Posts

Mwezi wa Maendeleo ya Jamii kufungua fursa za kiuchumi kwa Vijana Dodoma

Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Halmashauri ya Jiji la Dodoma imesema itaendelea kufungua na kuwawezesha vijana kutumia fursa mbalimbali za kiuchumi na kijamii kupitia Mwezi wa Maendeleo ya Jamii, kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuwawezesha kujitegemea.   Akizungumza kuhusu shughuli zitakazotekelezwa katika Mwezi wa Maendeleo ya Jamii, Afisa Vijana wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Ndulani alisema kuwa moja ya maeneo yatakayopewa kipaumbele ni kuwawezesha vijana kupata fursa za kiuchumi.   Aliongeza kuwa fursa hizo ni pamoja na mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa wafanyabiashara wadogo, maarufu kama machinga.   “Halmashauri pia itaendelea kutoa elimu ya ujasiriamali na stadi mbalimbali kwa vijana ili kuwajengea uwezo wa kutumia fursa zinazopatikana na kuendeleza shughuli zao za kiuchumi,” alisema Ndulani.   Aliongeza kuwa Halmashauri itaendelea kutekeleza Sera ya Maendeleo ya Vijana pamoja na kuwaunga...

Maadhimisho ya Mwezi wa Maendeleo ya Jamii kutilia mkazo usafi Dodoma

Na. Lulu Luvanda, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeandaa kampeni ya kuhamasisha wananchi kuhusu umuhimu wa usafi katika Maadhimisho ya Mwezi wa Maendeleo ya Jamii yanayofanyika jijini Dodoma Mwezi Septemba, 2026 kwa lengo la kuimarisha ushiriki wa jamii katika kutunza mazingira. Akizungumza kuhusu maandalizi ya maadhimisho hayo Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Charity Sichouna, alisema kuwa   wananchi watapewa elimu ya namna ya kuchangia katika utunzaji wa mazingira bora kupitia tabia sahihi za kila siku. Alisema kuwa moja ya maeneo yatakayopewa kipaumbele ni usimamizi wa taka ngumu, ambapo wananchi wataelimishwa kuhusu namna ya kuzihifadhi na kuzitenganisha kulingana na aina zake kuanzia zinapozalishwa. Kwa mujibu wa Sichona kutenganisha taka katika chanzo kutarahisisha ukusanyaji na uendeshaji wa taka, huku taka zinazoweza kutumika tena zikipata nafasi ya kurejelewa badala ya kuishia katika maeneo yasiyokusudiwa. Alisema ku...

Mwezi wa Maendeleo ya Jamii kujikita kutoa elimu ya Bima ya Afya Dodoma

Na. Mwandishi wetu, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kuwa na bima ya afya, ikiwa ni sehemu ya shughuli zinazofanyika katika Mwezi wa Maendeleo ya Jamii. Akizungumza kuhusu elimu hiyo, Mratibu wa Mfuko wa Afya ya Jamii Iliyoboreshwa (iCHF) wa Jiji la Dodoma, Patrick Batimo, alisema kuwa wananchi wanapatiwa elimu kuhusu bima ya afya, ikiwemo Mfuko wa Afya ya Jamii Iliyoboreshwa (iCHF) pamoja na Bima ya Afya kwa Wote. “Elimu hiyo inalenga kuwawezesha wananchi kuelewa umuhimu wa bima ya afya na namna wanavyoweza kupata huduma za afya kupitia mifumo hiyo”, alisema Batimo.   Aliongeza kuwa wananchi wanapaswa kutumia fursa ya elimu inayotolewa ili kufahamu aina mbalimbali za bima ya afya, huduma zinazopatikana pamoja na umuhimu wa kuwa na bima wakati wanapohitaji matibabu. Aidha, utoaji wa elimu hiyo ni sehemu ya juhudi za Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuhakikisha wananchi wanafahamu huduma za bima ya afya na umuhimu wa ku...

Wananchi kupatiwa elimu ya fursa za kiuchumi na mikopo ya 7%

Na. Mwandishi wetu, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu fursa mbalimbali za kiuchumi na mikopo inayotolewa kupitia mifuko ya uwezeshaji wananchi kiuchumi, ikiwa ni sehemu ya shughuli za Mwezi wa Maendeleo ya Jamii, unaolenga kuwawezesha wananchi kujikwamua kiuchumi na kupunguza umaskini. Akizungumza kuhusu shughuli za uwezeshaji zinazotekelezwa katika kipindi hicho, Mratibu wa Dawati la Uwezeshaji na Kupunguza Umaskini, Hidaya Mizega alisema kuwa wananchi wanaendelea kupewa elimu kuhusu fursa mbalimbali za kiuchumi, namna ya kuzifikia na kuzitumia kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao. “Elimu hiyo pia inalenga kuwafahamisha wananchi kuhusu mikopo inayotolewa na halmashauri, ikiwemo mikopo yenye riba ya asilimia saba kwa wafanyabiashara wadogo maarufu kama machinga, ili kuwawezesha kukuza biashara zao na kuongeza kipato,” alisema Mizega. Aliongeza kuwa wananchi wanapaswa kutumia fursa hizo kwa maendeleo yao, huku akisisitiza umuhimu wa ...

Jiji la Dodoma laimarisha huduma za Kilimo na Mifugo

Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamepokea taarifa ya utekelezaji wa shughuli za kilimo na mifugo kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026, ikiwemo utoaji wa chanjo, utambuzi na usajili wa mifugo, ukaguzi wa nyama na ‘Agrovet’, pamoja na udhibiti wa visumbufu vya mazao.   Akizungumza katika Mkutano wa Mwaka wa Baraza la Madiwani, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Vincent Odero, alisema kuwa katika Mwaka wa Fedha 2024/2025 na 2025/2026, halmashauri ilitekeleza shughuli mbalimbali za kilimo na mifugo kwa lengo la kuongeza uzalishaji, kuimarisha usalama wa chakula na kuboresha huduma kwa wananchi.   Alisema kuwa shughuli hizo zilihusisha utoaji wa chanjo kwa mifugo, utambuzi na usajili wa mifugo kwa kutumia hereni za kielektroniki, uhamasishaji wa msimu wa kilimo pamoja na udhibiti wa wadudu na magonjwa katika mazao ya bustani na zabibu.   “Katika kipindi hiki, tumetekeleza shughuli mbalimbali za kilimo na mifugo kwa lengo la ...

Ufaulu Elimu Sekondari wapanda Jiji la Dodoma

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Ufaulu wa mitihani ya taifa kwa wanafunzi wa sekondari Jiji la Dodoma umeimarika kwa Mwaka 2025/2026, ambapo Division I, II na III zikiongezeka.   Hayo yameelezwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Vincent Odero wakati akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 katika Mkutano wa Mwaka wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa jiji hilo.   Alisema kuwa mwelekeo huo unaashiria maendeleo chanya katika sekta ya elimu ya sekondari, yakichangiwa na usimamizi mzuri wa elimu pamoja na juhudi kubwa za walimu katika kuboresha ufundishaji na kuongeza ufaulu wa wanafunzi.   “Wanafunzi waliofanya mtihani waliongezeka kutoka 6,526 Mwaka 2024/2025 hadi 7,104 Mwaka 2025/2026, huku ufaulu wa ‘Division’ I, II na III ukiongezeka na ‘Division’ 0 na IV ukipungua. Hii inaashiria mwelekeo chanya unaoendelea,” alisema Odero.   Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Viwandani, Swal...

Jiji la Dodoma laimarisha huduma za afya, vituo vyafikia 163

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Huduma za afya katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma zimeendelea kuimarishwa, huku vituo vikifikia 163 na watumishi wa afya wakiongezeka hadi 950 mwaka 2025/2026, kutoka 885 mwaka 2024/2025, hatua inayoongeza upatikanaji wa huduma kwa wananchi.   Hayo yameelezwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Vincent Odero wakati akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 katika mkutano wa Mwaka wa Baraza la Madiwani, ambapo madiwani walipokea taarifa hiyo.   Alisema kuwa jiji limeendelea kuimarisha huduma za afya kupitia vituo vya serikali, mashirika ya dini, umma na binafsi, huku idadi ya watumishi ikiongezeka kutoka 885 hadi 950 kati ya mwaka 2024/2025 na 2025/2026.   “Jiji la Dodoma lina jumla ya vituo vya kutoa huduma za afya 163, hospitali zikiwa tisa, kati ya hizo hospitali tano ni za serikali, mbili ni za watu binafsi na mbili ni za mashirika ya dini. Vituo vya afya vipo 15, kati ya hivyo...

CCTV Camera zaimarisha usalama Jiji la Dodoma

Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Ufungaji wa kamera za CCTV katika maeneo mbalimbali umeendelea kuimarisha usalama, utii wa sheria za barabarani na ulinzi katika Jiji la Dodoma, huku madiwani wakipokea taarifa ya utendaji kazi wa TEHAMA.   Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Vincent Oderо wakati akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 katika mkutano wa Mwaka wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa jiji hilo.   Alisema kuwa Mwaka wa Fedha 2024/2025, maeneo 35 yalipangwa kufungwa kamera za CCTV, ambapo manne yalifungwa na maeneo 31 yakabaki kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026, maeneo 31 yalipangwa kufungwa CCTV, ambapo 26 yamekamilika na maeneo matano bado hayajafungwa.   “Katika utekelezaji wa mifumo ya TEHAMA, kwa mwaka wa fedha 2024/2025, taasisi 287 kati ya 333 zilizopangwa zilifungiwa mifumo. Kwa mwaka wa fedha 2025/2026, taasisi 179 kati ya 227 zilizopangwa zimefungiwa m...

Madiwani Dodoma wapongeza ukusanyaji mapato na utekelezaji Bajeti ya 2025/2026

Image
Na. Tutindaga Nkwindi, DODOMA   Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma limepokea taarifa ya utendaji kazi wa halmashauri kwa mwaka wa Fedha 2025/2026, huku wajumbe wakipongeza juhudi za menejimenti katika ukusanyaji wa mapato na utekelezaji wa bajeti.   Akiwasilisha taarifa hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Vincent Odero alisema kuwa juhudi za ukusanyaji wa mapato zimeiwezesha halmashauri kutekeleza mipango na bajeti wake kwa ufanisi.   Kwa upande wake Mbunge wa Viti Maalum, Aisha Msantu alisema kuwa menejimenti ya halmashauri imefanya kazi kubwa katika kukusanya mapato na kuhakikisha yanatumika kutekeleza bajeti.   “Nawapongeza kwa kazi kubwa ya kukusanya mapato na kuvuka lengo pia mmehakikisha yanatumika ipasavyo kutekeleza bajeti ya halmashauri” alisema Msantu.   Nae Diwani wa Kata ya Ihumwa, Edward Magawa ameipongeza menejimenti kwa utekelezaji wa bajeti na kusisitiza umuhimu wa kusimamia vyanzo vya mapato, ikiwemo Soko...

GCU Jiji la Dodoma yapongezwa umahiri katika kuhabarisha Umma

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma limekipongeza Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kwa kazi nzuri ya kuhakikisha wananchi wanapata taarifa na habari kuhusu shughuli na utekelezaji wa majukumu ya halmashauri kwa wakati. Pongezi hizo zilitolewa na Diwani wa Kata ya Mnadani, Mugendi Kerenge wakati akichangia kwenye mkutano wa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kupokea na kuajdili taarifa ya utekelezaji wa kazi za halmashauri kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026, uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.   Kerenge aliwapongeza wataalam wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kwa namna walivyokuwa wakitekeleza majukumu yao ya kuhabarisha umma kuhusu shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na halmashauri.   “Nawapongeza wataalam wetu wa habari kwa namna wanavyofanya kazi nzuri ya kuhabarisha umma kwa wakati. Wananchi wamekuwa wakipata habari mbalimbali kutoka katika maeneo yao. Mfano, mimi habari za kata yangu zimeku...