Jiji la Dodoma laibuka na zana za upaliliaji, Maonesho ya Nanenane
Na. Mwandhsi wetu, DODOMA Halmshauri ya Jiji la Dodoma imeendelea kungara katika Maonesho ya Nanenane kwa kuweka vitu vya kitofauti ambapo mojawapo ni uwepo wa zana za upaliliaji ambazo zimeundwa na mjasiriamali mdogo kutoka ndani ya jiji. Akizungumza na waandishi wa habari mjasiriamali, Zuberi Nguzo aliyepata fursa ya kuonesha ujuzi katika maonesho hayo alisema kuwa zana hizo zimeundwa kwa muundo wa ‘power tiller’ ya miguu mitatu zikiwa katika ubora wa hali ya juu. “Zana hizi za upaliliaji zinatumia injini ya guta lakini ina mfumo wa rejeta kama kawaida. Pia ina mfumo wa feni kama kawaida na upande wa nyuma kuna jembe ambalo hili ndilo linatumika kwa ajili ya upaliliaji. Katika upaliliaji inatumia mfumo wa matuta kwa maana kwamba inapita katikati ya mstari na kuweka matuta kwenye mashina ya mahindi kwasababu tairi zake tumeweka kwa kipimo cha sentimita 62, hiki ni kipimo sahihi kabisa kwa upana kwa kilimo cha mahindi,” alisema Nguzo. Alisema kuwa ameamua kubuni zana hizo k...