Watoto 328 wenye mahitaji maalum wabainishwa Jiji la Dodoma
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Afisa Elimu Maalum Jiji la Dodoma, Mwl. Issa Kambi, amekabidhi rasmi taarifa ya zoezi la ubainishaji wa watoto wenye mahitaji maalum kwa Kaimu Mkurugenzi wa Jiji hilo, Dkt. Pima Sebastian, katika hatua muhimu ya kuimarisha huduma za elimu jumuishi. Zoezi hilo la ubainishaji lililofanyika katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dodoma limepata watoto 328 ambao wamebainishwa ikiwa na lengo la kutambua watoto wenye mahitaji maalum, wakiwemo wenye ulemavu wa aina tofauti pamoja na changamoto za kujifunza ili waweze kupatiwa msaada stahiki wa kielimu na kijamii. Akikabidhi taarifa hiyo, Mwl. Kambi alieleza kuwa matokeo yanaonesha uwepo wa idadi kubwa ya watoto wanaohitaji uangalizi na mipango maalum ili waweze kunufaika kikamilifu na haki yao ya kupata elimu. Aidha, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya wazazi, walimu, wataalamu wa afya pamoja na wadau wengine wa maendeleo katika kuhakikisha watoto hao wanapatiwa mazingira rafiki ya kujifunzia. Aliongeza ...