Posts

DG TANESCO atembelea Banda la EWURA CCC, apongeza utendaji kazi

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Lazaro Twange, amelipongeza Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA CCC), kwa mchango wake katika kupokea, kusaidia na kufuatilia utatuzi wa malalamiko ya watumiaji wa huduma za nishati na maji, hatua inayosaidia huduma zinazodhibitiwa na EWURA ikiwemo huduma ya umeme kuboreshwa kwa maslahi ya wananchi. Twange ametoa pongezi hizo leo, Juni 19, 2026, baada ya kutembelea banda la EWURA CCC katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. Akizungumza katika banda hilo, Twange amesema kazi inayofanywa na EWURA CCC ya kupokea, kusaidia na kufuatilia utatuzi wa malalamiko ya huduma za umeme imekuwa chachu ya maboresho ya huduma hiyo, ikiwemo kupungua kwa baadhi ya changamoto zilizokuwa zikilalamikiwa mara kwa mara. “Tunatambua mchango mkubwa wa EWURA CCC katika kuwawakikisha wananchi na kufuatilia utatuzi wa changam...

Waziri Mkenda: Michezo na Sanaa shuleni haitaondolewa tena

Image
Na. Denis Mlowe, IRINGA WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema serikali imejipanga kuhakikisha michezo na sanaa zinaendelea kupewa nafasi kubwa katika mfumo wa elimu nchini, akisisitiza kuwa shughuli hizo hazitaondolewa tena shuleni kwa kuwa ni sehemu muhimu ya kukuza vipaji, afya, ajira na ushindani wa kimataifa. Waziri Mkenda alitoa kauli hiyo wakati akifungua rasmi Mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) 2026 yaliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Lugalo mkoani Iringa. Katika hotuba yake, Waziri Mkenda aliushukuru Mkoa wa Iringa kwa kuwa mwenyeji wa mashindano hayo, akisema mkoa huo umeendelea kuwa kivutio kutokana na mazingira yake mazuri na ukarimu wa wananchi wake. “Tunafurahi sana kuja Iringa tunawashukuru viongozi na wananchi wote wa Iringa kwa kutupokea na kuwa wenyeji wa mashindano haya muhimu kwa maendeleo ya michezo nchini,” alisema. Aidha, aliwapongeza wanafunzi, walimu na viongo...

DCF Nzalayaimisi atembelea Banda Wizara ya Mambo ya Nje: Atoa pongezi

Image
Na. Charles Kuzenza, DODOMA Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Naibu Kamishna (DCF) Puyo Nzalayaimisi ametembelea Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa lengo la kujionea shughuli zinazofanywa na Wizara hiyo kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea Jijini Dodoma Juni 19, 2026. DCF Nzalayaimisi ameishukuru Wizara hiyo kwa kuendelea kuliunganisha Jeshi hilo na Mahusiano mbalimbali ya Kimataifa na Mashirika ya Nje ambapo Maafisa na Askari wameweza kufaidika na mafunzo mbalimbali. Chanzo: Fullshangwe Blog

Makala: Tanzania inavyojiandaa kuvuna matunda ya AFCON 2027

Image
Na. John Walter, Manyara Mwezi Juni mwaka 2027 utaingia kwenye historia ya Tanzania kwa maandishi yasiyofutika kirahisi. Kwa mara ya kwanza tangu kupata uhuru, Tanzania itakuwa mwenyeji wa mashindano makubwa zaidi ya soka barani Afrika, Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON), yatakayoandaliwa kwa ushirikiano wa nchi tatu za Afrika Mashariki; Tanzania, Kenya na Uganda. Kwa wengi, AFCON ni mashindano ya mpira wa miguu yanayodumu kwa siku 30 pekee. Lakini kwa wachumi, wawekezaji na wafanyabiashara wadogo, ni injini kubwa ya uchumi inayoweza kuingiza mabilioni ya fedha, kuzalisha ajira na kuitangaza Tanzania mbele ya mamilioni ya watu duniani. Tayari maandalizi yameanza kuonekana kupitia miradi mikubwa ya miundombinu inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini. Mkoa wa Arusha, ambao umetajwa kuwa miongoni mwa wenyeji wa mashindano hayo, unashuhudia ujenzi wa Uwanja wa Kisasa wa Samia Suluhu Hassan katika eneo la Olmot. Uwanja huo wenye uwezo wa kubeba mashabiki 30,000 umefikia z...

Ofisi ya Waziri Mkuu yathibitisha nyenzo muhimu za kuimarisha usimamizi wa maafa nchini

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA   SERIKALI imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha mifumo ya usimamizi wa maafa nchini ili kuongeza uwezo wa kuzuia, kujiandaa, kukabiliana na kurejesha hali baada ya maafa, kufuatia kuongezeka kwa matukio yanayochochewa na mabadiliko ya tabianchi pamoja na vihatarishi vingine vya asili na kijamii.   Hayo yalielezwa jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Brigedia Jenerali Hosea Ndagala, wakati akifungua Kikao cha Jukwaa la Taifa la Wadau wa Usimamizi wa Maafa kilicholenga kupitia na kuthibitisha Mwongozo wa Urejeshaji Hali Baada ya Maafa, Mwongozo wa Uendeshaji na Uratibu wa Uhawilishaji Fedha kwa Walioathirika wa Maafa, pamoja na Mfumo wa Usimamizi wa Taarifa za Maafa (DMIS).   Brigedia Jenerali Ndagala alisema kuwa katika miaka ya hivi karibuni Tanzania imekumbwa na matukio mbalimbali ya maafa yakiwemo mafuriko, ukame, maporomoko ya ...

Waziri Kikwete Ahimiza Uwajibikaji na Ubunifu kwa Watumishi wa Umma

Image
Na. Bupe Mwaiseje - MAELEZO Watumishi wa umma nchini wamehimizwa kuzingatia uwajibikaji na ubunifu katika kutekeleza majukumu yao ili kuboresha huduma za Serikali zinazotolewa kwa wananchi. Akizungumza katika Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete wakati akifungua Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma, amesema kuwa Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya kazi kwa watumishi wa umma ili kuwawezesha kutoa huduma bora na zenye ufanisi.   Ambapo alitoa wito kwa watumishi wa umma kuiishi kauli mbiu ya mwaka 2026 inayosema “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu” inayolenga kuwakumbusha watumishi hao wa umma kutambua nafasi yao katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma zinazostahili. “Niwaombe watumishi wa umma wote kuuishi ujumbe huu, kwani uwajibikaji ndio msingi wa uongozi na utumishi wa umma unaozingatia mahitaji ya wananchi,” amesisitiza Mhe. Kikwet...

Waziri Mkuu aagiza usimamizi mzuri wa mitambo ya uchimbaji Visima

Image
Awataka watendaji kuacha mazoea katika utekelezaji wa majukumu   Na. Mwandishi wetu, WAZIRI Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka watendaji wa Wizara ya Maji pamoja na Wakuu wa Mikoa wasimamie vizuri mitambo ya uchimbaji visima ili iweze kufanya kazi iliyokusudiwa. Alisema kuwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan alinunua mitambo ya uchimbaji wa visima hivyo watendaji wachukue hatua na waache kufanya kazi kwa mazoea. “Nielekeze wakuu wa mikoa yote pamoja na wizara, kusimamia ili mitambo ile iweze kufanya kazi iliyokusudiwa, ni kweli kuna baadhi ya maeneo ya tunaendelea endelea na ile tabia ya ‘business as usual’ sasa ili kufikia matokeo ya Dira 2050, ni lazima tufanye kazi ‘business unusual’ tuache kufanya kazi kwa kuchukulia vitu kimazoea mazoea", alielekeza Waziri Mkuu. Dkt. Mwigulu alitoa maelekezo hayo leo (Alhamisi Juni 18, 2026) Bungeni jijini Dodoma katika kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu wakati akijibu swali la Mbunge wa Kwimba, Cosmas Bullala. Mbunge huyo alitaka ku...

Jukwaa la Uwekezaji baina ya Tanzania na Singapore

Image
 

Jukwaa la Uwekezaji Tanzania na Singapore

Image