Posts

Showing posts from July 21, 2026

Timu ya SHIMISEMITA ya Jiji la Dodoma yajipanga kutetea ubingwa

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Kikosi cha Timu ya Watumishi wa Jiji la Dodoma cha Mpira wa Miguu kinaendelea kujifua kwa mazoezi makali kuelekea mashindano ya SHIMISEMITA 2026 yatakayofanyika jijini Mbeya, kikiwa na malengo ya kufanya vizuri na kutwaa ubingwa. Hayo aliyasema Kocha wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Watumishi Jiji la Dodoma, Given Aristides wakati wa bonanza la kimichezo lililozikutanisha Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino na Halmashauri ya Wilaya ya Gairo katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Dodoma, ambapo timu hizo zilipata nafasi ya kupima uwezo wao kabla ya kuingia kambini kwa ajili ya mashindano hayo. Alisema kuwa ushindani katika SHIMISEMITA unazidi kuongezeka kila mwaka kutokana na halmashauri nyingi kujiandaa kwa umakini, jambo linalowalazimu kuongeza kiwango cha mazoezi na nidhamu ili kufikia malengo waliyojiwekea. “Tunafahamu kuwa SHIMISEMITA ni mashindano yenye ushindani mkubwa, hivyo tunaendelea kujinoa kwa bidii kila siku. Bonanza hil...

Timu ya Jiji la Dodoma yajinoa kuelekea SHIMISEMITA Mbeya, 2026

Image
Na. Mwandishi Wetu, Dodoma MSAKO wa kutetea ubingwa wa mashindano ya Shirikisho la Michezo la Serikali za Mitaa Tanzania (SHIMISEMITA) umeanza rasmi kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma baada ya watumishi wake kushiriki bonanza la michezo lililozikutanisha Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino na Halmashauri ya Wilaya ya Gairo katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Dodoma. Bonanza hilo limekuwa sehemu ya maandalizi ya kuelekea mashindano ya SHIMISEMITA yanayotarajiwa kufanyika mwezi Agosti mwaka huu jijini Mbeya, ambapo halmashauri mbalimbali nchini zitachuana kuwania ubingwa katika michezo tofauti. Akizungumza baada ya bonanza hilo, Afisa Michezo wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Neema Kilongola alisema kuwa maandalizi yanaendelea vizuri na mechi hizo zimewapa nafasi ya kupima uwezo wa kikosi kabla ya kuelekea Mbeya. “Bonanza hili limetupa nafasi ya kujipima, kurekebisha mapungufu na kuongeza ushindani ndani ya timu. Mwaka jana tulikuwa mabingwa, hivyo mwaka h...

Timu ya Jiji la Dodoma yatakiwa kudumisha nidhamu mashindano ya SHIMISEMITA

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Wachezaji wanaojiandaa kushiriki mashindano ya SHIMISEMITA watakiwa kuwa na malengo makubwa, nidhamu na ari ili kuweza kupata ushindi. Hayo aliyasema Mwenyekiti wa SHIMISEMITA Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Gerald Ruzika wakati wa kikao chake na washiriki wa timu ya Jiji la Dodoma kilichofanyika katika ukumbi wa mikutaho wa halmashauri jijini Dodoma. Aliseama kuwa malengo yetu ni kupambania nafasi ya juu. “Mnakwenda kuiwakilisha Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Muwe na malengo ya ushindi na mkapambane kuurudisha ubingwa kama mlivyofanya mwaka jana. Fanyeni mazoezi kwa bidii, muwe na nidhamu na mshikamano ili mkaandike historia nyingine ya mafanikio,” alisema Dkt. Ruzika. Aidha, aliwasisitiza washiriki kuongeza juhudi katika mazoezi na kuzingatia maelekezo ya makocha wao ili kuhakikisha wanakuwa katika kiwango bora kitakachowawezesha kufanya vizuri na kuipeperusha vema bendera ya Jiji la Dodoma. Kwa upande wake, Nahodha wa Mpira wa Pete, Mwajuma Ban...