Posts
Faini 300,000 wachafuzi wa Mazindira Dodoma
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
DC Shekimweri awatakia Heri ya Mtihani wanafunzi wa Darasa la Saba Dodoma
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Meya Chaula awatakia Heri Darasa la Saba Dodoma
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Taarifa kwa Umma kuhusu Mtihani wa PSLE Jiji la Dodoma
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Wananchi watakiwa kufanya usafi kila siku kuweka Dodoma safi
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Leah Mabalwe, DODOMA Wananchi na wafanyabiashara katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kufanya usafi kila siku katika maeneo yao badala ya kusubiri siku ya jumamosi ya mwisho wa wiki ili kuhakikisha mazingira yanakuwa safi, salama na rafiki kwa afya za jamii. Wito huo ulitolewa na Meneja Kanda Namba Moja, Nicholaus Mitembo mara baada ya kushiriki zoezi la usafi wa pamoja katika Soko la Miembeni Jijini Dodoma, ambapo amesisitiza kuwa usafi si jukumu la mamlaka pekee bali ni wajibu wa kila mwananchi na mfanyabiashara. Alisema kuwa msisitizo huo unatokana na kauli iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule katika kikao na Maafisa Mazingira pamoja na maafisa afya ambapo alisisitiza kuwa kufanya usafi siku ya Jumamosi pekee haitoshi. “Usafi wa Jumamosi pekee hautoshi. Kila mwananchi na mfanyabiashara ana wajibu wa kushiriki katika usafi kila siku. Niwasihi wananchi wote pamoja na wafanyabiashara tusisubiri siku ya Jumamosi pekee, bali tuwe tunafany...
Ukaguzi wa watumishi Kanda Namba Sita walenga kuboresha uwajibikaji na usimamizi wa rasilimali watu
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Zoezi la ukaguzi wa watumishi katika vituo vya kazi limefanyika katika Kanda Namba Sita, likilenga kuhakikisha uwepo wa taarifa sahihi za watumishi, kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili, pamoja na kuwakumbusha kuhusu umuhimu wa kujaza mfumo wa PEPMIS. Akizungumza kuhusu zoezi hilo, Afisa Utumishi Kanda, Jane Mwagalaba, alisema kuwa ukaguzi huo unahusisha kutembelea vituo vya kazi ili kuhakiki uwepo wa watumishi, kusikiliza changamoto zao na kupokea maoni yanayoweza kusaidia kuboresha mazingira ya kazi. “Zoezi hili linahusu ukaguzi wa watumishi katika vituo vya kazi, kusikiliza changamoto zao, kuchukua maoni, lakini pia kuwasisitiza kuhusu ujazaji wa PEPMIS,” alisema Mwagalaba. Alisema kuwa moja ya malengo makuu ya zoezi hilo ni kuwa na data sahihi za watumishi katika vituo vyao vya kazi, jambo ambalo ni muhimu katika kupanga na kusimamia rasilimali watu kwa ufanisi. Katika awamu ya kwanza, alisema kuwa zoezi hilo limewaleng...
Wafanyabiashara Soko la Miembeni Waazimia Kulinda Usafi
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Mohammed Ramadhani, DODOMA Wafanyabiashara wa Soko la Miembeni jijini Dodoma wameahidi kuendelea kuimarisha usafi wa mazingira katika maeneo yao ya biashara, wakieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kulinda afya na ustawi wa jamii. Akizungumza na waandishi wa habari, Katibu wa Soko la Miembeni, Adelgot Mbwani alisema kuwa uongozi wa soko unaendelea kuwahamasisha wafanyabiashara kufanya usafi mara kwa mara na kuhakikisha kila mmoja anawajibika kutunza mazingira yanayomzunguka katika eneo lake la biashara. Aliongeza kuwa juhudi hizo pia zinaendana na msisitizo wa serikali wa kuhakikisha miji na maeneo ya biashara yanakuwa safi, hivyo wafanyabiashara wataendelea kushiriki kikamilifu katika kampeni za usafi. “Tumekuwa tukiwahamasisha wafanyabiashara wetu kufanya usafi mara kwa mara na kuwasisitizia kuwa usafi ni jukumu lao katika maeneo yao ya kazi, kama ambavyo Mheshimiwa Rais anavyosisitiza kuwa majiji yote yawe safi,” alisema Mbwani. Kwa upande wake, Katibu wa Soko la Wauza ...
LAAC yaridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo jijini Dodoma
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Jesca Kipingu, DODOMA Kamati ya Hesabu za Mamlaka za Serikali za Mitaa (LAAC) imeridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma, huku ikipongeza juhudi zinazofanywa na Halmashauri kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa kuzingatia ubora, thamani ya fedha na mahitaji ya wananchi. Pongezi hizo zimetolewa leo na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya LAAC, Abdallah Chikota, wakati wa ziara ya kamati hiyo ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, ikiwemo ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami yenye urefu wa kilomita 1.6 inayoelekea Hospitali ya Jiji la Dodoma katika eneo la Nala pamoja na ujenzi wa jengo jumuishi katika Kituo cha Afya Makole, ambalo linajengwa kwa mfumo wa ghorofa. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Chikota aliipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa namna inavyotekeleza miradi hiyo, akieleza kuwa kamati imeridhishwa na matumizi ya fedha pamoja na ubora w...
Usafi wa Jumamosi, ni usafi wa kila siku
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amesisitiza wananchi kuacha dhana kwamba usafi wa mazingira ni jukumu la kufanyika siku ya Jumamosi pekee, akieleza kuwa usafi ni wajibu wa kila mwananchi na unapaswa kufanyika kila siku. Senyamule alitoa kauli hiyo jana wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini hapa, kilichowakutanisha maafisa watendaji wa kata, mitaa, wenyeviti wa mitaa, maafisa afya na maafisa mazingira kutoka Jiji la Dodoma, kwa lengo la kujadili utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu umuhimu wa kuhakikisha miji na maeneo ya makazi yanakuwa safi. Akizungumza katika kikao hicho, mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa utaratibu wa kufanya usafi wa mazingira kila Jumamosi umefutwa, akisisitiza kuwa wananchi wanapaswa kuufanya usafi kuwa sehemu ya maisha yao ya kila siku. “Nimefuta utaratibu wa kufanya usafi kila Jumamosi....