Mwezi wa Maendeleo ya Jamii kufungua fursa za kiuchumi kwa Vijana Dodoma
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imesema itaendelea kufungua na kuwawezesha vijana kutumia fursa mbalimbali za kiuchumi na kijamii kupitia Mwezi wa Maendeleo ya Jamii, kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuwawezesha kujitegemea. Akizungumza kuhusu shughuli zitakazotekelezwa katika Mwezi wa Maendeleo ya Jamii, Afisa Vijana wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Ndulani alisema kuwa moja ya maeneo yatakayopewa kipaumbele ni kuwawezesha vijana kupata fursa za kiuchumi. Aliongeza kuwa fursa hizo ni pamoja na mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa wafanyabiashara wadogo, maarufu kama machinga. “Halmashauri pia itaendelea kutoa elimu ya ujasiriamali na stadi mbalimbali kwa vijana ili kuwajengea uwezo wa kutumia fursa zinazopatikana na kuendeleza shughuli zao za kiuchumi,” alisema Ndulani. Aliongeza kuwa Halmashauri itaendelea kutekeleza Sera ya Maendeleo ya Vijana pamoja na kuwaunga...