Posts

Showing posts from August 21, 2023

ELIMU JUMUISHI KUTOA FURSA KWA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM KUSOMA JIJI LA DODOMA

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepongezwa kwa kujali elimu jumuishi katika shule za awali na msingi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kutoa fursa kwa watoto wengi kusoma. Mwanafunzi akisaidiwa na Mkuu wa Divisheni ya Elimu Awali na Msingi, Prisca Myalla (kulia) na Mkuu wa Seksheni ya Elimu Maalum, Issa Kambi (kustono) Pongezi hizo zilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Awali na Msingi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwl. Prisca Myalla alipoongoza zoezi la kutoa kadi za bima za afya na vifaa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum katika Shule ya Msingi Mlezi iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Mwl. Myalla alisema “siku ya leo ni siku jumuishi ya kuhimiza elimu jumuishi kwenye shule zetu. Tunamshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan anaendelea kulisimamia hilo kwenye shule zetu kama ambavyo leo tumekusanyika hapa kugawa vifaa kwa wanafunzi wetu wenye mahitaji maalum kwa shule nane zilizopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Tunao...

Rais Samia Aipa Cheti NMB Cha Mlipa Gawio Mkubwa

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan ametoa tuzo maalum kwa Benki ya NMB katika kutambua mchango na utendaji mzuri wa taasisi hiyo ya fedha nchini. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Ruth Zaipuna pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya NMB, Dkt. Edwin Mhede Cheti cha Mlipa gawio kubwa serikalini wakati wa kikao kazi cha wenyeviti wa bodi na watendaji wakuu wa taasisi za umma jijini Arusha. Benki hiyo ambayo serikali ina miliki asilimia 31.8, ilitoa gawio la biliioni 45.5 mwaka wa fedha 2021- 2022 Akizungumza katika kikao kazi cha wenyeviti wa bodi na watendaji wakuu wa taasisi za umma kinachofanyika katika ukumbi wa mikutano wa AICC jijini Arusha, Rais Samia amesema pamoja na kuwapongeza wale waliofanya vizuri, serikali pia itafanya tathmini ya utendaji wa taasisi na mashirika mengine nchini. “Kupitia mashirika, serikali inaweza kukusanya fedha nyingi za kutosha kujazia upungufu wa bajet...

KKKT Yaunga Mkono Uwekezaji, Yampongeza Rais Samia Kwa Hekima

Image
  ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Fredrick Shoo, amesema kuwa kanisa lake lina imani na namna ambavyo Rais Samia Suluhu Hassan analisimamia suala la uwekezaji kwenye bandari na kumpongeza Rais kwa uongozi wake wenye hekima. Kanisa la KKKT limesema kuwa linamuunga mkono Rais Samia na linaunga mkono uwekezaji nchini. KKKT pia imekemea watu wanaotaka kuligawa taifa kupitia kwa mjadala unaoendelea wa bandari kwa maslahi yao binafsi ya kidini, kisiasa na kiuchumi. Zifuatazo ni kauli 10 nzito zilizotolewa na KKKT kupitia kwa Askofu Mkuu Dk Shoo: 1. "Lipo hili la DP World Mheshimiwa (Rais). Kwanza naomba lieleweke wazi kwamba kanisa linaunga mkono uwekezaji. Hatupingi uwekezaji Mheshimiwa Rais" 2. "Tunajua wewe (Rais) kwenye nia yako unataka wawekezaji" 3. "Sisi viongozi wa dini zote kwa uwakilishi tuliomba kuja kukuona pale mwanzoni kabisa mwa jambo hili (mjadala wa DP World) na kwa uungwana wako na kwa unyenyekevu uli...

RAIS SAMIA ASHIRIKI MAADHIMISHO MIAKA 60 YA KANISA LA KKKT JIJINI ARUSHA

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo kutoka Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Askofu Fredrick Shoo ikiwa ni kwa ajili ya jitihada zake za kuleta Maendeleo nchini wakati wa Maadhimisho ya miaka 60 ya  Kanisa hilo yaliyofanyika katika Ukumbi wa Viwanja vya Mfuko wa Wastaafu Mkoani Arusha Maaskofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) pamoja na Waumini wa Kanisa hilo wakisikiliza kwa makini Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwenye Maadhimisho ya miaka 60 ya  Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Viwanja vya Mfuko wa Wastaafu Mkoani Arusha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Maaskofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) mara baada ya  kuzungumza nao kwenye Maadhimisho ya miaka 60 ya  Kanisa hilo yaliyofanyika katika Ukumbi wa V...