LAAC yalipongeza Jiji la Dodoma kwa ubunifu wa Jengo Jumuishi Kituo cha Afya Makole
Na. Mwandishi Wetu, VIWANDANI Halmshauri ya Jiji la Dodoma imepongezwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kwa ubunifu wa kujenga jengo jumuishi la huduma za afya la ghorofa tatu katika Kituo cha Afya Makole lenye gharama ya shilingi bilioni 6.9 hatua inayolenga kutatua changamoto ya uhaba wa eneo na kukidhi ongezeko la mahitaji ya huduma za afya katika jiji hilo. Pongezi hizo zilitolewa na Makamu Mwenyekiti wa (LAAC), Abdallah Chikota wakati wa ziara ya kamati hiyo ya kukagua miradi ya maendeleo Kata ya Viwandani Jiji la Dodoma. Chikota alisema kuwa mfumo wa kujenga ghorofa ulikuwa ndio mbadala sahihi wa kukabiliana na changamoto ya uhaba wa eneo na kupanua huduma za matibabu, bila kulazimika kutafuta eneo jipya nje ya kituo hicho cha afya. “Kwanza tunalipongeza Jiji la Dodoma kwa ubunifu wao na mawazo ya kisasa kwa sababu hapa Kituo cha Afya Makole kuna changamoto ya eneo, kwa hiyo ili kutatua tatizo hilo wameamu...