IPSIS yawarahisishia madiwani Dodoma kufanya maamuzi
Na. Lulu Luvanda, DODOMA Mfumo wa Kimataifa wa Uandishi na Uwasilishaji wa Taarifa za Fedha (IPSIS) umeelezwa kuwa umepunguza ugumu wa uandishi na uchakataji wa taarifa za fedha katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, huku ukirahisisha uwasilishaji wa hesabu na kuwawezesha madiwani kufanya maamuzi kwa uelewa zaidi. Akizungumza wakati wa mkutano maalumu wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma ililofanyika katika ukumbi wa mikutano ya halmashauri Diwani wa Kata ya Miyuji, Ringo Iringo alisema kuwa mfumo huo ni muhimu kwa Jiji la Dodoma kutokana na shughuli nyingi za kiuchumi na miradi mbalimbali ya maendeleo na ongezeko la shughuli za kifedha zinazohitaji usimamizi madhubuti. Alisema kuwa mfumo wa IPSIS umeleta urahisi katika uandishi na uwasilishaji wa taarifa za kifedha, pamoja na kufanya mchakato wa kuchakata taarifa kuwa mwepesi na hivyo kusaidia viongozi kupata taarifa zinazoweza kuwa msingi wa kufanya maamuzi kwa wakati. “Kwa sababu hiyo, IPSIS ni ...