Posts

Showing posts from December 20, 2023

Vikundi vyapatiwa Mil. 215 Kata ya Mnadani

Image
  Na. Dennis Gondwe, MNADANI VIKUNDI ya wanawake vijana na watu wenye ulemavu 18 vimepata mikopo ya shilingi 215,000,000 katika kipindi cha kuanzia mwaka 2021 hadi mwaka 2023 katika Kata ya Mnadani. Picha kutoka maktaba ya Jiji la Dodoma Takwimu hiyo ilitolewa na Afisa Mtendaji Kata ya Mnadani, Caroline Massawe alipokuwa akiwasilisha taarifa ya mafanikio ya serikali ya awamu ya sita kwenye mkutano wa hadhara wa wananchi wa Mtaa wa Mnadani. Massawe alisema kuwa sekta ya maendeleo ya jamii imepiga hatua kubwa katika kipindi cha miaka mitatu na kuwainua wananchi wa kata hiyo. “ Kuanzia mwaka 2021 hadi sasa katika Kata ya Mnadani, vikundi 18 vimepata mikopo na shilingi 215,000,000 zimetolewa. Kati ya vikundi hivyo, vikundi sita ni vya wanawake vilivyokopeshwa shilingi 49,000,000. Vikundi tisa vya vijana vimekopeshwa shilingi 142,000,000 na vikundi vitatu vya watu wenye ulemavu vimekopeshwa shilingi 24,000,000 na kufanya jumla ya shilingi 215,000,000. Mikopo hii imekuwa na manufaa...

Marufuku mifugo kuzurura Kata ya Mnadani

Image
Na. Dennis Gondwe, MNADANI WAFUGAJI wa Kata ya Mnadani wametakiwa kuacha tabia ya kuzurulisha mifugo yao na kufanya ufugaji wa ndani ili kwenda sambamba na mahitaji ya hadhi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Mifugo wa Kata ya Mnadani, Elizabeth Shirima alipokuwa akiongea na mamia ya wananchi wa Mtaa wa Mnadani katika mkutano wa hadhara. Shirima alisema kuwa kata hiyo inakabiliwa na ufugaji holela. “Mifugo inayozuzura ovyo ni ile ya ufugaji huria, Dodoma sasa ni Jiji hivyo, hakuna utaratibu wa kuzurulisha mifugo hasa katika barabara za lami na mitaa. Naomba wafugaji kama hamuwezi kufugia ndani mnashauriwa kuhamisha mifugo kutoka Jiji kwenda maeneo yanayokubalika hasa ufugaji wa wanyama wakubwa kama ng’ombe, mbuzi, punda, na ngamia. Kuna wakati gari la kubeba wagonjwa linakimbiza mgonjwa hospitali inabidi lisimame kusubiri mifugo ipite barabara kuu. Halmashauri ya Jiji imetenga maeneo kwa ajili ya wafugaji. Unapohitaji kununua eneo la kufuga mifugo nen...

KATA YA CHAMWINO YATOA ELIMU YA UKATILI WA KIJINSIA

Image
Na. Dennis Gondwe, CHAMWINO Timu ya wataalam kutoka Kata ya Chamwino yajikita katika utoaji wa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa makundi mbalimbali kwa lengo la kuhakikisha uelewa mpana katika mapambano hayo unaenea kwa jamii. Akielezea maeneo yaliyopewa  kipaumbele na timu hiyo katika kutoa elimu, Afisa Mtendaji kata ya Chamwino, Lucas Nkelege alisema kipaumbele ni kutoa elimu kwa jamii. Alisema kuwa timu hiyo ilijikita katika kuelezea wajibu wa wazazi na walezi katika makuzi ya watoto na sheria inayomlinda mtoto Namba 21 ya mwaka 2009. Maeneo mengine yaliyopewa msisitizo ni umuhimu wa ulinzi wa watoto wa kiume na madhara kwa watoto hao endapo hawatapewa uangalizi wa karibu na hatua za kufanya pale mtoto amapofanyiwa ukatili. Aidha, wazazi na walezi walitaarifiwa uwepo wa kituo cha huduma za pamoja na msaada kwa watoto waliofanyiwa ukatili (one stop center). Nkelege alisema kuwa timu shirikishi ya wataalamu ya Kata ya Chamwino iliongozwa na Afisa Mtendaj...