Posts

Showing posts from December 9, 2025

Kamati za kudumu zatakiwa kuchangia kasi utekelezaji miradi ya maendeleo

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula alimtangaza Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Maadili ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuwa ni Omary Omary, Diwani wa Kata ya Makole, aliyepata kura zote tano kutoka kwa wajumbe wa kamati hiyo. Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Omary Omary (kushoto) ambae ni Diwani wa Kata ya Makole. Kulia ni Naibu Meya wa Jiji la Dodoma, Bakari Fundikira ambae pia ni Diwani wa Kata ya Chang'ombe Alisema kuwa kamati hiyo ina jumla ya wajumbe watano ambao ni Omary Omary (Diwani Kata ya Makole), Swalihina Athuman (Diwani Kata ya Viwandani), Charles Ngh’ambi (Diwani Kaya ya Mbalawala), Judith Mushi (Diwani Viti Maalum) na Mwamrisho Kasule (Diwani Viti Maalum). Mstahiki Meya aliwasoma wajumbe wa kamati nyingine kuwa ni Robert Njama, Diwani wa Kata ya Mkonze na Flora Liacho, Diwani wa Viti Maalum kuwa wajumbe wa Kamati ya Mfuko wa Jimbo la Dodoma Mjini. Wengine ni Elis Kitendya, ...

Kamati ya Kudumu Uchumi, Elimu na Afya yapata Jembe!

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA DIWANI wa Viti Maalum, Joan Mazanda aliibuka kidedea kwa kupata kura 15 na kuongoza Kamati ya kudumu ya Uchumi, Elimu na Afya katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Uchumi, Elimu na Afya, Joan Mazanda Akitangaza matokeo hayo, Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula alisema kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya Uchumi, Elimu na Afya ni Joan Mazanda. “Kamati ya kudumu ya Uchumi, Elimu na Afya ilikuwa na wagombea watatu wa nafasi ya mwenyekiti. Matokeo yalikuwa ni kama ifuatavyo. Mheshimiwa Andrew Muholo, Diwani wa Ipala alipata kura tatu; Mheshimiwa Fatuma Zollo, Diwani wa Viti Maalum alipata kura nne na Mheshimiwa Joan Mazanda, Diwani wa Viti Maalum alipata kura 15. Hivyo, mshindi ni Mheshimiwa Joan Mazanda” alisema Chaula. Katika hatua nyingine, Diwani wa Kata ya Madukani, Prof. Davis Mwamfupe alitoa pongezi kwa Diwani Mazanda kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamat...

Diwani Gombo kuongoza Kamati ya Mipango Miji na Mazingira

Image
Na. Dennis Gondwe, DODOMA Diwani wa Kata ya Ipagala, Gombo Dotto apata ushindi mnono nafasi ya Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya Mipango Miji na Mazingira kwa kuibuka na kura 20 akiwaacha kwa mbali wagombea wawili. Akitangaza matokeo ya nafasi ya Mwenyekiti, Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Alimwoni Chaula, alisema kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ya Mipango Miji na Mazingira ni Mheshimiwa Gombo Dotto. “Kamati ya kudumu ya Mipango Miji ilikuwa na wagombea watatu wa nafasi ya mwenyekiti. Mheshimiwa Leonard Ndama, Diwani wa Kata ya Nzuguni alipata kura moja, Mheshimiwa Theobalt Mahina, Diwani wa Kata ya Ntyuka alipata kura moja na Mheshimiwa Gombo Dotto alipata kura 20” alitangaza Mstahiki Meya Chaula. Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri aliwapongeza viongozi wote waliochaguliwa katika nafasi za kamati za kudumu na kuwaasa kutumia nafasi hizo kuhakikisha wanasimami...