Silage suluhisho la uhaba wa chakula cha mifugo Dodoma
Na. Mwandishi wetu, NZUGUNI Wafugaji wa ng’ombe katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamehimizwa kuanza kutengeneza na kuhifadhi chakula cha mifugo kilichochachushwa (Silage) ili kuhakikisha mifugo inapata lishe ya kutosha wakati wa kiangazi, kipindi ambacho maeneo mengi hukumbwa na upungufu mkubwa wa malisho kutokana na ukame. Rai hiyo ilitolewa na Afisa Mifugo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Delila Mlamka wakati akiwaelezea wananchi waliotembelea banda la mifugo la halmashauri hiyo katika maonesho ya Nanenane yanayoendelea jijini hapa. Alisema kuwa Silage ni chakula kinachotengenezwa kwa kuchanganya majani mabichi yaliyokatwakatwa, kiasi kidogo cha majani makavu, pumba na molases, kisha kuhifadhiwa kwenye mazingira yasiyoruhusu hewa ya oksijeni kuingia kwa siku 21 ili kichachuke vizuri na kuwa salama kwa matumizi ya mifugo. Alisema kuwa chakula hicho kinaweza kutengenezwa kwenye mashimo au mapipa na kuhifadhiwa katika mifuko midogo ya plastiki na mifuko maalumu ya k...