Posts

Silage suluhisho la uhaba wa chakula cha mifugo Dodoma

Na. Mwandishi wetu, NZUGUNI Wafugaji wa ng’ombe katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamehimizwa kuanza kutengeneza na kuhifadhi chakula cha mifugo kilichochachushwa (Silage) ili kuhakikisha mifugo inapata lishe ya kutosha wakati wa kiangazi, kipindi ambacho maeneo mengi hukumbwa na upungufu mkubwa wa malisho kutokana na ukame. Rai hiyo ilitolewa na Afisa Mifugo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Delila Mlamka wakati akiwaelezea wananchi waliotembelea banda la mifugo la halmashauri hiyo katika maonesho ya Nanenane yanayoendelea jijini hapa. Alisema kuwa Silage ni chakula kinachotengenezwa kwa kuchanganya majani mabichi yaliyokatwakatwa, kiasi kidogo cha majani makavu, pumba na molases, kisha kuhifadhiwa kwenye mazingira yasiyoruhusu hewa ya oksijeni kuingia kwa siku 21 ili kichachuke vizuri na kuwa salama kwa matumizi ya mifugo. Alisema kuwa chakula hicho   kinaweza kutengenezwa kwenye mashimo au mapipa na kuhifadhiwa katika mifuko midogo ya plastiki na mifuko maalumu ya k...

Matenga yageuka lulu kilimo cha mbogamboga Dodoma

Image
Na. Mwandishi wetu, NZUGUNI Wananchi wanaoishi mijini, hususan kwenye nyumba za kupanga wametakiwa kutumia matenga, makopo ya maji na matairi yaliyotumika kuanzisha bustani za mbogamboga majumbani ili kujihakikishia upatikanaji wa chakula salama, kupunguza gharama za maisha na kuhifadhi mazingira. Wito huo ulitolewa na Afisa Kilimo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Zaidina Juma wakati wa maonesho ya 32 ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Malecela mjini Dodoma. Alisema kuwa kilimo cha kwenye matenga ni njia rahisi inayosaidia kuhifadhi mazingira huku kikitatua changamoto ya upatikanaji wa maeneo ya kulima. Alisema kuwa wananchi wengi wanaishi kwenye nyumba za kupanga au maghorofani ambako hakuna nafasi ya kuanzisha bustani za kawaida, lakini bado wanaweza kuzalisha mboga zao kwa kutumia vifaa vinavyotupwa na kula mboga zenye usalama, tofauti na baadhi ya mazao yanayouzwa sokoni ambayo wakati mwingine huvunwa muda mfupi baada ya kunyunyiziwa viuatilifu. ...

Kanda Namba Tatu yaimarisha ushirikiano na wamiliki wa vituo vya malezi ya watoto Dodoma

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Uongozi wa Kanda Namba Tatu umefanya kikao na wamiliki wa vituo vya malezi ya watoto (Daycare) vinavyopatikana ndani ya kanda hiyo kwa lengo la kuimarisha utoaji wa huduma za malezi na maendeleo ya watoto. Akizungumza katika kikao hicho kilihofanyika katika Ofisi ua Kanda, Meneja wa Kanda Namba Tatu, CPA. Christina Changwala aliwataka wamiliki wa vituo hivyo kuhakikisha wanatoa malezi yanayozingatia maadili, mila na tamaduni za kitanzania ili kujenga kizazi chenye maadili mema na chenye mchango chanya katika maendeleo ya taifa.   Aidha, aliwahimiza wamiliki wa vituo hivyo kuhakikisha wanakamilisha usajili wa vituo vyao ili vitambulike rasmi na viweze kuingizwa katika mifumo ya serikali ili kurahisisha usimamizi na utoaji wa huduma kwa mujibu wa sheria na taratibu. Wamiliki hao pia walikumbushwa umuhimu wa kutimiza wajibu wa kulipa kodi na tozo mbalimbali zinazotozwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma pamoja na mamlaka nyingine husika, kwa wakati kwa k...

Wakulima wahimizwa kupanda Marigold kufukuza wadudu shambani

Image
Na. Mwandishi wetu, NZUGUNI Wakulima wa vipando bustani katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kutumia maua aina ya Marigold kama njia ya asili ya kudhibiti wadudu na kuboresha mazingira ya mashamba, hatua inayolenga kupunguza matumizi ya dawa za viwandani katika kilimo. Ua aina ya Marigold Akizungumza katika maonesho ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Malecela Afisa Kilimo wa jiji hilo, Fatuma Doow alisema kuwa matumizi sahihi ya maua ya Marigold ni sehemu muhimu ya kuboresha afya ya mashamba na bustani kwa kuongeza thamani ya mandhari ya maeneo ya kilimo. Alisema kuwa maua ya Marigold yanapandwa pembezoni mwa vipando vya bustani na husaidia kuongeza urembo, sambamba na kusaidia kuzuia na kufukuza baadhi ya wadudu wanaoweza kuhamia kutoka katika mashamba mengine. “Ushauri wangu kwa wakulima wa mazao ya bustani ni kupanda maua pembezoni mwa mazao hayo ili kusaidia kupunguza matumizi ya dawa za wadudu na kuimarisha matumizi ya njia rafiki kwa mazingira...

Dodoma yazalisha Bayogesi kulinda utunzaji wa Mazingira na matumizi ya Nishati safi

Na. Mwandishi wetu, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeendelea kuonesha dhamira yake ya kulinda mazingira kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi kupitia uzalishaji wa bayogesi (Biogas) inayotokana na kinyesi cha mifugo na mabaki ya chakula ikiwa ni kuunga mkono za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania za kuhimiza matumizi ya nishati safi, uhifadhi wa mazingira na maendeleo endelevu. Akizungumza katika Maonesho ya Kitaifa ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Malecela, Nzuguni jijini Dodoma, Daktari wa Mifugo kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Innocent Kimweri alisema kuwa seksheni ya mifugo kimebuni mfumo wa kuzalisha bayogesi kwa kutumia kinyesi cha mifugo na mabaki ya chakula. Alisema kuwa ubunifu huo unalenga kupunguza uchafuzi wa mazingira, kuboresha usimamizi wa taka na kuongeza matumizi ya nishati mbadala. Akifafanua zaidi, alisema kuwa mfumo huo unahusisha kuchakata kinyesi cha mifugo na mabaki ya chakula kwa kuyapeleka kwenye mtambo maalu...

Barabara za Mtaa wa Mbwanga yafunguliwa, Diwani Kerenge aitaja kuwa chachu ya maendeleo

Image
Na. Mwandishi wetu, Dodoma Wakazi wa Mtaa wa Mbwanga katika Kata ya Mnadani wanatarajia kunufaika na usafiri rahisi, kuimarika kwa shughuli za biashara na kuongezeka kwa fursa za maendeleo kufuatia ufunguzi wa barabara za mtaa katika uboreshaji wa miundombinu kwa ajili ya maisha bora ya wananchi. Akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa barabara hiyo, iliyofanyika katika moja ya barabara hizo, Diwani wa Kata ya Mnadani, Mugendi Kerenge alisema kuwa uboreshaji wa miundombinu ya barabara ni nguzo muhimu ya maendeleo kwa kuwa unarahisisha usafirishaji wa watu na bidhaa, kuchochea biashara na kuongeza upatikanaji wa huduma za kijamii. “Kukamilika kwa barabara zaidi ya kilomita 14 zimefunguliwa   hii ni hatua muhimu katika safari ya maendeleo ya Kata ya Manadani. Itaondoa changamoto zilizokuwa zikiwakabili wananchi, hasa wakati wa mvua, na kufungua fursa zaidi za kiuchumi kwa wakazi wa Mbwanga na maeneo jirani. Natoa shukrani kwa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kwa kutuwezesha kufani...

Jiji la Dodoma lawapa vijana fursa mikopo ya 10%

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeendelea kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia mikopo ya asilimia 10, hatua inayowapa nafasi ya kuanzisha na kuendeleza shughuli mbalimbali za uzalishaji, ikiwemo viwanda vidogo, utengenezaji wa bidhaa na utunzaji wa mazingira. Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’wale, Husna Toni mara baada ya kutembelea vikundi vya vijana vinavyofanya shughuli mbalimbali katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alisema kuwa ziara hiyo imetoa fursa ya kujifunza namna vijana wa Jiji la Dodoma wanavyotumia mikopo ya asilimia 10 kujiajiri, kuongeza kipato na kuchangia maendeleo ya jamii. “Vijana wa Dodoma wana uthubutu mkubwa katika shughuli za uzalishaji, viwanda na utunzaji wa mazingira. Hii inatuonesha kwamba fursa zipo na vijana wakipewa mitaji na mazingira mazuri wanaweza kujiajiri na kuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya taifa” alisema Toni. Aliongeza kuwa vijana wanapaswa kutumia fursa zinazopatikana, husus...

Meya Chaula: Kanda za utoaji huduma kusogeza huduma kwa wananchi Dodoma

Image
Na. Mwandishi wetu, MAKUTUPORA Uanzishwaji wa kanda za utoaji huduma katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ni mkakati unaolenga kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi, kuongeza ufanisi wa utendaji kazi na kuharakisha maendeleo katika maeneo yote ya jiji. Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika jijini Dodoma, Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula   alisema kuwa mfumo wa kanda utarahisisha upatikanaji wa huduma mbalimbali za halmashauri, kupunguza muda wa wananchi kufuata huduma katika makao makuu ya jiji na kuongeza uwajibikaji kwa watendaji. Chaula ambae ni Diwani wa Kata ya Makutupora alisema kuwa kata hiyo ipo katika Kanda Namba Sita hivyo,   wananchi watapata huduma kwa urahisi zaidi, zikiwemo huduma za usafi wa mazingira, ukusanyaji wa mapato, usimamizi wa miradi ya maendeleo, pamoja na kushughulikia changamoto zinazojitokeza katika maeneo yao kwa wakati. “Madhumuni ya uanzishwaji wa kanda hizi ni kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora ...

Jiji la Dodoma laibuka na zana za upaliliaji, Maonesho ya Nanenane

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeendelea kung’ara katika Maonesho ya Nanenane kwa kuweka vitu vya kitofauti kama zana za upaliliaji ambazo zimeundwa na mjasiriamali mdogo wa ndani ya jiji. Akizungumza na waandishi wa habari mjasiriamali, Zuberi Nguzo aliyepata fursa ya kuonesha ujuzi katika maonesho hayo alisema kuwa zana hizo zimeundwa kwa muundo wa ‘power tiller’ ya miguu mitatu zikiwa katika ubora wa hali ya juu. “Zana hizi za upaliliaji zinatumia injini ya guta lakini ina mfumo wa rejeta kama kawaida. Pia ina mfumo wa feni na upande wa nyuma kuna jembe ambalo hili ndilo linatumika kwa ajili ya upaliliaji. Katika upaliliaji inatumia mfumo wa matuta kwa maana kwamba inapita katikati ya mstari na kuweka matuta kwenye mashina ya mahindi kwasababu tairi zake tumeweka kwa kipimo cha sentimita 62, hiki ni kipimo sahihi kabisa kwa upana kwa kilimo cha mahindi,” alisema Nguzo. Alisema kuwa ameamua kubuni zana hizo kwasababu baadhi ya vifaa vya kuundia vina...

Hospitali ya Jiji la Dodoma yatoa elimu ya unyonyeshaji maziwa ya mama

Image
Na. Mwandishi wetu, NALA Hospitali ya Jiji la Dodoma iliyopo Kata ya Nala imetoa elimu ya unyonyeshaji wa maziwa ya mama na lishe bora kwa akina mama 43 waliofika kupata huduma za kliniki, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Unyonyeshaji wa Maziwa ya Mama Duniani. Akifungua maadhimisho ya wiki hiyo, Afisa Lishe katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alpha Fanuel alisema kuwa mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo akina mama kuhusu unyonyeshaji sahihi na kuzingatia lishe bora ili kuboresha afya ya mama na mtoto. “Mama anaponyonyesha anachangia ukuaji bora wa mtoto, kuimarisha uhusiano kati ya mama na mtoto, kupunguza hatari ya baadhi ya magonjwa kama mzio kwa mtoto. Pia unyonyeshaji unasaidia kupunguza hatari ya saratani ya matiti kwa mama anayenyonyesha ipasavyo,” alisema Fanuel. Aliongeza kuwa washiriki wamepata mafunzo kwa vitendo kuhusu makundi sita ya chakula na namna ya kuandaa uji wenye virutubisho unaomsaidia mama anayenyonyesha kupata lishe bora na kuongeza uzalis...