Afisa Elimu Jiji la Dodoma anunua jina la Rais Samia kwa Laki 5
Na. Dennis Gondwe, MIYUJI MKUU wa Divisheni ya Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Zainab Abdallah amefurahishwa na uwezo wa mwanafunzi mwenye mahitaji maalum, Angel Elias alipoandika jina la Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutumia mdomo wake na kununua jina hilo kwa shilingi 500,000. Mwanafunzi Angel Elias wa shule ya Msingi Hombolo Bwawani anayeandika kwa kutumia mdomo Furaha hiyo aliionesha katika kikao cha wadau wa elimu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kilichoambatana na utoaji tuzo za kitaaluma na kufanyika katika Shule ya Msingi St. Gasper iliyopo Miyuji jijini hapa. “Mheshimiwa Mwenyekiti kabla ya yote, ninaomba kwa ridhaa yako kama hautajari, hilo neno lililoandikwa na mtoto wangu Angel ‘I am so excited’. Nitalinunua kwa shilingi 500,000. Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma ni ukweli kwamba hata wale wanafunzi wasio na mahitaji maalum tunaowafundisha hawajifunzi haraka kama huyu anavyo fanya” alisisitiza Mwl. Abdallah. Akiunga mkono tukio hilo, Mkuu wa Di...