Posts

Showing posts from April 21, 2025

Timu ya Mpira wa Wavu ya Wanaume Watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma yatinga nusu fainali kibabe baada ya kuicharaza seti 2 - 0 Timu ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).

Image
  Timu ya Mpira wa Wavu ya Wanaume Watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma yatinga nusu fainali kibabe baada ya kuicharaza seti 2 - 0 Timu ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).

Timu ya Mpira wa Kikapu ya Wavulana ya Watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma yavuna alama 2 baada ya wapinzani wao Timu ya Uchukuzi kushindwa kufika kiwanjani.

Image
  Timu ya Mpira wa Kikapu ya Wavulana ya Watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma yavuna alama 2 baada ya wapinzani wao Timu ya Uchukuzi kushindwa kufika kiwanjani.

Timu ya Mpira wa Miguu ya watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma waiangushia kipigo cha magoli 2 - 0 Timu ya Bohari ya Dawa (MSD) mashindano ya Mei Mosi Singida

Image
  Timu ya Mpira wa Miguu ya watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma waiangushia kipigo cha magoli 2 - 0 Timu ya Bohari ya Dawa (MSD) katika mashindano ya michezo ya Mei Mosi inayoendekea mkoani Singida.

Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

Image
Na. Leah Mabalwe, NALA Ujenzi wa mradi wa Maji Nala unaotekelezwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) kwa gharama ya shilingi bilioni 1.3 kutatua changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji katika Kata ya Nala. Kauli hiyo ilitolewa na Diwani wa Kata ya Nala, Herman Masila alipokuwa akiongea na waandishi wa habari waliotembelea miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Kata ya Nala. “Nichukue nafasi hii kuishukuru serikali kutuletea mradi wa maji katika Kata ya Nala. Mradi huu utasaidia sana wananchi kuondokana na adha ya maji. Mradi huu ni mkubwa utasaidia maeneo mbalimbali katika kata yetu inayokuwa kwa kiasi. Kwa siku za usoni tumeshuhudia idadi kuwa ya watu wanakuja kujenga makazi na viwanda. Hivyo, mradi huu utakapo kamilika utasaidia kwa kiasi kikubwa na kupunguza adha ya maji” alisema Masila. Nae, Mary Kaka ambae ni mkazi wa Kata ya Nala aliipongeza serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kupeleka maendeleo katika Kata ya Nala na kumshukuru rais kw...

Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

Image
Na. Leah Mabalwe, NALA Shule ya Sekondari Nala imefanikiwa kupandisha kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi kutokana na utekelezaji wa dhamira ya serikali ya awamu ya sita wa kuhakikisha wanafunzi wanapata huduma ya chakula na lishe shuleni. Kauli hiyo ilitolewa na Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Nala, Mwl. Joseph Chambo alipokuwa mwenyeji wa waandishi wa habari waliotembelea shule yake kuona utekelezaji wa miradi ya maendeleo na utoaji wa huduma ya chakula na lishe shuleni hapo katika kipindi cha miaka minne ya serikali. “Katika utekelezaji wa Muongozo wa kitaifa wa ulaji wa huduma ya chakula na lishe kwa wanafunzi wa elimumsingi umetunufaisha sana. Hapo awali kulikuwa na mahudhurio hafifu sana shuleni kwetu. Pia hata tukiwa darasani wanafunzi walikuwa na uelewa wa chini na hata ufaulu ulikuwa sio mzuri sana. Kufuatia utelekezaji wa mwongozo huu shule yetu sasa imekuwa ni ya mfano. Watoto wanahamasika kuja shule na hata ufaulu umepanda kwa kiasi kikubwa kulinganisha na hapo awali. ...

Hospitali ya Jiji la Dodoma mkombozi kwa wananchi wa Kata ya Nala

Image
Na. Leah Mabalwe, NALA Mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Jiji la Dodoma, uliopo katika Kata ya Nala umegharimu kiasi cha shilingi 1,000,000,000 umekamilika na umeanza kutumika ukiwanufaisha wananchi. Akizungumza na waandishi wa habari, Diwani wa Kata ya Nala, Herman Masila alisema kuwa hospitali hiyo ni msaada mkubwa kwa wananchi. “Kipekee nitoe pongezi kwa serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kuboresha sekta ya afya katika kata yetu ya Nala. Serikali imetupendelea sana kwa kutujengea hospitali kubwa na ya kisasa zaidi kwaajili ya wananchi wa Kata ya Nala na kata jirani wanaweza kupata huduma katika hospitali hii. Ni kweli wananchi tayari wameshaanza kupata huduma katika hospitali yetu na tunanufaika nayo” alisema Masila. Nea, Marry Kaka mwananchi wa Kata ya Nala akaishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utekelezaji wa mradi wa Hospitali ya Jiji la Dodoma. “Tunaishukurun sana serikali chini ya Rais, Samia, kwa kutujengea Hospitali ya Jiji kwenye kata yetu. Hospit...