Posts

Showing posts from January 24, 2025

Jiji la Dodoma kuanza ujenzi wa Jengo Jumuishi Kituo cha Afya Makole

Image
Na. Faraja Mbise, MAKOLE Halmashauri ya Jiji la Dodoma inatarajia kuanza ujenzi wa Jengo Jumuishi katika Kituo cha Afya Makole ambao unatarajiwa kuanza tarehe 27 Januari, 2025 chini ya Mkandarasi Mohanmmedi Builders Limited. Akizungumzia kuhusu huduma zitakazokuwa zinapatikana katika jengo hilo jumuishi Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Makole, Dkt. Revocatus Baltazary alisema zitapatikana huduma mbalimbali kwa ajili ya kukidhi huduma zote za kiafya. “Jengo hili linaenda kujibu yote hayo, kwasababu huduma zitakazoenda kupatikana ni huduma za ‘emergency’, radiolojia, maabara, vyumba vya madaktari vitaongezwa. Pia kuna wodi za kulaza watoto chini ya umri wa miaka mitano, magonjwa ya ndani kwa wanawake na wanaume. Vilevile, wodi za upasuaji na ‘floor’ ya wakina mama wajawazito” alisema Dkt. Baltazary. Sambamba na hilo, alisema kuwa lengo hasa la kujenga jengo hilo ni kukosekana kwa baadhi ya huduma kama ‘emergency’, huduma za kulaza, na jengo la upasua. “Jengo hili linajengwa kutoka...

Matukio katika Picha Mafunzo ya NeST kwa Wakuu wa Shule ya Sekondari Jiji la Dodoma

Image
 

Wakuu wa Shule Jiji la Dodoma wapewa mafunzo ya mfumo wa NeST

Image
  Na. Coletha Charles, DODOMA Wakuu wa Shule za Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dodoma wamewezeshwa mafunzo ya ununuzi kwa njia ya mtandao serikalini ‘ National e-Procurement System of Tanzania’ (NeST) yatakayoboresha utendaji kazi na kuwawezesha kupata mafundi na watoa huduma kupitia mfumo wa manunuzi. Mafunzo hayo yalitolewa na Kitengo cha Manunuzi na Ugavi kwa lengo la kuongeza ufanisi na uwazi kwa kufanya shughuli za ununuzi kutokana na mabadiliko ya Sheria ya Mwaka 2023 na Kanuni za Manunuzi za Mwaka 2024, katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Umonga. Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Afisa Elimu Vifaa na Takwimu, Fredrick Mwakisambwe, alifafanua mfumo wa manunuzi kwa njia ya kielektroniki, ni mfumo ambao unarahisisha mchakato wa manunuzi na kuleta ufanisi mkubwa katika utendaji kazi. Alisema kuwa mafunzo hayo ni mahususi kwa wakuu wa shule wakiambatana na walimu wanaohusika kuratibu na kusimamia fedha ambazo zinapelekwa katika shule za sekondari kw...

Ziara ya Kamati ya Fedha na Utawala katika Kituo cha Afya Zuzu

Image
  Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma (route 2) Naibu Meya, Fadhili Chibago ilifanya ziara ya kutembelea na kukagua ujenzi wa ukamilishaji wa maabara tatu katika Shule ya Sekondari Zuzu iliyopo Kata ya Zuzu.   Mradi huo unagharama ya shilingi 85,000,000.00 fedha kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji.   Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma (route 2) Naibu Meya, Fadhili Chibago ilifanya ziara ya kutembelea na kukagua ujenzi wa ukamilishaji wa maabara tatu katika Shule ya Sekondari Zuzu iliyopo Kata ya Zuzu.   Mradi huo unagharama ya shilingi 85,000,000.00 fedha kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji.