Mwenge wa Uhuru 2026 wakabidhi gari la shilingi 121 Kikundi cha Vijana
Na. Dennis Gondwe, DODOMA KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2026, Wazo Mwang’onda ametembelea na kukabidhi gari lenye thamani ya shilingi 121,871,152.50 fedha kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kupitia mkopo ya asilimia nne kwa kundi la vijana baada ya kujiridhisha na utendaji kazi wa Kikundi cha Mwamko wa Vijana Kiuchumi. Tukio hilo lilifanyika katika Shule ya Sekondari Umonga baada ya kupokea taarifa ya Kikundi cha Mwamko wa Vijana Kiuchumi (MVK) na kushuhudia makala fupi ya safari na shughuli za kikundi. Kiongozi wa Mwenge wa Uhuru Kitaifa Wazo Mwang’onda alisema kuwa utaratibu wa serikali kutoa mikopo isiyo na riba kwa vijana ni uamuzi bora. Lengo la mikopo hii ni kuwakomboa vijana kwa kuwapatia mitaji kwa ajili ya kuendesha biashara na kufanya shughuli za kujiongezea kipato. Aidha, aliwapongeza vijana hao kwa ubunifu wao katika kutekeleza majukumu yao. Akisoma taarifa ya mradi wa Kikundi cha Mwamko wa Vijana Kiuchumi kinachojishughulisha ...