Wananchi watakiwa kufanya usafi kila siku kuweka Dodoma safi
Na. Leah Mabalwe, DODOMA Wananchi na wafanyabiashara katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kufanya usafi kila siku katika maeneo yao badala ya kusubiri siku ya jumamosi ya mwisho wa wiki ili kuhakikisha mazingira yanakuwa safi, salama na rafiki kwa afya za jamii. Wito huo ulitolewa na Meneja Kanda Namba Moja, Nicholaus Mitembo mara baada ya kushiriki zoezi la usafi wa pamoja katika Soko la Miembeni Jijini Dodoma, ambapo amesisitiza kuwa usafi si jukumu la mamlaka pekee bali ni wajibu wa kila mwananchi na mfanyabiashara. Alisema kuwa msisitizo huo unatokana na kauli iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule katika kikao na Maafisa Mazingira pamoja na maafisa afya ambapo alisisitiza kuwa kufanya usafi siku ya Jumamosi pekee haitoshi. “Usafi wa Jumamosi pekee hautoshi. Kila mwananchi na mfanyabiashara ana wajibu wa kushiriki katika usafi kila siku. Niwasihi wananchi wote pamoja na wafanyabiashara tusisubiri siku ya Jumamosi pekee, bali tuwe tunafany...