Na. Dennis Gondwe, DODOMA WILAYA ya Dodoma imepokea shilingi 8,318,810,005 kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu zikihusisha elimu bila malipo na ujenzi wa miundombinu ya elimu kwa ajili ya kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Alisema kuwa katika kipindi cha Julai, 2025 hadi Aprili, 2026 Wilaya ya Dodoma ilipokea shilingi 8,318,810,005 kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu. Alisema kuwa kati ya fedha hizo, shilingi 3,777,397,654 ni kwa ajili ya elimu bila malipo kwa shule za Awali, Msingi na Sekondari na shilingi 4,541,412,351 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu. ” Mheshimiwa Rais , k wa Kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia, ufaulu umepanda katika shule za msingi k...