Vipando bustani vya Jiji la Dodoma yamvutia DC, Dkt. Mashinji
Na. Nancy Kivuyo , DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Manyoni, Dkt. Vi n cent Mashinji ametembelea banda la vipando bustani ya mbogamboga la Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kujionea aina mbalimbali za mboga na matunda zilizoandaliwa kwaajili ya kutolea elimu na kuhamasisha wananchi kuzingatia mlo kamili. Teknolojia hizo za kisasa zinawezesha mbogamboga kupandwa kwenye vitu mbalimbali kama kiroba, kopo la maji au eneo dogo kutokana na ufinyu wa maeneo na zikaendelea kustawi kwa ubora unaotakiwa. Baada ya kupewa maelezo ya kina kuhusiana na aina mbalimbali za teknolojia ya upandaji wa mbogamboga ali sema kuwa anawapongeza wataalam kwa kubuni njia za kisasa za kuhakikisha wananchi wanakuwa na afya njema. “ Hiki kilimo cha mjini mnapaswa kukiangalia kwa jicho la ziada kwa kuhakikisha mnatoa elimu nzuri zaidi, lakini pia mshirikiane na watu wa mipango miji ili kuhakikisha watu wanapata maeneo mazuri yenye nafasi ya kufanya hiki mnachowaelekeza ” alisema Dkt. Mashinji. Kwa upande wake Afis...