Posts

Showing posts from September 13, 2026

Usafi wa mitaro na njia za maji Kusaidia kujikinga na mafuriko Dodoma Makulu

Image
Na. Amoni Sambulila, DODOMA   Wito umetolewa kwa wananchi kuhakikisha mitaro na njia za maji zinakuwa safi na wazi wakati wote, ili kuruhusu maji ya mvua kupita kwa urahisi na kuzuia maji kufurika na kuingia kwenye makazi ya wananchi.   Wito huo umetolewa na Kaimu Meneja wa Kanda Namba Nne, Evodius Canisto wakati wa zoezi la usafi wa mazingira lililofanyika katika kata hiyo ambapo aliwataka wananchi kufanya usafi katika maeneo yote yanayoweza kuathiriwa na maji ya mvua.   Evodius alisema kuwa mabadiliko ya tabianchi yanaweza kusababisha mvua kubwa na kwa nyakati tofauti hivyo wananchi wanapaswa kuchukua hatua mapema kwa kusafisha mitaro, kuondoa taka na vitu vingine vinavyoweza kuziba njia za maji.   Aliongeza kuwa usafi wa mazingira ni jukumu la kila mwananchi na haupaswi kufanyika wakati wa zoezi maalum pekee bali inapaswa kuwa sehemu ya maisha ya kila siku ili kulinda afya, usalama na mali za wananchi.   Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Shina en...

Mwenyekiti Mtaa wa Karume, Kata ya Mnadani ahamasisha usafi

Image
Na. Mwandishi wetu, MNADANI   Zoezi la usafi wa mazingira limehamasishwa katika Mtaa wa Karume, Kata ya Mnadani, kwa lengo la kuimarisha usafi na afya ya wananchi pamoja na kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira. Zoezi hilo pia limehusisha wataalam wa Kanda Namba Sita, ambao wamekuwa mstari wa mbele kutoa elimu na ushauri kwa wananchi kuhusu umuhimu wa usafi wa mazingira, utunzaji wa taka na namna ya kuzuia magonjwa yanayoweza kusababishwa na mazingira machafu.   Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Mwenyekiti wa Mtaa wa Karume, Waziri Matwiga amewataka wananchi kushiriki kikamilifu katika usafi wa mazingira na kujenga utamaduni wa kufanya usafi mara kwa mara.   “Usafi wa mazingira ni jukumu la kila mmoja wetu. Tunapaswa kushirikiana kuhakikisha mtaa wetu unakuwa safi na salama kwa afya ya wananchi,” amesema Matwiga.   Kwa upande wao, wataalam wa Kanda Namba Sita wameendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira, ikiwa ...

Kata ya Ihumwa yaanza usafi kutekeleza agizo la RC Dodoma

Na. Rahma Magona, DODOMA Kata ya Ihumwa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeanza zoezi la usafi wa mazingira ikiwa ni hatua ya utekelezaji wa maagizo ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule ya kuhakikisha wananchi wanaimarisha usafi wa mazingira na kulinda afya zao.   Hatua hiyo imekuja baada ya viongozi wa Kata ya Ihumwa kuanza kuhamasisha wananchi kufanya usafi mtaa kwa mtaa kwa kushirikiana na maafisa afya kutoka Kanda Namba Mbili, huku ukaguzi wa vyoo katika kaya ukiwa miongoni mwa hatua zinazotekelezwa.   Akizungumza katika zoezi hilo, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Chang’ombe, Kata ya Ihumwa, Yoram Ndumizi alisema kuwa wamejipanga vizuri kuhakikisha wananchi wanashiriki katika usafi huku wakifanya ukaguzi wa vyoo baada ya kubaini baadhi ya kaya kutokuwa na vyoo, hali hiyo inaweza kuongeza hatari ya mlipuko wa magonjwa kutokana na uwezekano wa mvua nyingi za El Niño.   Ndumizi aliongeza kuwa kwa kushirikiana na maafisa afya, wanaendelea kut...

Wafanyabiashara Soko la Sabasaba wahimizwa usafi

Image
Na. Mohammed Ramadhani, DODOMA Wafanyabiashara katika Soko la Sabasaba jijini Dodoma wametakiwa kuendelea kufanya usafi wa mazingira kila siku badala ya kusubiri siku maalum ya usafi, hatua inayolenga kuweka mazingira ya biashara katika hali ya usalama na usafi. Akizungumza wakati wa zoezi la usafi katika Soko la Sabasaba, Afisa Mazingira wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Gwantwa Mbwile, alisema kuwa zoezi hilo limeanza tangu Jumatatu na kuendelea hadi Jumamosi, huku akiwataka wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla kufanya usafi kuwa sehemu ya maisha yao ya kila siku. Alisema kuwa kufanya usafi kila siku kunasaidia kupunguza muda na nguvu zinazotumika wakati wa kufanya usafi wa pamoja, kwani taka zinapokusanywa kwa muda mrefu huongezeka na kufanya zoezi kuwa gumu zaidi. “Wito wangu kwa wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla ni kujitahidi kuzoea kufanya usafi kila siku. Hii inarahisisha siku ambayo tunataka kufanya usafi maeneo yetu yanakuwa safi na hatuchukui muda mrefu. Si kusub...

Wananchi Dodoma Makulu wajitokeza kwa wingi zoezi la usafi wa Mazingira

Image
Na. Amoni Sambulila, DODOMA MAKULU Wananchi wa Kata ya Dodoma Makulu wamejitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi la usafi wa mazingira, ikiwa ni hatua ya kuhamasisha usafi na kuhakikisha mazingira yanakuwa safi na salama kwa jamii.   Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Msangalale Magharibi, Lucy Michael amewataka wananchi kuendelea kujitoa kwa wingi kufanya usafi na kuhakikisha unafanyika kila siku ili kuepuka magonjwa mbalimbali yanayoweza kusababishwa na uchafu wa mazingira. “Nawasihi wananchi wenzangu kujitokeza kwa wingi katika zoezi la usafi. Pia nasisitiza kuwa usafi wa mazingira ufanyike kila siku kwasababu utatuepusha na magonjwa mbalimbali yanayotokana na uchafu wa mazingira,” alisema Michael.   Kwa upande wake, Mwananchi Kalleb Wilson alisema kuwa wananchi wanapaswa kuendelea kushiriki katika zoezi la usafi wa mazingira na kuhakikisha maeneo yao yanakuwa safi wakati wote.   Nae, Afisa Biashara Kanda Namba Nne, Johari Fadhili...