Posts

Showing posts from March 29, 2025

Waziri Mavunde asisitiza miradi mikubwa ya madini iliyopewa leseni kuanza kazi haraka

Image
Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, ameagiza miradi mikubwa na ya kati ya Madini ambayo tayari imekwishapewa leseni kuanza utekelezaji wake mara moja ili kuchochea ukuaji wa sekta na kuleta manufaa kwa taifa na kutimiza azma ya serikali kutoa leseni hizo. Waziri wa Madini, Anthony Mavunde Aliyasema jijini Dodoma wakati akizungumza katika mkutano maalum na Chemba ya Migodi Tanzania (TCM) kwa lengo kujadili masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya Madini ili kuboresha uendelezaji na usimamizi wa shughuli za uchimbaji na biashara ya Madini kwa manufaa ya sekta na taifa kwa ujumla. Waziri Mavunde alisema serikali inataka kuhakikisha kuwa miradi yote ya uchimbaji Madini iliyopangwa kuanza inaanza mara moja bila kucheleweshwa, na kuwa serikali kwa upande wake imejitahidi kurahisisha taratibu kwa wawekezaji na sasa ni wakati wa sekta binafsi kuchukua hatua kwa upande wao. ā€œSerikali imefanya kazi yake, tumeondoa vikwazo vingi na kurahisisha utaratibu. Sasa ni juku...

Shule shikizi Ipala, mkombozi kwa wanafunzi wanaotembea umbali mrefu

Image
Na. John Masanja, IPALA Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa, aishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha miundombinu ya elimu msingi katika kata hiyo kwa kujenga shule shikizi ili kutengeneza mazingira rafiki kwa wanafunzi wenye umri mdogo kupata elimu bora. Diwani wa Kata ya Ipala, George Magawa Aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari waliofanya ā€˜media tourā€™ kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali katika Kata ya Ipala kuanzia mwaka 2021 hadi 2025. Diwani Magawa alisema kuwa katika miaka minne ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita, elimu katika Kata ya Ipala imekuwa kwa kasi. ā€œSerikali yetu tukufu imetuletea elimu hadi kwenye kata yetu. Tuna shule shiziki mbili zimeanzishwa kwa lengo la kusaidia wanafunzi wadogo wanaotembea umbali mrefu karibu kilomita tano kufuata elimu. Sasa hivi uwepo wa madarasa haya matatu nafuu imekuwa kubwa sana kwa kuwapunguzia watoto wadogo kutembea umbari mrefuā€ ...

Nyumba ya mtumishi kuchangia huduma masaa 24 Zahanati ya Ipala

Image
Na. Nancy Kivuyo, IPALA Mradi wa ujenzi wa nyumba ya mtumishi katika Zahanati ya Ipala uliogharimu kiasi cha shilingi 55,000,000, umeleta maboresho katika utoaji wa huduma ya afya katika kata hiyo. Nyumba ya Mtumishi Zahanati ya Ipala Hayo yalielezwa na Muuguzi kutoka Zahanati ya Ipala, Tumain Sanga alipokuwa akiwaelezea waandishi wa habari waliofanya ā€˜media tourā€™ kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na serikali katika kata hiyo kuanzia mwaka 2021 hadi 2025. Alisema kuwa anatoa pongezi kwa serikali kuwajengea nyumba hiyo ili kurahisisha utoaji wa huduma za afya katika kata hiyo. ā€œTunaipongeza serikali kutujengea nyumba ya mtumishi, uwepo wa nyumba hii imeturahisishia kutendaji wa kazi mzuri. Laiti tungekuwa mbali tungeshindwa kuwahudumia wananchi vizuri na kwa wakati, lakini sasa wagonjwa wanaweza kuja muda wowote na wakatukuta na tukawahudumia kwa masaa 24. Tunaishukuru sana serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, tuna...

Wananchi wa Mtaa wa Mwaja, Jiji la Dodoma washiriki kufanya usafi wa mazingira wa Jumamosi ya mwisho wa Mwezi, Machi, 2025

Image
Leo tarehe 29.03.2025, wananchi wa Mtaa wa Mwaja, Kata ya Chamwino, Halmashauri ya Jiji la Dodoma wameshiriki zoezi la usafi wa Mazingira wa kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi kwa lengo la kuweza mazingira safi kwa ajili ya afya zao. Usafi huo uliongozwa na Mwenyekiti wa Mtaa wa Mwaja, Athumani Makuka ambaye aliambatana na Afisa Mtendaji wa Mtaa, Mwanaasha Mani. Zoezi hilo la usafi lilifanyika katika mtaro unaopita pembezoni mwa Shule ya Msingi Chinangali ambao umehusisha kuzibua mtaro wenye urefu wa mita 100 sambamba na kutoa taka ngumu kama makopo na mifuko kwenye mtaro huo ili kuruhusu maji yaliyotuwama kwa sababu ya mvua kutiririka pasina kizuizi chochote.