Posts

Showing posts from August 5, 2025

Vipando bustani vya Jiji la Dodoma yamvutia DC, Dkt. Mashinji

Na. Nancy Kivuyo , DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Manyoni, Dkt. Vi n cent Mashinji ametembelea banda la vipando bustani ya mbogamboga la Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kujionea aina mbalimbali za mboga na matunda zilizoandaliwa kwaajili ya kutolea elimu na kuhamasisha wananchi kuzingatia mlo kamili. Teknolojia hizo za kisasa zinawezesha mbogamboga kupandwa kwenye vitu mbalimbali kama kiroba, kopo la maji au eneo dogo kutokana na ufinyu wa maeneo na zikaendelea kustawi kwa ubora unaotakiwa. Baada ya kupewa maelezo ya kina kuhusiana na aina mbalimbali za teknolojia ya upandaji wa mbogamboga ali sema kuwa anawapongeza wataalam kwa kubuni njia za kisasa za kuhakikisha wananchi wanakuwa na afya njema. “ Hiki kilimo cha mjini mnapaswa kukiangalia kwa jicho la ziada kwa kuhakikisha mnatoa elimu nzuri zaidi, lakini pia mshirikiane na watu wa mipango miji ili kuhakikisha watu wanapata maeneo mazuri yenye nafasi ya kufanya hiki mnachowaelekeza ” alisema Dkt. Mashinji. Kwa upande wake Afis...

Dkt. Mashinji: Tuimarishe Ubunifu wa Kilimo cha Zabibu Dodoma

               Na. Leah Mabalwe , DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Manyoni, Dkt. Vi n cent Mashinji amewataka m aafisa k ilimo wa Jiji la Dodoma kuongeza juhudi na ubunifu katika kukuza kilimo cha zabibu, kilimo ambacho ni uti wa mgongo wa uchumi wa Jiji la Dodoma. Hayo aliyasema mara baada ya kutembelea banda la Halmashauri ya Jiji la Dodoma katika maonesho ya kilimo Nanenane , ambapo alipata fursa ya kuona bidhaa mbalimbali zinazotokana na zabibu, ikiwemo juisi, divai na zabibu kavu. A li sema kuwa pamoja na jitihada zinazofanyika, bado kuna nafasi kubwa ya kuboresha na kuongeza thamani katika zao hilo. “ Jiji la Dodoma l ina nafasi kubwa ya kuwa kitovu cha zabibu Afrika Mashariki. Kwa upande wenu nyie maafisa kilimo mnapaswa kuwa wabunifu zaidi na hata kufuata zile kanuni ambazo zao hili la zabibu linapaswa kuwa hasa katika hatua ya upandaji” alisema Dkt. Mashinji. Kwa upande wake Afisa Kilimo Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Emmanuel Mayyo...