Posts

Timu ya SHIMISEMITA ya Jiji la Dodoma yajipanga kutetea ubingwa

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Kikosi cha Timu ya Watumishi wa Jiji la Dodoma cha Mpira wa Miguu kinaendelea kujifua kwa mazoezi makali kuelekea mashindano ya SHIMISEMITA 2026 yatakayofanyika jijini Mbeya, kikiwa na malengo ya kufanya vizuri na kutwaa ubingwa. Hayo aliyasema Kocha wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Watumishi Jiji la Dodoma, Given Aristides wakati wa bonanza la kimichezo lililozikutanisha Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino na Halmashauri ya Wilaya ya Gairo katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Dodoma, ambapo timu hizo zilipata nafasi ya kupima uwezo wao kabla ya kuingia kambini kwa ajili ya mashindano hayo. Alisema kuwa ushindani katika SHIMISEMITA unazidi kuongezeka kila mwaka kutokana na halmashauri nyingi kujiandaa kwa umakini, jambo linalowalazimu kuongeza kiwango cha mazoezi na nidhamu ili kufikia malengo waliyojiwekea. “Tunafahamu kuwa SHIMISEMITA ni mashindano yenye ushindani mkubwa, hivyo tunaendelea kujinoa kwa bidii kila siku. Bonanza hil...

Timu ya Jiji la Dodoma yajinoa kuelekea SHIMISEMITA Mbeya, 2026

Image
Na. Mwandishi Wetu, Dodoma MSAKO wa kutetea ubingwa wa mashindano ya Shirikisho la Michezo la Serikali za Mitaa Tanzania (SHIMISEMITA) umeanza rasmi kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma baada ya watumishi wake kushiriki bonanza la michezo lililozikutanisha Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino na Halmashauri ya Wilaya ya Gairo katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Dodoma. Bonanza hilo limekuwa sehemu ya maandalizi ya kuelekea mashindano ya SHIMISEMITA yanayotarajiwa kufanyika mwezi Agosti mwaka huu jijini Mbeya, ambapo halmashauri mbalimbali nchini zitachuana kuwania ubingwa katika michezo tofauti. Akizungumza baada ya bonanza hilo, Afisa Michezo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Neema Kilongola alisema kuwa maandalizi yanaendelea vizuri na mechi hizo zimewapa nafasi ya kupima uwezo wa kikosi kabla ya kuelekea Mbeya. “Bonanza hili limetupa nafasi ya kujipima, kurekebisha mapungufu na kuongeza ushindani ndani ya timu. Mwaka jana tulikuwa mabingwa, hivyo mwaka h...

Timu ya Jiji la Dodoma yatakiwa kudumisha nidhamu mashindano ya SHIMISEMITA

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Wachezaji wanaojiandaa kushiriki mashindano ya SHIMISEMITA watakiwa kuwa na malengo makubwa, nidhamu na ari ili kuweza kupata ushindi. Hayo aliyasema Mwenyekiti wa SHIMISEMITA Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Gerald Ruzika wakati wa kikao chake na washiriki wa timu ya Jiji la Dodoma kilichofanyika katika ukumbi wa mikutaho wa halmashauri jijini Dodoma. Aliseama kuwa malengo yetu ni kupambania nafasi ya juu. “Mnakwenda kuiwakilisha Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Muwe na malengo ya ushindi na mkapambane kuurudisha ubingwa kama mlivyofanya mwaka jana. Fanyeni mazoezi kwa bidii, muwe na nidhamu na mshikamano ili mkaandike historia nyingine ya mafanikio,” alisema Dkt. Ruzika. Aidha, aliwasisitiza washiriki kuongeza juhudi katika mazoezi na kuzingatia maelekezo ya makocha wao ili kuhakikisha wanakuwa katika kiwango bora kitakachowawezesha kufanya vizuri na kuipeperusha vema bendera ya Jiji la Dodoma. Kwa upande wake, Nahodha wa Mpira wa Pete, Mwajuma Ban...

Wananchi Kata ya Chang’ombe wahimizwa kulinda miundombinu

Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Wananchi wa Kata ya Chang’ombe watakiwa kuendelea kuitunza na kuilinda miradi ya maendeleo ili iweze kutoa huduma kwa muda mrefu na kuvinufaisha vizazi vya sasa na vijavyo. Hayo aliyasema Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Bakari Fundikira mara baada ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Kata ya Chang’ombe jijini Dodoma. Alisema kuwa serikali imeendelea kuwekeza fedha nyingi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo yenye lengo la kuboresha huduma za kijamii na kuinua ustawi wa wananchi. “Hivyo, ni wajibu wa kila mwananchi kushiriki katika kuilinda na kuitunza. Leo tumetembelea miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa Ofisi ya Mtaa wa Kishoka, Ofisi ya Mtaa wa Chang’ombe Juu, Ofisi ya Mtaa wa Hamvu, kisima cha maji Shule ya Msingi Chang’ombe na ujenzi wa Wodi ya Mama na Mtoto katika Kituo cha Afya Chang’ombe ambapo miradi hii imejengwa kwa fedha za serikali jumla ya shilingi 456,926,355. Lakini pia nitoe rai kuwa ni m...

Usafi Jumamosi Tarehe 18 Julai, 2026

Image
 

Wataalam Ilemela MC wajifunza mfumo wa utenganishaji taka Dodoma Jiji

  Wataalam kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela wamefanya ziara ya mafunzo ya mbinu bora za usimamizi wa usafi wa mazingira hasa mfumo wa kutenganisha taka na kuona vihifadhio vinavyotumika kutenganishia taka katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Ziara hiyo ya mafunzo ilijifunza jinsi kampuni maalum ya kutekeleza miradi (SPV) ya halmashauri inavyotumika kutekeleza miradi ya maendeleo na kutembelea miradi inayotekelezwa ya Bustani ya Mapumziko ya Chinangali na Duka kuuza vifaa vya ujenzi.

Jiji la Dodoma lajinoa kuelekea SHIMISEMITA 2026

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Timu ya Mpira wa Pete ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma inaendelea kujinoa kuelekea mashindano ya SHIMISEMITA 2026 yanayotarajiwa kufanyika Mwezi Agosti, 2026 jijini Mbeya, mara baada ya kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Timu ya Jamhuri kabla ya kuingia kwenye dimba la mashindano rasmi. Hayo aliyasema Afisa Michezo wa Jiji la Dodoma, Neema kilongola mara baada ya kutamatika kwa mchezo huo katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma Alisema kuwa michezo ya kirafiki ni sehemu muhimu ya maandalizi kwa kuwa husaidia kubaini mapungufu na kuyafanyia kazi mapungufu hayo. "Lengo la mchezo huu wa kirafiki halikuwa kushinda pekee, bali ilikuwa ni kujipima uwezo wetu, kubaini mapungufu yaliyopo na kuyafanyia kazi kabla ya kuanza mashindano ya SHIMISEMITA. Tunaendelea kujenga timu imara na tunaamini tutafika Mbeya tukiwa katika kiwango kizuri cha ushindani " alisema Kilongola. Aliongeza kuwa kikosi hicho kinaendelea na programu maalum za mazoezi zinazolenga ...

Jiji la Dodoma kinara utekelezaji afua za Lishe

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imepata alama ya kijani katika kadi alama ya viashiria vya utekelezaji wa afua za lishe ikiwa ni hatua nzuri kwa kipindi cha Robo ya Nne kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026. Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Lishe kwa kipindi hicho, Kaimu Afisa Lishe wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Happiness Mlamka alisema kuwa utekelezaji umeendelea kufanyika kwa mafanikio makubwa ambapo kadi alama ya lishe imeonesha rangi ya kijani. Alisema kuwa rangi hiyo ni kiashiria kwamba halmashauri imefikia viwango vinavyotakiwa katika utekelezaji wa afua za lishe. Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wake, Sakina Mbugi, aliyemuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Dodoma alipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kuendelea kufanya vizuri katika utekelezaji wa shughuli za lishe. Alisisitiza umuhimu wa kuendeleza utoaji wa elimu ya lishe kwa kutumia kaulimbiu mbalimbali zinazotolewa kupitia Mbio za Mwenge wa Uhuru, ikiwemo “Zingatia lishe yak...

Wadau wa Lishe watakiwa kuzingatia Sheria

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Maafisa lishe na watendaji wa kata wametakiwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu katika utekelezaji wa shughuli za lishe pamoja na kuwashirikisha wadau mbalimbali ili kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa afua za lishe. Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Kikao cha Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa Robo ya Nne ya Mwaka wa Fedha 2025/2026, Sakina Mbugi alipoongoza kikao hicho kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Dodoma kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. “Katika utekelezaji wa shughuli za lishe ni muhimu kuwashirikisha wadau mbalimbali, wakiwemo viongozi wa dini, wazee na vijana, ili kuwapatia uelewa kuhusu umuhimu wa lishe bora. Tunapompa mzee elimu sahihi ya lishe, tunamsaidia kupunguza changamoto za uzeeni na kujikinga dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza. Hivyo, nitumie nafasi hii kuwaelekeza maafisa lishe na maafisa watendaji wa kata kuzingatia sheria, kanuni na taratibu katika utekelezaji majukumu yenu,” alisema Mbugi. Mw...

Jiji la Dodoma latakiwa kushirikisha wadau afua za Lishe

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imetakiwa kuongeza ushirikishaji w a makundi mbalimbali ya jamii katika kuimarisha afua za lishe ili kuhakikisha elimu na huduma za lishe bora zinawafikia wananchi wote. Wito huo ulitolewa na Mwenyekiti wa Kikao cha Tathmini ya Mkataba wa Lishe kwa Robo ya Nne Aprili-Juni, 2026 Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Sakina Mbugi alipoongoza kikao hicho kwa niaba ya mkuu wa wilaya kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. Mbugi ambae ni katibu tawala wilaya ya Dodoma alisema kuwa ni muhimu kuwashirikisha vijana waliopo nje ya mfumo rasmi, wazee, viongozi wa dini, viongozi wa mila, taasisi za serikali na binafsi, watu mashuhuri pamoja na kaya katika kuhamasisha na kutoa elimu ya lishe bora. Ali sema kuwa ushirikishwaji wa makundi mbalimbali ya jamii ni muhimu katika kuongeza uelewa na kuleta matokeo chanya na kubainisha kuwa lishe bora haih usu watoto pekee bali watu wa rika zote. “Sisi, timu ya wataalam, tupo tayar...