Posts

LAAC yalipongeza Jiji la Dodoma kwa ubunifu wa Jengo Jumuishi Kituo cha Afya Makole

Image
Na. Mwandishi Wetu, VIWANDANI   Halmshauri ya Jiji la Dodoma imepongezwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kwa ubunifu wa kujenga jengo jumuishi la huduma za afya la ghorofa tatu katika Kituo cha Afya Makole lenye gharama ya shilingi bilioni 6.9 hatua inayolenga kutatua changamoto ya uhaba wa eneo na kukidhi ongezeko la mahitaji ya huduma za afya katika jiji hilo.   Pongezi hizo zilitolewa na Makamu Mwenyekiti wa (LAAC), Abdallah Chikota wakati wa ziara ya kamati hiyo ya kukagua miradi ya maendeleo Kata ya Viwandani Jiji la Dodoma.   Chikota alisema kuwa mfumo wa kujenga ghorofa ulikuwa ndio mbadala sahihi wa kukabiliana na changamoto ya uhaba wa eneo na kupanua huduma za matibabu, bila kulazimika kutafuta eneo jipya nje ya kituo hicho cha afya.   “Kwanza tunalipongeza Jiji la Dodoma kwa ubunifu wao na mawazo ya kisasa kwa sababu hapa Kituo cha Afya Makole kuna changamoto ya eneo, kwa hiyo ili kutatua tatizo hilo wameamu...

LAAC yaridhishwa, yalipongeza Jiji la Dodoma ujenzi wa Barabara ya KM 1.6

Image
Na. Maandishi wetu, NALA   Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imelipongeza Jiji la Dodoma kwa ukamilishaji wa barabara ya kiwango cha lami yenye urefu wa kilomita 1.6 inayoelekea Hospitali ya Jiji na kuufanya mradi huo kuwa wa kipekee ukilinganishwa na miradi iliyotekelezwa katika maeneo mengine.   Akizungumza wakati wa ziara ya kamati hiyo ya kukagua miradi ya maendeleo Makamu Mwenyekiti wa LAAC, Abdallah Chikota, alisema kuwa kamati imeridhishwa na ubora wa utekelezaji wa mradi huo uliogharimu shilingi bilioni 2.8 kwa kutumia mapato ya ndani ya Jiji la Dodoma.   Alisema kuwa uwekaji wa miundombinu ya usalama ikiwamo taa za barabarani ni hatua muhimu inayoongeza thamani ya mradi na kurahisisha wananchi kufika Hospitali ya Jiji wakati wowote. Aidha, uwekaji wa taa, mitaro na alama za barabarani umeboresha mpangilio na matumizi salama ya njia hiyo.   “Mradi umejengwa kwa kiwango ambacho tumeridhika. Pia, tumeridhishwa na hatu...

Kanda Namba Sita kushiriki Usafi wa mwisho wa Wiki tarehe 5 Septemba, 2026

Image
 

Watumishi wa Elimu watakiwa kuongeza tija kazini

Image
Na. Mwandishi wetu, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amewapongeza watumishi wa wizara hiyo kwa kazi kubwa na mafanikio waliyoyapata katika mwaka wa fedha uliopita, huku akiwataka kuendelea kuyasema kwa ujasiri mafanikio hayo yaliyoiwezesha sekta ya elimu kung’aa kitaifa na kimataifa.   Prof. Nombo alisema kuwa mafanikio hayo yametokana na uongozi imara wa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, na Naibu Waziri, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, pamoja na ushirikiano wa Wakurugenzi, Wakuu wa Idara na watumishi wote. Prof. Nombo alisema hayo jijini Dodoma wakati alipoongoza kikao cha tafakuri cha uongozi na watumishi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, kilicholenga kutathmini utekelezaji wa majukumu yaliyokabidhiwa kwa wizara. Aliwashukuru watumishi kwa utekelezaji mzuri wa majukumu yao na kusisitiza umuhimu wa kuendeleza ushirikiano katika kufikia malengo ya wizara. Aidha, Prof. Nombo alisema kuwa mabadiliko makubw...

Wazazi wahimizwa kufuatilia elimu na tabia za watoto nyumbani

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Wazazi wamehimizwa kuwa na ushirikiano wa karibu na walimu katika kufuatilia maendeleo ya watoto wao wanapokuwa nyumbani, ili kusaidia kukuza uwezo wao kitaaluma na kujenga msingi bora wa elimu, badala ya kutegemea walimu pekee katika jukumu hilo.   Wito huo ulitolewa na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Shekinah Pre & Primary School, Obadia Mwambapa wakati wa siku maalumu ya kufunga shule, ambapo alisema kuwa ushirikiano kati ya wazazi na walimu ni muhimu katika kuhakikisha watoto wanapata malezi na elimu bora.    Alisema kuwa wazazi wanapaswa kutenga muda wa kufuatilia masomo ya watoto wao, kujua changamoto wanazokutana nazo na kushirikiana na walimu katika kutafuta suluhisho.   Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa Shule hiyo, Juliana Sabrere alisema kuwa ulinzi na usalama wa watoto ni jukumu la pamoja kati ya walimu na wazazi, akisisitiza umuhimu wa kushirikiana katika kulinda maadili mema ya watoto na kuhakikisha wanakua kati...

Waziri wa Ulinzi na JKT akutana na vijana walioshiriki ujenzi wa Ikulu ya Chamwino

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Rhimo Nyansaho (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na wawakilishi wa vijana wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) walioshiriki katika ujenzi wa mradi wa kihistoria wa Ikulu ya Chamwino, jijini Dodoma.   Mazungumzo hayo yalilenga kuwasikiliza vijana hao, kuwapongeza na kuwashukuru kwa mchango wao mkubwa katika kutekeleza ujenzi wa Ikulu ya Chamwino, ambayo ni moja ya alama muhimu za Taifa na Ofisi ya Juu katika mfumo wa Utawala na Uongozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Akizungumza na vijana hao, Waziri wa Ulinzi na JKT, Dkt. Rhimo Nyansaho alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt. Samia Suluhu Hassan, inatambua na kuthamini mchango, uzalendo na kujituma kwa vijana hao katika utekelezaji wa mradi huo wa kihistoria. Dkt. Nyansaho alisema kuwa serikali inatambua uvumilivu, nidhamu na kujitolea kwa vijana hao, ambao walishirik...

Tanzania na Uingereza zakubali kuimarisha ushirikiano katika sekta ya Madini

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Marianne Young amekutana na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, kwa ajili ya mazungumzo kuhusu sekta ya madini nchini Tanzania na fursa za kuimarisha ushirikiano kati ya Uingereza na Tanzania. Mkutano huo ulijadili kuhusu uwekezaji, uongezaji wa thamani, na kuhakikisha sekta hiyo inachangia katika ukuaji wa uchumi unaoshirikisha wote.   Tanzania na Uingereza zitaendelea kushirikiana katika maeneo yenye manufaa kwa pande zote mbili ili kudumisha ustawi wa mataifa yote mawili.

Serikali yaweka Mkakati wa kukabiliana na madhara ya El Nino

Image
  Na. Okuly Julius, OKULY BLOG, DODOMA  SERIKALI imeandaa Mpango wa Taifa wa Dharura wa Kukabiliana na Madhara ya El Niño, huku ikikadiria kuwa inahitaji takribani Shilingi bilioni 730 kutekeleza hatua mbalimbali za kukabiliana na athari zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua kubwa zinazotarajiwa katika msimu wa Vuli 2026/27.   Akizungumza jijini Dodoma, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Prof. Palamagamba Kabudi alisema kuwa serikali imeandaa mpango huo kwa lengo la kuimarisha utayari na kuchukua hatua za mapema katika kuzuia, kujiandaa, kukabili na kurejesha hali baada ya madhara yanayoweza kusababishwa na El Niño.   Alisema kuwa mpango huo umeandaliwa kufuatia utabiri uliotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Agosti 18, 2026, uliotabiri uwepo wa hali ya El Niño yenye nguvu katika msimu wa Vuli 2026/27.   Kwa mujibu wa Prof. Kabudi, miongoni mwa hatua zilizopangwa na Serikali ni kukarabati na kub...

Serikali yafikisha Umeme katika maeneo 582 ya wachimbaji wadogo, kilimo na viwanda Tanzania bara

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Naibu Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imetekeleza Mradi wa Usambazaji Umeme katika maeneo 582 ya wachimbaji wadogo, kilimo na viwanda Tanzania Bara, kwa gharama ya shilingi bilioni 115.   Makamba aliyasema hayo bungeni jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mwanahamisi Athumani, Mbunge wa Viti Maalumu, aliyetaka kujua ni lini serikali itatekeleza Mpango Mkakati Maalumu wa kuhakikisha maeneo ya wachimbaji wadogo yanafikishiwa umeme wa kutosha kwa lengo la kupunguza gharama za uzalishaji.   Akijibu swali hilo, Makamba alisema kuwa mradi huo ulianza kutekelezwa Aprili, 2023 na kwa sasa umefikia hatua za mwisho za utekelezaji. Aidha, alisema kuwa Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na Wizara ya Madini inaendelea kuainisha maeneo ya kipaumbele yatakayofikishiwa huduma ya umeme katika hatua zinazofuata, kwa kuzingatia upatikanaji wa fedha.   Sambamba na hilo, alisema ...

NW. Salome: Wizara ya Nishati ina wajibu wa kuhakikisha wananchi wanapata Umeme wa uhakika

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Naibu Waziri wa Nishati, Salome Makamba amesema jukumu kuu la Wizara ya Nishati ni kuhakikisha wananchi wanapata umeme wa uhakika na wanapatiwa taarifa kwa wakati pindi changamoto zinapojitokeza. Makamba aliyasema hayo wakati akijibu swali la Exaud Kigahe, Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kaskazini aliyetaka kufahamu lini serikali itabadilisha mkataba wa usambazaji wa umeme kwa wananchi kutoka Mwenga Power kwenda TANESCO, ili Mwenga Power ibaki kuwa mzalishaji wa umeme. Akijibu swali hilo, Makamba alisema kuwa utoaji na usimamizi wa leseni za uzalishaji na usambazaji wa umeme nchini ni jukumu la kisheria la Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), kwa mujibu wa Sheria ya Umeme ya mwaka 2008 na taratibu za utoaji wa leseni hizo. “Jukumu namba moja la Wizara ya Nishati ni kuhakikisha wananchi wanapata umeme wa uhakika na wanapata taarifa kwa wakati kunapotokea changamoto,” alisema Makamba. Alieleza kuwa uamuzi wowote wa kubadili muundo wa leseni ya usa...