Posts

Prof. Mohamed ahimiza wanafunzi kusoma kwa bidii na kuwapongeza wazazi

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Makutupora watakiwa kuwa na nidhamu na kusoma kwa bidii ili kufikia malengo yao ya kielimu na maisha kwa ujumla. Hayo aliyasema Katibu Mtendaji Baraza la Mitihani la Tanzania, Prof. Said Mohamed wakati wa Uzinduzi wa Upandaji Miti mwaka 2025/2026 uliofanyika katika Shule ya Sekondari Makutupora Jijini Dodoma. Alisema kuwa juhudi za wanafunzi katika masomo ni msingi muhimu wa maendeleo yao binafsi na taifa kwa ujumla. “Msingi mzuri wa watoto ni kupata elimu hivyo niwasihi wanafunzi muendelee kusoma kwa bidii ili kuweza kufikia ndoto zenu, kwasababu hapa kuna viongozi wa baadae ambao wataweza kuongoza taifa letu, lakini pia muwe na nidhamu kwasababu nidhamu ndio hupelekea kufika mbali hususan katika masomo yenu” alisema Prof. Mohamed. Aidha aliwapongeza wazazi kwa juhudi wanazozifanya katika malezi ya watoto. “Nipende kuwapongeza wazazi kwa namna ambavyo mnaendelea kuwalea watoto katika misingi bora, lakini pia nisisitize u...

EID Mubarak toka Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma

Image
 

Meya Chaula atoa Salam za Eid Dodoma

Image
 

Jiji la Dodoma kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Image
 

Wanawake watakiwa kulipa kodi na kukuza uchumi katika Jiji la Dodoma

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Wanawake wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, hususan wafanyabiashara na wajasiriamali, wametakiwa kuendelea kulipa kodi na tozo kwa wakati ili kuchangia maendeleo ya jiji pamoja na kukuza uchumi wao na wa jamii kwa ujumla. Wito huo ulitolewa na Diwani wa Viti Maalum Tarafa ya Zuzu, Pilly Hassan, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayotarajiwa kufanyika tarehe 8 Machi, 2026. Alisema kuwa ulipaji wa kodi ni moja ya njia muhimu inayosaidia serikali   kupata mapato ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo kuboresha miundombinu ya masoko, barabara na huduma nyingine muhimu kwa wananchi. “Wanawake wengi wa Jiji la Dodoma tunajishughulisha na shughuli za biashara na ujasiriamali. Hivyo, tunapaswa kuwa mfano mzuri kwa kuhakikisha tunatimiza wajibu wetu wa kulipa kodi na tozo za serikali kwa hiari na kwa wakati. Kupitia kodi hii itaweza kutusaidia mambo mbalimbali na ya muhimu kama vile kujeng...

Mstahiki Meya Chaula ashauri Baraza kutumia mkakati wa hoja kwa hoja

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula ameshauri Baraza la Madiwani kujenga utaratibu wa kuwasilisha hoja moja na kuiazimia hadi itakapokamilika ndio hoja nyingine ifanyiwe kazi. Aliyazungumza hayo kwa msisitizo katika mkutano wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri jijini Dodoma. Alisema kuwa mkakati huo wa hoja moja ‘Focus Strategy’ ndiyo njia pekee ya kuleta maendeleo yanayoonekana na yenye tija kwa wananchi wanaowaongoza. "Ili tuwe na ufanisi, niwaombe kwa unyenyekevu mkubwa sana tuchague jambo moja na kuliazimia hadi mwisho. Kwa mfano, kama baraza linaona kipaumbele ni ujenzi wa matundu ya vyoo kwa shule zote za msingi katika jiji letu, basi nguvu, fedha, na usimamizi wetu wote uelekezwe hapo. Tukimaliza na kujiridhisha kuwa kila shule ina vyoo bora, ndipo tunahamia hoja nyingine ya msingi na kuendelea na mtiririko huo" alisema Chaula. Alimalizia kwa kutoa rai kuwa umoja na maamu...

Shule ya Msingi Mazengo ipo moto

Image

Huduma ya Lishe kwa Shule za Dodoma

Image
 

Stadi za Maisha Kuwa mkombozi kwa wanafunzi wa Sekondari jijini Dodoma

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Elimu ya Stadi ya Maisha imetajwa kuwa ni chachu ya mabadiliko chanya kwa wanafunzi katika kuwajengea uwezo wa kujitambua na kukabiliana na changamoto za maisha katika shule za sekondari jijini Dodoma. Hayo aliyasema Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Daniel Mapilya wakati akifungua mafunzo kwa wawezeshaji wa stadi za maisha katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Dodoma. Alieleza kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha wawezeshaji wanapata uelewa wa kutosha juu ya namna bora ya kuwafikia wanafunzi na kuwajengea misingi imara ya maisha. “Tunapozungumzia stadi za maisha, tunalenga kumsaidia mwanafunzi kujitambua, kujiamini na kufanya maamuzi sahihi. Elimu hii itawawezesha vijana wetu kuepukana na vishawishi vinavyoweza kuathiri masomo na mustakabali wa maisha yao” alisema Mapilya. Aliongeza kwa kusema kuwa changamoto nyingi zimekuwa zikiwakumba watoto wa kike. ”…zikiwemo shinikizo la rika na mazingira yasiyo rafiki, hivyo elimu hiyo it...

Utatuzi mgogoro wa Mahomanyika watangazwa

Image
Na. Nancy Kivuyo , NZUGUNI Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeunda timu mbili ya wataalam wa upangaji na upimaji na timu ya uhakiki kwaajili ya kutatua mgogoro wa ardhi wa muda mrefu katika eneo la Mahomanyika. Timu hizo zimeundwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt. Leonard Akwilapo alipokuwa akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika eneo la Mahomanyika, Kata ya Nzuguni jijini Dodoma. Alisema kuwa timu hizo zitaanza kazi mara moja ili kuhakikisha zoezi hilo linakamilika kwa wakati. “Eneo la Mahomanyika ni la serikali kwahiyo , naagiza lipangwe na kupimwa kwaajili ya kutatua mgogoro huu na kuwa kielelezo cha utatuzi wa migogoro mingine iliyopo ndani ya Jiji la Dodoma. Timu hizi zinapaswa kufanya kazi ndani ya siku 60 na kukamilisha zoezi hili ili kila mmoja ajue amepata nini na anaenda wapi” alisema Dkt. Akwilapo. A liongeza kuwa wale wote waliohusika kwenye kadhia ya mgogoro huo wa ardhi watachukuliwa kwaajili ya maho...