Posts

Habitat for Humanity yaunga mkono usafi Soko la Sabasaba

Na. Mohammed Ramadhani, DODOMA Shirika la Habitat for Humanity Tanzania limeunga mkono juhudi za kuimarisha usafi katika Soko la Sabasaba jijini Dodoma kwa kutoa vifaa mbalimbali vitakavyotumika katika shughuli za usafi wa mazingira. Mratibu wa shirika hilo, Elnoth Lekaaya alisema kuwa wameweza kushirikiana na wadau wa maendeleo pamoja na Jiji la Dodoma katika kuhakikisha suala la usafi linafanyika kwa ufanisi katika maeneo ya jamii. Alisema kuw kupitia ushirikiano huo, shirika limechangia vifaa vya usafi vyenye thamani ya shilingi milioni moja, vikiwemo mifagio, reki, toroli na vifaa vingine mbalimbali. Lekaaya alisema kuwa msaada huo unalenga kuwawezesha wafanyabiashara na wadau wengine kushiriki kikamilifu katika kutunza mazingira ya soko, ili wananchi wanaofika kwa shughuli mbalimbali waweze kupata mazingira safi na salama. Aliongeza kuwa Habitat for Humanity Tanzania inatekeleza shughuli zake katika maeneo mbalimbali yanayolenga kuboresha maisha ya jamii, ikiwemo masuala...

RC Dodoma amtaka Mkandarasi kuongeza kasi ukarabati Soko la Majengo

Na. Mohammed Ramadhani, MAJENGO Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amemtaka mkandarasi anayetekeleza ukarabati wa Soko la Majengo jijini Dodoma kuongeza kasi ya kazi ili kukamilisha mradi huo ndani ya muda wa nyongeza wa siku 60 uliotolewa. Senyamule alitoa kauli hiyo wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ukarabati wa Soko la Majengo, akieleza kuwa soko hilo lina mchango mkubwa katika kutoa huduma na kukidhi mahitaji ya wananchi wa Jiji la Dodoma. Akizungumza baada ya kukagua maendeleo ya mradi huo, mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa utekelezaji wa kazi unaelekea vizuri, lakini mkandarasi anapaswa kutumia kikamilifu muda wa nyongeza aliopewa ili kuhakikisha kazi zilizobaki zinakamilika kwa wakati. Aidha, alishauri kuwa mkandarasi kuongeza muda wa utekelezaji wa kazi kwa kufanya kazi hadi nyakati za usiku kwa kutumia taa, akisema hatua hiyo itasaidia kuongeza kasi ya ujenzi na kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati. Alisisitiza umuhimu wa kukamilisha kazi kabla ya kuan...

Usafi Soko la Sabasaba watakiwa kufanyika kila siku

Na. Mohammed Ramadhani, DODOMA Diwani wa Kata ya Viwandani, Swalihina Athuman amewataka viongozi na wafanyabiashara katika Soko la Sabasaba jijini Dodoma kuimarisha usimamizi wa usafi wa mazingira, akisisitiza kuwa usafi wa soko hilo unapaswa kuwa jukumu la kila siku kutokana na umuhimu wake kwa shughuli za biashara na afya za wananchi. Athuman alitoa kauli hiyo wakati akizungumza kuhusu hali ya usafi katika Soko la Sabasaba, akieleza kuwa soko hilo ni miongoni mwa masoko makubwa yanayohudumia wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Jiji la Dodoma, hivyo linahitaji usimamizi madhubuti wa mazingira ili kuhakikisha shughuli za biashara zinafanyika katika mazingira salama. Diwani huyo alisema kuwa mazingira ya soko hilo yana mchango mkubwa katika ustawi wa wafanyabiashara na wateja, hivyo kila mmoja anapaswa kutambua wajibu wake katika kuhakikisha taka zinadhibitiwa na maeneo ya biashara yanakuwa safi wakati wote. “Tusipokuwa makini kuzingatia usafi katika Soko la Sabasaba na maeneo ...

Jiji la Dodoma laweka mkakati wa kudhibiti msongamano wa Bajaj na Daladala Stendi ya Mnada mpya

Image
Na. Mwandishi wetu, KIZOTA   Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeanza kuchukua hatua za kuboresha matumizi ya Kituo cha Mabasi Mnada Mpya kilichopo Kata ya Kizota kwa kuhakikisha daladala na bajaji zinaingia ndani ya kituo hicho wakati wa kupakia na kushusha abiria, badala ya kusimama nje ya kituo.   Hatua hiyo inalenga kuweka utaratibu katika eneo hilo, kupunguza msongamano wa vyombo vya usafiri pamoja na kuimarisha usalama na urahisi wa huduma kwa wananchi wanaotumia kituo hicho.   Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Stendi ya Mnada Mpya iliyopo Kata ya Kizota, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, alisisitiza umuhimu wa halmashauri kuhakikisha kituo hicho kinatumika kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa.   Senyamule alielekeza daladala na bajaji kuingia ndani ya kituo wakati wa kupakia na kushusha abiria, akieleza kuwa hatua hiyo itasaidia kuboresha mtiririko wa usafiri na kuhakikisha mazingira ya kituo yanakuwa sal...

Halmashauri ya Jiji la Dodoma yafanyia marekebisho Barabara ya kuingia Stendi ya Mnadani, Kizota

Image
Na. Mwandishi wetu, KIZOTA Halmashauri ya Jiji la Dodoma inaendelea na zoezi la kufanya marekebisho ya barabara ya kuingia katika Stendi ya Mnadani Kata ya Kizota, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule.   Hatua hiyo imekuja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kuzungumza na wamiliki wa daladala na bajaji jana, ambapo alisisitiza umuhimu wa vyombo hivyo kuingia na kupaki ndani ya stendi badala ya kusimama na kupaki nje ya eneo la stendi, hali ambayo ni kinyume na utaratibu na sheria zilizowekwa.   Halmashauri imeanza kuchukua hatua za haraka kuhakikisha mazingira ya kuingia na kutoka katika Stendi ya Mnadani, Kata ya Kizota yanakuwa rafiki na salama kwa daladala, bajaji, abiria na watumiaji wengine wa barabara.   Marekebisho hayo yanatarajiwa kurahisisha utekelezaji wa maelekezo hayo na kuhakikisha Stendi ya Mnadani Kata ya Kizota inatumika kwa utaratibu unaostahili, huku ikisaidia kupunguza msongamano n...

Kliniki ya Ardhi Kata ya Kikuyu Kaskazini

Image
 

Zoezi la Kuua Mbwa Wanao Zurura Lafanyika Kata ya Msalato

Image
Na. Manase Malima, MSALATO   Zoezi la kuua mbwa wanao zurura limefanyika katika Kata ya Msalato, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, likihusisha maeneo ya Machinjioni, Magereza na Mnadani, kutokana na kero na hatari zinazowakabili wananchi ambapo mbwa zaidi ya 20 waliuliwa. Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Afisa Mifugo wa Kanda Namba Sita ya utoaji huduma Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prisca Mottee alisema kuwa mbwa hao wamekuwa wakisababisha usumbufu kwa wananchi, wakiwemo watoto na wanafunzi wanaokwenda na kurudi shuleni, Afisa Mifugo kanda Namba Sita aliongeza kuwa zoezi hilo ni endelevu na litafanyika katika maeneo mengine yenye changamoto hiyo, huku akiwataka wafugaji kuwafungia mbwa wao na kuzingatia kuwapatia chanjo. Kwa upande wake Afisa Mifugo Kata ya Msalato, Maisha Jiwa alisema kuwa hatua hiyo imechukuliwa kufuatia malalamiko ya wananchi kuhusu mbwa wanao zurura katika maeneo mbalimbali ya kata hiyo. “Kumekuwa na adha kubwa ya mbwa wanaozurura katika maeneo ya Machi...

AI Ultrasound kuokoa maisha ya Mama na Mtoto Dodoma

Image
Na. Lulu Luvanda, MKONZE Mkoa wa Dodoma umechaguliwa kuwa mkoa wa majaribio katika matumizi ya teknolojia ya AI Ultrasound, kupitia Mradi wa The Study of AI-Facilitated Ultrasound Feasibility and Assessment of Resources and Integration (SAFARI Project), unaolenga kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto. Hatua hiyo imekuja wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa vya AI Ultrasound kwa vituo 32 vya kutolea huduma za afya katika Mkoa wa Dodoma, iliyofanyika katika Kituo cha Afya Mkonze, jijini Dodoma. Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, alikipongeza   Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kwa kuendelea kufanya tafiti zenye uhalisia na zinazolenga kutatua changamoto mbalimbali katika jamii, ikiwemo tafiti katika sekta za Utalii, Mazingira pamoja na Lishe. Alisema kuwa matumizi ya vifaa hivyo katika vituo vya afya yatawezesha wananchi kupata huduma za awali kwa ukaribu zaidi, hivyo kupunguza changamoto ya kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma za uchunguzi...

Wanafunzi watakiwa kujua umuhimu wa utunzaji Mazingira Dodoma Makulu

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA MAKULU   Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Sechelela jijini Dodoma wamepata elimu kuhusu umuhimu wa utunzaji na uhifadhi wa mazingira, ikiwa ni sehemu ya kuwajengea uelewa na kuhamasisha ushiriki wao katika shughuli za maendeleo ya jamii.   Akizungumza na wanafunzi hao, Afisa Maendeleo ya Jamii Kanda ya utoaji huduma Namba Nne, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mariam Nyirenda, amesisitiza umuhimu wa kila mmoja kuwa na jukumu katika kulinda mazingira.   Amewahimiza wanafunzi kushiriki katika shughuli za usafi, upandaji miti na uhifadhi wa mazingira kwa ajili ya afya na ustawi wa jamii.   Aidha, amewataka wanafunzi kuwa mabalozi wa mazingira katika shule, familia na jamii kwa ujumla, kwa kuhamasisha wengine kuchukua hatua katika kuyatunza.   Kwa upande wake Dorcas Alex, Mwanafunzi    alisema kuwa wanafunzi wanashiriki usafi wa mazingira kwa lengo la kuhakikisha wanasoma katika maeneo masafi   Ujumbe huo una...

Kata ya Ipala yatekeleza agizo la usafi wa Mazingira

Image
Na. Mwandishi wetu, IPALA   Zoezi la uhamasishaji wa Usafi wa Mazingira katika Kanda Namba Saba limekua lenye mafanikio makubwa. Zoezi hilo limefanyika katika mitaa mitano iliyopo ndani ya Kata ya Ipala Mtaa wa Sokoine, Madukani, Azimio, Ukombozi na Mwinyi.   Usafi wa Mazingira ulishilikisha wataalamu kutoka Kanda Namba Saba, wenyeviti wa mitaa, Diwani pamoja na wananchi waliojitoa kusafisha mitaa yote mitano kwa ushirikiano mkubwa kufuatia agiza la Mkuu wa Mkoa wa Dodoma la kusafisha Jiji la Dodoma kila siku.   Akizungumza baada ya zoezi la Usafi wa Mazingira, DIwani wa Kata ya Ipala, Andrew Muhulo aliwapongeza wananchi kwa kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo la usafi wa Mazingira na kuwasihi wasiishie hapo tu maana zoezi la usafi ni maisha ya kila siku ya mtu mmoja mmoja.   “Niwapongeze wananchi wote kwa kujitokeza kwenu kwa wingi mkuu wetu wa mkoa amesema zoezi la usafi ni la kila siku hivyo tudumishe usafi katika maeneo yote na viongozi kutoka ka...