Posts

Dodoma Jiji yaifunga Mji Ifakara 41-3 Mpira wa Pete Mashindano ya SHIMISEMITA

Image
Na. Mwandishi wetu, MBEYA Timu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya Mpira wa Pete Wanawake imeishushia kipigo kizito Timu ya Halmashauri ya Mji Ifakara cha magoli 41-3 katika siku ya pili ya Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa Tanzania (SHIMISEMITA) yanayoendelea jijini Mbeya. Mchezo huo ulianza kwa kasi katika dakika za mwanzo, lakini kadri muda ulivyokuwa ukiendelea Timu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilionekana kuumiliki mchezo. Hadi kufikia tamati ya mchezo huo Timu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliibuka na ushindi mnono wa magoli 41-3 ya Halmashauri ya Mji Ifakara. Mchezo wa Mpira wa Mikono Wanaume Halmashauri ya Jiji la Dodoma ililazimishwa sare ya 5-5 dhidi ya Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Aidha, katika Mchezo wa Mpira wa Kikapu ya Wanaume Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliichakaza Timu ya Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kwa vikapu 28-7. Halmashauri ya Dodoma la Jiji iliendeleza kasi kwenye mchezo wa Mpira wa Wavu kwa Wanaume, ikiichapa Ha...

Magu DC yalazimisha sare dhidi ya Dodoma CC Handball SHIMISEMITA

Image
 

Dodoma Jiji 28-07 Kibaha DC Basketball SHIMISEMITA

Image
 

Kibaha DC yaangukia pua dhidi ya Dodoma CC Basketball SHIMISEMITA

Image
 

MEMKWA daraja kwa watoto waliokosa elimu rasmi

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Wananchi wa Jiji la Dodoma wametakiwa kuhakikisha watoto waliokosa kuanza elimu rasmi kwa wakati hawabaki nyuma, bali watumie fursa ya Elimu ya Watu Wazima na Mfumo wa Elimu Nje ya Mfumo Rasmi (MEMKWA) kupata elimu na kujenga msingi bora wa maisha yao.   Wito huo ulitolewa na Mwenyekiti wa Maafisa Elimu Jiji la Dodoma, Yassin Mponda katika Maadhimisho ya Wiki ya Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi (MEMKWA) yanayofanyika katika Viwanja vya Mapumziko vya Nyerere Square, ambapo shughuli mbalimbali zinaendelea kuanzia tarehe 17 hadi 21 Agosti, 2026.   Mponda alisema kuwa elimu ya watu wazima ina nafasi kubwa katika kuwapatia wananchi waliokosa fursa ya elimu rasmi uwezo wa kusoma, kuandika, kuhesabu pamoja na kupata ujuzi unaowawezesha kujitegemea na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii.   Aliongeza kuwa mtoto anayepaswa kuanza Darasa la Kwanza akiwa na umri wa miaka sita, lakini akakosa fursa hiyo na baad...

Mahitaji Maalumu Hombolo Bwawani wakumbukwa

Image
  Walimu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametembelea Kitengo cha Watoto Wenye Mahitaji Maalum katika Shule ya Msingi Hombolo Bwawani na kutoa msaada wa mahitaji mbalimbali kwa watoto hao. Ziara hiyo imelenga kuonesha upendo, kujali na kuimarisha ushirikiano katika kuwasaidia watoto wenye mahitaji maalum kupata mazingira bora ya kujifunzia na kukua.  

Jiji la Dodoma laaga Timu ya Watumishi kuelekea SHIMISEMITA Mbeya

Image
Na. Rahma Magona, DODOMA Uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma umeiaga rasmi timu ya watumishi itakayoiwakilisha Halmashauri hiyo katika mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa Tanzania (SHIMISEMITA), yanayotarajiwa kufanyika jijjni Mbeya. Hafla hiyo ya kuwaaga watumishi hao ilifanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, ambapo watumishi hao wamepewa jukumu la kuiwakilisha Dodoma katika mashindano hayo na kurudi na ushindi. Akizungumza katika hafla hiyo Kocha wa Timu ya Mpira wa Miguu, Leonard Mkinga alisema kuwa kabla ya kuingia kwenye mashindano, watumishi wamejiandaa vizuri katika kipindi chote kwa kufanya mazoezi ya viwango vya juu. “Tumejiandaa vizuri na matarajio yetu lazima tukaoneshe ushindani wa hali ya juu na kutetea vikombe tulivyovipata mwaka jana” alisema Mkinga.   Alisema kuwa ushiriki wa watumishi hao katika michezo unapaswa kwenda sambamba na utekelezaji wa majukumu yao ya msingi ya utumishi, huku michezo ikiwa na nafasi muhim...

Timu ya Watumishi Jiji la Dodoma yadaiwa ushindi mashindano ya SHIMISEMITA

Image
Na. Lulu Luvanda, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeiaga timu ya watumishi itakayoliwakilisha jiji hilo katika Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa (SHIMISEMITA) 2026 yatakayofanyika jijini Mbeya na kutakiwa kurejea na ushindi. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akiiaga timu hiyo katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. Akizungumza katika hafla ya kuwaaga wachezaji hao jijini Dodoma, alisema kuwa mashindano hayo ni fursa ya kulitangaza Jiji la Dodoma kupitia michezo, huku akiwataka wachezaji hao kuzingatia nidhamu, maadili na misingi ya utumishi wa umma. Aliwakumbusha umuhimu wa michezo katika kuimarisha afya, mshikamano na uhusiano miongoni mwa watumishi, huku akiwataka kulitangaza vizuri Jiji la Dodoma kwa kuonesha uwezo, nidhamu na ushindani wa hali ya juu. Kwa upande wake Meneja wa Timu ya watumishi wa Jiji la Dodoma, Dkt. Sebastian Pima alisema kuwa wamefurahia kumuona Mkurugenzi...

Dodoma Jiji imejipanga!

Image
 

Jiji la Dodoma kushiriki SHIMISEMITA jijini Mbeya

Image