Posts

Jiji la Dodoma Biashara saa 24, usafi saa 24

Image
  Na. Mwandishi wetu, MSALATO   Wananchi wa Jiji la Dodoma wametakiwa kuendesha biashara saa 24 huku wakihakikisha usafi wa mazingira unafanyika muda wote, ili huduma ziendelee kupatikana bila kuathiri usafi wa maeneo yao.   Rai hiyo imetolewa wakati wa Uzinduzi wa Kampeni Endelevu ya Usafi wa Mazingira katika eneo la Mnada wa Msalato, jijini Dodoma, ambapo ilisisitizwa kuwa dhana ya “biashara saa 24” inapaswa kwenda sambamba na “usafi saa 24.”   Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alisema kuwa maafisa afya pamoja na watendaji wa kata na mitaa watakuwa wakifanya ukaguzi wa mara kwa mara katika maeneo ya biashara ili kuhakikisha usafi unazingatiwa muda wote.   “Biashara masaa 24, lakini usafi masaa 24. Maafisa afya, watendaji wa kata na mitaa watakuwa wakipita kufanya ukaguzi, na atakayekaidi maelekezo ya usafi atatozwa faini ya shilingi 50,000 hadi shilingi 300,000,” alisema Alhaj Shekimweri. ...

Mvua za El Nino: DC Shekimweri awaasa wananchi wa Dodoma Kuchukua Tahadhari

Image
Na. Mwandishi wetu, NZUGUNI   Wananchi wanaoishi katika maeneo hatarishi wametakiwa kuchukua tahadhari mapema dhidi ya mvua za El Nino, ikiwemo kuepuka maeneo yanayoweza kukumbwa na mafuriko na kuhakikisha usalama wa familia zao.   Akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi wa bwawa la kuvunia maji ya mvua katika viwanja vya Dkt. John Malecela (Nanenane), Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alisema kuwa wananchi wanaoishi katika maeneo hatarishi wanapaswa kuzingatia tahadhari zinazotolewa na mamlaka.   Alisema kuwa wananchi wanaoishi mabondeni, karibu na mito na maeneo yanayoweza kuathiriwa na mafuriko wanapaswa kuwa makini na kuchukua hatua mapema ili kuepusha madhara yanayoweza kusababishwa na mvua kubwa.   Aidha, aliwataka wananchi kuhakikisha mifereji na njia za maji hazizibwi kwa taka, akieleza kuwa hali hiyo inaweza kuzuia mtiririko wa maji na kuongeza uwezekano wa kutokea kwa mafuriko katika maeneo ya makazi.   Katika ziara hiyo, ...

Wananchi Kata ya Msalato wapongezwa kujitokeza kwa wingi uzinduzi wa Kampeni ya Usafi wa Mazingira Dodoma

Image
Na. Amoni Sambulila, MSALATO Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri amewapongeza na kuwashukuru wananchi kwa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika uzinduzi wa Kampeni ya Usafi wa Mazingira mkoani Dodoma, uliofanyika katika eneo la Mnada wa Msalato, Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Alhaj Shekimweri alisema kuwa ushiriki wa wananchi unaonesha umuhimu wa jamii kushirikiana katika kutunza mazingira na kuhakikisha maeneo yanayowazunguka yanakuwa safi na salama. Aliongeza kwa kuwataka wananchi kuendelea kufanya usafi katika maeneo yao na kushiriki kikamilifu katika shughuli za usafi ili kuimarisha afya na ustawi wa jamii. Kwa upande wake, mwananchi wa Kata ya Msalato, Amani Merick alisema kuwa kampeni hiyo ni muhimu katika kuhamasisha jamii kuwa na utamaduni wa kutunza mazingira na kuzingatia usafi katika maeneo wanayoishi na kufanyia shughuli zao. Nae, mkazi wa Dodoma, Hadija Yusuf aliwataka wananchi kuendeleza ushiriki wao kat...

Wananchi Dodoma wahimizwa kufanya usafi wa Mazingira kila siku

Image
Na. Amoni Sambulila, MSALATO Wananchi mkoani Dodoma wamehimizwa kufanya usafi   wa mazingira kila siku na kuhakikisha mazingira yanayowazunguka yanakuwa safi na salama kwa afya na ustawi wa jamii. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Usafi wa Mazingira mkoani Dodoma, uliofanyika katika eneo la Mnada wa Msalato, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyemule alisema kuwa kufanya usafi ni wajibu wa kila mwananchi na si jukumu la taasisi au mamlaka pekee. Aliongeza Kwa kuwataka wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za usafi, kutunza maeneo yao na kuendelea kuzingatia usafi wa mazingira katika maisha yao ya kila siku. Kwa upande wake, mwananchi wa Msalato, Juma Ally alisema kuwa ushiriki wa jamii ni muhimu katika kuhakikisha kampeni hiyo inakuwa na matokeo chanya na kuleta mabadiliko katika maeneo mbalimbali. Nae, mwananchi wa Msalato, Neema Ramadhani aliwahimiza wananchi kufanya usafi kuwa sehemu ya maisha yao ya kila siku, ikiwemo kutunza maeneo ya makazi na maene...

Wafanyabiashara Mnada wa Msalato waahidi kudumisha usafi

Image
Na. Mwandishi wetu, MSALATO   Wafanyabiashara na wakazi wa Kata ya Msalato wameiomba serikali kuendeleza kampeni za usafi wa mazingira na kuongeza vifaa pamoja na matunzio ya taka katika maeneo yao ili kuboresha mazingira.   Wananchi hao wametoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi wa Kampeni Endelevu ya Usafi wa Mazingira uliofanyika katika Mnada wa Msalato, Jiji la Dodoma, yenye kaulimbiu ‘Dodoma Fahari Yetu, Usafi Wajibu Wetu’ uliofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule.   Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mwenyekiti wa Mtaa wa Senje, Kata ya Msalato, Jackson Chaula alisema kuwa wananchi wamehamasika kushiriki shughuli za usafi bila kujali umri, huku akiwataka kuendeleza utamaduni huo katika maeneo yao ya makazi na biashara kila siku.   “Vijana na wazee wote nawaomba tuendelee kuhamasika kufanya usafi kila siku, tuweke vitunzia taka majumbani na kuhakikisha maeneo yetu ya makazi na biashara yanatunzwa vizuri muda wote. Kwa kufanya hivyo, tuta...

Soko la Mnada mpya wapangwa wafanyabiashara 150

Image
Na. Mwandishi wetu, KIZOTA   Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeendelea kuboresha Soko la Mnada Mpya lililopo Kata ya Kizota, kwa kufanya ukarabati wa barabara na kuwapangia wafanyabiashara wadogo maeneo ya kufanyia biashara ndani ya soko hilo, hatua inayolenga kuweka mazingira bora na yenye utaratibu. Akizungumza kuhusu zoezi hilo, Afisa Biashara wa Kanda Namba Tatu, Halmashauri ya Jiji la Dodoma Stephen Maufi alisema kuwa halmashauri imewapangia wafanyabiashara maeneo kulingana na aina ya biashara zao, zikiwemo samaki, matunda na mbogamboga, mishikaki, kuku na viazi. Alisema kuwa zaidi ya wafanyabiashara 150 wamepangiwa maeneo ndani ya soko hilo.   Maufi alisema kuwa awali wafanyabiashara wapatao 55 walikuwa wakifanya biashara nje ya eneo la soko, hivyo zoezi hilo limefanyika kuwaingiza ndani ya soko na kuhakikisha shughuli za biashara zinafanyika katika maeneo yaliyotengwa.   Alisisitiza kuwa maeneo hayo yametolewa bure kwa ajili ya kufanyia biashara na si kw...

Wafanyabiashara Sabasaba watakiwa kujitokeza kupata elimu ya mikopo ya 10%

Na. Leah Mabalwe, DODOMA Wafanyabiashara katika Soko la Sabasaba jijini Dodoma wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika ofisi ya soko hilo kwa ajili ya kupata elimu na uelewa kuhusu utaratibu wa upatikanaji wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa makundi mbalimbali ya wananchi. Hayo yalisemwa na Afisa Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Peter Mallya wakati alipofika katika Soko la Sabasaba kwa ajili ya kutoa huduma mbalimbali zinazohusiana na maendeleo ya jamii, ikiwemo kutoa elimu kwa wafanyabiashara kuhusu fursa ya mikopo hiyo katika Mwezi wa Maendeleo ya Jamii. Alisema kuwa katika kuadhimisha Mwezi wa Maendeleo ya Jamii, Maafisa Maendeleo ya Jamii wameamua kuwafuata wananchi katika maeneo yao badala ya kusubiri wananchi wafike ofisini, hatua inayolenga kuhakikisha taarifa na elimu kuhusu fursa mbalimbali zinawafikia wananchi wengi zaidi. “Kupitia Mwezi huu wa Maendeleo ya Jamii, sisi kama Maafisa Maendeleo ya Jamii tumeamua ...

Habitat for Humanity yaunga mkono usafi Soko la Sabasaba

Image
Na. Mohammed Ramadhani, DODOMA Shirika la Habitat for Humanity Tanzania limeunga mkono juhudi za kuimarisha usafi katika Soko la Sabasaba jijini Dodoma kwa kutoa vifaa mbalimbali vitakavyotumika katika shughuli za usafi wa mazingira. Mratibu wa shirika hilo, Elnoth Lekaaya alisema kuwa wameweza kushirikiana na wadau wa maendeleo pamoja na Jiji la Dodoma katika kuhakikisha suala la usafi linafanyika kwa ufanisi katika maeneo ya jamii. Alisema kuw kupitia ushirikiano huo, shirika limechangia vifaa vya usafi vyenye thamani ya shilingi milioni moja, vikiwemo mifagio, reki, toroli na vifaa vingine mbalimbali. Lekaaya alisema kuwa msaada huo unalenga kuwawezesha wafanyabiashara na wadau wengine kushiriki kikamilifu katika kutunza mazingira ya soko, ili wananchi wanaofika kwa shughuli mbalimbali waweze kupata mazingira safi na salama. Aliongeza kuwa Habitat for Humanity Tanzania inatekeleza shughuli zake katika maeneo mbalimbali yanayolenga kuboresha maisha ya jamii, ikiwemo masuala ya ...

RC Dodoma amtaka Mkandarasi kuongeza kasi ukarabati Soko la Majengo

Image
Na. Mohammed Ramadhani, MAJENGO Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amemtaka mkandarasi anayetekeleza ukarabati wa Soko la Majengo jijini Dodoma kuongeza kasi ya kazi ili kukamilisha mradi huo ndani ya muda wa nyongeza wa siku 60 uliotolewa. Senyamule alitoa kauli hiyo wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ukarabati wa Soko la Majengo, akieleza kuwa soko hilo lina mchango mkubwa katika kutoa huduma na kukidhi mahitaji ya wananchi wa Jiji la Dodoma. Akizungumza baada ya kukagua maendeleo ya mradi huo, mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa utekelezaji wa kazi unaelekea vizuri, lakini mkandarasi anapaswa kutumia kikamilifu muda wa nyongeza aliopewa ili kuhakikisha kazi zilizobaki zinakamilika kwa wakati. Aidha, alishauri kuwa mkandarasi kuongeza muda wa utekelezaji wa kazi kwa kufanya kazi hadi nyakati za usiku kwa kutumia taa, akisema hatua hiyo itasaidia kuongeza kasi ya ujenzi na kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati. Alisisitiza umuhimu wa kukamilisha kazi kabla ya kuanza k...

Usafi Soko la Sabasaba watakiwa kufanyika kila siku

Image
Na. Mohammed Ramadhani, DODOMA Diwani wa Kata ya Viwandani, Swalihina Athuman amewataka viongozi na wafanyabiashara katika Soko la Sabasaba jijini Dodoma kuimarisha usimamizi wa usafi wa mazingira, akisisitiza kuwa usafi wa soko hilo unapaswa kuwa jukumu la kila siku kutokana na umuhimu wake kwa shughuli za biashara na afya za wananchi. Athuman alitoa kauli hiyo wakati akizungumza kuhusu hali ya usafi katika Soko la Sabasaba, akieleza kuwa soko hilo ni miongoni mwa masoko makubwa yanayohudumia wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Jiji la Dodoma, hivyo linahitaji usimamizi madhubuti wa mazingira ili kuhakikisha shughuli za biashara zinafanyika katika mazingira salama. Diwani huyo alisema kuwa mazingira ya soko hilo yana mchango mkubwa katika ustawi wa wafanyabiashara na wateja, hivyo kila mmoja anapaswa kutambua wajibu wake katika kuhakikisha taka zinadhibitiwa na maeneo ya biashara yanakuwa safi wakati wote. “Tusipokuwa makini kuzingatia usafi katika Soko la Sabasaba na maeneo me...