Posts

Timu ya Watumishi Jiji la Dodoma yadaiwa ushindi mashindano ya SHIMISEMITA

Image
Na. Lulu Luvanda, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeiaga timu ya watumishi itakayoliwakilisha jiji hilo katika Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa (SHIMISEMITA) 2026 yatakayofanyika jijini Mbeya na kutakiwa kurejea na ushindi. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko alipokuwa akiiaga timu hiyo katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. Akizungumza katika hafla ya kuwaaga wachezaji hao jijini Dodoma, alisema kuwa mashindano hayo ni fursa ya kulitangaza Jiji la Dodoma kupitia michezo, huku akiwataka wachezaji hao kuzingatia nidhamu, maadili na misingi ya utumishi wa umma. Aliwakumbusha umuhimu wa michezo katika kuimarisha afya, mshikamano na uhusiano miongoni mwa watumishi, huku akiwataka kulitangaza vizuri Jiji la Dodoma kwa kuonesha uwezo, nidhamu na ushindani wa hali ya juu. Kwa upande wake Meneja wa Timu ya watumishi wa Jiji la Dodoma, Dkt. Sebastian Pima alisema kuwa wamefurahia kumuona Mkurugenzi...

Dodoma Jiji imejipanga!

Image
 

Jiji la Dodoma kushiriki SHIMISEMITA jijini Mbeya

Image
 

Timu ya Watumishi Dodoma Jiji kushiriki Mpira wa Kikapu SHIMISEMITA

Image
 

Timu ya Watumishi Jiji la Dodoma inayoshiriki SHIMISEMITA yatakiwa kurejea na ushindi

Image
Na. Lulu Luvanda, DODOMA Timu ya watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma itakayoshiriki Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa Tanzania (SHIMISEMITA) wametakiwa kulitangaza vema jiji hilo katika michezo kwa kuzingatia nidhamu na misingi ya utumishi wa umma na kurejea na ushindi.   Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko wakati wa tukio la kuwaaga wanamichezo hao watakaoshiriki michezo ya SHIMISEMITA jijini Mbeya.   Akizungumza katika hafla ya kuwaaga wachezaji hao iliyofanyika katika ukumbi wa halmashauri jijini Dodoma, alisema kuwa mashindano hayo ni fursa ya kulitangaza Jiji la Dodoma kupitia michezo, huku akiwataka wachezaji kuzingatia nidhamu, maadili na misingi ya utumishi wa umma.   Alitumia hafla hiyo kumpongeza Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa, Neema Kilongola kwa mchango wake katika kuimarisha michezo ndani ya halmashauri hiyo, akisisitiza kuwa mafanikio ya ...

Timu ya Jiji la Dodoma yatakiwa kuzingatia uzalendo michezo ya SHIMISEMITA

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Jumla ya wanamichezo 60 wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, wakiwemo makocha wanne, wametakiwa kuzingatia nidhamu na uzalendo katika Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa Tanzania (SHIMISEMITA) yanayofanyika mkoani Mbeya ili kulinda hadhi ya makao makuu.   Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko katika hafla fupi ya kuwaaga wanamichezo hao iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri.   Aliwataka kuitumia michezo hiyo kuiwakilisha Dodoma kwa nidhamu, uzalendo na kujiamini, wakitambua kuwa wanatokea makao makuu ya nchi. “Nendeni mkifahamu kuwa mnatokea makao makuu ya nchi. Nendeni mkalete tabasamu kwa Watanzania na si huzuni, maana Dodoma ni fahari ya Watanzania. Nidhamu ni miongoni mwa sababu zilizochangia mafanikio ya mwaka jana. Hivyo, dumisheni nidhamu, kufuata misingi ya utumishi wa umma na kulinda hadhi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma,” alisema Dkt. ...

Timu ya Watumishi Jiji la Dodoma waagwa kuelekea SHIMISEMITA

Image
  Timu ya Watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, inayokwenda kushiriki SHIMISEMITA, 2026 jijini Mbeya   imeagwa rasmi na Uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika ukumbi wa halmashauri. Katika hafla hiyo, uongozi umeihimiza timu hiyo kwenda kushiriki kwa nidhamu, umoja, ari na ushindani wa hali ya juu, ili kuiwakilisha vema Halmashauri na Jiji la Dodoma na kurudi na ushindi wa kishindo.

Makutupora kupata Zahanati Mpya, Mbunge wa Mtumba aweka nguvu kwenye ujenzi

Image
Na. Mwandishi wetu, MAKUTUPORA   Jitihada za kukamilisha ujenzi wa Zahanati ya Mchemwa zimepata nguvu baada ya kuchangiwa matofali 5,000, mifuko 250 ya saruji pamoja na gharama za mafundi hadi hatua ya kufunika jengo, huku wananchi wakihimizwa kushiriki kikamilifu kuhakikisha zahanati hiyo inakamilika na kuanza kutoa huduma.   Mbunge wa Jimbo la Mtumba Anthony Mavunde alisema kuwa lengo la mchango huo ni kuhakikisha wananchi wa Makutupora wanapata huduma za afya karibu na makazi yao, akisisitiza kuwa ujenzi wa zahanati hiyo haupaswi kuwa jukumu la mtu mmoja, bali ni mradi wa wananchi wote.   “Zahanati si ya kwangu. Zahanati ni ya kwetu. Kila mmoja ahakikishe pale mchanga wake unaingia kwenye zahanati. Naomba mtoe ushirikiano. Kuna baadhi ya gharama si lazima nilipie mimi ila nguvu kazi yenu nayo inaweza kufanikisha jambo hili natamani kuwaona vijana wa hapa wakichapa kazi,” alisema Mavunde.   Mbunge huyo pia alisema kuwa anaamini serikali itaendelea kuu...

Jiji la Dodoma lavuna Tuzo Tano Nanenane, 2026

Na. Mwandishi wetu, DODOMA   Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeibuka kidedea katika Maonesho ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ya Nanenane Kitaifa 2026 baada ya kutwaa tuzo tano, hatua inayoonesha mafanikio makubwa ya jiji hilo katika kuendeleza sekta za kilimo, mifugo na uvuvi.   Maonesho hayo yaliyofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela jijini Dodoma na kuhitimishwa Agosti 8, 2026 yaliwakutanisha washiriki mbalimbali kutoka maeneo tofauti ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kuonesha ubunifu, teknolojia na fursa zilizopo katika sekta za uzalishaji.   Katika maonesho hayo, Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilitwaa nafasi ya kwanza katika makundi ya Kilimo Ndani ya Uwanja, Mifugo Ndani ya Uwanja na Malisho Ndani ya Uwanja kwa upande wa Kanda ya Kati.   Aidha, jiji hilo lilipata nafasi ya pili katika kundi la Ufugaji Samaki katika Maonesho ya Ndani ya Uwanja Kanda ya Kati na kutunukiwa tuzo maalum (trophy) iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa T...

Timu ya Kikapu yajinoa kualekea SHIMISEMITA Mbeya, 2026

Image
  TIMU ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya Mchezo Kikapu itakayoshiriki mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa Tanzania (SHIMISEMITA) inaendelea na mazoezi ya utimamu wa mwili katika uwanja wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) jijini Dodoma.