Posts

Showing posts from November 8, 2023

AWAMU II YA KLINIKI YA ARDHI JIJI LA DODOMA KUTATUA MIGOGORO KATA KWA KATA

Na. Dennis Gondwe, DODOMA Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Dodoma inaendesha Kliniki ya Ardhi kwa lengo la kutatua migogoro ya Ardhi na kuwaondolea kero wananchi. Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo alipokuwa akitoa taarifa ya katibu katika Mkutano wa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kupokea taarifa za utendaji kazi kwa kamati za kudumu za halmashauri kwa kipindi ya robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2023/2024 uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Kayombo alisema “baada ya Kliniki ya Ardhi ya kwanza kufanikiwa vizuri, tumeendelea na kliniki ya pili iliyoanza Jumamosi tarehe 4 Novemba na itaendelea hadi tarehe 20 Novemba, 2023. Tumepanga watu kikata, kwa siku tunasikiliza na kuhudumia kata nne. Baada ya tarehe 20 tutajipima tena kuona tumefanikiwa kiasi gani na kama watu bado wanashida zoezi litakuwa endelevu. Tunaishukuru Wizara ya Ardhi, Nyumba na...

PROF. MWAMFUPE APONGEZA UFANISI KLINIKI YA ARDHI DODOMA

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Mwenyekiti wa Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe amepongeza ufanisi wa Kliniki ya Ardhi inayoendelea jijini hapa na kusema ni mafanikio makubwa. Mwenyekiti wa Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe akitoa pongezi kwa Kliniki ya Ardhi Jiji la Dodoma Pongezi hizo alizitoa katika Mkutano wa Baraza la Madiwani wa robo ya kwanza uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri. Prof. Mwamfupe ambae ni Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema “kniliki hiyo ni muendelezo wa mafanikio katika sekta ya Ardhi. Jana pekee zimetolewa hati 217, zikijumuisha maombi yaliyopokelewa papo kwa hapo. Tuendelee kutoa mapendekezo ya namna ya kuboresha kliniki hii”. Katika hatua nyingine, Prof. Mwamfupe ambae pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya Fedha na Utawala alimteua Diwani wa viti maalum, Rosemary Nitwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Fed...

MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI JIJI LA DODOMA

Image