Posts

Hazina Volleyball yaiduwaza Dodoma Jiji Seti 2-0 Mwenge Super Cup

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA TIMU ya Wanaume ya Mpira wa Mikono ya Hazina (Hazina Volleyball Club) imeibuka na ushindi wa Seti 2-0 dhidi ya Timu ya Dodoma Jiji mchezo uliochezwa katika viwanja vya Chinangali Park mapema leo. Akiongelea mchezo huo, Nahodha wa Timu ya Hazina Volleyball Club, George Kalunde alisema timu yake ilijiandaa vizuri kuelekea mchezo huo ndio sababu ya kupata ushindi wa Seti 2-0. Aidha, aliipongeza Wilaya ya Dodoma kwa kuandaa mashindano ya Mwenge Super Cup Mwaka 2026 na kutaja maandalizi hayo kuwa ni ubunifu mkubwa. “Nitumie nafasi hii kuwahamasisha vijana wenzangu kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mapokezi na mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 katika Wilaya ya Dodoma, karibuni sana. Nae Nahodha wa Timu ya Mpira wa Mikono ya Dodoma Jiji, Muhidin Mwenda alisema kuwa mchezo ulikuwa mzuri pamoja na kufugwa. “Tunapenda kumshukuru Mungu tumemaliza mechi salama, pamoja na kuwa tumepoteza mechi kwa seti 2-0, siyo matokeo mazuri kwetu. Mashindano haya yamekuwa c...

Dodoma Jiji yaangukia pua dhidi ya Ujenzi Queens Mwenge Super Cup

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA TIMU ya Mpira wa Pete ya Wizara ya Ujenzi (Ujenzi Queens) imeibuka kidedea kwa kuifunga Timu ya Mpira wa Pete ya Dodoma Jiji kwa magoli 37-33 katika mchezo wa kuvutia uliochezwa katika viwanja vya Chinangali Park. Mchezo huo ulianza kwa kasi ya kawaida na kuendelea kushika kasi kadri muda ulivyokuwa ukisogea. Hadi mchezo unamalizika, Timu ya Ujenzi Queens iliikuba na ushindi wa magoli 37 dhidi ya 33 ya Dodoma Jiji. Awali Kocha wa Timu ya Mpira wa Pete ya Ujenzi Queens Mwamvita Mzee alisema kuwa wamekuwa wakipata matokeo mazuri kutokana na kufanya mazoezi mara kwa mara. “Timu yetu inaamini katika mazoezi ya mara kwa mara. Kama unavyofahamu mazoezi hayadanganyi, tumekuwa tukifanya mazoezi kwa bidii ndiyo siri ya mafanikio yetu. Zidi ni kupendana kama timu na watu kujitoa kwa ajili ya timu na kuupenda mchezo. Pia, kwetu ni utekelezaji wa maelekezo ya Mheshimiwa Rais wa Tanzania ya kufanya mazoezi kwa watumishi mahala pa kazi” alisema Mzee.   Kwa upa...

Ujenzi Queens bega kwa bega na Mwenge wa Uhuru, 2026 Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WIZARA ya Ujenzi inaunga mkono Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 utakaoanza mbio zake tarehe 1 Juni, 2026 katika Wilaya ya Dodoma kwa kushiriki katika mashindano ya Mwenge Super Cup yakilenga kuhamasisha jamii kujiandaa na mapokezi ya Mwenge huo kwa kudumisha amani na umoja wa kitaifa. Kocha wa Timu ya Wizara ya Ujenzi (Ujenzi Queens), Mwamvita Mzee Kauli hiyo ilitolewa na Kocha wa Mchezo wa Mpira wa Pete wa Timu ya Wizara ya Ujenzi (Ujenzi Queens), Mwamvita Mzee alipokuwa akiongea na mwandishi wetu muda mfupi kabla ya kuanza mchezo wao na Timu ya Mpira wa Pete ya Dodoma Jiji katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. Mzee alisema kuwa hamasa ya Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 kwa wanamichezo ni kubwa katika Wilaya ya Dodoma. “Sisi Timu ya Mpira wa Pete ya Wizara ya Ujenzi tumehamasika kuja kuunga mkono ujio wa Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 katika Wilaya ya Dodoma. Lengo ni kuonesha umoja na mshikamano baina ya wanamichezo kama dhamira ya Mwenge wa Uhuru Mwaka 2...

MIL. 544,335,626 ZAJENGA SHULE YA SEKONDARI MICHESE

Na. Dennis Gondwe, MKONZE SHILINGI 544,335,626 zimekamilisha ujenzi wa Shule ya Sekondari Michese na kuwawezesha wanafunzi 555 kupata elimu ya sekondari karibu na maeneo wanayoishi na kuwaondolea kero ya kutembea umbari mrefu kufuata elimu. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo alipokuwa akisoma taarifa ya ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari Michese kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya TAMISEMI iliyotembelea na kukagua ujenzi wa shule hiyo. Fungo alisema “k iasi cha fedha kilichotolewa kwa ajili ya ujenzi ni shilingi 544,225,626 chanzo cha fedha kikiwa ni SEQUIP. Fedha zilipokelewa Mwezi Oktoba, 2023 na ujenzi ulianza rasmi Mwezi Novemba, 2023 na kukamilika Mwezi Mei, mwaka 2024. Utaratibu wa ujenzi uliotumika ni force akaunti na mradi ulikamilíka kwa wakati na shule ilianza rasmi mwaka 2024 na kusajiliwa kwa jina la Michese Sekondari, Namba ya usajili S.6625”. Alisema kuwa u jenzi wa shule hiyo ulifanyika kwa awamu tatu, awamu ya kw...

JIJI LATEKELEZA MKAKATI WA KUBORESHA MAENEO YA WAZI

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma inatekeleza mkakati wa uboreshaji maeneo ya wazi kwa kusimamia udhibiti na usimamizi wa sheria na kufanya uondoaji wa maendelezo ya kudumu yaliyokiuka masharti na kuboresha miundombinu ya maeneo ya michezo. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo alipokuwa akisoma taarifa ya uboreshaji wa maeneo ya wazi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) iliyofanya ziara katika jiji hilo. Fungo alisema kuwa halmashauri ilifanya zoezi la mapitio ya hali ya maeneo ya wazi ili kubaini kama yanatumika kwa mujibu wa sheria. “Halmashauri inatekeleza mkakati wa u dhibiti na usimamizi wa sheria katika maeneo ya wazi, zoezi la uondoaji wa maendelezo ya kudumu yaliyokiuka masharti ya uendelezaji limefanyika katika eneo la wazi lililopo Majengo maarufu kama kwa Kato, eneo la Rose Garden na maeneo mengine 47 ambayo tayari wame...

JIJI LA DODOMA LATUMIA MIL. 23 KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imetumia zaidi ya shilingi milioni 23 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo fedha kutoka serikali kuu, mapato ya ndani na wahisani pamoja na bakaa. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Fungo alipokuwa akiwasilisha taarifa fupi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI). Alisema kuwa katika kipindi cha kuanzia Julai, 2025 hadi kufikia Machi, 2026 halmashauri imetumia jumla ya shilingi 23,815,713,415.02 sawa na asilimia 91.19 ya fedha zilizopokelewa kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo. “Kati ya fedha hizo, shilingi 6,406,582,002.56 ni fedha kutoka serikali kuu, shilingi 16,807,859,627.46 mapato ya ndani, shilingi 601,771,785.00 fedha za wahisani na shilingi 5,279,467,344.52 ni fedha za bakaa. Kwa kipindi cha kuanzia Julai, 2025 hadi kufikia Machi, 2026, hal...

JIJI LA DODOMA LATOA VIWANJA 1,900 KWA WAFANYAKAZI

Image
  Na. Mwandishi wetu, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeibuka kivingine katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani kwa kuachia viwanja zaidi ya 1,900 vya matumizi mbalimbali kwa ajili ya wafanyakazi na wananchi kwa ujumla ili waweze kufurahia fursa ya kumiliki kiwanja katika makao makuu ya nchi. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa Baraza la Wafanyakazi la Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dennis Gondwe alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu nafasi ya Halmashgauri ya Jiji la Dodoma katika kujali makazi ya wafanyakazi katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika ngazi ya mkoa katika Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma. “Nitumie nafasi hii kuwashauri na kuwashawishi wafanyakazi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma na wengine wote kuhakikisha wananunua viwanja katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Hii itaweka alama kwa utumishi wao katika halmshauri, lakini kwa wale walio nje ya halmshauri itaweka alama kwa kumiliki kiwanja kihalali katika makao makuu...

MADIWANI JIJI LA DODOMA WATAKIWA KUTATUA KERO ZA WANANCHI

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma watakiwa kusikiliza kero za wananchi na kuhakikisha zinapatiwa ufumbuzi kwa wakati ili kuimarisha maendeleo na ustawi wa jamii. Hayo aliyasema Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaji Jabir Shekimweri, wakati alipokuwa akizungumza katika Mkutano wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alisema kuwa madiwani ni kiungo muhimu kati ya serikali na wananchi, hivyo wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kushughulikia changamoto zinazowakabili wananchi katika maeneo yao. “Madiwani ni sauti ya wananchi. Ni muhimu msikilize kwa umakini kero zao na kuzitatua kwa wakati ili kuondoa malalamiko yasiyo ya lazima na kuongeza imani ya wananchi kwa serikali yao” alisema Alhaji Shekimweri. Aliongeza kuwa utekelezaji wa majukumu hayo unahitaji uwajibikaji, ushirikiano na ufuatiliaji wa karibu wa miradi ya maendeleo ili kuhakikisha inaleta matokeo yaliyokusudiwa. Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya ...

OFISI ZA KANDA ZASOGEZA HUDUMA KWA WANANCHI DODOMA

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Jiji la Dodoma lilianzisha Kanda Saba kwaajili ya kusogeza huduma kwa wananchi lakini lengo kuu likiwa ni kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato ya ndani ya halmashauri ambayo yanatumika katika kuleta maendeleo kwa jamii. Akizungumza katika Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma la kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa kazi zilifanyika kwa kipindi cha robo ya tatu, Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula alisisitiza umuhimu wa matumizi ya mfumo wa kanda katika kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya ndani. Aidha, alisisitiza umuhimu wa kubuni vyanzo vipya na kuviimarisha vilivyopo. Alisema kuwa mfumo wa kanda umeendelea kutoa mafanikio makubwa kwa kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa mapato, kuimarisha usimamizi wa vyanzo vya mapato na kuongeza uwajibikaji kwa wataalam waliopo katika maeneo husika. "Katika kipindi cha robo ya tatu, matumizi ya mfumo wa kanda yamesaidia kuongeza ufuatiliaji wa karibu wa vyanzo ...

KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI KUTOA ELIMU YA KINGA KWA VIJANA DODOMA

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Kamati ya Kuzuia na Kudhibiti UKIMWI ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kushirikiana na Taasisi ya DOYODO imeendelea kutoa elimu na mafunzo kwa jamii, hususan kwa vijana, ili kuhakikisha wanapata uelewa sahihi wa namna ya kujikinga na ugonjwa huo. Hayo aliyasema Mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Dodoma (WASEMI), Leticia Sanga tarehe 29 Aprili, 2026 wakati alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za kudhibiti UKIMWI kwa kipindi cha robo ya tatu kuanzia Januari hadi Machi, 2026 katika Mkutano wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alisema kuwa juhudi hizo zimeanza kuzaa matunda, lakini bado kuna haja ya kupanua wigo wa elimu hiyo. “Tumekuwa tukiwalenga zaidi vijana, lakini sasa tumeona umuhimu wa kuwafikia pia wazee. Wazee wengi wamekuwa waathirika wakubwa wa janga hili kwa sababu wanabeba jukumu la kuwahudumia watoto wao wanaoishi na virusi vya UKIMWI. Hivyo, nao wanahitaji elimu hii kwa kina zaidi” al...