Posts

Showing posts from April 17, 2025

Timu ya Mpira wa Pete ya watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma yajipima na BOT

Image
  T imu ya Mpira wa Pete ya w atumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wakiwa katika mchezo wa kirafiki na t imu ya w atumishi wa Benki K uu ya Tanzania , m chezo uliochezwa katika uwanja wa Chuo cha VETA mkoani Sin g ida. Mchezo huo u li chezwa ikiwa ni maandalizi ya ushiriki wa mashindano ya michezo ya watumishi kuelekea kilele cha Mei Mosi i takayofanyika k itaifa m koani Singida.

Matukio katika Picha Timu ya Menejimenti ya Jiji la Dodoma (CMT) ikipatiwa Mafunzo ya Mfumo wa IFT-MIS

Image
 

Barabara ya Dodoma Makulu – Ntyuka kuboresha maisha ya wananchi

Image
Na. Abdul Juma, DODOMA MAKULU Ujenzi wa Barabara ya kilometa 5.2 inayounganisha Kata ya Dodoma Makulu na Ntyuka kutatua changamoto ya usafi kwa kata hizo na kufanya maisha ya wananchi kuwa bora. Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Mtaa wa Msangalale Magharibi Kata ya Dodoma Makulu, Leonard Ndama alipokuwa akiongelea mchango wa Barabara ya lami yenye urefu wa kilometa 5.2 katika mafanikio ya serikali ya awamu ya sita kwa kipindi cha miaka minne. Alisema kuwa serikali ya awamu ya sita chini ya Rais, Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kipindi cha miaka minne ilianza ujenzi wa barabara yenye kiwango cha lami iliyokuwa ni changamoto kwa wakazi wa Kata ya Dodoma Makulu walipotaka kwenda Ntyuka kufuata huduma za kijamii. Alisema kuwa walikuwa wakitumia muda mrefu njiani na kuchelewa shughuli zao jambo lililosababisha uchumi wao kuwa chini. “Tumepata mradi huu wa barabara inayotoka Dodoma Makulu kwenda Ntyuka ambayo imeleta manufaa ya kibiashara hata katika usafiri kwasababu wananchi wa...

Kata ya Dodoma Makulu yanufaika na mkopo wa asilimia 10

Image
Na. Abdul Juma, DODOMA MAKULU Mkopo wa mapato ya ndani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma usio na riba wa shilingi 328,800,000 umewawezesha wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kujikwamua kiuchumi katika kata ya Dodoma Makulu. Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Maendeleo ya Jamii wa Kata ya Dodoma Makulu, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Sophia Abdallah alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu mikopo ya mapato ya ndani iliyokopeshwa kwa wanavikundi wa kata hiyo kwa kipindi cha serikali ya awamu ya sita. Alisema kuwa serikali ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kipindi cha miaka minne imewezesha vikundi vya wanawake 21, vikundi vya vijana vitatu na vikundi vya watu wenye ulemavu sita kujikwamua kiuchumi na kuboresha maisha yao. Alisema kuwa mikopo hiyo imekuwa fursa kwa vijana kufanya biashara mbalimbali katika kata hiyo. “Baadhi ya vikundi vimeweza kununua bajaji na pikipiki ili kufanya biashara ya usafirishaji wa abiria kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma kwenda Sabasaba. Eneo la mare...

Nishati safi, yapewa kipaumbele Kikuyu Kaskazini

Image
Na. Leah Mabalwe, KIKUYU KASKAZINI   Kampeni ya kuhakikisha jamii inabaki salama na utunzaji wa mazingira kwa kutumia nishati safi katika Kata ya Kikuyu Kaskazini, imeongeza tija na uelewa kwa taasisi za elimu kuhamia katika matumizi ya nishati safi. Hayo yalielezwa na Diwani wa Kata ya Kikuyu Kaskazini, Israel Mwansasu mbele ya waandishi wa habari waliotembelea kata yake kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha miaka minne. Alisema kuwa nishati safi ni jambo muhimu sana katika kuhakikisha mazingira yanabaki salama kutokana na uharibifu uliokithiri. “Suala la matumizi ya nishati safi katika kata yetu linafanyika kwa weledi mkubwa sana, tunatumia mikutano ya hadhara kuelimisha wananchi kwasababu ndio mahali rahisi kukutana na wananchi kwa wakati mmoja. Nishati safi ina faida nyingi ikiwemo kuokoa muda, inatunza mazingira na kukuza uchumi. Tupo katika harakati za kupunguza matumizi ya mkaa kwa watu wetu wa hapa mjini na matumizi ya mkaa na kuni kwa wananc...

Zahanati ya Mpamaa yaboresha huduma Kata ya Miyuji

Image
Na. Abdul Juma, MIYUJI Wananchi wa Mtaa wa Mpamaa, Kata ya Miyuji jijini Dodoma, wameeleza kufurahia kwao maboresho makubwa yaliyofanywa na serikali katika Zahanati ya Mpamaa kuanzia ujenzi wa miundombinu, ununuzi wa vifaa tiba na usimikaji wa mfumo wa Tehama yamerahisisha upatikanaji wa huduma na kuboresha mazingira ya kufanyika kazi. Katika mahojiano na wanahabari waliotembelea zahanati hiyo kwa ajili ya kufuatilia maboresho yaliyofanywa katika zahanati hiyo wananchi walielezea kufurahia maboresho hayo na huduma zinazotolewa. Mkazi wa Mtaa wa Mpamaa, Anifa Sagika alisema kuwa anaishukuru serikali kwa kuwajengea zahanati ya Mpamaa. “Hapo awali, tulikosa huduma muhimu, hasa sisi akina mama wajawazito tulilazimika kutembea umbali mrefu au kujifungulia nyumbani. Sasa tuna huduma inatolewa karibu nasi” alisema Sagika. Nae Malimi Charles alisema kuwa anapongeza juhudi za serikali kuhakikisha huduma za afya zinapatikana katika kata hiyo. Alisema kuwa zahanati hiyo imesaidia kupunguza vifo v...