Posts

Showing posts from August 3, 2024

Wafanyabiashara wanufaika na ufunguzi wa Nanenane na uzinduzi wa SGR

Image
Na. Rahma Abdallah, NANENANE NA KIKUYU KUISNI Wafanyabiashara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamenufaika kutokana na ufunguzi wa maonesho ya siku ya Nanenane yaliyofanyika katika viwanja vya Nanenane Nzuguni jijini Dodoma pamoja na ufunguzi wa treni ya kisasa ya mwendo kasi inayotumia umeme (SGR), ufunguzi huo uliofanyika Kata ya Kikuyu Kusini jijini Dodoma.   Hayo yamezungumzwa na wafanyabiashara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma mapema jana katika ufunguzi wa maonesho ya Nanenane pamoja ufunguzi wa Treni ya kisasa inayotumia umeme (SGR). “Nashukuru Mungu mimi nikiwa kama mfanyabiashara wa chakula nimenufaika sana kwa sababu watu ni mengi sana hatuna budi kumenya viazi vingi ili wateja wetu wanapokuja kukuta kila kitu kiko vizuri pia kupitia ufunguzi huu sisi kama wafanyabiashara tumepata fursa kwasababu kabla ya uzinduzi huu biashara haikuwa nzuri kabisa kwa sababu ya ukosefu wa watu (wateja) lakini kwa kupitia uzinduzi huu tumechangamkia na kufanya biashara’’ alisema ...

Viongozi wamshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kukuza sekta za Mifugo na Uvuvi

Image
Na . Flora Nadoo , NANENANE Naibu Waziri wa M ifugo na U vuvi , Alexander Mnyet i amshukuru Rais , Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo ameendelea kuzipa kipaumbele sekta za mifugo na uvuvi ili zichangie katika uchumi wa taifa.     Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan (picha na maktaba) Shukrani hizo alizitoa wakati akitoa salamu za Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika uzinduzi wa maonesho ya Nanenane yanayofanyika katika viwanja vya Nanenane Nzuguni Dodoma. Mnyeti a lisema "Mh eshimiwa Rais ameongeza bajeti ya wizara yangu yangu kutoka shilingi bilion i 295.9 mwaka 2023/2024 hadi shilingi bilion i 460.3 kw a mw a ka 2024/2025 sawa na nyongeza ya 50.5%. Fedha hizi zitatumika katika kuimarisha sekta ya mifugo na uvuvi na kuongeza mchango wake katika pato la Taifa. Pia Waziri wa Kilimo Mh.Husein Bashe alianza kwa kumshukuru mgeni rasmi Waziri mkuu Mh.Kasim Majaliwa Kasim kwa kutenga muda wake na kuifanya kazi hiyo.Awashukuru kwa mchango wao mkubwa sana kwenye kilim...

Uwanja wa Maonesho wa Nanenane wafurika

Image
Na. Flora Nadoo, NANENANE Uwanja wa maonesho ya Nanenane Kanda ya Kati Dodoma, wafurika watu kutoka sehemu mbalimbali kwa ajili ya kushuhudia ufunguzi huo. Mbali na ufunguzi huo wa maonesho ya Nanenane, wananchi washuhudia uzinduzi wa Tukutuku (Pikipiki za miguu mitatu) takribani 100 ambazo zitagawiwa kwa vijana. Kupitia pikipiki hizo vijana watapata faida kubwa sana kwasababu ni pikipiki zilizotengenezwa kisasa zaidi na hivyo zitakuwa zinatoa kahawa ya viwango vya juu sana. Kwa upande wa burudani, wananchi walifurahia sana wagogo wakicheza ngoma zao za asili kwa umahili mkubwa wakiongozwa na mwalimu wao aliyefahamika kwa jina la Malima.   Kutokana na kufurika kwa watu hao, watu wenye vyombo vya moto kama bajaji, pikipiki na magari wajipatia faida kubwa tofauti na siku zote kufuatia kutoa huduma ya usafiri. Habari hii imehaririwa na Janeth Gerald MWISHO

TLS yashauriwa kusimamia haki na usawa nchini

Image
Na. Janeth Gerald, DODOMA Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Dotto Biteko amekitaka Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) na mawakili kusimamia haki na usawa nchini ili kuhakikisha haki inatendeka kwa watu kwa lengo la kuchochea maendeleo. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Dotto Biteko  Kauli hiyo aliitoa wakati akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufungua mkutano mkuu wa mwaka wa (TLS) uliofanyika jijini Dodoma. Dkt. Biteko alisema, TLS wakati inaadhimisha miaka 70 tangu kuanzishwa kwake, wanachama wake wanatakiwa kutafakari mwelekeo wa chama hicho kitaaluma ili kuendana na azma ya serikali ya awamu ya sita ambayo imeweka nia thabiti katika kuhakikisha haki inaonekana ikitendeka. "Tumieni muda kusema na kusikiliza hoja za watu wanaojua na wasiojua kwa kuwa nchi hii inaendeshwa kwa mujibu wa sheria kuhakikisha kuna hekima mahala pa kazi" alisema Dkt. Biteko. Aidha, aliwataka wanachama wa TLS kutumia taaluma yao kushiriki kikam...

Serikali kuboresha viwanja vya maonesho ya Nanenane

Image
Na. Moureen John, NANENANE Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema serikali itaendelea kufanya maboresho katika viwanja vya maonesho ya Nanenane ikiwa ni mkakati wa kuchangia ukuaji wa uchumi nchini. Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe Kauli hiyo aliitoa wakati wa uzinduzi maonesho ya kimataifa ya Nanenane kanda ya kati katika uwanja wa Nanenane Nzuguni jijini Dodoma. Waziri Bashe alisema “Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan alitoa maelekezo mwaka jana jijini Mbeya kwamba serikali ianze kufanya mabadiliko ya ujenzi kwa viwanja vya maonesho ya Nanenane. Kiwanja cha kwanza ni Nzuguni, Dodoma na Mwakangale, Mbeya katika hali ya kawaida tungesema tumehairisha shughuli za Nanenane mpaka tumalize hali ya ujenzi lakini tukasema Nanenane itaendelea na ujenzi utaendelea kwa wakati mmoja. Ujenzi umeanza wa uwanja huu na ujenzi huo utakuwa ni wa awamu tatu mpaka utakapokamilika na awamu ya kwanza ndio imeanza na ilikuwa shughuli ya kuondoa watu waliokuwa wamevamia eneo hili tunawahukuru sana wa...

Wafanyabiashara wanufaika na ufunguzi wa Nanenane na uzinduzi wa SGR

Image
Na. Rahma Abdallah, NANENANE NA KIKUYU KUISNI Wafanyabiashara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamenufaika kutokana na ufunguzi wa maonesho ya siku ya Nanenane yaliyofanyika katika viwanja vya Nanenane Nzuguni jijini Dodoma pamoja na ufunguzi wa treni ya kisasa ya mwendo kasi inayotumia umeme (SGR), ufunguzi huo uliofanyika Kata ya Kikuyu Kusini jijini Dodoma. Hayo yamezungumzwa na wafanyabiashara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma mapema jana katika ufunguzi wa maonesho ya Nanenane pamoja ufunguzi wa Treni ya kisasa inayotumia umeme (SGR). “Nashukuru Mungu mimi nikiwa kama mfanyabiashara wa chakula nimenufaika sana kwa sababu watu ni mengi sana hatuna budi kumenya viazi vingi ili wateja wetu wanapokuja kukuta kila kitu kiko vizuri pia kupitia ufunguzi huu sisi kama wafanyabiashara tumepata fursa kwasababu kabla ya uzinduzi huu biashara haikuwa nzuri kabisa kwa sababu ya ukosefu wa watu (wateja) lakini kwa kupitia uzinduzi huu tumechangamkia na kufanya biashara’’ alisema mfanyabias...

PM azindua Pikipiki za miguu mitatu kuwawezesha vijana

Image
Na . Flora Nadoo , NANENANE Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kas s im Majaliwa amezindua zoezi la usambazaji wa pikipiki za miguu mitatu 100 kwa ajili ya vijana katika viwanja vya N anenane j ijini Dodoma. Alisema kuwa p ikipiki hizo zitatolewa kwa mkopo nafuu sana na marejesho hayatakuwa na riba yoyote. “ Pikipiki hizi zinamashine ya kusagia kahawa, sehemu za kukaa watu kwa ajili ya kusambaza kahawa ” alisema Waziri Bashe . Alisema kuwa Shirika la kuhudumia viwanda vidogo SIDO wanatengeneza tera la miguu mitatu. “Ndani yake zitakuwa na friji dogo, brenda na sehemu za kuonesha mazao . M tu ataweza akaihamisha au akakaa sehemu moja ya kudumu. Pia t ela hizo zitakuwa na ‘ solar panel ’ kwa ajili ya kuifanya kazi hiyo. Tunaanza kugawa kwa ajili ya viwanda ” alisema Waziri Bashe .   Aidha, serikali ilitoa rai kwa vijana wajitokeze kwa wingi kuchukua pikipiki hizo kwasababu ni chachu ya maendeleo katika jamii na taifa kiujumla. Kupitia pikipiki hizo zitaw...

Nanenane ni muhimu kujifunza Kilimo na Ufugaji bora

Image
Na. Rahma Abdallah na Jackline Patrick, NANENANE Maadhimisho ya siku ya wakulima Nanenane ni maonesho ya muhimu ambayo humwezesha mwananchi kujifunza katika kilimo, ufugaji pamoja na uvuvi. Maonesho hayo ni mahususi kwa kila mtanzania katika kuzalisha mazao yenye tija kwa kutumia teknolojia ya kisasa. Hayo yalizungumzwa na Diwani wa Kata ya Kikombo, Emmanuel Manyono alipokua akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maonesho ya kimataifa ya Nanenane jijini Dodoma. Manyono alisema kuwa maadhimisho hayo yanaleta tija kwa jamii na pia kuwapa wakulima elimu ya kilimo na ufugaji bora. “Maonesho haya yamekua yakileta tija, kumekua na mafunzo mengi yakisaidia wakulima kuondokana na kilimo cha zamani na sasa kulima kwa kuzingatia kilimo cha kisasa. Kilimo cha kisasa kinamafanikio makubwa, mkulima analima shamba dogo linalotoa mazao mengi na bora. Hivyo, rai yangu wakulima wajifunze kulima kilimo cha kisasa. Wananchi wajitokeze katika maonesho ya Nanenane hapa Nzuguni kujifunza mbinu bora...

Maandalizi ya Nanenane 2024 Dodoma yapamba moto

Image
Na. Flora Nadoo, DODOMA Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri ampongeza Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka alama katika maboresho ya miundombinu ya maonesho ya Nanenane Kanda ya Kati Dodoma. Kauli hiyo aliitoa mjini Dodoma alipokuwa akiongelea maandalizi ya maadhimisho ya sherehe za Nanenane zinazofanyika katika viwanja vya Nanenane Nzuguni. Alhaj Shekimweri alisema kuwa mwaka jana Rais wakati akiahirisha maonesho ya Nanenane Kanda ya Nyanda za Juu Kusini kwenye Uwanja wa John Mwakangale jijini Mbeya alielekeza maboresho ya viwanja vya Nanenane. Alisema kuwa viwanja viwili vimechaguliwa kuanza kufanyiwa ukarabati. Alisema kuwa Waziri wa Kilimo, Husein Bashe na viongozi wa Wizara chini ya Katibu Mkuu wa wizara ya Kilimo Gerald Mweli wameanza ukarabati wa viwanja hivyo. “Tumeanza kufanya kazi mbalimbali, miongoni mwa kazi hizo ni pamoja na udhibiti na uendeshaji wa uwanja kwa kujenga uzio, kujenga sehemu ya upashanaji habari (Information Centre). Shekimweri a...