Posts

Showing posts from November 19, 2024

Mtaa wa Chikole washauriwa kujitokeza kupiga kura

Image
Na. Faraja Mbise, MSALATO Wananchi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, wametakiwa kutumia haki yao ya msingi na ya kikatiba ya kupiga kura na kuchagua viongozi walio bora na wenye tija kwa maendeleo ya mitaa yao katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba, 2024. Hayo, yalisemwa na mkazi wa Mtaa wa Chikole, Glory Kondo, Kata ya Msalato, alipokuwa akifanyiwa mahojiano kuhusu muitikio wa wananchi kujitokeza kupiga kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. “Kuna umuhimu wa kuchagua kiongozi kwasababu ni bora ukamchagua kiongozi ambae unaona kwako wewe atakufaa kuongoza vizuri, kuliko kutokupiga kura ina maana kwamba, utakuwa umeburuzwa, unaweza ukachaguliwa kiongozi ambaye ulikuwa haumuhitaji lakini itabidi ukubaliane nae kwasababu haujajiandikisha ili kuchagua kiongozi unayemtaka. Hivyo, ni muhimu kujiandikisha na ukamchagua kiongozi unayemtaka” alisema Kondo. Akiongolea kuhusu wananchi kujitokeza kupiga kura, alitoa wito kwa wakazi wote waliojiand...

Taasisi zatakiwa kupanda miti kukijanisha Dodoma

Image
  Na. Faraja Mbise, DODOMA Taasisi zilizopo Halmashauri ya Jiji la Dodoma pamoja na wananchi, wamehimizwa kupanda miti katika maeneo wanayofanyia kazi na wanayoishi ili kuifanya Dodoma iwe ya kijani na kukabiliana na madiliko ya tabia ya nchi. Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Kaspar Mmuya akipanda mti  Hayo yalisemwa na Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Kaspar Mmuya alipokuwa akizungumza na wadau mbalimbali katika zoezi la upandaji miti kwa awamu ya pili lililohusu wazaliwa wa mwezi Novemba lililofanyika tarehe 18 Novemba, 2024 katika eneo la Jakaya Kikwete Square, Chuo Kikuu cha Dodoma. “Tumeshaanza kuyagundua maeneo kama matatu hivi, lakini hili ni la pili tutatekeleza Januari au Februari, tayari tumeshaongea na Halmashauri ya Jiji la Dodoma na watatupatia. Maeneo katika Jiji la Dodoma yapo, Dodoma kuwa kijani inawezekana. Watu wanaishi na historia kuwa Dodoma haistawi, ni kavu, ni kame. Hapana, Dodoma sio kame na mifano ipo, mimi ninawaambieni, tafuteni muda, mzunguke mitaan...