Posts

Showing posts from August 7, 2024

Jiji la Dodoma lavuka lengo na kukusanya 103% makusanyo ya mapato ya ndani 2023/2024

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imefanikiwa kukusanya fedha za mapato ya ndani shilingi 51,402,342,226 sawa na asilimia 103 ya lengo la mwaka wa fedha 2023/2024 wakati ikipeleka fedha nyingi kwenye miradi ya maendeleo. Katibu wa Mkutano wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa Mkutano wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani wa kupokea na kujadili taarifa za utendaji kazi kwa kipindi cha robo ya nne (Aprili-Juni, 2024) uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Kayombo ambae ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema kuwa bajeti ya mapato ya ndani ya mwaka 2023/2024 ilikuwa shilingi 50,097,458,280. Fedha iliyokusanywa ni shilingi 51,402,342,226 sawa na asilimia 103. Alisema kati ya fedha hizo za mapato ya ndani, asilimia 73.4 ilipelekwa kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo na asilimi...

Ujenzi wa Kituo Kipya cha Afya Chang'ombe kusaidia wananchi zaidi ya 200 kwa siku

Image
Na. John Masanja, CHANG’OMBE Wananchi wa Kata ya Chang’ombe waishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kupunguza kadhia ya upatikanaji wa huduma za afya kupitia ujenzi wa Kituo kipya cha Afya Chang’ombe.   Diwani wa Kata ya Chang’ombe, Bakari Fundikila akifafanua jambo Akizungumza katika mahojiano maalum na wanahabari, Diwani wa Kata ya Chang’ombe, Bakari Fundikila alisema kuwa ujenzi wa kituo hicho uliogharimu zaidi ya shilingi Milioni 500 umekuwa na msaada mkubwa kwa wakazi wa kata hiyo. Kituo hicho ni msaada pia kwa wananchi wa maeneo ya pembezoni kwakuwa awali walikuwa wanatembea umbali mrefu kutafuta huduma za kiafya.   Diwani Fundikila alisema kuwa kwasasa kituo hicho kinaendelea kutoa huduma mbalimbali za kawaida na za kibingwa kwa wananchi. Alisema kuwa kabla ya ujenzi wa kituo hicho huduma hizo walikuwa wakizifuata katika hospitali kubwa zilizo mbali ikiwemo Hospitali ya Mkoa wa Dodoma.   “Ukienda kutazama taarifa za wagonjwa, utakuta kwa siku kituo h...

Jiji la Dodoma lakusanya 103% mapato ya ndani 2023/2024

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imefanikiwa kukusanya fedha za mapato ya ndani shilingi 51,402,342,226 sawa na asilimia 103 ya lengo la mwaka wa fedha 2023/2024 wakati ikipeleka fedha nyingi kwenye miradi ya maendeleo. Katibu wa Mkutano wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo Kauli hiyo ilitolewa na Katibu wa Mkutano wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, John Kayombo wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani wa kupokea na kujadili taarifa za utendaji kazi kwa kipindi cha robo ya nne (Aprili-Juni, 2024) uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Kayombo ambae ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma alisema kuwa bajeti ya mapato ya ndani ya mwaka 2023/2024 ilikuwa shilingi 50,097,458,280. Fedha iliyokusanywa ni shilingi 51,402,342,226 sawa na asilimia 103. Alisema kati ya fedha hizo za mapato ya ndani, asilimia 73.4 ilipelekwa kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo na asilimi...