Posts

Showing posts from September 17, 2023

KATA YA CHAMWINO YAADHIMISHA SIKU YA USAFI DUNIANI

Image
  Na. Dennis Gondwe, CHAMWINO KATA ya Chamwino yaadhimisha maadhimisho ya Siku ya Usafi Duniani kwa kufanya usafi wa mazingira katika maeneo mbalimbali ya kata hiyo. Akiongelea maadhimisho hayo, Afisa Mtendaji wa Kata ya Chamwino, Lucas Nkelege alisema kuwa maadhimisho hayo yamefanyika kwa kufanya usafi wa mazingira katika barabara inayotoka makutano ya Wajenzi mpaka kona ya Viva la vida. Alisema kuwa usafi huo ulihusisha kusafisha mtaro wenye urefu wa mita 1,500. “U safi wa mazingira pia ulifanyika katika mitaro yote inayozunguka Shule ya Sekondari ya Hijra na wananchi walijitokeza na kufanya usafi katika korongo karibu na uwanja wa Shell Complex. Zaidi ya kusafisha mitaro, usafi huo ulihusisha kutoa taka ngumu na kuokota makopo na mifuko kwenye mtaro na maeneo ya pembezoni mwa barabara na korongo” alisema Nkelege . Akiongelea mafanikio ya maadhimisho Siku ya Usafi Duniani, alisema kuwa yametokana na ushirikiano wa karibu na wadau mbalimbali. “Napenda kutoa shukurani ...

CHANG’OMBE WATAKIWA KUSAFISHA MAZINGIRA KUZUIA WAHALIFU

Image
Na. Dennis Gondwe, WAKAZI wa Kata ya Chang’ombe wametakiwa kudumisha usafi wa mazingira kwa lengo la kuzuia maficho ya wahalifu na kulinda afya zao ili waweze kufanya shughuli za kujitelea maendeleo. Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Mtendaji wa Kata ya Chang’ombe, Tunu Dachi alipoongoza uzinduzi wa kampenzi ya usafi wa mazimgira katika kata hiyo tukio lililofanyika katika Mtaa wa Mazengo jijini Dodoma. Dachi alisema “nilipofika Kata ya Chang’ombe niligundua kuwa kata yetu ni chafu sana. Na katika kufanya vikao na wadau wa usafi wa mazingira tulikubaliana kuwa Mtaa wa Mazengo ndio mtaa mchafu kuliko mitaa yote. Leo nataka tushirikishane jambo rahisi sana, vikundi vya uzoaji taka vimeridhia kwamba kila Jumamosi wataungana kwa umoja wao na jamii ya mtaa husika kuja kufanya usafi wa maeneo ambayo mwenyekiti atakuwa amependekeza”. Aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mazoezi ya usafi wa mazingira kila siku ya Jumamosi. “Kwa hiyo, mwananchi akisema anaenda kumfanyia ...

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Dodoma Mjini, John Kayombo akiwaapisha wasimamizi na wasimamizi wasaidizi wa vituo vya kupigia kura kwa uchaguzi wa Diwani Kata ya Nala

Image