Posts

Showing posts from March 6, 2025

Wanawake waaswa kupaza sauti unyanyasaji wa Kijinsia

Image
Na. Leah Mabalwe, DODOMA Wanawake na wasichana waaswa kutoa taarifa za unyanyasaji wa kijinsia kwa wakati pindi wanapofanyiwa ukatili huo. Hayo yalisemwa na Afisa Maendeleo ya Jamii Dawati la Kisheria, Rehema Mwalyambi wakati alipotembelea Kituo cha Redio A FM, wakati wa ziara ya wanawake wa Jiji la Dodoma katika vyombo mbalimbali vya habari ikiwa ni shamrashamra kuelekea kilele cha Siku ya Wanawake Duniani, ambapo kwa mwaka huu maadhimisho yake kitaifa yatafanyika mkoani Arusha. Mwalyambi alisema ā€œwanawake wote pamoja na watoto wa kike tunaomba msiogope kutoa taarifa katika dawati la kijinsia lilipo katika   Halmashauri   ya Jiji la Dodoma kwasababu tunaona wanawake wengi wanaogopa sana kutoa taarifa pale wanapofanyiwa unyanyasaji wa kijinsia. Naomba sana msiogope kwasababu sasa hivi kuna haki kwa kila mtu awe mwanamke au mwanaume, kuna sheria na adhabu pia pale tuu mtu atakapofanyiwa vitendo ukatili. Sisi kama dawati la msaada wa kisheria tupo kwaajili ya kutoa msaada kw...

Matukio katika Picha Wanawake wa Jiji ndani ya Studio za A FM kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani

Image
 

Jiji la Dodoma latembelea Studio za Dodoma FM kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Image
  Wataalam wa Maendeleo ya Jamii kutoka Jiji la Dodoma na wadau wakiwa katika Studio za Dodoma FM 98.4 kuelezea maandalizi ya Siku ya Wanawake Duniani chini ya Kaulimbiu isemayo  "WANAWAKE NA WASICHANA 2025, TUIMARISHE HAKI, USAWA NA UWEZESHAJI"

Jiji latoa Mil 20 kukuza mtaji Kikundi cha Winning Star

  Na. Faraja Mbise, IPAGALA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma ilikipatia mkopo usio na riba wa shilingi 20,000,000 Kikundi cha Winning Star kwa ajili ya kuongeza mtaji kwa shughuli ya ufugaji kuku wa mayai na nyama na kuongeza wigo wa ajira. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Patrick Sebyiga wakati akisoma taarifa ya Kikundi cha Winning Star kinachojishughulisha na ufugaji wa kuku wa mayai na nyama katika Kata ya Ipagala mbele ya kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Dodoma ilitotembelea kikundi hicho. Sebyiga alisema ā€œl engo kuu la kikundi hiki ni kutumia fursa ya ufugaji ili kuajiri na kutoa ajira kwa wengine hasa vijana . Ai dha , kujikwamua kiuchumi kwa sababu kwa kufanya hivyo , kikundi kimeondoa u tegemezi na umasiki kwenye familia hupungua. Matamanio ya kikundi ni kufuga kuku 10,000 kutokana na uhitaji mkubwa wa mayai hapa Dodoma ā€ . Akiongelea mtaji wa kikundi hicho, Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii Jij...

Jiji latoa 25,000,000 kumalizia Bweni Mbalawala Sec

Na. Nancy Kivuyo, NALA HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma yatoa shilingi 25,000,000 kwa ajili ya umaliziaji wa ujenzi wa bweni kwa Shule ya Sekondari Nala kwa lengo la kuwaondolea wanafunzi kutembea umbali mrefu kwenda shule na kuongeza ufaulu. Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Fredrick Mwakisambwe alipokuwa akisoma taarifa ya umaliziaji wa bweni, vyoo na utengenezaji wa vitanda katika Shule ya Sekondari Nala kwa Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Dodoma. Mwl. Mwakisambwe alisema ā€œs hule hii ilianza rasmi tarehe 05 Aprili, 2005 ikiwa na wanafunzi 71 . Idadi ya wanafunzi iliendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka na shule kukumbwa na changamoto mbalimbali , mojawapo ikiwa ni wanafunzi wengi kutembea umbali mrefu kutoka nyumbani. Hata hivyo , changamoto hi yo ilikuwa kubwa zaidi kwa wanafunzi wa kike na hivyo , uongozi wa shule pamoja na b odi waliomba kujengewa mabweni kwaajili ya wanafunzi wa kike kwa lengo la kuwaep...