Posts

Showing posts from October 18, 2023

MATUKIO KATIKA PICHA SIKU YA TATU YA KLINIKI YA ARDHI DODOMA

Image
 

WANANCHI WAASWA KUIBUA MALALAMIKO YA ARDHI YALIYOFUNGWA JIJI LA DODOMA

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA WANANCHI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kuacha tabia ya kufanya bahati nasibu ya kupata haki isiyostahili baada ya kuwa malalamiko yao yamekwisha tatuliwa kwa mujibu wa taratibu na sheria. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule akiongea na wananchi waliojitokeza kupata huduma ya Ardhi katika Kliniki ya Ardhi jijini Dodoma Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule alipokuwa akiongea na mamia ya wananchi waliojitokeza kutatuliwa kero na malalamiko yao kwenye Kliniki ya Ardhi inayoendelea katika siku yake ya tatu jijini hapa. Senyamule alisema “nisisitize tunaposhughulikia kero hizi niombe wananchi wa Dodoma na kutoa wito najua kuna watu wanajirudiarudia kila wakati ambao kero zao zilishafungwa ila wanajaribu bahati nasibu nyingine. Nitoe rai wale ambao kero zao zilishafungwa huna haja ya kutumia masaa yako hapa, utapata jibu lilelile ambalo ulishalipata. Tukimaliza tatizo lako tunalifunga na tunapeana taarifa, naka...

DODOMA ISIYO NA KERO ZA ARDHI YATAJWA

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA RAIS, Dkt. Samia Suluhu Hassan anataka wananchi wa Dodoma wafurahie makao makuu yasiyokuwa na kero wala migogoro ya Ardhi. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule (kushoto) akikabidhi moja ya Hati zilizotolewa siku a tatu ya utekelezaji wa Kliniki ya Ardhi jijini Dodoma Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule alipokuwa akiongea na mamia ya wananchi waliojitokeza kuhudumiwa na kutatuliwa kero zao katika Kliniki ya Ardhi iliyo katika siku yake ya tatu jijini Dodoma. Senyamule alisema “niwahakikishie Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, mama mwenye upendo na mama anayewapenda watanzania, jambo hili halitaki na anatamani wananchi wa Dodoma wafurahie makao makuu ya Dodoma na watafurahia kama watapa haki zao. Ndiyo maana amekuwa akituagiza kutatua kero zao hasa za Ardhi katika Jiji la Dodoma. Kama mkoa baada ya kupokea maelekezo ya Mheshimiwa Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi wametuagi...