Posts

Showing posts from July 19, 2024

Hospitali ya Wilaya ya Dodoma kuboresha huduma za Afya

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Halmashauri ilianza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma kwa lengo la kusogeza huduma za afya kwa wananchi ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kaimu Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma, Dkt. Revocatus Baltazary akisoma taarifa ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma, Dkt. Revocatus Baltazary alipokuwa akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma mbele ya Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma. Dkt. Baltazary alisema “kutokana na changamoto ya kukosa hospitali ya wilaya kwa muda mrefu na changamoto ya umbali wa kupata huduma za afya kwa ngazi ya wilaya, halmashauri na serikali kuu iliamua kuanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Dodoma ili kusogeza huduma kwa wananchi. Hatua hii itawezesha wananchi kupata huduma za afya kwa ngazi ya wilaya”. Akiongelea mapokezi ya fedha, alisema kuwa serikali kuu ilitoa kiasi cha shi...

CCM yaridhishwa na miradi Jiji la Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma kimeridhishwa na utendaji kazi wa serikali baada ya kutembelea na kukagua miradi saba ya maendeleo yenye thamani ya shilingi 600,424,100,099 inayotekelezwa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.   Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Donald Mejiti akiongea wakati wa majumuisho ya ziara ya Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Dodoma Kauli hiyo ilitolewa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Donald Mejiti alipoongoza Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Dodoma kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.   Mejiti alisema kuwa kazi iliyofanyika ni kubwa na nzuri. Alisema kuwa timu yake imetembelea na kukagua miradi saba ya maendeleo yenye thamani ya shilingi 600,424,100,099 na kujiridhisha kuwa imetekelezwa kwa kiwango bora.   Aidha, alipongeza ushirikiano baina ya serikali na Chama Cha Mapinduzi kuwa ni mzuri....