Teknolojia ya Kinengunengu mkombozi kwa vifaranga vya kuku Dodoma
Na. Mwandishi wetu, NZUGUNI Halmashauri ya Jiji la Dodoma limeibua ubunifu mpya wa teknolojia ya banda maalumu la kufugia vifaranga vya kuku maarufu kama ‘Kinengunengu’ linalolenga kuwasaidia wafugaji kupata njia bora ya kuwapatia vifaranga joto, chakula, malazi na mazingira salama ya ukuaji. Banda hilo limekuwa miongoni mwa vivutio vikubwa katika maonesho ya Nanenane yanayofanyika katika viwanja vya Dkt. John Malecela, Nzuguni kupitia banda la Jiji la Dodoma, ambapo wananchi wamekuwa wakijitokeza kwa wingi kujifunza namna ya kuanza na kuendeleza ufugaji wa kuku kwa njia rahisi na salama. Akielezea banda hilo, Afisa Mifugo wa Jiji la Dodoma, Delila Mlamka alisema kuwa wafugaji wengi wamekuwa wakitegemea matumizi ya taa na mkaa kwa ajili ya kuwapatia vifaranga joto, lakini teknolojia ya Kinengunengu imekuja kuondoa utegemezi huo kwa kutumia muundo unaoweza kuhifadhi joto ndani ya banda. Alisema kuwa Kinengunengu kimeundwa katika mfumo wenye sehemu mbili muhimu, sehemu ya kul...