Posts

Vita dhidi ya Mbegu feki vyazaa matunda

Image
Na. Janeth Raphael MichuziTv - Bungeni Dodoma Serikali imeendelea kuimarisha hatua za kudhibiti na kutokomeza tatizo la mbegu feki nchini kupitia mifumo ya kisasa ya uthibitishaji wa ubora, ukaguzi wa mara kwa mara na utoaji wa elimu kwa wakulima. Akijibu swali la Mbunge wa Mbozi, Onesmo Merdson Mnkondya, kuhusu mpango wa Serikali wa kukomesha mbegu feki nchini, Naibu Waziri wa Kilimo, David Silinde amesema kuwa kwa mujibu wa Kifungu cha 15 cha Sheria ya Mbegu (Sura ya 308, Toleo la Urekebu la mwaka 2023), mbegu zote zinazouzwa nchini zinapaswa kuthibitishwa ubora wake na Taasisi ya Uthibitishaji wa Mbegu Tanzania (TOSCI). Silinde aliaema kuwa TOSCI imeanzisha matumizi ya lebo za kielektroniki zinazotolewa kwa kampuni za mbegu ili kuwasaidia wakulima kuhakiki uhalisia wa mbegu wanazonunua. Kupitia mfumo huo, mkulima anaweza kukwangua lebo maalum iliyowekwa kwenye kifungashio cha mbegu na kuingiza namba husika kwenye simu yake ya mkononi ili kupata taarifa za uthibitisho wa mbegu h...

Waziri Mavunde akabidhi vifaa vya Michezo UMISETA Dodoma

Image
  Na. Mwandishi wetu, DODOMA Wanafunzi wanaojiandaa kushiriki mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISETA) ngazi ya mkoa wamepata hamasa mpya baada ya kupokea vifaa vya michezo vilivyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Mtumba na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde. Vifaa hivyo vilikabidhiwa katika Shule ya Sekondari Dodoma kwa niaba ya Mbunge huyo kupitia Katibu wake, Silas Makanyaga, ambae alisema kuwa Jiji la Dodoma kupitia Ofisi ya Afisa Elimu Sekondari liliwasilisha ombi la vifaa vya michezo kwa ajili ya mashindano ya UMMISETA ngazi ya wilaya na mkoa, ambapo Mbunge amejitoa kusaidia kwa kununua jezi kwa kila mchezo. “Tunawaomba vijana wetu kucheza kwa nidhamu, kuwasikiliza walimu wao na kuendelea kufanya vizuri kama ilivyo desturi ya Jiji la Dodoma ambalo limeendelea kuwa kinara kwa ushindi wa makombe mbalimbali” alisema Makanyaga. Kwa upande, Afisa Elimu Sekondari Jiji la Dodoma, Mwl. Daniel Mapilya alisema kuwa tayari wanafunzi 120 kuto...

VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA JIJI LA DODOMA WAPEWA MAFUNZO YA MAADILI KATIKA UONGOZI NA UMUHIMU WA MAWASILIANO KWA VIONGOZI

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA VIONGOZI wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma watakiwa kusimamia misingi ya maadili na mawasiliano ili kulinda imani ya wananchi katika huduma wanazopewa.   Rai hiyo imetolewa wakati wa mafunzo maalumu ya uongozi yaliyofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, yakilenga kuwajengea uwezo viongozi hao katika kusimamia rasilimali na kuhudumia umma kwa uadilifu, huku wakionywa kuwa mmomonyoko wa maadili duniani sasa ni tishio linalohitaji udhibiti wa pamoja. Akiwasilisha mada kuhusu maadili na umuhimu wa mawasiliano katika uongozi, Mhadhiri kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa (Hombolo), Ng'omange Merkiad alisisitiza kuwa kuwepo kwa taratibu na kanuni madhubuti za kimaadili ni jambo la lazima ili kuwepo na tabia inayofanana na inayotabirika wakati wa kuwahudumia wananchi. "Maadili sio masimulizi tu ya maneno, bali ni maelekezo ya vitendo yanayomwongoza kiongozi kujua nini cha kufanya na kwa wakati gani katika utekelezaj...

Viwanda 17 vya kurejesha Taka za Plastiki vyaanzishwa Wilaya ya Dodoma

Na. Dennis Gondwe, DODOMA WILAYA ya Dodoma imefanikiwa kuanzisha viwanda 17 vya kurejesha taka za plastiki na kugawa vifaa 12 vya kutenganisha na kuhifadhi taka kwa lengo la kuweka mazingira safi na salama kwa shughuli na maisha kuendelea. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Alisema kuwa wilaya kwa kushirikiana na wadau wa mazingira ilifanikiwa kuanzisha viwanda 17 vya kurejeresha taka za plastiki, kugawa vifaa 12 vya kutenganisha na kuhifadhi taka na elimu inaendelea kutolewa kwa wananchi, mashirika na taasisi katika kudumisha utamaduni wa usafi na uhifadhi wa mazingira. “ Mheshimiwa Rais, wilaya inakadiriwa kuzalisha wastani wa tani 458 za taka ngumu kwa siku, ambapo wastani wa tani 305 sawa na asilimia 66.5 hupelekwa kwenye Da...

Shilingi 8,318,810,005 zatolewa kuboresha sekta ya Elimu Dodoma

Na. Dennis Gondwe, DODOMA WILAYA ya Dodoma imepokea shilingi 8,318,810,005 kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu zikihusisha elimu bila malipo na ujenzi wa miundombinu ya elimu kwa ajili ya kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Alisema kuwa katika kipindi cha Julai, 2025 hadi Aprili, 2026 Wilaya ya Dodoma ilipokea shilingi 8,318,810,005 kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu. Alisema kuwa kati ya fedha hizo, shilingi 3,777,397,654 ni kwa ajili ya elimu bila malipo kwa shule za Awali, Msingi na Sekondari na shilingi   4,541,412,351 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu. ” Mheshimiwa Rais , k wa Kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia, ufaulu umepanda katika shule za msingi k...

Shilingi Bil. 2.1 zatolewa kujenga miundombinu Sekta ya Afya

Na. Dennis Gondwe, DODOMA WILAYA ya Dodoma imepokea shilingi 2,145,756,727.12 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu na ununuzi wa samani na vifaa tiba katika jitihada za serikali kuboresha huduma za afya wilayani hapa. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Alisema kuwa k atika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2025/2026 wilaya ilipokea kiasi cha shilingi 2,145,756,727.12 kwa ajili ya sekta ya afya. “Kati ya fedha hizo shilingi 1,945,756,727.12 ni kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya afya na kiasi cha shilingi 200,000,000 ni kwa ajili ya ununuzi wa samani na vifaa tiba. Wilaya inakamilisha ujenzi wa Hospitali ya Jiji, Kituo cha Afya Zuzu, Chang’ombe, Msalato, Zahanati ya Kiwanja cha Ndege, Tambukareli na Jengo jumuishi Makole. Fedha hizi zim...

Mashine za Kieletroniki zakusanya Bil. 54.8 wilayani Dodoma

Na. Dennis Gondwe, DODOMA WILAYA ya Dodoma imekusanya shilingi 54,886,235,688.85 sawa na asilimia 76.6 ya lengo la mwaka la kukusanya shilingi 71,675,239,000 kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 kwa kutumia mashine za kieletroniki. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Akiongelea ukusanyaji kodi na mapato kwa mfumo wa TEHAMA, alisema kuwa wilaya inakusanya mapato ya serikali kupitia mfumo wa TAUSI. ” Mheshimiwa Rais, katika Mwaka wa Fedha 2023/2024 wilaya ilianza kutumia mfumo mpya uitwao TAUSI katika ukusanyaji wa vyanzo vyote vya mapato. Kwa kipindi cha kuanzia Julai, 2025 hadi Aprili, 2026, wilaya imefanikiwa k ukusanya shilingi 54,886,235,688.85 sawa na asilimia 76 .6 ya lengo la shilingi 71,675,239,000 kwa mwaka kwa kutumia mashine za...

Jiji la Dodoma lachangia Mil. 70 Mwenge wa Uhuru 2026

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imechangia shilingi 70,000,000 kufanikisha Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Wilaya ya Dodoma Mwaka 2026 zilizoongozwa na kaulimbiu isemayo ‘Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa pamoja Kuleta Maendeleo’. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Akiongelea michango ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026, alisema kuwa ulichangiwa na sekta ya umma na sekta binafsi. ” Mheshimiwa Rais, Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 zimechangiwa michango yenye jumla ya shilingi 100,944,500. Wananchi wamechangia shilingi 24,044,500, Halmashauri ya Jiji la Dodoma shilingi 70,000,000 na sekta binafsi pamoja na Mashirika ya Umma shilingi 6,900,000. Kati ya fedha hizo shilingi 5,460,000 zimerejeshwa kuchangia un...

Huduma ya Maji kuimarika Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALI ya upatikanaji wa huduma ya Maji safi na salama imeendelea kuimarika hadi kufikia lita 88.7 kwa siku sawa na asilimia 55 ya mahitaji yote. Kauli ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Alisema kuwa h ali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama ni lita Mil. 88.7 kwa siku sawa na asilimia 55 ya mahitaji ya wakazi wote ambayo ni lita Mil. 159.9. DUWASA imeendelea kutekeleza miradi 38 ya shilingi bilioni 91. ambayo ikikamilika itaongeza upatikanaji wa Maji kwa zaidi ya asilimia 75 ya mahitaji ya siku. MWISHO  

Dodoma kuvuna Tani 40,930 Chakula na Nafaka

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WILAYA ya Dodoma inatarajia kuvuna tani 40,930 za mazao ya chakula na biashara katika kuwahakikishia wananchi lishe bora na kujikwamua kiuchumi. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Alisema kuwa w ilaya kupitia Divisheni ya Kilimo Mjini na wadau iliendelea kuhakikisha wananchi wanapata lishe bora na kujikwamua kiuchumi kwa kulima mazao ya chakula na biashara. “Hali ya upatikanaji wa chakula na bei ni ya wastani kwa msimu wa kilimo 2025/2026. Wakulima wameanza kuvuna na kiasi cha tani 40,930 kinatarajiwa kuzalishwa. Hata hivyo, kuna mtiririko mzuri wa mazao ya chakula yanayoingia na kupatikana katika masoko yote. Hivyo, kuhakikisha upatikanaji wa chakula katika kipindi chote cha mwaka” alisema Mbugi. Akiong...