Posts

Waziri Kikwete kufungua Wiki ya Kitaifa ya Utumishi wa Umma 2026

Image
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete Jumatano tarehe 17/06/2026 anatarajiwa kufungua Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 kwenye Viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma. Kaulimbiu ya Mwaka 2026 ni “ Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Maendeleo Endelevu ”

Kigamboni Vijana Unity wakabidhiwa Bajaji 5, Mkopo usio ya riba wa Jiji la Dodoma

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Kikundi cha Kigamboni Vijana Unity kutoka Mtaa wa Kigamboni, Kata ya Kikuyu Kaskazini kimekabidhiwa Bajaji tano kupitia mkopo usio na riba wa asilimia 10 unaotolewa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kupitia Benki ya NMB ili kukiwezesha kikundi kujiajiri na kujikwamua kiuchumi. Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano hayo yaliyofanyika katika viunga vya Manispaa ya zamani jijini hapa, Kaimu Meneja wa Kanda ya Kati wa NMB, Amos Mubusi alisema kuwa benki hiyo inaendelea kushirikiana na serikali katika kuwawezesha vijana na makundi maalum ili kukuza biashara na kuongeza ushiriki wao katika uchumi. Mubusi alisema kuwa Benki ya NMB imetoa mikopo yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni tatu kwa vikundi 304 nchini, wakati Halmashauri ya Jiji la Dodoma, vikundi 19 vikipatiwa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 228. Aidha, aliwataka wanachama wa Kigamboni Vijana Unity kutumia fursa hiyo kwa uwazi, nidhamu na uaminifu ili kuhakikisha mradi huo unaleta ...

Bodaboda Mtaa wa Kigamboni wanufaika na Kliniki ya kutatua kero

Image
Na. Mwandishi wetu, KIKUYU KASKAZINI MTAA wa Kigamboni umewatembelea maafisa usafirishaji kusikiliza changamoto zao na kuwaelezea fursa ya mikopo isiyo na riba ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa makundi ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu ili waweze kunufaika nayo. Akizungumza na maafisa usafirishaji wa Mtaa wa Kigamboni Kata ya Kikuyu Kaskazini, Afisa Mtendaji Mtaa wa Kigamboni, Farijala Kunga alisema kuwa serikali ina wajibu wa kuwatembelea na kuwasikiliza wananchi wake. “Leo Serikali ya Mtaa wa Kigamboni imewatembelea maafisa usafirishaji (waendesha bodaboda) katika Mtaa wa Kigamboni kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi. Huu ni utekelezaji wa maelekezo ya serikali wa kuyafikia makundi mbalimbali kuyasikiliza na kutatua kero zao. Aidha, tumewaelezea fursa za mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri ya jiji la Dodoma kwa makundi ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu. Tumewapa elimu kuhusu manufaa ya kiuchumi ya mikopo hiyo ukiwa ...

Ujenzi wa madarasa 3 S/M Mazengo kukamilika Julai, 2026

Image
Na. Mwandishi wetu, KIKUYU KASKAZINI   Uongozi wa Mtaa wa Kigamboni, Kata ya Kikuyu Kaskazini umepongeza kasi ya ujenzi madarasa matatu katika Shule ya Msingi Mazengo kwa gharama ya shilingi 71,373,640 kwa lengo la kuboresha mazingira ya wanafunzi kujifunzia na kuelekeza mradi huo kukamilika kwa wakati.   Pongezi hizo zilitolewa na Afisa Mtendaji Kata ya Kigamboni, Farijala Kunga alipoongoza wajumbe wa Serikali ya Mtaa wa Kigamboni na maafisa ugani wa Kata ya Kikuyu Kaskazini kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa madarasa matatu katika Shule ya Msingi Mazengo. Alisema kuwa wameridhika na kasi ya ujenzi wa madarasa hayo ambayo yanatarajiwa kukamilika Mwezi Julai, 2026 kabla ya shule kufunguliwa. “Ni matumaini yangu kuwa ujenzi huu utakamilika kwa muda ulipangwa ili wanafunzi watakapofungua shule waweze kuyatumia. Madarasa haya ni utekelezaji wa ahadi ya Rais, kuleta tabasamu kwa wananchi, hapa ni wanafunzi na walimu watakaotabasamu” alisema Kunga. ...

Vita dhidi ya Mbegu feki vyazaa matunda

Image
Na. Janeth Raphael MichuziTv - Bungeni Dodoma Serikali imeendelea kuimarisha hatua za kudhibiti na kutokomeza tatizo la mbegu feki nchini kupitia mifumo ya kisasa ya uthibitishaji wa ubora, ukaguzi wa mara kwa mara na utoaji wa elimu kwa wakulima. Akijibu swali la Mbunge wa Mbozi, Onesmo Merdson Mnkondya, kuhusu mpango wa Serikali wa kukomesha mbegu feki nchini, Naibu Waziri wa Kilimo, David Silinde amesema kuwa kwa mujibu wa Kifungu cha 15 cha Sheria ya Mbegu (Sura ya 308, Toleo la Urekebu la mwaka 2023), mbegu zote zinazouzwa nchini zinapaswa kuthibitishwa ubora wake na Taasisi ya Uthibitishaji wa Mbegu Tanzania (TOSCI). Silinde aliaema kuwa TOSCI imeanzisha matumizi ya lebo za kielektroniki zinazotolewa kwa kampuni za mbegu ili kuwasaidia wakulima kuhakiki uhalisia wa mbegu wanazonunua. Kupitia mfumo huo, mkulima anaweza kukwangua lebo maalum iliyowekwa kwenye kifungashio cha mbegu na kuingiza namba husika kwenye simu yake ya mkononi ili kupata taarifa za uthibitisho wa mbegu h...

Waziri Mavunde akabidhi vifaa vya Michezo UMISETA Dodoma

Image
  Na. Mwandishi wetu, DODOMA Wanafunzi wanaojiandaa kushiriki mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISETA) ngazi ya mkoa wamepata hamasa mpya baada ya kupokea vifaa vya michezo vilivyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Mtumba na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde. Vifaa hivyo vilikabidhiwa katika Shule ya Sekondari Dodoma kwa niaba ya Mbunge huyo kupitia Katibu wake, Silas Makanyaga, ambae alisema kuwa Jiji la Dodoma kupitia Ofisi ya Afisa Elimu Sekondari liliwasilisha ombi la vifaa vya michezo kwa ajili ya mashindano ya UMMISETA ngazi ya wilaya na mkoa, ambapo Mbunge amejitoa kusaidia kwa kununua jezi kwa kila mchezo. “Tunawaomba vijana wetu kucheza kwa nidhamu, kuwasikiliza walimu wao na kuendelea kufanya vizuri kama ilivyo desturi ya Jiji la Dodoma ambalo limeendelea kuwa kinara kwa ushindi wa makombe mbalimbali” alisema Makanyaga. Kwa upande, Afisa Elimu Sekondari Jiji la Dodoma, Mwl. Daniel Mapilya alisema kuwa tayari wanafunzi 120 kuto...

VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA JIJI LA DODOMA WAPEWA MAFUNZO YA MAADILI KATIKA UONGOZI NA UMUHIMU WA MAWASILIANO KWA VIONGOZI

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA VIONGOZI wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma watakiwa kusimamia misingi ya maadili na mawasiliano ili kulinda imani ya wananchi katika huduma wanazopewa.   Rai hiyo imetolewa wakati wa mafunzo maalumu ya uongozi yaliyofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, yakilenga kuwajengea uwezo viongozi hao katika kusimamia rasilimali na kuhudumia umma kwa uadilifu, huku wakionywa kuwa mmomonyoko wa maadili duniani sasa ni tishio linalohitaji udhibiti wa pamoja. Akiwasilisha mada kuhusu maadili na umuhimu wa mawasiliano katika uongozi, Mhadhiri kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa (Hombolo), Ng'omange Merkiad alisisitiza kuwa kuwepo kwa taratibu na kanuni madhubuti za kimaadili ni jambo la lazima ili kuwepo na tabia inayofanana na inayotabirika wakati wa kuwahudumia wananchi. "Maadili sio masimulizi tu ya maneno, bali ni maelekezo ya vitendo yanayomwongoza kiongozi kujua nini cha kufanya na kwa wakati gani katika utekelezaj...

Viwanda 17 vya kurejesha Taka za Plastiki vyaanzishwa Wilaya ya Dodoma

Na. Dennis Gondwe, DODOMA WILAYA ya Dodoma imefanikiwa kuanzisha viwanda 17 vya kurejesha taka za plastiki na kugawa vifaa 12 vya kutenganisha na kuhifadhi taka kwa lengo la kuweka mazingira safi na salama kwa shughuli na maisha kuendelea. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Alisema kuwa wilaya kwa kushirikiana na wadau wa mazingira ilifanikiwa kuanzisha viwanda 17 vya kurejeresha taka za plastiki, kugawa vifaa 12 vya kutenganisha na kuhifadhi taka na elimu inaendelea kutolewa kwa wananchi, mashirika na taasisi katika kudumisha utamaduni wa usafi na uhifadhi wa mazingira. “ Mheshimiwa Rais, wilaya inakadiriwa kuzalisha wastani wa tani 458 za taka ngumu kwa siku, ambapo wastani wa tani 305 sawa na asilimia 66.5 hupelekwa kwenye Da...

Shilingi 8,318,810,005 zatolewa kuboresha sekta ya Elimu Dodoma

Na. Dennis Gondwe, DODOMA WILAYA ya Dodoma imepokea shilingi 8,318,810,005 kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu zikihusisha elimu bila malipo na ujenzi wa miundombinu ya elimu kwa ajili ya kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Alisema kuwa katika kipindi cha Julai, 2025 hadi Aprili, 2026 Wilaya ya Dodoma ilipokea shilingi 8,318,810,005 kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu. Alisema kuwa kati ya fedha hizo, shilingi 3,777,397,654 ni kwa ajili ya elimu bila malipo kwa shule za Awali, Msingi na Sekondari na shilingi   4,541,412,351 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu. ” Mheshimiwa Rais , k wa Kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia, ufaulu umepanda katika shule za msingi k...

Shilingi Bil. 2.1 zatolewa kujenga miundombinu Sekta ya Afya

Na. Dennis Gondwe, DODOMA WILAYA ya Dodoma imepokea shilingi 2,145,756,727.12 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu na ununuzi wa samani na vifaa tiba katika jitihada za serikali kuboresha huduma za afya wilayani hapa. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Alisema kuwa k atika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2025/2026 wilaya ilipokea kiasi cha shilingi 2,145,756,727.12 kwa ajili ya sekta ya afya. “Kati ya fedha hizo shilingi 1,945,756,727.12 ni kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya afya na kiasi cha shilingi 200,000,000 ni kwa ajili ya ununuzi wa samani na vifaa tiba. Wilaya inakamilisha ujenzi wa Hospitali ya Jiji, Kituo cha Afya Zuzu, Chang’ombe, Msalato, Zahanati ya Kiwanja cha Ndege, Tambukareli na Jengo jumuishi Makole. Fedha hizi zim...