Jiji la Dodoma lavuna Tuzo Tano Nanenane, 2026
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeibuka kidedea katika Maonesho ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ya Nanenane Kitaifa 2026 baada ya kutwaa tuzo tano, hatua inayoonesha mafanikio makubwa ya jiji hilo katika kuendeleza sekta za kilimo, mifugo na uvuvi. Maonesho hayo yaliyofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela jijini Dodoma na kuhitimishwa Agosti 8, 2026 yaliwakutanisha washiriki mbalimbali kutoka maeneo tofauti ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kuonesha ubunifu, teknolojia na fursa zilizopo katika sekta za uzalishaji. Katika maonesho hayo, Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilitwaa nafasi ya kwanza katika makundi ya Kilimo Ndani ya Uwanja, Mifugo Ndani ya Uwanja na Malisho Ndani ya Uwanja kwa upande wa Kanda ya Kati. Aidha, jiji hilo lilipata nafasi ya pili katika kundi la Ufugaji Samaki katika Maonesho ya Ndani ya Uwanja Kanda ya Kati na kutunukiwa tuzo maalum (trophy) iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa T...