Posts

Showing posts from December 17, 2023

Bodaboda ni kazi, epukeni uhalifu

Image
Na. Dennis Gondwe, MNADANI VIJANA waendesha Pikipiki (bodaboda) katika Kata ya Mnadani wametakiwa kuichukulia kazi ya kuendesha pikipiki kama kazi nyingine na kujiepusha na kujiunga kwenye makundi ya uhalifu. Picha kutoka mtandaoni Kauli hiyo ilitolewa na Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, Focus Ishika alipokuwa akiongea na wananchi wa Mtaa wa Mnadani katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika mtaa huo. Mkaguzi Msaidizi Ishika ambae pia ni Polisi Kata ya Mnadani alisema kuwa vijana waendesha bodaboda wanakosa elimu ya umuhimu wa kazi wanayofanya. “Vijana wetu wa bodaboda wanakosa elimu juu ya umuhimu wa kuichukulia kazi ya bodaboda kama kazi nyingine. Wazazi wenye watoto wanaoendesha pikipiki toeni elimu kwa vijana wenu ajira ya udereva pikipiki waichukulie kama yule anayeamka asubuhi na kwenda benki au kwenda kufundisha (mwalimu) wanatakiwa kuifanya kazi hiyo kwa moyo na bidii. Kwa hiyo makosa tunayo sisi. Mwanao anatoka asubuhi na pikipiki hujui anapaki kituo gani, hujui rafiki zake n...

Afisa Mifugo Kata ya Mnadani anaupiga mwingi

Image
Na. Dennis Gondwe, MNADANI KATA ya Mnadani inajivunia utendaji kazi wa Afisa Mifugo kwa kuhakikisha wananchi wanakuwa na mifugo yenye afya kutokana na kupata huduma zote za chanjo kwa wakati. Afisa Mifugo Kata ya Mnadani, Elizabeth Shirima Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Mtendaji Kata ya Mnadani, Caroline Massawe alipokuwa akitoa taarifa ya mafanikio ya Kata ya Mnadani kwa kipindi cha miaka mitatu (2021-2023) katika mkutano wa hadhara wa wananchi wa Mtaa wa Mnadani. Massawe alisema “nikiwa Afisa Mtendaji wa Kata ya Mnadani, napenda kumpongeza Afisa Mifugo wa Kaya ya Mnadani, anajitahidi kwa kweli kutekeleza majukumu yake ya kazi anajituma na ni muwajibikaji mzuri sana. Kwa wale wanaofuga natumaini wanalitambua hilo, anawatembelea wananchi kuchanja mifugo yao kwa wakati na mbwa wanaozurura anawachanja pamoja na majukumu mengine, mama huyu anaupiga mwingi”. Akiongelea mafanikio ya sekta ya mifugo, alisema kuwa sekta hiyo imefanikiwa kudhibiti magonjwa ya mlipuko na magonjwa mengine...

Serikali awamu ya sita yaipaisha Mnadani

Image
  Na. Dennis Gondwe, MNADANI SERIKALI ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa fedha nyingi za kutekeleza miradi ya maendeleo katika sekta ya elimu kwenye Kata ya Mnadani ikiwa ni pamoja na ujenzi wa shule mpya za msingi zinazojengwa kwenye Kata ya Mnadani hii imesaidia kuboresha miundombinu ya kujifunzia na kufundishia. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Mtendaji Kata ya Mnadani, Caroline Massawe alipokuwa akielezea mafanikio ya serikali ya awamu ya sita katika mkutano wa hadhara wa wananchi wa Mtaa wa Mnadani uliofanyika katika ofisi ya kata hiyo. Massawe alisema kuwa kwa asilimia kubwa mafanikio mengi ya sekta ya elimu katika Kata ya Mnadani yametokana na serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Mafanikio katika sekta ya elimu ni uongezekaji wa miundombinu shuleni, idadi ya wanafunzi imeongezeka, shule mpya kuanzishwa, mafunzo ya walimu kazini, al...

Mnadani yaweka kipaumbele ulinzi na usalama

Image
  Na. Dennis Gondwe, MNADANI WAKAZI wa Mtaa wa Mnadani katika Kata ya Mnadani wametakiwa kuweka kipaumbele swala la ulinzi na usalama ili jamii iwe salama katika kipindi cha sherehe za mwisho wa mwaka. Mwenyekiti wa Mtaa wa Mnadani, Hema Wawa akisisitiza jambo Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Mtaa wa Mnadani, Hema Wawa alipokuwa akiwahutubia mamia ya wananchi wa Mtaa wa Mnadani katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika mtaa huo. Wawa alisema “tunapoelekea katika sherehe za Krismasi na mwaka mpya, niwaombe sana wananchi wangu msiache makazi bila mtu anayebaki nyumbani. Kipindi hicho kina mkesha, unakuta watu wamefunga nyumba wameenda kwenye mkesha, unarudi nyumbani unakutana na kitu ambacho hukutegemea. Tuchukue tahadhari, kama mnaenda kwenye mkesha mjipe ratiba, wengine waende kwenye mkesha na wengine wabaki waende ibada ya asubuhi. Ulinzi unaanzia kwako mwenyewe kujilinda wewe na mali yako. Niwaombe sana tulisimamie hili ili kuepuka changamoto zinazoweza kudhibitiwa”...

Mnadani wakumbushwa kuchukua tahadhari ya athari za mvua

Image
  Na. Dennis Gondwe, MNADANI WANANCHI wa Mtaa wa Mnadani wametakiwa kuchukua tahadhari ya athari inayoweza kusababishwa na mvua kwa kuhakikisha mazingira yanakuwa safi na mitaro ya kupitisha maji ya mvua haijaziba ili kuepusha mafuriko kwenye makazi ya watu. Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mnadani, Hema Wawa alipokuwa akiongea na wananchi wa Mtaa wa mnadani Tahadhari hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mnadani, Hema Wawa alipokuwa akiwahutubia mamia ya wananchi wa Mtaa wa Mnadani katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika mtaa huo. Wawa alisema “tupo katika kipindi cha mvua, katika kipindi hiki milipuko ya magonjwa mbalimbali huwa inatokea. Ni vizuri tujitahadhari na mazingira ambayo ni hatarishi. Kama tulivyojadili suala la usafi wa mazingira linagusa kila mmoja wetu. Hivyo, tuchukue tahadhari kadri inavyohitajika. Kipindi hiki kuna watu kuharibiwa nyumba zao na vitu vyao kutokana na maji ya mvua. Tuhakikishe mitaro ya kupitishia maji ni safi na haijaziba...

Kata ya Mnadani watakiwa kuandikisha watoto Darasa la Kwanza

Image
  Na. Dennis Gondwe, MNADANI JAMII imetakiwa kuhakikisha watoto wenye umri wa kuandikishwa shule za msingi wanaandikishwa kwa wakati waweze kupata elimu kwa mujibu wa sheria. Wanafunzi wakiwa darasani (picha kutoka maktaba) Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Elimu Kata ya Mnadani, Robert Tesha alipokuwa akiongea kwenye mkutano wa hadhara wa wananchi wa Mtaa wa Mnadani katika Kata ya Mnadani jijini Dodoma. Tesha alisema “zoezi la uandikishaji kwa shule za msingi limeanza tangu mwezi Oktoba mwaka huu. Watoto wanaoandikishwa ni darasa la awali kuanzia miaka minne hadi mitano na darasa la kwanza miaka sita hadi nane na uandikishaji hauna gharama yoyote. Mzazi unapokwenda unatakiwa kwenda na cheti cha mtoto cha kuzaliwa na kama hauna unapitia kwa Afisa Mtendaji wa Mtaa anakuandikia barua na majina kamili ya mwanafunzi kwa sababu majina yanaingizwa kwenye mfumo na hilo jina halitabadilika mpaka chuo kikuu. Niombe sana waleteni watoto tuwaandikishe shule, madarasa yameshajengwa na mama...

Kata ya Mnadani kuwatambua watoto wenye mahitaji maalum

Image
Na. Dennis Gondwe, MNADANI JAMII imetakiwa kuhakikisha watoto wenye umri wa kuandikishwa shule za msingi wanaandikishwa kwa wakati waweze kupata elimu kwa mujibu wa sheria. Afisa Elimu Kata ya Mnadani, Robert Tesha akiongea na wananchi Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Elimu Kata ya Mnadani, Robert Tesha alipokuwa akiongea kwenye mkutano wa hadhara wa wananchi wa Mtaa wa Mnadani katika Kata ya Mnadani jijini Dodoma. Tesha alisema “zoezi la uandikishaji kwa shule za msingi limeanza tangu mwezi Oktoba mwaka huu. Watoto wanaoandikishwa ni darasa la awali kuanzia miaka minne hadi mitano na darasa la kwanza miaka sita hadi nane na uandikishaji hauna gharama yoyote. Mzazi unapokwenda unatakiwa kwenda na cheti cha mtoto cha kuzaliwa na kama hauna unapitia kwa Afisa Mtendaji wa Mtaa anakuandikia barua na majina kamili ya mwanafunzi kwa sababu majina yanaingizwa kwenye mfumo na hilo jina halitabadilika mpaka chuo kikuu. Niombe sana waleteni watoto tuwaandikishe shule, madarasa yameshajengwa n...