Ufaulu Elimu Sekondari wapanda Jiji la Dodoma
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Ufaulu wa mitihani ya taifa kwa wanafunzi wa sekondari Jiji la Dodoma umeimarika kwa Mwaka 2025/2026, ambapo Division I, II na III zikiongezeka. Hayo yameelezwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Vincent Odero wakati akiwasilisha taarifa ya utendaji kazi kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 katika Mkutano wa Mwaka wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa jiji hilo. Alisema kuwa mwelekeo huo unaashiria maendeleo chanya katika sekta ya elimu ya sekondari, yakichangiwa na usimamizi mzuri wa elimu pamoja na juhudi kubwa za walimu katika kuboresha ufundishaji na kuongeza ufaulu wa wanafunzi. “Wanafunzi waliofanya mtihani waliongezeka kutoka 6,526 Mwaka 2024/2025 hadi 7,104 Mwaka 2025/2026, huku ufaulu wa ‘Division’ I, II na III ukiongezeka na ‘Division’ 0 na IV ukipungua. Hii inaashiria mwelekeo chanya unaoendelea,” alisema Odero. Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Viwandani, Swal...