Posts

Watoto 328 wenye mahitaji maalum wabainishwa Jiji la Dodoma

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Afisa Elimu Maalum Jiji la Dodoma, Mwl. Issa Kambi, amekabidhi rasmi taarifa ya zoezi la ubainishaji wa watoto wenye mahitaji maalum kwa Kaimu Mkurugenzi wa Jiji hilo, Dkt. Pima Sebastian, katika hatua muhimu ya kuimarisha huduma za elimu jumuishi. Zoezi hilo la ubainishaji lililofanyika katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dodoma limepata watoto 328 ambao wamebainishwa ikiwa na lengo la kutambua watoto wenye mahitaji maalum, wakiwemo wenye ulemavu wa aina tofauti pamoja na changamoto za kujifunza ili waweze kupatiwa msaada stahiki wa kielimu na kijamii. Akikabidhi taarifa hiyo, Mwl. Kambi alieleza kuwa matokeo yanaonesha uwepo wa idadi kubwa ya watoto wanaohitaji uangalizi na mipango maalum ili waweze kunufaika kikamilifu na haki yao ya kupata elimu. Aidha, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya wazazi, walimu, wataalamu wa afya pamoja na wadau wengine wa maendeleo katika kuhakikisha watoto hao wanapatiwa mazingira rafiki ya kujifunzia. Aliongeza ...

Bucha 59 za uuzaji nyama Kanda Namba Sita zakaguliwa

Image
Na. Mwandishi Wetu, MIYUJI Timu ya wataalamu kutoka Kanda Namba Sita imefanya operesheni maalum ya kukagua bucha za nyama na samaki, lengo likiwa ni kudhibiti uuzaji wa nyama ambayo haijakaguliwa wala kupigwa muhuri na mamlaka husika ili kulinda afya za walaji. Akizungumza wakati wa kuhitimisha zoezi lililofanyika takribani kwa siku tatu, Afisa Mifugo Kanda Namba Sita, Prisca Henry alisema kuwa jumla ya bucha 59 zimekaguliwa ambapo ukaguzi uliofanyika ulihusisha leseni, usafi wa bucha na vifaa vya kuhifadhia nyama na samaki na uvaaji wa sare kwa wauzaji. “Zoezi hili limetufanya kujua jumla ya idadi ya bucha zilizopo kwenye kanda hii, pia imetupa fursa ya kutoa elimu kwa wafanyabiashara mmoja mmoja kuhusu usafi na umuhimu wa kulipa leseni, ushuru wa huduma na upimaji wa afya kwa wauzaji” alisema Henry. Alisema kuwa zoezi hilo ni endelevu na kila mwezi watafanya ukaguzi ili kutokomeza uuzaji haramu wa nyama na mazao yatokanayo na mifugo na samaki. MWISHO

Prof. Mohamed ahimiza wanafunzi kusoma kwa bidii na kuwapongeza wazazi

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Makutupora watakiwa kuwa na nidhamu na kusoma kwa bidii ili kufikia malengo yao ya kielimu na maisha kwa ujumla. Hayo aliyasema Katibu Mtendaji Baraza la Mitihani la Tanzania, Prof. Said Mohamed wakati wa Uzinduzi wa Upandaji Miti mwaka 2025/2026 uliofanyika katika Shule ya Sekondari Makutupora Jijini Dodoma. Alisema kuwa juhudi za wanafunzi katika masomo ni msingi muhimu wa maendeleo yao binafsi na taifa kwa ujumla. “Msingi mzuri wa watoto ni kupata elimu hivyo niwasihi wanafunzi muendelee kusoma kwa bidii ili kuweza kufikia ndoto zenu, kwasababu hapa kuna viongozi wa baadae ambao wataweza kuongoza taifa letu, lakini pia muwe na nidhamu kwasababu nidhamu ndio hupelekea kufika mbali hususan katika masomo yenu” alisema Prof. Mohamed. Aidha aliwapongeza wazazi kwa juhudi wanazozifanya katika malezi ya watoto. “Nipende kuwapongeza wazazi kwa namna ambavyo mnaendelea kuwalea watoto katika misingi bora, lakini pia nisisitize u...

Wamiliki wa Viwanja watakiwa kuvisafisha na kuviendeleza Dodoma

Image
  Na. Mwandishi Wetu, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imewataka wananchi na taasisi kusafisha, kuendeleza na kulinda mipaka ya viwanja vyao na kueleza kuwa kushindwa kufanya hivyo, vitatolewa kwa watu wengine wenye uhitaji wa viwanja kwa mujibu wa sheria. Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dennis Gondwe alisema kuwa wananchi na wamiliki wote wa viwanja wana wajibu wa kusafisha viwanja vyao. “Ndugu waandishi wa habari, Halmashauri ya Jiji la Dodoma inapenda kuwataarifu wananchi wote pamoja na taasisi ambazo zinamiliki viwanja ndani ya Jiji la Dodoma kuendeleza viwanja hivyo kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi Namba 4 ya Mwaka 1999 (Sura ya 113). Sheria hiyo, inawataka wananchi wote pamoja na taasisi zinazomiliki viwanja kuviendeleza viwanja hivyo ndani ya muda usiozidi miezi 36 tangu walipokabidhiwa au kumilikishwa” alisema Gondwe.   Alisema kuwa limeibuka wimbi la watu wasio na nia njema wanaovami...

Kata ya Mnadani yahimizwa kuzingatia usafi wa Mazingira

Image
  Na. Mwandihsi wetu, MNADANI Diwani wa Kata ya Mnadani, Mugendi Kerenge amewakumbusha wananchi wa Mtaa wa Mnadani kuzingatia usafi wa mazingira ikiwemo utoaji wa taka mapema na pia ulipaji wa ada ya taka ambayo ni mapato ya halmashauri. Aliyazungumza hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mtaa wa Mnadani jijini Dodoma. Alisema kuwa usafi wa mazingira unafanywa ili kujikinga na magonjwa pamoja na kuboresha mandhari ya eneo husika. Pia alisisitiza kuwa usafi wa mazingira ni jukumu la kila mwananchi na si la serikali pekee. "Ni wajibu wetu sote kuhakikisha mazingira yanakuwa safi wakati wote. Tukifanya hivyo, tutajikinga na magonjwa ya mlipuko na kuongeza hadhi ya mtaa wetu, niwatake vikundi vinavyohusika katika uondoshaji wa taka kwenye kata hii muwe na ratiba ambayo itamjulisha mwanchi ni siku gani mtapita katika mtaa anaoishi" alisema Kerenge. Aidha, aliwataka wananchi kuacha tabia ya kutupa taka hovyo na badala yake kutumia maeneo maalum yaliyotengwa kwa ...

Diwani Kerenge atoa shukrani kwa wananchi kumchagua

Image
Na. Mwandhishi wetu, MNADANI Diwani wa Kata ya Mnadani, Mugendi Kerenge awashukuru wananchi wa kata hiyo kwa kumchagua na kuonesha imani katika uongozi wake, akisisitiza umuhimu wa kushirikiana ili kuboresha maisha ya wananchi wa Mtaa wa Mnadani. Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mtaa wa Mnadani alisema kuwa moja ya majukumu yake makuu ni kusikiliza kero za wananchi, kuzitatua kwa haraka kadri inavyowezekana na kuhakikisha maendeleo yanashikamana na mahitaji halisi ya wananchi. “Najivunia kuwa kiongozi wenu, lakini nawaomba tushirikiane kwa moyo mmoja, kila kero yenu ni muhimu kwangu, na tutaendelea kufanya kazi kwa bidii kuhakikisha matatizo yanapatiwa ufumbuzi” alisema Kerenge. Aidha, alisisitiza kuwa mikutano kama hiyo ni nafasi muhimu ya wananchi kutoa maoni, mapendekezo na kushirikiana na uongozi wa kata ili kuhakikisha huduma zinaboreshwa, zinapatikana kwa wakati na zinakidhi mahitaji ya wananchi wote. Diwani Kerenge aliahidi kuendelea kufuatilia ...

Prof. Mohamed ahimiza wanafunzi kusoma kwa bidii na kuwapongeza wazazi

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Makutupora watakiwa kuwa na nidhamu na kusoma kwa bidii ili kufikia malengo yao ya kielimu na maisha kwa ujumla. Hayo aliyasema Katibu Mtendaji Baraza la Mitihani la Tanzania, Prof. Said Mohamed wakati wa Uzinduzi wa Upandaji Miti mwaka 2025/2026 uliofanyika katika Shule ya Sekondari Makutupora Jijini Dodoma. Alisema kuwa juhudi za wanafunzi katika masomo ni msingi muhimu wa maendeleo yao binafsi na taifa kwa ujumla. “Msingi mzuri wa watoto ni kupata elimu hivyo niwasihi wanafunzi muendelee kusoma kwa bidii ili kuweza kufikia ndoto zenu, kwasababu hapa kuna viongozi wa baadae ambao wataweza kuongoza taifa letu, lakini pia muwe na nidhamu kwasababu nidhamu ndio hupelekea kufika mbali hususan katika masomo yenu” alisema Prof. Mohamed. Aidha aliwapongeza wazazi kwa juhudi wanazozifanya katika malezi ya watoto. “Nipende kuwapongeza wazazi kwa namna ambavyo mnaendelea kuwalea watoto katika misingi bora, lakini pia nisisitize u...

EID Mubarak toka Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma

Image
 

Meya Chaula atoa Salam za Eid Dodoma

Image
 

Jiji la Dodoma kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Image