Posts
Showing posts from July 6, 2025
TANZANIA YAENDELEA KUTANGAZA NA KUKUZA KISWAHILI NA UTAMADUNI WAKE KIMATAIFA
- Get link
- X
- Other Apps
By Halmashauri ya Jiji la Dodoma
Jiji la Dodoma
Lugha ya kiswahili na utamaduni wa mtanzania vimeendelea kuwa kivutio kikubwa kwa wageni mbalimbali wa kimataifa waliotembelea banda la Tanzania katika Wiki ya utamaduni na Kiswahili inayoendelea kwenye maonesho ya biashara ya dunia (Expo 2025) yanayofanyika Osaka, Japan. Kuelekea maadhimisho ya siku ya Kiswahili duniani yanayofanyika kila ifikapo tarehe 7 Julai lugha ya Kiswahili inaendelea kuwafikia watu wengi duniani na mwaka huu 2025 maadhimisho hayo yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Kiswahili kwa amani na mshikamano”. Viongozi waandamizi wa mataifa mbalimbali, wametembelea banda hilo ikiwemo Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi la Japani, Bw. Koichiro Gemba, Mfalme wa Lesotho, Mhe. Letsie III na Mhe. Prudence Sebahizi, Waziri wa Biashara na Viwanda wa Rwanda. Viongozi hao wameonesha kuvutiwa kwa kiasi kikubwa na lugha ya Kiswahili na Utamaduni kupata nafasi katika Maonesho hayo ya Dunia yenye hadhi kubwa. Akizungumza wakati alipotembelea banda hilo Mhe. Sebahizi alie...