Jiji la Dodoma laaga Timu ya Watumishi kuelekea SHIMISEMITA Mbeya
Na. Rahma Magona, DODOMA Uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma umeiaga rasmi timu ya watumishi itakayoiwakilisha Halmashauri hiyo katika mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Serikali za Mitaa Tanzania (SHIMISEMITA), yanayotarajiwa kufanyika jijjni Mbeya. Hafla hiyo ya kuwaaga watumishi hao ilifanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, ambapo watumishi hao wamepewa jukumu la kuiwakilisha Dodoma katika mashindano hayo na kurudi na ushindi. Akizungumza katika hafla hiyo Kocha wa Timu ya Mpira wa Miguu, Leonard Mkinga alisema kuwa kabla ya kuingia kwenye mashindano, watumishi wamejiandaa vizuri katika kipindi chote kwa kufanya mazoezi ya viwango vya juu. “Tumejiandaa vizuri na matarajio yetu lazima tukaoneshe ushindani wa hali ya juu na kutetea vikombe tulivyovipata mwaka jana” alisema Mkinga. Alisema kuwa ushiriki wa watumishi hao katika michezo unapaswa kwenda sambamba na utekelezaji wa majukumu yao ya msingi ya utumishi, huku michezo ikiwa na nafasi muhim...