Posts

Showing posts from June 4, 2026

Jiji la Dodoma lachangia Mil. 70 Mwenge wa Uhuru 2026

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imechangia shilingi 70,000,000 kufanikisha Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Wilaya ya Dodoma Mwaka 2026 zilizoongozwa na kaulimbiu isemayo ‘Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa pamoja Kuleta Maendeleo’. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Akiongelea michango ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2026, alisema kuwa ulichangiwa na sekta ya umma na sekta binafsi. ” Mheshimiwa Rais, Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2026 zimechangiwa michango yenye jumla ya shilingi 100,944,500. Wananchi wamechangia shilingi 24,044,500, Halmashauri ya Jiji la Dodoma shilingi 70,000,000 na sekta binafsi pamoja na Mashirika ya Umma shilingi 6,900,000. Kati ya fedha hizo shilingi 5,460,000 zimerejeshwa kuchangia un...

Huduma ya Maji kuimarika Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALI ya upatikanaji wa huduma ya Maji safi na salama imeendelea kuimarika hadi kufikia lita 88.7 kwa siku sawa na asilimia 55 ya mahitaji yote. Kauli ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Alisema kuwa h ali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama ni lita Mil. 88.7 kwa siku sawa na asilimia 55 ya mahitaji ya wakazi wote ambayo ni lita Mil. 159.9. DUWASA imeendelea kutekeleza miradi 38 ya shilingi bilioni 91. ambayo ikikamilika itaongeza upatikanaji wa Maji kwa zaidi ya asilimia 75 ya mahitaji ya siku. MWISHO  

Dodoma kuvuna Tani 40,930 Chakula na Nafaka

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WILAYA ya Dodoma inatarajia kuvuna tani 40,930 za mazao ya chakula na biashara katika kuwahakikishia wananchi lishe bora na kujikwamua kiuchumi. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Alisema kuwa w ilaya kupitia Divisheni ya Kilimo Mjini na wadau iliendelea kuhakikisha wananchi wanapata lishe bora na kujikwamua kiuchumi kwa kulima mazao ya chakula na biashara. “Hali ya upatikanaji wa chakula na bei ni ya wastani kwa msimu wa kilimo 2025/2026. Wakulima wameanza kuvuna na kiasi cha tani 40,930 kinatarajiwa kuzalishwa. Hata hivyo, kuna mtiririko mzuri wa mazao ya chakula yanayoingia na kupatikana katika masoko yote. Hivyo, kuhakikisha upatikanaji wa chakula katika kipindi chote cha mwaka” alisema Mbugi. Akiong...

Dodoma kupambana na VVU

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WILAYA ya Dodoma imeendelea kupambana na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU) ikiwa na maambukizi ya asilimia 2.7 kwa Mwaka 2025. Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma, Sakina Mbugi alipokuwa akisoma Risala ya Utii kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilaya ya Dodoma katika uwanja wa Shule ya Msingi Kizota jijini Dodoma. Alisema kuwa mapambano dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI yanapewa uzito mkubwa. ” Mheshimiwa Rais, hali ya ushamiri wa maambukizi ya VVU wilayani kwa mwaka 2025 ni asilimia 2.7. Aidha, chini ya Kaulimbiu inayosema   “Imarisha mwitikio; Tokomeza UKIMWI”, kwa kipindi cha Januari, 2025 hadi Desemba, 2025 j umla ya watu 89,562 (Me 34, 806 Ke 54,756) walijitokeza kupima maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kwa hiari, kati yao watu 2,432 walikutwa na maambukizi na kuunganishwa na huduma za tiba na matunzo kwa WAVIU.   Hata hivyo, katika ...