Posts

IPSIS yawarahisishia madiwani Dodoma kufanya maamuzi

Image
Na. Lulu Luvanda, DODOMA Mfumo wa Kimataifa wa Uandishi na Uwasilishaji wa Taarifa za Fedha (IPSIS) umeelezwa kuwa umepunguza ugumu wa uandishi na uchakataji wa taarifa za fedha katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, huku ukirahisisha uwasilishaji wa hesabu na kuwawezesha madiwani kufanya maamuzi kwa uelewa zaidi.   Akizungumza wakati wa mkutano maalumu wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma ililofanyika katika ukumbi wa mikutano ya halmashauri Diwani wa Kata ya Miyuji, Ringo Iringo alisema kuwa   mfumo huo ni muhimu kwa Jiji la Dodoma kutokana na shughuli nyingi za kiuchumi na miradi mbalimbali ya maendeleo na ongezeko la shughuli za kifedha zinazohitaji usimamizi madhubuti. Alisema kuwa mfumo wa IPSIS umeleta urahisi katika uandishi na uwasilishaji wa taarifa za kifedha, pamoja na kufanya mchakato wa kuchakata taarifa kuwa mwepesi na hivyo kusaidia viongozi kupata taarifa zinazoweza kuwa msingi wa kufanya maamuzi kwa wakati. “Kwa sababu hiyo, IPSIS ni ...

Baraza la Madiwani Jiji la Dodoma lapitisha taarifa ya ufungaji hesabu 2025/2026

Image
Na. Manase Malima, DODOMA Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma limeridhia na kuthibitisha taarifa ya ufungaji wa hesabu za halmashauri za hadi kufikia tarehe 30 Juni, 2026 huku madiwani wakisisitiza umuhimu wa kuendeleza uwazi na uwajibikaji katika uongozi na usimamizi wa fedha za umma. Taarifa hiyo iliwasilishwa katika mkutano maalum wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, ambapo Mkuu wa kitengo cha Fedha na Uhasibu, CPA. David Rubibira aliwasilisha taarifa hiyo kwa ajili ya kuhakikiwa na kuthibitishwa na baraza. CPA. Rubibira alisema kuwa taarifa za ufungaji wa hesabu za halmashauri kwa tarehe 30 Juni, 2026 ikiwa ni sehemu ya utaratibu wa kuwasilisha taarifa za kifedha kwa ajili ya kuhakikisha kuwa taarifa za halmashauri zinaakisi hali halisi ya matumizi na usimamizi wa fedha. Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Zuzu, Jenesta Malingo alisema kuwa ameridhishwa na taarifa hiyo na anaamini kuwa uwazi katika uwasil...

Wilaya ya Dodoma kuchanja watoto zaidi ya laki 2 chanjo ya Polio

Image
Na. Coletha Charles, NKUHUNGU   Wilaya ya Dodoma imejipanga kuchanja watoto 207,096 chini ya miaka 10 dhidi ya ugonjwa wa Polio, sawa na asilimia 21 ya lengo la mkoa mzima, ikiwa ni utekelezaji wa kampeni ya kitaifa ya kujikinga na mlipuko wa ugonjwa huo. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, iliyofanyika katika Shule ya Msingi Nkuhungu, Kata ya Nkuhungu Halmshauri ya Jiji la Dodoma Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alisema kuwa wilaya hiyo imekamilisha maandalizi yote ya kimkakati kupitia vikao vya ngazi tatu wataalamu, makundi ya hamasa na Kamati ya Afya ya Msingi ya Wilaya. “Waliopewa kazi ya kuhamasisha, wafanye kazi hiyo ya uhamasishaji kikamilifu. Na kwa bahati njema, kama ambavyo tumeona hapa, wanatoka kwenye ngazi ya jamii, kwa hiyo wanafahamu namna ya kushirikiana na jamii. Tumepewa lengo la kuchanja watoto 207,096,” alisema Alhaj Shekimweri. Alitumia nafasi hiyo kubainisha kuwa nchi haina mgonjwa wa Polio kwa sasa, hatua hiyo ni maelekezo ...

Wilaya ya Dodoma kutumia vyombo vya habari katika kampeni ya dhidi ya chanjo ya Polio

Image
Na. Coletha Charles, NKUHUNGU Wilaya ya Dodoma imeweka mkakati wa kutumia vyombo vya habari, viongozi wa dini, shule na kampuni za simu ili kuwahamasisha wazazi kuwapeleka watoto kupata chanjo salama dhidi ya ugonjwa wa Polio, lengo likiwa ni kutokomeza kabisa hatari ya maambukizi ya ugonjwa huo. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa zoezi hilo katika Shule ya Msingi Nkuhungu, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri, alisema kuwa vipindi vya redio na televisheni, hususani vipindi vya asubuhi, vitatumika kutoa elimu kwa wananchi na kujibu maswali kuhusu umuhimu na usalama wa chanjo hiyo. Alisema kuwa viongozi wa dini nao wamepewa nafasi muhimu katika uhamasishaji huo, kutokana na ushawishi wao katika jamii na uwepo wa watoto katika maeneo ya ibada, ikiwemo ‘Sunday Schools’, madrasa na jumuiya mbalimbali za kidini. “Tumeona pia kupitia eneo hilo kila mtoto wa Tanzania apate nafasi ya kupata chanjo hiyo. Tumewahamasisha shule zote, kamati na bodi za shule kufikisha ujumbe...

Tarura Dodoma yatakiwa kukamilisha miradi kwa wakati

Image
 

Wanafunzi Kizota S/M wapatiwa chanjo dhidi ya Polio

Image
Na. Jesca Kipingu, KIZOTA   Wataalamu wa afya kutoka Kituo cha Afya Kizota wamefika katika Shule ya Msingi Kizota, Kata ya Kizota, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, kwa ajili ya kutoa chanjo ya Polio kwa watoto wenye umri wa kuanzia miezi 0 hadi miaka 10, ikiwa ni sehemu ya kampeni inayoendelea ya kuwakinga watoto dhidi ya ugonjwa huo na madhara yake, ikiwemo ulemavu wa kudumu. Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Katibu wa Afya katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ambaye pia ni Msimamizi wa Kampeni ya Chanjo ya Polio, Hapiness Kaungya, aliwashukuru wazazi kwa mwitikio mkubwa walioonesha katika kuhakikisha watoto wao wanapatiwa chanjo. Alisisitiza kuwa ushiriki wa wazazi na walezi ni muhimu katika kuhakikisha watoto wanapata kinga dhidi ya ugonjwa wa Polio.   Aidha, Kaungya aliitaka jamii kuendelea kupata na kuzingatia taarifa sahihi zinazotolewa na wataalamu wa afya ili kuondokana na dhana potofu kuhusu chanjo. Alisema kuwa ushirikiano wa wazazi, walezi na jamii kwa ujumla ...

Bwawa kujengwa kudhibiti mafuriko Nzuguni, Dodoma

Image
 

DC Dodoma aagiza utambuzi wa kaya maeneo hatarishi

Image
 

DC Shekimweri aagiza kuzingatia usalama maeneo ya uchimbaji madini

Image
 

DC Dodoma aagiza Kampeni Maalumu ya Usafi kukabiliana na El Nino

Image