Posts

Showing posts from November 12, 2025

Changia Damu kuokoa maisha

Image
  ‎Na. Mwandishi Wetu, DODOMA ‎ ‎Wananchi wahimizwa kuchangia damu ili kuokoa maisha ya wale wanaopata dharura ya kuhitaji huduma ya kuongezewa damu. ‎ ‎Hamasa hiyo ilitolewa na Mkuu wa Timu za Ukusanyaji Damu Kanda ya Kati, Dr. Leah Kitundya katika kliniki ya upimaji wa bure wa magonjwa yasiyoambukiza inayoendelea katika bustani ya mapumziko Nyerere Square jijini Dodoma. ‎ ‎Alisema kuwa kila mwananchi anawajibu wa kuchangia damu kwasababu inasaidia wakati wa uhitaji. "Wananchi mliopo hapa Nyerere Square tunawaomba na kuwakumbusha kuchangia damu kwasababu itatusaidia sote wakati wa uhitaji. Damu yako inaweza kumsaidia mtu ambae hukutegemea ingemfikia. Changia kuboresha afya za wengine" alisema Dr. Kitundya. ‎ ‎Aliwaita wananchi kuchangia damu huku akiwakumbusha kujitokeza kwa wingi kujitolea kwasababu zinapotokea ajali ama dharura za kuhitaji damu kwaajili ya kuokoa maisha wapo pia ndugu na jamaa wa karibu wanaweza kukumbwa na kadhia hiyo. ‎ ‎"Ndugu z...

Wananchi waitwa kupima magonjwa yasiyoambukiza bure Nyerere Square

Image
  Na. Mwandishi Wetu, DODOMA Mratibu wa Magonjwa Yasiyoambukiza Mkoa wa Dodoma, Dkt. Missana Yango amewataka wananchi jijini Dodoma kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi la upimaji wa magonjwa yasiyoambukiza linaloambatana na utoaji wa elimu ya afya kuhusu magonjwa mbalimbali.   Alitoa wito huo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika bustani ya mapumziko Nyerere Square, ambapo maadhimisho hayo ya wiki ya upimaji wa magonjwa yasiyoambukizwa yakiendelea jijini Dodoma.   Alisema kuwa huduma hizo zinatolewa bila malipo na zinahusisha upimaji wa magonjwa kama shinikizo la damu, kisukari, saratani, magonjwa ya moyo pamoja na utoaji wa elimu ya lishe bora na mtindo wa maisha wenye afya. “Lengo letu ni kuwafikia wananchi wengi kadri iwezekanavyo, ili wajitambue kiafya na kuchukua hatua mapema kabla magonjwa haya hayajawa sugu. Huduma zote tunazotoa hapa ni bure, hivyo tunawahimiza wananchi wajitokeze kwa wingi” alisema Dkt. Yango.   Aliongeza ku...