Posts

Kampeni ya Chanjo ya Polio kuwafikia watoto 207,096 jijini Dodoma

Na. Mwandishi wetu, DODOMA Wizara ya Afya kupitia Idara ya Kinga, Sehemu ya Elimu ya Afya kwa Umma, imewataka wananchi wa Jiji la Dodoma kujitokeza na kuwapeleka watoto wenye umri wa chini ya miaka 10 kupata chanjo ya matone ya Polio, ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kuongeza kinga dhidi ya ugonjwa huo. Akizungumza kuhusu kampeni hiyo, Magdalena Dinawi kutoka Wizara ya Afya, Idara ya Kinga, alisema kuwa chanjo ya Polio inayotolewa kwa njia ya matone ni muhimu katika kuzuia ugonjwa wa kupooza unaosababishwa na virusi vya Polio. Alisema kuwa ugonjwa huo hauna tiba, hivyo kinga kupitia chanjo ndiyo njia muhimu ya kumkinga mtoto dhidi ya madhara yanayoweza kusababishwa na Polio. “Chanjo hii ina umuhimu kwa watoto kwa sababu inazuia ugonjwa wa kupooza ambao kitaalamu tunauita Polio. Ugonjwa wa Polio hauna tiba, ila kinga iliyopo ni kwa kupewa matone ya chanjo ya Polio. Aidha, watoto wanatarajiwa kupata huduma hiyo katika vituo vya kutolea huduma za afya, shule, maeneo ya ibada, masoko,...

Mratibu wa Huduma za Chanjo Atoa Wito kwa Mabalozi Kushiriki Kampeni ya Chanjo ya Polio

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Mratibu wa Huduma za Chanjo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Victor Kweka amewataka mabalozi kushiriki kikamilifu katika kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa Kampeni ya Chanjo ya Polio, akisisitiza kuwa ushirikiano wa jamii ni muhimu katika kuhakikisha watoto wote wanapata chanjo kwa wakati.   Akizungumza na mabalozi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri, alisema kuwa wazazi na walezi wana wajibu mkubwa wa kuhakikisha kila mtoto anapatiwa chanjo kwa wakati, ili kuimarisha ulinzi dhidi ya ugonjwa wa Polio na kulinda kizazi cha sasa na kijacho.   Alisema kuwa mafanikio ya kampeni hiyo yanategemea ushiriki wa kila mmoja, hususan mabalozi ambao wana nafasi muhimu ya kufikisha ujumbe wa chanjo katika jamii na kuwahamasisha wazazi kuchukua hatua.   Aliwataka wazazi kutosubiri hadi mtoto aonekane mgonjwa, bali kuhakikisha anapata chanjo kwa kufuata ratiba iliyowekwa, kwa kuwa chanjo ni kinga muhi...

NGO's Dodoma zahimizwa kuanzisha miradi ya ili kuwa endelevu

Image
Na. Paulo Paulo, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma, kupitia Jukwaa la Mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGOs), limehimiza mashirika hayo kuanzisha miradi ya ndani ya kiuchumi ili kujitegemea kifedha badala ya kutegemea ufadhili wa nje pekee. ​ Akizungumza katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Afisa Tathimini na Ufuatiliaji kutoka Taasisi ya Reaching the Unreached Tanzania, Eliud Edward alisema kuwa ingawa fursa za kifedha zipo kwa wingi, upatikanaji wake unahitaji jitihada na mbinu za kimkakati kutoka kwa waombaji. ​ “Upatikanaji wa fedha kwa NGOs ni mchakato unaohitaji kujitoa kwa dhati. Pesa zipo nyingi sana, ila ili uzipate inategemea sana wazo la mradi wako,” alisema Edward. ​ Aliongeza kuwa ni muhimu kwa mashirika kuhakikisha wazo linalowasilishwa linakuwa endelevu na lenye ubunifu wa ndani ili kuweza kujitofautisha na waombaji wengine wanawania fursa hizo. ​ Kwa upande wake Katibu wa Shirika la Afya Ustawi Foundation, Dominica Kanje ...

NGO’s Wilaya ya Dodoma wahimizwa ushirikiano

Image
Na. Rahma Magona, DODOMA Mashirika yasiyo ya kiserikali wilayani Dodoma yameaswa kuimarisha ubia, ubunifu na matumizi ya vyanzo vya ndani vya rasilimali fedha ili kuongeza uendelevu wa shughuli zao na kutoa mchango zaidi katika maendeleo ya jamii. Rai hiyo ilitolewa katika mkutano wa Jukwaa la Mashirika Yasiyo  ya Kiserikali wilayani Dodoma uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, ambapo mgeni rasmi alikuwa mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Joan Mazanda ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya Halmashauri ya Jiji Dodoma. Akizungumza katika mkutano huo, alisema kuwa mashirika yasiyo ya kiserikali yanachangia katika kujenga ushirikiano na kuibua fikra endelevu zinazolenga kuimarisha maendeleo ya wananchi. Vilevile, aliongeza kuwa mashirika hayo yamekuwa yakitekeleza shughuli mbalimbali katika jamii, zikiwemo afua za afya na mazingira, pamoja na kutoa misaada kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu. Kwa upande wake mmoja w...

NGOs zatakiwa kuzingatia uwazi na uwajibikaji Dodoma

Image
Na. Manase Malima, DODOMA Mashirika yasiyo ya kiserikali wilayani Dodoma yamehimizwa kuzingatia uwazi na uwajibikaji katika utekelezaji wa shughuli na miradi yao ili kuongeza uaminifu na kuhakikisha rasilimali zinatumika kwa manufaa ya jamii. Akizungumza katika mkutano wa Jukwaa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mratibu na Msajili Msaidizi wa Mashirika yasiyo ya kiserikali wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Peter Mallya alisema kuwa, mashirika yanapaswa kuwa wazi katika utekelezaji wa shughuli zao na kuwajibika kwa wadau pamoja na jamii wanazozihudumia. Aliongeza kuwa uwazi katika utoaji wa taarifa, utekelezaji wa miradi na matumizi ya rasilimali ni muhimu katika kuimarisha uaminifu na ufanisi wa mashirika hayo. Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa Shirika la SAIKO SENTA (Psychology Sensitization Networking of Tanzania), Sylvia Siriwa alisema kuwa uwazi na uwajibikaji vinasaidia kujenga imani kati ya mashirika, wadau na jamii,...

NGOs zahimizwa kubuni vyanzo vya mapato kujiendesha

Image
Na. Lulu Luvanda Dodoma Mashirika yasiyo ya kiserikali   (NGO's) wilayani Dodoma yamehimizwa kuibua ubunifu katika utekelezaji wa shughuli zao kwa kuachana na utegemezi wa kifedha na ufadhili kutoka nje ya nchi na kuanzisha miradi itakayowezesha taasisi hizo kujitegemea kifedha na kujiendesha   wenyewe.   Ni katika kikao cha mwaka, cha wadau wa mashirika yasiyo ya kiserikali wilayani Dodoma kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri kikiwa na kaulimbiu isemayo ‘Fikra kuhusu uendelevu wa mashirika yasiyo ya kiserikali: ubunifu, ubia na upatikanaji wa rasilimali fedha kupitia vyanzo vya ndani’.   Akizungumza katika jukwaa hilo kuhusu ubunifu katika shughuli za mashirika hayo, Meneja wa Helvetas Tanzania, Abraham Mtongole alisema kuwa mashirika yanapaswa kufikiria nje ya mazoea ya kawaida na kubuni njia mbalimbali za kuongeza mapato ili kuendelea kuendesha miradi yao.   Mtongole alisema kuwa mashirika yanapaswa kutafuta vyanzo mbalimbali vya rasilimali...

TRA yatoa elimu ulipaji kodi kwa NGOs Dodoma

Image
Na. Muhamad Ahmed, DODOMA Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGOs) wilayani Dodoma yametakiwa kuzingatia wajibu wao wa ulipaji wa kodi na kuhakikisha yanakuwa na Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN), ikiwa ni sehemu ya kuimarisha uwajibikaji na uendeshaji wa shughuli zao kwa mujibu wa sheria. Msisitizo huo ulitolewa katika Jukwaa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Wilaya ya Dodoma leo katika ukumbi wa halmashauri na Afisa Usimamizi wa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Thomas Lengite wakati akiwasilisha mada isemayo ‘Ulipaji wa Kodi kwa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali na Upatikanaji wa TIN’. Alisema kuwa mada hiyo inawapa wadau wa NGOs fursa ya kupata uelewa kuhusu wajibu wao katika masuala ya kodi, pamoja na umuhimu wa kuwa na TIN katika kutambulika na kutekeleza shughuli zao kwa kuzingatia taratibu zinazotakiwa. Nae Mkurugenzi wa Taasisi ya Moses Mihayo Foundation, Moses Mihayo alisema kuwa amepata elimu na kufahamu namna ya kuweza kuweka mipango na mikakati ya kuendel...

Uendelevu wa NGOs wapatiwa msukumo wilayani Dodoma

Image
Na. Amoni Sambulila, DODOMA   Halmashauri ya Jiji la Dodoma kupitia Jukwaa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali imeendelea kutoa msukumo kwa mashirika hayo kuimarisha uendelevu wa shughuli na miradi wanayoitekeleza, ili kuhakikisha huduma zinazotolewa zinaendelea kuwa na manufaa kwa jamii kwa muda mrefu.   Akizungumza katika mkutano wa Jukwaa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Afisa Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Ester Erick alisema kuwa uendelevu wa mashirika hayo ni muhimu katika kuhakikisha miradi na huduma zinazotekelezwa kwa ajili ya wananchi zinaendelea kutoa matokeo chanya.   Alisema kuwa katika kipindi cha utekelezaji, jumla ya miradi 30 ilitekelezwa katika maeneo mbalimbali, ikiwemo afya, elimu, utunzaji wa mazingira, msaada wa kisheria pamoja na shughuli zinazohusisha Dawati la Jinsia.   “Jumla ya miradi 30 imetekelezwa katika maeneo ya afya, elimu, utunzaji wa m...

Mratibu wa Huduma za Chanjo Atoa Wito kwa Mabalozi Kushiriki Kampeni ya Chanjo ya Polio

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Mratibu wa Huduma za Chanjo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Victor Kweka amewataka mabalozi kushiriki kikamilifu katika kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa Kampeni ya Chanjo ya Polio, akisisitiza kuwa ushirikiano wa jamii ni muhimu katika kuhakikisha watoto wote wanapata chanjo kwa wakati.   Akizungumza na mabalozi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri, alisema kuwa wazazi na walezi wana wajibu mkubwa wa kuhakikisha kila mtoto anapatiwa chanjo kwa wakati, ili kuimarisha ulinzi dhidi ya ugonjwa wa Polio na kulinda kizazi cha sasa na kijacho.   Alisema kuwa mafanikio ya kampeni hiyo yanategemea ushiriki wa kila mmoja, hususan mabalozi ambao wana nafasi muhimu ya kufikisha ujumbe wa chanjo katika jamii na kuwahamasisha wazazi kuchukua hatua.   Aliwataka wazazi kutosubiri hadi mtoto aonekane mgonjwa, bali kuhakikisha anapata chanjo kwa kufuata ratiba iliyowekwa, kwa kuwa chanjo ni kinga muhi...

Dodoma yasisitiza Elimu nje ya mfumo rasmi

Image
Na. Rahma Magona, DODOMA Juma la Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi limefikia kilele leo katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma, huku serikali ikisisitiza umuhimu wa kuimarisha fursa za elimu kwa wananchi ambao hawakupata nafasi ya kusoma katika mfumo rasmi. Akizungumza katika maadhimisho hayo, mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ambae ni Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia elimu, Kiduma Mageni alisema kuwa serikali imeendelea kuwekeza katika uimarishaji wa miundombinu ya elimu ili kuhakikisha wananchi wanapata fursa ya kujifunza.   Alisema kuwa Mkoa wa Dodoma ulipokea zaidi ya shilingi bilioni 22 kwa ajili ya uimarishaji wa miundombinu ya elimu, hatua inayolenga kuhakikisha kila mwanafunzi anapata fursa ya kupata elimu katika mfumo rasmi.   Vilevile, wananchi ambao walishindwa kupata elimu katika mfumo rasmi bado wana nafasi ya kuendelea na masomo kupitia elimu nje ya mfumo rasmi kwa kutumia miundombinu iliyopo, aliongeza.   Kwa up...