Posts
Afisa Biashara Arusha apongeza ukuwaji wa Biashara wa Jiji la Dodoma
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Mwandishi wetu, DAR ES SALAAM HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imepongezwa kwa kasi ya ukuaji wa shughuli za biashara na uwekezaji na kutajwa kuwa ni fursa kwa watanzania na wageni kuwekeza. Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Biashara, Viwanda na Uwekezaji Halmashauri ya Jiji la Arusha, John Kilunge alipotembelea banda la Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam. Kilunge alipongeza kasi ya ukuaji wa shughuli za biashara na uwekezaji ndani ya jiji hilo na kusema kuwa ni fursa kwa watanzania na wageni kuwekeza na kufungua zaidi fursa za ajira. Akiwa katika banda hilo, alipata maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma pamoja na fursa za uwekezaji zilizopo, hususan katika sekta za ardhi, biashara na maendeleo ya kiuchumi. Alisema kuwa Jiji la Dodoma linaonesha mafanikio makubwa katika kukuza mazingira ya biashara na kuvutia wawekezaji k...
Jiji la Dodoma lashauriwa kulinda hadhi ya Makao Makuu ya Nchi
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Mwandishi wetu, DAR ES SALAAM HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeshauriwa kuendelea kusimamia Mpango Kabambe wake ili kuhakikisha jiji linakuwa na mpangilio wa kisasa na kulinda hadhi ya makao makuu ya nchi. Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, Jenifa Omolo (kushoto) akiongea na wataalam wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana, Jenifa Omolo alipotembelea banda la Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwl. Julius Nyerere jijini hapa. Alisema kuwa ukuaji wa Jiji la Dodoma unapaswa kwenda sambamba na upangaji bora wa maeneo, miundombinu na mazingira ya mji ili kuongeza mvuto zaidi kwa wakazi, wawekezaji na wageni wanaofika kwa shughuli mbalimbali za kiserikali na kiuchumi. Alisisitiza kuwa taswira ya mji ambao ni makao makuu ya nchi inapaswa kuonekana wazi kupitia mpangilio wa kisasa, unaozing...
Jiji la Dodoma latangaza fursa za Uwekezaji katika Maonesho ya Sabasaba, 2026
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Mwandishi wetu, DAR ES SALAAM Halmashauri ya Jiji la Dodoma imejipanga kujitangaza kama kitovu cha uwekezaji, biashara na maendeleo ya kisasa kutokana na kuwa na fursa nyingi kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi jambo linalokuza ustawi wa wananchi na taifa kwa ujumla. Afisa Habari, Nancy Kivuyo kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma (kulia) akielezea fursa za uwekezaji kwa mdau aliyetembelea banda ya halmashauri Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Habari katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Nancy Kivuyo alipokuwa akiwaelezea wananchi waliotembelea banda lao jinsi Halmashauri ya Jiji la Dodoma inavyoshiriki katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) mwaka 2026 yanayofanyika katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini hapa. Kivuyo alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika kuhakikisha inavutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi, imeendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji. “Mazingira ya uwekezaji yameboreshwa sambamba na mazingira ya kufanya...
Maafisa Biashara wa Morogoro na Ruvuma watembelea Banda ya Jiji la Dodoma katika Maonesho ya Sabasaba, 2026
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Maafisa Biashara kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma leo tarehe 1 Julai, 2026 wametembelea Banda la Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. Wakiwa katika banda hilo, maafisa hao walipata maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma, ikiwemo ushauri na miongozo kwa wananchi na wawekezaji kuhusu upatikanaji wa maeneo ya uwekezaji na huduma za ardhi, fursa za biashara katika sekta za kimkakati zinazokuwa kwa kasi pamoja na taratibu za uwekezaji ndani ya jiji Akizungumza baada ya kutembelea banda hilo, Mkuu wa Divisheni ya Biashara, Viwanda na Uwekezaji kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Lusajo Mwasongwe alisema kuwa wamejifunza mambo mbalimbali yanayoweza kuwasaidia kuboresha utoaji wa huduma katika mamlaka zao. “Tumepata uzoefu mzuri ...
Katibu Mkuu Uchukuzi aipa tano TASAC kwa kuendelea kuwafikia wadau
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Immaculate Ruzika, DODOMA Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara, leo ametembelea banda la Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) katika maonesho yanayoendelea kwenye viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. Akiwa katika banda hilo, Prof. Kahyarara alipatiwa maelezo kuhusu juhudi za TASAC katika kuhakikisha usalama, ulinzi na ubora wa huduma za usafiri wa majini kwa wananchi. Akizungumza baada ya kutembelea banda hilo, Prof. Kahyarara aliipongeza TASAC kwa kushiriki maonesho hayo na kutumia jukwaa hilo kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu na huduma zake kwani elimu hiyo inasaidia kuongeza uelewa na kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi na wananchi. Maonesho hayo yenye kauli mbiu ya "Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu" yalianza rasmi tarehe 16 na yanataria kufika tamati kesho tarehe 23 juni, 2026.
Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali Inafanya Kazi Kubwa – Prof. Kahyarara
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Aipongeza Wizara ya Habari Maandalizi AFCON 2027 Na. Adelina Johnbosco - MAELEZO Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara, ameipongeza Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali na kusema inafanya kazi kubwa ya kuzitangaza shughuli zinazotekelezwa na Serikali pamoja na kuwafikia wananchi. Prof. Kahyarara alisema hayo Juni 22, 2026, alipotembelea banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na taasisi zake katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kwenye viwanja vya Chinangali, jijini Dodoma. "Serikali ina shughuli nyingi zinazofanyika ikiwemo miradi mbalimbali, mipango na malengo kwa ajili ya maendeleo na maslahi ya wananchi, hata ukisema kila siku au kila wiki utoke na kitu kimoja lakini bado inakuwa haitoshi, lakini Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali inajitahidi kwa kufanya kazi kubwa kwani taarifa zinatolewa kuhusu yanayotekelezwa na Serikali kwa wananchi wake" aliongeza Prof. Kahyarara. Kwa upande mwingine, aliipongeza...
Zaidi ya wananchi 300 watembelea banda la TARURA Wiki ya Utumishi wa Umma
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
# Wananchi wa Kimara kunufaika na ujenzi wa barabara ya TRA - King'ongo Na. Mwandishi wetu, DODOMA ZAIDI ya wananchi 300 wametembelea banda la Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) tangu kuanza kwa Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, wakipata elimu na ufafanuzi kuhusu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya barabara za wilaya katika maeneo yao. Hatua hiyo imeendelea kuimarisha uhusiano kati ya wananchi na taasisi hiyo, huku ikitoa fursa ya kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi moja kwa moja. Akizungumza katika maonesho hayo, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma, Catherine Sungura alisema kuwa wananchi wanaowasilisha kero zao huunganishwa moja kwa moja na mameneja wa maeneo husika ili kupata maelezo ya kina na ufumbuzi wa haraka. “Tunawapokea wananchi wengi kutoka maeneo tofauti ya Tanzania ambao wengi wanataka kufahamu ujenzi au matengenezo ya barabara katika maeneo yao na hivyo wengi wao wanapata majibu hapo hapo kwani wan...
DG TANESCO atembelea Banda la EWURA CCC, apongeza utendaji kazi
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Lazaro Twange, amelipongeza Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA CCC), kwa mchango wake katika kupokea, kusaidia na kufuatilia utatuzi wa malalamiko ya watumiaji wa huduma za nishati na maji, hatua inayosaidia huduma zinazodhibitiwa na EWURA ikiwemo huduma ya umeme kuboreshwa kwa maslahi ya wananchi. Twange ametoa pongezi hizo leo, Juni 19, 2026, baada ya kutembelea banda la EWURA CCC katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. Akizungumza katika banda hilo, Twange amesema kazi inayofanywa na EWURA CCC ya kupokea, kusaidia na kufuatilia utatuzi wa malalamiko ya huduma za umeme imekuwa chachu ya maboresho ya huduma hiyo, ikiwemo kupungua kwa baadhi ya changamoto zilizokuwa zikilalamikiwa mara kwa mara. “Tunatambua mchango mkubwa wa EWURA CCC katika kuwawakikisha wananchi na kufuatilia utatuzi wa changam...
Waziri Mkenda: Michezo na Sanaa shuleni haitaondolewa tena
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Na. Denis Mlowe, IRINGA WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema serikali imejipanga kuhakikisha michezo na sanaa zinaendelea kupewa nafasi kubwa katika mfumo wa elimu nchini, akisisitiza kuwa shughuli hizo hazitaondolewa tena shuleni kwa kuwa ni sehemu muhimu ya kukuza vipaji, afya, ajira na ushindani wa kimataifa. Waziri Mkenda alitoa kauli hiyo wakati akifungua rasmi Mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) 2026 yaliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Lugalo mkoani Iringa. Katika hotuba yake, Waziri Mkenda aliushukuru Mkoa wa Iringa kwa kuwa mwenyeji wa mashindano hayo, akisema mkoa huo umeendelea kuwa kivutio kutokana na mazingira yake mazuri na ukarimu wa wananchi wake. “Tunafurahi sana kuja Iringa tunawashukuru viongozi na wananchi wote wa Iringa kwa kutupokea na kuwa wenyeji wa mashindano haya muhimu kwa maendeleo ya michezo nchini,” alisema. Aidha, aliwapongeza wanafunzi, walimu na viongo...