulinzi na ubora wa huduma za usafiri wa majini kwa wananchi. Akizungumza baada ya kutembelea banda hilo, Prof. Kahyarara aliipongeza TASAC kwa kushiriki maonesho hayo na kutumia jukwaa hilo kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu na huduma zake kwani elimu hiyo inasaidia kuongeza uelewa na kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi na wananchi. Maonesho hayo yenye kauli mbiu ya "Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu" yalianza rasmi tarehe 16 na yanataria kufika tamati kesho tarehe 23 juni, 2026.

Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali Inafanya Kazi Kubwa – Prof. Kahyarara

Image
Aipongeza Wizara ya Habari Maandalizi AFCON 2027 Na. Adelina Johnbosco - MAELEZO Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara, ameipongeza Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali na kusema inafanya kazi kubwa ya kuzitangaza shughuli zinazotekelezwa na Serikali pamoja na kuwafikia wananchi.   Prof. Kahyarara alisema hayo Juni 22, 2026, alipotembelea banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na taasisi zake katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kwenye viwanja vya Chinangali, jijini Dodoma. "Serikali ina shughuli nyingi zinazofanyika ikiwemo miradi mbalimbali, mipango na malengo kwa ajili ya maendeleo na maslahi ya wananchi, hata ukisema kila siku au kila wiki utoke na kitu kimoja lakini bado inakuwa haitoshi, lakini Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali inajitahidi kwa kufanya kazi kubwa kwani taarifa zinatolewa kuhusu yanayotekelezwa na Serikali kwa wananchi wake" aliongeza Prof. Kahyarara. Kwa upande mwingine, aliipongeza...

Zaidi ya wananchi 300 watembelea banda la TARURA Wiki ya Utumishi wa Umma

Image
# Wananchi wa Kimara kunufaika na ujenzi wa barabara ya TRA - King'ongo   Na. Mwandishi wetu, DODOMA ZAIDI ya wananchi 300 wametembelea banda la Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) tangu kuanza kwa Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, wakipata elimu na ufafanuzi kuhusu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya barabara za wilaya katika maeneo yao. Hatua hiyo imeendelea kuimarisha uhusiano kati ya wananchi na taasisi hiyo, huku ikitoa fursa ya kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi moja kwa moja. Akizungumza katika maonesho hayo, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma, Catherine Sungura alisema kuwa wananchi wanaowasilisha kero zao huunganishwa moja kwa moja na mameneja wa maeneo husika ili kupata maelezo ya kina na ufumbuzi wa haraka. “Tunawapokea wananchi wengi kutoka maeneo tofauti ya Tanzania ambao wengi wanataka kufahamu ujenzi au matengenezo ya barabara katika maeneo yao na hivyo wengi wao wanapata majibu hapo hapo kwani wan...

DG TANESCO atembelea Banda la EWURA CCC, apongeza utendaji kazi

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Lazaro Twange, amelipongeza Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA CCC), kwa mchango wake katika kupokea, kusaidia na kufuatilia utatuzi wa malalamiko ya watumiaji wa huduma za nishati na maji, hatua inayosaidia huduma zinazodhibitiwa na EWURA ikiwemo huduma ya umeme kuboreshwa kwa maslahi ya wananchi. Twange ametoa pongezi hizo leo, Juni 19, 2026, baada ya kutembelea banda la EWURA CCC katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. Akizungumza katika banda hilo, Twange amesema kazi inayofanywa na EWURA CCC ya kupokea, kusaidia na kufuatilia utatuzi wa malalamiko ya huduma za umeme imekuwa chachu ya maboresho ya huduma hiyo, ikiwemo kupungua kwa baadhi ya changamoto zilizokuwa zikilalamikiwa mara kwa mara. “Tunatambua mchango mkubwa wa EWURA CCC katika kuwawakikisha wananchi na kufuatilia utatuzi wa changam...

Waziri Mkenda: Michezo na Sanaa shuleni haitaondolewa tena

Image
Na. Denis Mlowe, IRINGA WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema serikali imejipanga kuhakikisha michezo na sanaa zinaendelea kupewa nafasi kubwa katika mfumo wa elimu nchini, akisisitiza kuwa shughuli hizo hazitaondolewa tena shuleni kwa kuwa ni sehemu muhimu ya kukuza vipaji, afya, ajira na ushindani wa kimataifa. Waziri Mkenda alitoa kauli hiyo wakati akifungua rasmi Mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) 2026 yaliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Lugalo mkoani Iringa. Katika hotuba yake, Waziri Mkenda aliushukuru Mkoa wa Iringa kwa kuwa mwenyeji wa mashindano hayo, akisema mkoa huo umeendelea kuwa kivutio kutokana na mazingira yake mazuri na ukarimu wa wananchi wake. “Tunafurahi sana kuja Iringa tunawashukuru viongozi na wananchi wote wa Iringa kwa kutupokea na kuwa wenyeji wa mashindano haya muhimu kwa maendeleo ya michezo nchini,” alisema. Aidha, aliwapongeza wanafunzi, walimu na viongo...

DCF Nzalayaimisi atembelea Banda Wizara ya Mambo ya Nje: Atoa pongezi

Image
Na. Charles Kuzenza, DODOMA Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Naibu Kamishna (DCF) Puyo Nzalayaimisi ametembelea Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa lengo la kujionea shughuli zinazofanywa na Wizara hiyo kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea Jijini Dodoma Juni 19, 2026. DCF Nzalayaimisi ameishukuru Wizara hiyo kwa kuendelea kuliunganisha Jeshi hilo na Mahusiano mbalimbali ya Kimataifa na Mashirika ya Nje ambapo Maafisa na Askari wameweza kufaidika na mafunzo mbalimbali. Chanzo: Fullshangwe Blog

Makala: Tanzania inavyojiandaa kuvuna matunda ya AFCON 2027

Image
Na. John Walter, Manyara Mwezi Juni mwaka 2027 utaingia kwenye historia ya Tanzania kwa maandishi yasiyofutika kirahisi. Kwa mara ya kwanza tangu kupata uhuru, Tanzania itakuwa mwenyeji wa mashindano makubwa zaidi ya soka barani Afrika, Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON), yatakayoandaliwa kwa ushirikiano wa nchi tatu za Afrika Mashariki; Tanzania, Kenya na Uganda. Kwa wengi, AFCON ni mashindano ya mpira wa miguu yanayodumu kwa siku 30 pekee. Lakini kwa wachumi, wawekezaji na wafanyabiashara wadogo, ni injini kubwa ya uchumi inayoweza kuingiza mabilioni ya fedha, kuzalisha ajira na kuitangaza Tanzania mbele ya mamilioni ya watu duniani. Tayari maandalizi yameanza kuonekana kupitia miradi mikubwa ya miundombinu inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini. Mkoa wa Arusha, ambao umetajwa kuwa miongoni mwa wenyeji wa mashindano hayo, unashuhudia ujenzi wa Uwanja wa Kisasa wa Samia Suluhu Hassan katika eneo la Olmot. Uwanja huo wenye uwezo wa kubeba mashabiki 30,000 umefikia z...

Ofisi ya Waziri Mkuu yathibitisha nyenzo muhimu za kuimarisha usimamizi wa maafa nchini

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   SERIKALI imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha mifumo ya usimamizi wa maafa nchini ili kuongeza uwezo wa kuzuia, kujiandaa, kukabiliana na kurejesha hali baada ya maafa, kufuatia kuongezeka kwa matukio yanayochochewa na mabadiliko ya tabianchi pamoja na vihatarishi vingine vya asili na kijamii.   Hayo yalielezwa jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Brigedia Jenerali Hosea Ndagala, wakati akifungua Kikao cha Jukwaa la Taifa la Wadau wa Usimamizi wa Maafa kilicholenga kupitia na kuthibitisha Mwongozo wa Urejeshaji Hali Baada ya Maafa, Mwongozo wa Uendeshaji na Uratibu wa Uhawilishaji Fedha kwa Walioathirika wa Maafa, pamoja na Mfumo wa Usimamizi wa Taarifa za Maafa (DMIS).   Brigedia Jenerali Ndagala alisema kuwa katika miaka ya hivi karibuni Tanzania imekumbwa na matukio mbalimbali ya maafa yakiwemo mafuriko, ukame, maporomoko ya ...