Wananchi Kata ya Chang’ombe wahimizwa kulinda miundombinu
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Wananchi wa Kata ya Chang’ombe watakiwa kuendelea kuitunza na kuilinda miradi ya maendeleo ili iweze kutoa huduma kwa muda mrefu na kuvinufaisha vizazi vya sasa na vijavyo. Hayo aliyasema Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Bakari Fundikira mara baada ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Kata ya Chang’ombe jijini Dodoma. Alisema kuwa serikali imeendelea kuwekeza fedha nyingi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo yenye lengo la kuboresha huduma za kijamii na kuinua ustawi wa wananchi. “Hivyo, ni wajibu wa kila mwananchi kushiriki katika kuilinda na kuitunza. Leo tumetembelea miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa Ofisi ya Mtaa wa Kishoka, Ofisi ya Mtaa wa Chang’ombe Juu, Ofisi ya Mtaa wa Hamvu, kisima cha maji Shule ya Msingi Chang’ombe na ujenzi wa Wodi ya Mama na Mtoto katika Kituo cha Afya Chang’ombe ambapo miradi hii imejengwa kwa fedha za serikali jumla ya shilingi 456,926,355. Lakini pia nitoe rai kuwa ni m...