Posts

Showing posts from December 7, 2023

Serikali ya Dkt. Samia inawajali wafanyakazi wa Sekta ya Afya

Image
Na. Dennis Gondwe, MAKOLE SERIKALI ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan inawajali wafanyakazi wa sekta ya Afya na kuthamini huduma wanazotoa kwa wananchi katika kuelekea kipindi cha miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri akiongea na waandishi wa habari Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alipokuwa akiongea na wafanyakazi wa Kituo cha Afya Makole katika kuelekea kilele cha miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara. Alhaj Shekimweri alisema “tunaposherehekea Uhuru wa nchi yetu, hawa wanaohudumiwa ni watanzania wenzetu ambao wapo huru. Hivyo, tunawajibu wa kuwasaidia ili wajifungue wakiwa salama na wengine wanaopata huduma mbalimbali za Afya. Serikali ya awamu ya sita inawajali na milango yetu ipo wazi kuwasikiliza pale mtakapohitaji kusikilizwa. Najua Mganga Mkuu, Dkt. Andrew Method anafanya kazi vizuri na sisi tunamtegemea sana na anawaunganisha vizuri. Najua mpo salama kwenye mi...

Wilaya ya Dodoma yatoa zawaid kwa waliojifungua Kituo cha Afya Makole kuelekea Miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara

Image
Na. Dennis Gondwe, MAKOLE MIAKA 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara Wilaya ya Dodoma imewapatia zawadi kina mama waliojifungua katika Kituo cha Afya Makole na kuwatakia heri na kuwahakikishia kuwa serikali inataendelea kutoa huduma bora kwao. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabi Shekimweri akimkabidhi zawadi mama aliyejifungua katika Kituo cha Afya Makole jijini Dodoma Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri alipoongoza timu ya wataalam wa wilaya na halmashauri kukagua hali ya huduma katika Kituo cha Afya Makole, kutembelea kina mama wanaotarajia kujifungua na waliojifungua na kuwapatia zawadi mbalimbali. Alhaj Shekimweri alisema kuwa Wilaya ya Dodoma katika kuelekea maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Tanzania Bara imetembelea Kituo cha Afya Makole kukagua hali ya utoaji huduma. “Kwa niaba ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan tumekuja kuona huduma zinatolewaje hapa sehemu ya kujifungulia.  Tunafahamu hapa kuna wastani wa kujifungua kawaida wanawake kat...