Posts

Showing posts from October 5, 2024

“Maandalizi Uandikishaji Uchaguzi Serikali za Mitaa yamekamilika” Dkt. Sagamiko

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko amesema kuwa maadalizi katika uandikishaji kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa yamekamilika kwa asilimia mia moja. Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko akifafanua jambo Dkt. Sagamiko alitoa kauli hiyo wakati akimkaribisha mgeni rasmi kufungua Bonanza kubwa la kihistoria la kuhamasisha umma kushiriki mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 katika uwanja wa Shule ya Sekondari Dodoma. Msimamizi huyo alisema kuwa maandalizi katika uandikishaji kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa yamekamilika. Vifaa vyote vimefika na rasilimali fedha, Rais amewezesha kwa asilimia mia moja. “Kwa maandalizi, tupo timamu. Matamanio yetu tukamilishe zoezi la uandikishaji katika siku tatu” alisisitiza Dkt. Sagamiko. Aidha, aliwapongeza watumishi na wananchi waliojitokeza kwa wingi kushiriki ‘jogging’ n...

Madiwani Jiji la Dodoma wapo tayari kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MADIWANI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wapo tayari kushiriki mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa asilimia 100. Mwakilishi wa Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Daud Mkhandi alipotoa salamu katika Bonanza kubwa la kihistoria la kuhamasisha umma kushiriki mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 Kauli hiyo ilitolewa na Mwakilishi wa Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Daud Mkhandi alipotoa salamu katika Bonanza kubwa la kihistoria la kuhamasisha umma kushiriki mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 lililofanyika katika uwanja wa Shule ya Sekondari Dodoma. Mkhandi ambae ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mipango Miji na Mazingira alisema “kwa niaba ya waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, tupo tayari kushiriki zoezi la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa asilimia 100. Waheshimiwa Madiwani tupo tayari kuwahamasisha wananchi kwenda kujiandikisha. Waheshimiwa Madiwani tupo tayari kuwahamasish...

RC Dodoma atamani Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ufanikiwe kwa 100%

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA MKOA wa Dodoma unatamani kuona zoezi la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa linafanikiwa kwa asilimia mia moja kwa kuhakikisha kila mwananchi anashiriki kikamilifu katika uchaguzi huo. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri wakati akifungua Bonanza kubwa la kihistoria la kuhamasisha umma kushiriki mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Shule ya Sekondari Dodoma Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri wakati akifungua Bonanza kubwa la kihistoria la kuhamasisha umma kushiriki mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa lililofanyika katika uwanja wa Shule ya Sekondari Dodoma. Alhaj Shekimweri alisema “Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma anatufundisha kujitambua na kujithamini kupitia kaulimbiu yake isemayo ‘Dodoma Fahari ya Watanzania’. Pia Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan anatekeleza miradi mkubwa katika Dodoma ikiwemo ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa kimataifa Msalato. Ujenzi wa Barabara ya Mzunguko na ujen...