Kampeni ya Chanjo ya Polio kuwafikia watoto 207,096 jijini Dodoma
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Wizara ya Afya kupitia Idara ya Kinga, Sehemu ya Elimu ya Afya kwa Umma, imewataka wananchi wa Jiji la Dodoma kujitokeza na kuwapeleka watoto wenye umri wa chini ya miaka 10 kupata chanjo ya matone ya Polio, ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kuongeza kinga dhidi ya ugonjwa huo. Akizungumza kuhusu kampeni hiyo, Magdalena Dinawi kutoka Wizara ya Afya, Idara ya Kinga, alisema kuwa chanjo ya Polio inayotolewa kwa njia ya matone ni muhimu katika kuzuia ugonjwa wa kupooza unaosababishwa na virusi vya Polio. Alisema kuwa ugonjwa huo hauna tiba, hivyo kinga kupitia chanjo ndiyo njia muhimu ya kumkinga mtoto dhidi ya madhara yanayoweza kusababishwa na Polio. “Chanjo hii ina umuhimu kwa watoto kwa sababu inazuia ugonjwa wa kupooza ambao kitaalamu tunauita Polio. Ugonjwa wa Polio hauna tiba, ila kinga iliyopo ni kwa kupewa matone ya chanjo ya Polio. Aidha, watoto wanatarajiwa kupata huduma hiyo katika vituo vya kutolea huduma za afya, shule, maeneo ya ibada, masoko,...