Posts

Showing posts from August 7, 2026

Jiji la Dodoma kuwa kinara ushirikiano na TBS

Image
Na. Mwandishi wetu, DODOMA Halmashauri ya Jiji la Dodoma imewataka maafisa afya na watumishi wa sekta mbalimbali kuimarisha ushirikiano na kutumia ipasavyo mafunzo ya matumizi ya mfumo wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) ili kuongeza ufanisi katika ukaguzi na usajili wa bidhaa. Akifungua mafunzo hayo, Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma, Dkt. Sebastian Pima alisema kuwa mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo washiriki kutumia mfumo wa TBS kwa usahihi ili shughuli zote za ukaguzi na usajili ziweze kufanyika kwa ufanisi kupitia mfumo huo. “Kila mmoja anatakiwa kushirikiana na wenzake, hizi ni kazi za timu, si za mtu mmoja. Tunataka Dodoma iwe mfano wa kuigwa nchini katika utekelezaji wa majukumu ya ushirikiano kati ya TBS na halmashauri, kila afisa atapangiwa malengo ya kila siku na kila wiki yatakayosaidia kuongeza utendaji na kufikia malengo ya ukusanyaji wa mapato pamoja na kuboresha huduma kwa wananchi," alisema Dkt. Pima. Aidha, aliwahimiza washiriki kutumia fursa ya uwepo wa...

Dodoma Jiji yajiandaa Ngoma na Kwaya SHIMISEMITA, 2026

Image
    Watumishi wa Timu ya Halmasahuri ya Jiji la Dodoma inayoshiriki Mashindano ya SHIMISEMITA 2026 jijini Mbeya wanaendelea na kujifua katika mazoezi makali kwa ajili ya mashindano ya ngoma na kwaya, mazoezi yanayoendelea katika viwanja vya Shule ya Sekondari Dodoma. Mashindano ya SHIMISEMITA ya Mwaka 2026 yanaongozwa na kaulimbiu isemayo “Tupo Tayari kwa AFCON 2027”.