Usafi wa mitaro na njia za maji Kusaidia kujikinga na mafuriko Dodoma Makulu
Na. Amoni Sambulila, DODOMA Wito umetolewa kwa wananchi kuhakikisha mitaro na njia za maji zinakuwa safi na wazi wakati wote, ili kuruhusu maji ya mvua kupita kwa urahisi na kuzuia maji kufurika na kuingia kwenye makazi ya wananchi. Wito huo umetolewa na Kaimu Meneja wa Kanda Namba Nne, Evodius Canisto wakati wa zoezi la usafi wa mazingira lililofanyika katika kata hiyo ambapo aliwataka wananchi kufanya usafi katika maeneo yote yanayoweza kuathiriwa na maji ya mvua. Evodius alisema kuwa mabadiliko ya tabianchi yanaweza kusababisha mvua kubwa na kwa nyakati tofauti hivyo wananchi wanapaswa kuchukua hatua mapema kwa kusafisha mitaro, kuondoa taka na vitu vingine vinavyoweza kuziba njia za maji. Aliongeza kuwa usafi wa mazingira ni jukumu la kila mwananchi na haupaswi kufanyika wakati wa zoezi maalum pekee bali inapaswa kuwa sehemu ya maisha ya kila siku ili kulinda afya, usalama na mali za wananchi. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Shina en...