Posts

Showing posts from November 1, 2024

Mwenyekiti UWT Taifa awataka wanawake kuchangamkia mikopo ya Jiji la Dodoma

Image
  Na. Faraja Mbise. DODOMA Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa, Mary Chatanda amewataka wanawake wafanyabiashara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuachana na mikopo ya Kausha damu na mwendokasi inayowanyanyasa na kuwadhalilisha wanawake kutokana na muda wa marejesho na kiwango cha riba kuwa kikubwa na hivyo kushindwa kujikwamua kiuchumi na kuwaongezea umasikini zaidi. Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa, Mary Chatanda Kauli hiyo aliitoa wakati akizungumza katika Uzinduzi wa Umoja wa Wanawake Wafanyabiashara Masoko yote katika Jiji la Dodoma (UWAWAMA), uliofanyika Cathedral Social Hall, tarehe 01 Novemba, 2024. Chatanda aliwataka wanawake wafanyabiashara kuachana na mikopo ya kausha damu na kujiunga na vikundi ili kupata mikopo ambayo inatolewa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma. "Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluh Hassan imerejesha utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi vya wanawake, vijana na ...

Ofisi wazi kuchukua na kurejesha fomu za wagombea nafasi za uongozi wa Serikali za Mitaa

Image
Na. Asteria Frank, DODOMA   Vituo 222 vya Ofisi za Mitaa ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma zimefunguliwa mapema zaidi leo tarehe 1 Novemba, 2024 kwa lengo la kuweka upana mkubwa kwaajili ya kuchukua na kurejesha fomu za wagombea nafasi ya uongozi Serikali za Mitaa.   Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko   Kauli hiyo ilitolewa na Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko asubuhi ya leo katika ofisi yake wakati akizungumza na waandishi wa habari akiuhabarisha umma kuhusu tamati ya zoezi la uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kugombea uongozi wa serikali za mitaa katika Jiji la Dodoma.   Dkt. Sagamiko alisema ā€œhakuna ofisi yoyote katika Jiji la Dodoma ambayo itafungwa wakati zoezi hilo likiendelea. Naomba nitoe rai kwa viongozi wa vyama vya siasa vyote 19 katika Jiji letu la Dodoma kuhakikisha wanatumia siku hii muhimu ambayo ni siku ya mwisho k...

Ofisi kufunguliwa hadi saa 10 jioni siku ya mwisho kuchukua na kurudisha fomu kugombea nafasi za uongozi Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Image
 

Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Jiji la Dodoma atoa hakikisho ofisi kufunguliwa na kufungwa kwa wakati siku ya mwisho kuchukua na kurudisha fomu

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MSIMAMIZI wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 Halmashauri ya Jiji la Dodoma Dkt. Frederick Sagamiko amewataka viongozi wa vyama 19 vya siasa kuwahamasisha wananchi kuchukua na kurejesha fomu akiwahakikishia kuwa ofisi zitafunguliwa na kufungwa kwa muda uliopangwa. Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 Halmashauri ya Jiji la Dodoma Dkt. Frederick Sagamiko akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake leo asubuhi Dkt. Sagamiko alitoa kauli hiyo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake leo asubuhi kuwakumbusha wananchi kuwa ni siku ya mwisho ya kuchukua na kurejesha fomu za kugombea nafasi za uongozi wa serikali za mitaa. ā€œLeo tarehe 1 Novemba, 2024 ni siku ya mwisho ya kuchukua na kurejesha fomu za kugombea nafasi za uongozi wa serikali za mitaa. Ofisi zimefunguliwa mapema zaidi ili saa 2:00 asubuhi kuanza kutoa huduma hadi saa 10:00 jioni. Hakuna ofisi itakayochelewa kufunguliwa wala itakayowahi kufungwa. Hivyo, viongo...