Posts

Showing posts from August 4, 2025

Wasimamizi Wasaidizi Uchaguzi wapewa Semina Dodoma

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata wametakiwa kusoma katiba, sheria na miongozo inayotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa weledi na kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani. Msisitizo huo ulitolewa na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Dodoma Mjini na Mtumba, Wakili Cosmas Nsemwa wakati akifungua mafunzo kwa wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alianza kwa kuwapongeza washiriki wa mafunzo kwa kuteuliwa kuwa wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata. “Someni kwa umakini katiba, sheria, kanuni, miongozo na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na yatakayotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na ulizeni maswali ili mpate kufafanuliwa kwenye maeneo ambayo kwa namna moja au nyingine pengone yatakuwa na changamoto za kufahamu ili kuwarahisishia katika utekelezaji wenu wa kazi za uchaguzi” alisema Wakili Nsemwa. ...

Kilimo cha Mbogamboga kukuza Afya na kipato kwa wananchi Jiji la Dodoma

Na. Eupilio Anthony, DODOMA Mamia ya wananchi wameonesha hamasa kubwa kutembelea mabanda ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma yenye teknolojia mpya za kilimo, mifugo bora, ufugaji wa kisasa wa samaki, pamoja na bidhaa za viwandani zinazotengenezwa na wajasiriamali wa ndani kutokana na mazao ya kilimo na mifugo katika maonesho ya Nanenane. Kauli hii ilitolewa na Afisa Kilimo Mwandamizi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Nkunde Kimweri alipozungumza na waandishi wa habari waliofika kwenye banda la kilimo cha mbogamboga upande wa bustani kwenye maonesho ya wakulima Nanenane Nzuguni jijini Dodoma. Alisema kuwa kilimo cha kisasa cha mbogamboga kina njia nyingi za kukifanya kiwe na faida kwa afya na kiuchumi. “Hapa tunakipando cha bustani kichuguu ambacho tumepanda mboga mbalimbali, tuna mboga tofauti tofauti ambazo tunazitumia nyumbani. Kwa sasa tunahamasisha wananchi kulima mboga mboga hata kwenye maeneo madogo ya nyumbani kwao, kwa kutumia vichuguu kwasababu ni njia rahisi na safi sana. Pia...