Posts

Showing posts from January 8, 2025

SHIKUHA kutatua kero za Abiria

Image
Na. Coletha Charles, Dodoma Katibu Mkuu wa Shirika la Kutetea Haki za Abiria nchini (SHIKUHA), Mhandisi Hashim Ramadhani, amewataka abiria kuelewa elimu na haki zao wanapotumia huduma za usafiri kwa kushirikiana na Afisa Usalama barabarani ili kuhakikisha mabasi yanazingatia sheria na huduma bora.   Akizungumza katika mkutano na wajumbe wa shirika hilo kutoka mikoa mbalimbali katika ukumbi wa mikutano wa Rafiki Hoteli jijini Dodoma, Katibu Mkuu alifafanua kampeni za elimu zimekuwa muhimu katika kuhakikisha abiria wanakuwa na uelewa wa kina kuhusu haki zao. Alisema kuwa, elimu hiyo inatolewa kupitia stendi za mabasi, masoko na sehemu zenye mikusanyiko. Pia alibainisha kuwa maafisa wa shirika hilo watashirikiana na wadau wa sekta ya usafiri kuhakikisha sheria na kanuni zinatekelezwa kwa maslahi ya abiria. ā€œTumeweka msisitizo katika kuwaelimisha abiria juu ya jinsi ya kuripoti changamoto wanazokumbana nazo, kama vile kucheleweshwa kwa safari, kupotea kwa mizigo, au huduma zisi...

SHIKUHA yatakiwa kutoa elimu ya haki za Abiria

Image
Na. Asteria Frank, DODOMA Shirika la Kutetea Haki za Abiria (SHIKUHA) latakiwa kuwapa elimu ya kutosha abiria kwa lengo la kutatua changamoto za usalama barabarani na kufanya abiria wajuwe haki na wajibu wao. Kauli hiyo imetolewa na Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe, katika mkutano uliofanyika ukumbi wa Rafiki Hoteli Dodoma alipomuwakilisha Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini. Prof. Mwamfupe alisema kuwa elimu itolewe wakati safari inapoanza ili abiria akipata sehemu ya kujitetea wanakuwa na amani na dereva akienda tofauti na sheria za barabarani waweze kutoa taarifa kuhusu tukio hilo kwa watu sahihi. ā€œRai yangu kubwa kama kuna kitu ambacho ningewahasa nyie kama shirika kulifanya hili basi ni kuwa na mpango mkakati na huo mpango utaonesha dira yenu kama mlivyosema kwenye risala na lakini mnataka kufikia wapi mwaka huu na je, tunapimaje viongozi maana nyie ni viongozi wa kitaifa kwa kutunza na kusaidia abiriaā€ alisema Prof. Mwamfupe. Mwenyekiti wa Taifa SHIKUHA, ...

DC Shekimweri ahimiza mpango wa lishe bora shuleni

Image
Na. Aisha Ibrahim, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri aliwataka wakuu wa shule na walimu wakuu kutekeleza mpango wa huduma ya chakula kwa wanafunzi wote shuleni ili kuhakikisha wanapata lishe bora jambo litakalopelekea kujifunza kwa ufanisi. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri  Aliyasema hayo ofisini kwake wakati akihamasisha wazazi na walezi kujitokeza kwa wingi kuandikisha watoto shuleni katika ngazi ya awali na msingi pia wale wanaojiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka wa masomo 2025. Akisisitiza kuhusu mpango wa huduma ya chakula kwa wanafunzi shuleni, ā€œā€¦ā€¦kuna uhusiano mkubwa sana kati ya ufaulu na lishe, mtoto ambaye hajashiba ni ngumu sana kumsikiliza mwalimu akamuelewa na akazingatia, ni tofauti na mtoto aliyepata chakula shuleniā€ alisema Alhaj Shekimweri. Kwa upande wa wazazi na walezi katika Jiji la Dodoma walisema kuwa wamepokea vizuri mpango wa huduma ya chakula kwa wanafunzi shuleni ili kuhakikisha wanapata lishe bora ikiwa ni c...