Posts

Wananchi watakiwa kufanya usafi kila siku kuweka Dodoma safi

Image
Na. Leah Mabalwe, DODOMA Wananchi na wafanyabiashara katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kufanya usafi kila siku katika maeneo yao badala ya kusubiri siku ya jumamosi ya mwisho wa wiki ili kuhakikisha mazingira yanakuwa safi, salama na rafiki kwa afya za jamii. Wito huo ulitolewa na Meneja Kanda Namba Moja, Nicholaus Mitembo mara baada ya kushiriki zoezi la usafi wa pamoja katika Soko la Miembeni Jijini Dodoma, ambapo amesisitiza kuwa usafi si jukumu la mamlaka pekee bali ni wajibu wa kila mwananchi na mfanyabiashara.   Alisema kuwa msisitizo huo unatokana na kauli iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule katika kikao na Maafisa Mazingira pamoja na maafisa afya ambapo alisisitiza kuwa kufanya usafi siku ya Jumamosi pekee haitoshi. “Usafi wa Jumamosi pekee hautoshi. Kila mwananchi na mfanyabiashara ana wajibu wa kushiriki katika usafi kila siku. Niwasihi wananchi wote pamoja na wafanyabiashara tusisubiri siku ya Jumamosi pekee, bali tuwe tunafany...

Ukaguzi wa watumishi Kanda Namba Sita walenga kuboresha uwajibikaji na usimamizi wa rasilimali watu

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Zoezi la ukaguzi wa watumishi katika vituo vya kazi limefanyika katika Kanda Namba Sita, likilenga kuhakikisha uwepo wa taarifa sahihi za watumishi, kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili, pamoja na kuwakumbusha kuhusu umuhimu wa kujaza mfumo wa PEPMIS.   Akizungumza kuhusu zoezi hilo, Afisa Utumishi Kanda, Jane Mwagalaba, alisema kuwa ukaguzi huo unahusisha kutembelea vituo vya kazi ili kuhakiki uwepo wa watumishi, kusikiliza changamoto zao na kupokea maoni yanayoweza kusaidia kuboresha mazingira ya kazi. “Zoezi hili linahusu ukaguzi wa watumishi katika vituo vya kazi, kusikiliza changamoto zao, kuchukua maoni, lakini pia kuwasisitiza kuhusu ujazaji wa PEPMIS,” alisema Mwagalaba. Alisema kuwa moja ya malengo makuu ya zoezi hilo ni kuwa na data sahihi za watumishi katika vituo vyao vya kazi, jambo ambalo ni muhimu katika kupanga na kusimamia rasilimali watu kwa ufanisi. Katika awamu ya kwanza, alisema kuwa zoezi hilo limewaleng...

Wafanyabiashara Soko la Miembeni Waazimia Kulinda Usafi

Image
Na. Mohammed Ramadhani, DODOMA Wafanyabiashara wa Soko la Miembeni jijini Dodoma wameahidi kuendelea kuimarisha usafi wa mazingira katika maeneo yao ya biashara, wakieleza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kulinda afya na ustawi wa jamii. Akizungumza na waandishi wa habari, Katibu wa Soko la Miembeni, Adelgot Mbwani alisema kuwa uongozi wa soko unaendelea kuwahamasisha wafanyabiashara kufanya usafi mara kwa mara na kuhakikisha kila mmoja anawajibika kutunza mazingira yanayomzunguka katika eneo lake la biashara. Aliongeza kuwa juhudi hizo pia zinaendana na msisitizo wa serikali wa kuhakikisha miji na maeneo ya biashara yanakuwa safi, hivyo wafanyabiashara wataendelea kushiriki kikamilifu katika kampeni za usafi. “Tumekuwa tukiwahamasisha wafanyabiashara wetu kufanya usafi mara kwa mara na kuwasisitizia kuwa usafi ni jukumu lao katika maeneo yao ya kazi, kama ambavyo Mheshimiwa Rais anavyosisitiza kuwa majiji yote yawe safi,” alisema Mbwani. Kwa upande wake, Katibu wa Soko la Wauza ...

LAAC yaridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo jijini Dodoma

Image
Na. Jesca Kipingu, DODOMA   Kamati ya Hesabu za Mamlaka za Serikali za Mitaa (LAAC) imeridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma, huku ikipongeza juhudi zinazofanywa na Halmashauri kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kwa kuzingatia ubora, thamani ya fedha na mahitaji ya wananchi. Pongezi hizo zimetolewa leo na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya LAAC, Abdallah Chikota, wakati wa ziara ya kamati hiyo ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, ikiwemo ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami yenye urefu wa kilomita 1.6 inayoelekea Hospitali ya Jiji la Dodoma katika eneo la Nala pamoja na ujenzi wa jengo jumuishi katika Kituo cha Afya Makole, ambalo linajengwa kwa mfumo wa ghorofa.   Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Chikota aliipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa namna inavyotekeleza miradi hiyo, akieleza kuwa kamati imeridhishwa na matumizi ya fedha pamoja na ubora w...

Usafi wa Jumamosi, ni usafi wa kila siku

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amesisitiza wananchi kuacha dhana kwamba usafi wa mazingira ni jukumu la kufanyika siku ya Jumamosi pekee, akieleza kuwa usafi ni wajibu wa kila mwananchi na unapaswa kufanyika kila siku.   Senyamule alitoa kauli hiyo jana wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma uliopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini hapa, kilichowakutanisha maafisa watendaji wa kata, mitaa, wenyeviti wa mitaa, maafisa afya na maafisa mazingira kutoka Jiji la Dodoma, kwa lengo la kujadili utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu umuhimu wa kuhakikisha miji na maeneo ya makazi yanakuwa safi. Akizungumza katika kikao hicho, mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa utaratibu wa kufanya usafi wa mazingira kila Jumamosi umefutwa, akisisitiza kuwa wananchi wanapaswa kuufanya usafi kuwa sehemu ya maisha yao ya kila siku. “Nimefuta utaratibu wa kufanya usafi kila Jumamosi....

Dodoma yaweka mkakati wa kuimarisha usafi wa Mazingira

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Dkt. Khatibu Kazungu amewataka watendaji wa kata na mitaa kusimamia ipasavyo usafi wa mazingira na kuhakikisha sheria ndogo zinazohusu udhibiti wa wanyama zinafuatwa, ili kudhibiti ongezeko la wanyama wanaozurura katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dodoma.   Akizungumza katika kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya jiji la Dodoma uliopo Mji wa Mtumba, jijini Dodoma, aliwasisitiza umuhimu wa watendaji kujipanga kukabiliana na changamoto zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua kubwa za El Niño, kwa kuandaa mipango ya kukabiliana na athari zake kuanzia ngazi ya kata hadi mtaa. Aliwataka watendaji kutumia mamlaka walizonazo katika kuchukua hatua stahiki pindi wanapobaini ukiukwaji wa sheria na taratibu za usafi na mazingira. Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi aliwataka watumishi kuwa na utayari wa kuchukua hatua katika utekelezaji wa majukumu yao, badala y...

Vijana Dodoma na Iringa Kukutana Kupaza Sauti Dhidi ya Rushwa

Image
Na. Muhamad Said, IRINGA Wanafunzi kutoka klabu za wapinga rushwa za shule za msingi na sekondari za mikoa ya Dodoma na Iringa leo wanatarajiwa kukutana katika mdahalo maalumu wa mapambano dhidi ya rushwa. Mdahalo huo utafanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Lugalo, mkoani Iringa, ukilenga kuwajengea wanafunzi uelewa, kuimarisha maadili na kuongeza ushiriki wa vijana katika mapambano dhidi ya rushwa ndani ya shule na jamii kwa ujumla. Kupitia mdahalo huo, wanafunzi wanatarajiwa kutoa hoja kuhusu madhara ya rushwa kwa jamii na taifa pamoja na changamoto zinazoweza kujitokeza katika mapambano dhidi ya vitendo hivyo. Aidha, mjadala unatarajiwa kutoa nafasi kwa vijana kueleza namna wanavyoweza kuwa sehemu ya mabadiliko katika kujenga jamii inayozingatia uadilifu. Ushirikishwaji wa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari unatarajiwa pia kuifanya shughuli hiyo kuwa sehemu ya kuwaandaa vijana kuwa mabalozi wa maadili na mapambano dhidi ya rushwa, kwa kuanza kujenga uelewa na msi...

RC Kheri James: Elimu iwe silaha yenu dhidi ya rushwa

Image
Na. Muhamad  Said, IRINGA Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James amewataka wanafunzi wa klabu za wapinga rushwa kutoka mikoa ya Iringa na Dodoma kuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya rushwa, akisisitiza kuwa elimu na uadilifu ni msingi muhimu wa kujenga taifa lenye maendeleo endelevu. Akizungumza katika mdahalo wa klabu za wapinga rushwa za shule za msingi na sekondari unaofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Lugalo, amewahimiza wanafunzi kutambua madhara ya rushwa na kuanza mapema kujenga utamaduni wa kuikataa, akieleza kuwa kizazi cha leo ndicho kitakachobeba dhamana ya uongozi na maendeleo ya taifa hapo baadaye.   Alisisitiza kuwa suala la kupinga rushwa linapaswa kupigwa vita na watu wote wakiwemo wanafunzi, akiongeza kuwa vijana wanapaswa kuwa mabalozi wa uadilifu katika shule zao, familia na jamii kwa ujumla kwa kukataa vitendo vya rushwa na kuhamasisha wenzao kusimamia haki na uwajibikaji.   Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka wanafunzi kutumi...

LAAC yalipongeza Jiji la Dodoma kwa ubunifu wa Jengo Jumuishi Kituo cha Afya Makole

Image
Na. Mwandishi Wetu, VIWANDANI   Halmshauri ya Jiji la Dodoma imepongezwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kwa ubunifu wa kujenga jengo jumuishi la huduma za afya la ghorofa tatu katika Kituo cha Afya Makole lenye gharama ya shilingi bilioni 6.9 hatua inayolenga kutatua changamoto ya uhaba wa eneo na kukidhi ongezeko la mahitaji ya huduma za afya katika jiji hilo.   Pongezi hizo zilitolewa na Makamu Mwenyekiti wa (LAAC), Abdallah Chikota wakati wa ziara ya kamati hiyo ya kukagua miradi ya maendeleo Kata ya Viwandani Jiji la Dodoma.   Chikota alisema kuwa mfumo wa kujenga ghorofa ulikuwa ndio mbadala sahihi wa kukabiliana na changamoto ya uhaba wa eneo na kupanua huduma za matibabu, bila kulazimika kutafuta eneo jipya nje ya kituo hicho cha afya.   “Kwanza tunalipongeza Jiji la Dodoma kwa ubunifu wao na mawazo ya kisasa kwa sababu hapa Kituo cha Afya Makole kuna changamoto ya eneo, kwa hiyo ili kutatua tatizo hilo wameamu...

LAAC yaridhishwa, yalipongeza Jiji la Dodoma ujenzi wa Barabara ya KM 1.6

Image
Na. Maandishi wetu, NALA   Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imelipongeza Jiji la Dodoma kwa ukamilishaji wa barabara ya kiwango cha lami yenye urefu wa kilomita 1.6 inayoelekea Hospitali ya Jiji na kuufanya mradi huo kuwa wa kipekee ukilinganishwa na miradi iliyotekelezwa katika maeneo mengine.   Akizungumza wakati wa ziara ya kamati hiyo ya kukagua miradi ya maendeleo Makamu Mwenyekiti wa LAAC, Abdallah Chikota, alisema kuwa kamati imeridhishwa na ubora wa utekelezaji wa mradi huo uliogharimu shilingi bilioni 2.8 kwa kutumia mapato ya ndani ya Jiji la Dodoma.   Alisema kuwa uwekaji wa miundombinu ya usalama ikiwamo taa za barabarani ni hatua muhimu inayoongeza thamani ya mradi na kurahisisha wananchi kufika Hospitali ya Jiji wakati wowote. Aidha, uwekaji wa taa, mitaro na alama za barabarani umeboresha mpangilio na matumizi salama ya njia hiyo.   “Mradi umejengwa kwa kiwango ambacho tumeridhika. Pia, tumeridhishwa na hatu...