Posts

JIJI LA DODOMA LAITANDIKA CHAMWINO DC 38-9 MPIRA WA PETE SHIMISEMITA

Na. Mwandishi wetu, MBEYA   Timu ya Wanawake ya Mpira wa Pete ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeitandika Timu ya Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino magoli 38-9 ikiwa ni muendelezo wa juhudi zake za kufukuzia ubingwa katika mashindano ya SHIMISEMITA yanayoendelea jijini Mbeya.   Akizungumzia mchezo huo, Afisa Michezo wa Jiji la Dodoma, Neema Kilongola mara baada ya mchezo huo kutamatika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Mbeya alisema kuwa timu yake imejipanga kushindana. Alisema kuwa timu hiyo inaendelea vizuri katika mashindano hayo na anaamini kuwa ubingwa wa SHIMISEMITA bado utaendelea kubaki mikononi mwao. “Tunaendelea vizuri na mashindano. Tunaamini ubingwa bado utabaki kwetu kwa sababu sisi ndio mabingwa wa mashindano haya. Hivyo, tunataka kuhakikisha tunautetea ubingwa wetu” alisema Kilongola.   Aliongezea kuwa ushindi wa magoli 38–9 umeipa Halmashauri ya Jiji la Dodoma mwanzo mzuri wa kampeni yake ya kutetea ubingwa, huku matarajio yakiongezeka kwa...

Dodoma CC 2 - 0 Siha DC (SHIMISEMITA Volleball Wanaume)

Image
 

Dodoma CC 8-1 Mkuranga DC (SHIMISEMITA Hand Ball Wanaume)

Image
 

Dodoma CC 9-1 Mbulu DC (SHIMISEMITA Hand Ball Wanawake)

Image
 

Dodoma CC 1-1 Sumbawanga DC (SHIMISEMITA Football Wanaume)

Image
 

Ukarabati Soko Kuu Majengo wafikia 80%

Image
Ukarabati wa Soko la Majengo umefikia asilimia 80 ya utekelezaji, hatua inayoashiria kuwa mradi huo unakaribia kukamilika na kuanza kutoa huduma zilizokusudiwa kwa wananchi na wafanyabiashara. Mradi huo wenye thamani ya shilingi bilioni 4.8 unalenga kuboresha mazingira ya soko, kuimarisha miundombinu na kuongeza ufanisi wa shughuli za biashara kwa wafanyabiashara na wananchi. Ukarabati huo unatarajiwa kuongeza usalama, usafi na mvuto wa soko, sambamba na kutoa mazingira bora zaidi ya biashara na kuchochea shughuli za kiuchumi katika eneo hilo.

Chuo Kikuu Huria chaungamkono kaulimbiu ya Kisomo kwa manufaa ya jamii

Image
Na. Rahma Magona, DODOMA   Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kimeeleza namna kinavyotekeleza kaulimbiu ya Maadhimisho ya Juma la Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi kupitia programu mbalimbali zinazolenga kuwapatia wanafunzi maarifa na ujuzi wenye manufaa kwa watu, dunia na ustawi wa jamii. Maelezo hayo yalitolewa leo tarehe 18 Agosti, 2026 katika maadhimisho ya Juma la Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi yanayofanyika katika Viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma. Akizungumza katika banda la Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Afisa Udahili wa Chuo Kikuu Huria Tawi la Dodoma, Eliud Asajile alisema kuwa chuo hicho kinakwenda sambamba na kaulimbiu ya maadhimisho hayo kupitia programu zinazolenga kuandaa wanafunzi wenye uwezo wa kukidhi mahitaji ya jamii. “Tuna programu kama ‘Certificate in Social Work’ inayotekeleza kaulimbiu ya ‘Kisomo kwa Manufaa ya Watu, Dunia na Ustawi wa Jamii’, kwa kumpa mwanafunzi maarifa ya kuwasiliana na jamii, kutambua mahitaji yak...

Elimu changamani yawawezesha vijana walio nje ya mfumo rasmi wa elimu

Image
Na. Amoni Sambulila, DODOMA Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino kupitia mpango wa Elimu Changamani kwa Vijana Walio Nje ya Mfumo Rasmi wa Elimu (IPOSA) inaendelea kuwawezesha vijana waliokumbwa na changamoto mbalimbali na kushindwa kuendelea na masomo katika mfumo rasmi wa elimu, kwa kuwapatia elimu, ujuzi wa ujasiriamali na ufundi stadi. Akizungumza kuhusu mpango huo, Afisa Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi, wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, Annamaria Kidunda alisema kuwa IPOSA huwapa vijana walio nje ya mfumo rasmi wa Elimu fursa ya kupata ujuzi wa ujasiriamali na ufundi stadi, ikiwemo ushonaji wa nguo, unaowasaidia kujitegemea na kukabiliana na changamoto za maisha. Alisema hayo leo, Jumanne, tarehe 18 Agosti, 2026 katika muendelezo wa maadhimisho ya Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi, yanayofanyika Nyerere Square, Jijini Dodoma. Kwa upande wake Maria Jofrey, mmoja wa wanufaika wa IPOSA, alisema kuwa mpango huo umemsaidia kupata ujuzi mbalimbali ...

Vijana watakiwa kujiendeleza nje ya mfumo rasmi

Image
Na. Lulu Luvanda, DODOMA Jamii imetakuwa kuwahamasisha vijana waliokosa elimu katika mfumo rasmi kujiunga na Mpango wa Elimu Changamani kwa Vijana walio nje ya shule nchini Tanzania (IPOSA) ili kupata fursa ya kujiendeleza kielimu nje ya mfumo rasmi. Akizungumza katika maadhimisho ya Juma la Elimu ya Watu wazima na nje ya mfumo rasmi yanayofanyika katika viwanja vya Nyerere square, Afisa Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi wa Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, Annamaria Kidunda, alisema kuwa IPOSA inalenga kuwapa fursa vijana na wanafunzi ambao walishindwa kuendelea na mfumo rasmi wa elimu kupata nafasi nyingine ya kupata elimu nje ya mfumo rasmi. Kwa mujibu wa Kidunda, IPOSA ni darasa linalowahusisha wanafunzi waliokatisha masomo au kushindwa kuendelea na mfumo rasmi wa elimu, kwa kuwawezesha kupata elimu na mafunzo yatakayowasaidia kukabiliana na mahitaji ya maisha ya sasa. Alisema kuwa programu hiyo inalenga kuondoa pengo katika elimu kwa kuwapatia wa...

Tunduma yalala Seti 2-0 kwa Dodoma CC

Image
  Halmashauri ya Dodoma la Jiji iliendeleza kasi kwenye mchezo wa Mpira wa Wavu kwa Wanaume, ikiichapa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduma kwa seti 2-0. Seti ya kwanza ilimalizika kwa 25-1, kabla ya Dodoma Jiji kushinda seti ya pili kwa 25-7 katika Michezo ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa Tanzania (SHMISEMITA) inayoendelea jijini Mbeya.